Serikali mkoani Rukwa imekiri kuwepo uzembe katika usimamizi na ufuatiliaji wa ujenzi wa Vituo vya Afya Viwili na Hospitali ya Manispaa ya Sumbawanga,Mkoani Rukwa, yenye gharama ya shilingi Bilioni 2.6 ambayo imeshindwa kukamilika kama ilivyopanga lakini fedha zote zimekwisha.
Mkuu wa mkoa wa Rukwa QUEEN SENDIGA ameendelea na ziara ya kukagua na kutembelea miradi ya ujenzi wa miundombinu ya sekta ya afya, katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, ambapo imebainika matumizi ya fedha hayalingani na thamani ya fedha iliyotengwa na serikali.
Sendiga amesema mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Mollo kilichotengewa shilingi Milioni 400 fedha zimekwisha majengo matano hayajakamilika, Kituo cha Afya cha Matanga kilichopelekewa shilingi Milioni 500 fedha zimeisha majengo hayajakamilika, Ujenzi wa Hospitali ya Manispaa ya Sumbawanga yua ISOFU iliyotumia shilingi Bilioni 1.8 majengo yake hayajakamilika.
Amesema kuna uzembe ambao umetumika kutekeleza miradi hiyo, na uzembe umejitoikeza katika usimamizi na ufuatiliaji, kwani utekelezaji wa miradi yote hiyo inakwenda kwa mfumo wa Force akaunti, Wananchi hawashirikishi katika utekelezaji wa miradi.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Sumbawanga SEBASTIAN WARYUBA naye amekiri watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga wamemuangusha kwasababu uzembe huo unawahusu, ikiwemo idara ya uhandisi, idara ya manunuzi na watendaji wengine.
Hata hivyo Mganga Mkuu wa mkoa wa Rukwa Dokta IBRAHIMU ISAACK amebaini ukikwaji wa miongozo ya utekelezaji wa mfumo wa Force akaunti, ambapo ofisi ya manunuzi katika ofisi ya mkurugenzi iliwanunulia vifaa wananchi badala ya wajumbe wa kamati ya ujenzi wa vituo vya afya.
*********************MWISHO*******************
Trending
- Nilikuwa Mwembamba Kupita Kiasi Licha ya Kula Vizuri Hatua Nilizochukua Kuanza Kuongeza Uzito kwa Afya
- Nilikuwa Nakunjamana kwa Maumivu Kila Nikifika Siku Zangu Njia Nilizojifunza Kudhibiti Maumivu ya Hedhi Bila Kukata Tamaa
- NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATOA TABASAMU KWA KITUO CHA TUMAINI LA WAZEE JIJINI MBEYA.
- LIVE: JUBILEE YA MIAKA 25 KATIKA NDOA. YA MR. & MRS. PATRICK ADKIN MWALUNENGE
- Alinilikataa Kimapenzi Mara Kadhaa Hatua Moja Iliyobadilisha Mtazamo Wake
- Hatua Moja Iliyanifanya Nimepata Mali Yangu
- Mtoto Wangu Alichelewa Kutembea na Kuongea Hatua Moja Iliibua Maendeleo Yake
- Nilianza Januari Bila Pesa ya Mahitaji Hatua Moja Ilinisaidia Kusimama Tena
