Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

VIDEO: ZIARA YA KUSHTUKIZA YA WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA, HOSPITALI YA RUFAA YA DODOMA

November 15, 2025

Kutoka Kupoteza Kazi Hadi Kujiamini Tena Safari Yangu Ya Kurudi Kuwa Mwanaume wa Nyumba

November 15, 2025

Nilivyopata Utajiri Usionisumbua Baada ya Kuacha Kufuata Marafiki Wenye Mashinikizo

November 15, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • VIDEO: ZIARA YA KUSHTUKIZA YA WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA, HOSPITALI YA RUFAA YA DODOMA
  • Kutoka Kupoteza Kazi Hadi Kujiamini Tena Safari Yangu Ya Kurudi Kuwa Mwanaume wa Nyumba
  • Nilivyopata Utajiri Usionisumbua Baada ya Kuacha Kufuata Marafiki Wenye Mashinikizo
  • BAKWATA YATOA TAMKO JUU YA MATUKIO YA OKT 29 SIKU YA UCHAGUZI MKUU LASOMWA KWA WAISLAMU NCHI NZIMA
  • Nilivyofanikiwa Kuacha Kukasirika Haraka na Kuishi Kwa Amani na Watu
  • Nilivyopata Upendo wa Kweli Baada ya Miaka ya Kutumiwa na Kuumizwa
  • Rais Samia Atoa Msamaha kwa Waliojiingiza Kwenye Machafuko Bila Kudhamiria
  • Dkt. Samia Amuapisha Dkt. Mwigulu: Tanzania Yapata Waziri Mkuu Mpya
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WATUHUMIWA MBARONI KWA WIZI WA MIFUGO NA UTOROSHAJI.
Video Mpya

WATUHUMIWA MBARONI KWA WIZI WA MIFUGO NA UTOROSHAJI.

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMarch 12, 2024No Comments4 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Na Abel Paul,Jeshi la Polisi- Tinde Shinyanga.

Jeshi la Polisi kikosi cha kuzuia wizi wa mifugo STPU Kimesema Kinawashikilia watuhumiwa kadhaa kwa tuhuma za wizi wa mifugo na utoroshaji Mifugo nje ya nchi huku likisema kuwa litaendelea kushirikiana na wananchi kwa karibu ili kudhibiti uhalifu huo hapa nchini.

Akitoa taarifa hiyo leo Machi 12,2024 na kamanda wa Polisi kikosi cha kuzuia wizi wa mifugo Nchini Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi SACP Simon Pasua wakati alipotembelea mnada wa Tinde uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga Mkoani Shinyanga amesema Jeshi hilo linawashirikilia watuhumiwa wa wizi wa mifugo katika maeneo tofauti tofauti hapa nchini.

Kamanda Pasua ameongeza kuwa watuhumiwa waliokamatwa kwa tuhuma za wizi wa mifugo katika maeneo tofauti hapa nchini majina yao yamehifadhiwa kwa sababu za kiuchunguzi ambapo amesema kikosi hicho kitaendelea kuwakamata wale wote watakao bainika katika kujihusisha na wizi wa mifugo.

Aidha amewaomba wananchi kote nchini kuendelea kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi za baadhi ya watu wanaojihusisha na wizi wa mifugo Pamoja na kutorosha mifugo nje ya nchi.

Kwa upande wake afisa biashara Kutoka Shinyanga vijijini Upendo Milisho amebainisha kuwa wananchi na wafanya biashara mifugo katika mnada wa Tinde uliopo halmashauri ya Shinyanga wamekuwa na mwitikio Chanya katika ulipaji Ushuru kwa kielektroniki mnadani hapo.

Afisa Mapato Wilaya ya Shinyanga Bw. Victor Moleli Pamoja na kushukuru kikosi cha kuzuia wizi wa mifugo amebainsha kuwa Jeshi la Polisi pamoja na wananchi wameendelea kudhibiti uhalifu katika eneo hilo la mnada wa Tinde kitendo kilichopelekea mnada huo kuwa miongoni mwa minada yenye kukusanya mapato vizuri na usalama wa kutosha.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

VIDEO: ZIARA YA KUSHTUKIZA YA WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA, HOSPITALI YA RUFAA YA DODOMA

November 15, 2025

BAKWATA YATOA TAMKO JUU YA MATUKIO YA OKT 29 SIKU YA UCHAGUZI MKUU LASOMWA KWA WAISLAMU NCHI NZIMA

November 14, 2025

Rais Samia Atoa Msamaha kwa Waliojiingiza Kwenye Machafuko Bila Kudhamiria

November 14, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025229

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025220

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024200

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025127
Don't Miss
Video Mpya

VIDEO: ZIARA YA KUSHTUKIZA YA WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA, HOSPITALI YA RUFAA YA DODOMA

By Mbeya YetuNovember 15, 202513

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 15, 2025 amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na kuziagiza hospitali zote nchini zihakikishe wajawazito wanapofika hospitali wahudumiwe kwa haraka ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Pia, Waziri Mkuu ameiagiza Wizaya ya Afya, Bohari ya Dawa (MSD) na Hospitali zote nchini ziweke vipaumbele vya kuwa na dawa kulingana na mahitaji ya eneo husika. “ Haipendezi mwananchi kufika hospitali na kupatiwa vipimo vyote kisha anaambiwa dawa akanunue kwingine, kama duka binafsi linaweza kupata dawa hizo, inawezekanaje hospitali za serikali hapati? Naagiza Hospitali zote ziwe na dawa.”

Ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wananchi nje ya hospitali hiyo baada ya kutembelea wananchi waliofika hospitalini hapo kupata huduma mbalimbali za kitabibu ambapo amesisitiza wananchi waendelee kuhudumiwa vizuri kwa kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini vikiwemo vifaa tiba na dawa.

Kadhalika Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zihakikishe zinakuwa na vifaa vya usafi binafsi vya dharura vikiwemo ndoo na beseni katika wodi za wazazi ili viwasaidie akinamama wasiokuwa na vifaa hivyo. “Ujauzito sio suala la dharura vifaa kama ndoo tunapaswa kuwa navyo katika hospitali zetu za serikali.”

Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya katika uboreshaji wa huduma za afya nchini. Waziri Mkuu akiwa hospitalini hapo, wananchi walimueleza kuwa wanahudumiwa vizuri na kwa uangalizi wa karibu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wagonjwa na wananchi wanaoguza ndugu zao wamempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za afya.

Kutoka Kupoteza Kazi Hadi Kujiamini Tena Safari Yangu Ya Kurudi Kuwa Mwanaume wa Nyumba

November 15, 2025

Nilivyopata Utajiri Usionisumbua Baada ya Kuacha Kufuata Marafiki Wenye Mashinikizo

November 15, 2025

BAKWATA YATOA TAMKO JUU YA MATUKIO YA OKT 29 SIKU YA UCHAGUZI MKUU LASOMWA KWA WAISLAMU NCHI NZIMA

November 14, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

VIDEO: ZIARA YA KUSHTUKIZA YA WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA, HOSPITALI YA RUFAA YA DODOMA

November 15, 2025

Kutoka Kupoteza Kazi Hadi Kujiamini Tena Safari Yangu Ya Kurudi Kuwa Mwanaume wa Nyumba

November 15, 2025

Nilivyopata Utajiri Usionisumbua Baada ya Kuacha Kufuata Marafiki Wenye Mashinikizo

November 15, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025229

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025220

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024200
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.