Na. Mwandishi wetu Jeshi la Polisi- Arusha
Ikiwa leo ni Machi 08,2024 kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani, Mtaandao wa
Polisi Wanawake Mkoa wa Arusha wameunga na wanawake wengine Mkoani humo huku
Mtandao huo wakiitumia siku hiyo kuwawekea akiba ya fedha katika mfuko wa uwekezaji (UTT)
kwa Watoto wawili wa askari wanandoa waliofariki kwa ajali ya gari.
Akiongea katika Viwanja vya Ngarenaro Complex Jijini Arusha Mwenyekiti wa Mtandao huo
Mkoa wa Arusha Mrakibu mwandamizi wa Polisi SSP Zauda Mohamed amesema mtaandao huo
katika kuelekea kilele hicho ulianza mapema kutoa elimu maeneo mbalimbali Pamoja na
kufanya ibada ya kuwaombea marehemu.
SSP Zauda ameongeza kuwa katika kuadhimisha siku hiyo waliona vyema kuunga na
kuwawekea akiba ya fedha kwa Watoto wa askari wanandoa waliofariki katika ajali ya gari
ambapo amebainisha kuwa fedha hizo zitawasaidia Watoto hao katika swala la elimu na
mahitaji mengine ya kibinadamu.
Aidha ametoa wito kwa wanawake wengine Mkoani humo kufanya kazi kwa bidii,nidhamu na
kutenda haki ili ustawi bora na wajikwamue kiuchumi na maendeleo ya Taifa kwa Ujumla.
Nae mrakibu msaidizi wa Polisi Lucy Teesa kutoka Makao Makuu ya kikosi cha Kuzuia wizi wa
Mifugo STPU amewaomba wanaweka wenzake kushiriki vyema katika mapambano dhidi
uhalifu ambapo amewaomba kutoa taarifa za uhalifu na kujikitaa katika malezi bora ya Watoto
ili kujenga Jamii iliyostarabika.
Kwa upande wake Mkuu wa kituo cha Polisi Wilaya ya Kipolisi Murieti Mrakibu msaidizi wa Polisi
ASP Tausi Mbalamwezi amewaomba wanawake wenzake kujiamini na kujituma katika
kutekeleza majukumu yao huku akiwaomba kuumuunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuliinua taifa kiuchumi.
Trending
- TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
- Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
- MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
- Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
- Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
- WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI
- SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA
- INEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO

