Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri

September 17, 2025

Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake

September 17, 2025

Kongamano la Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050 Kufanyika Mbeya

September 17, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri
  • Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake
  • Kongamano la Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050 Kufanyika Mbeya
  • Prof. Makulilo: Watanzania Wajiandae kwa Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050
  • Tajiri wa madini aliyefilisika arejea tena katika biashara kwa kishindo
  • Nilirogwa Nipoteze Kila Kitu ila Hatua Niliyopiga Ilinivunja Minyororo Ya Uchawi
  • Niliibiwa Gari Yangu Usiku, Lakini Hatua Niliyopiga Ilifanya Wezi Wenyewe Walirudishe Hadi Getini
  • Nilipoteza Mume Wangu Kwa Mpango wa Kando ila Kitu Nilichojaribu Kilimfanya Aombe Radhi Hadharani
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WATENDAJI UBORESHAJI WATAKIWA KUHAMASISHA WANACHI KUJIANDIKISHA
Uncategorized

WATENDAJI UBORESHAJI WATAKIWA KUHAMASISHA WANACHI KUJIANDIKISHA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJanuary 4, 2025Updated:January 4, 2025No Comments0 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura (Elimu)  Dkt. Rose Likangaga akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mjumbe wa Tume, Dkt. Zakia Mohamed Abubakar. 

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura (Elimu)  Dkt. Rose Likangaga akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mjumbe wa Tume, Dkt. Zakia Mohamed Abubakar. 

Mwenyekiti wa Mafunzo, Bw. Khalid Khalif akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo. 
Na Mwandishi wetu, Songea
Watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura mkoani Ruvuma wametakiwa kuhamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao baadae mwaka huu.
 
Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Zakia Mohamed Abubakar kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura (Elimu)  Dkt. Rose Likangaga wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa watendaji hao mkoani Ruvuma.
 
“Mnahimizwa kuhamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao,” ilisema sehemu ya hotuba hiyo.
 
Dkt Likangaga akisoma hotuba hiyo alisema ni matarajio ya Tume kuwa, mara baada ya zoezi hili lililopo mbele yao kukamilika watu watakaokuwa wamepatiwa kadi watakuwa ni Wapiga Kura Halali.
 
Aidha alisema, jukumu la uhamasishaji linawahusu moja kwa moja wao watendaji kwa kushirikiana na wadau wengine katika maeneo yao kupitia nyenzo walizonazo.
 
“Ninasisitiza kwamba, mabango na vipeperushi mtakavyopewa na Tume mvisambaze mapema katika kata zote zilizopo katika halmashauri zenu. Kazi yenu kubwa ni kusimamia na kuendesha shughuli zote za uboreshaji katika halmashauri zenu,”ilisisitiza hotuba hiyo.
 
 Watendaji hao wameatakiwa kuisoma kwa umakini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, Sheria za Uchaguzi, Kanuni za Uboreshaji, Maelekezo na Miongozo yote inayotolewa na Tume ili kazi yao ifanyike kwa uadilifu na haki.
 
Pia wametakiwa kuwasiliana na Tume kwa ajili ya ufafanuzi wa masuala yote yanayohusiana na utekelezaji wa majukumu yao pindi wanapokutana na changamoto zozote.
 
“Tume imetekeleza jukumu lake katika hatua ya mafunzo na hivyo nanyi mna wajibu wa kuhakikisha kuwa mnatekeleza kikamilifu majukumu yote mliyokasimiwa,” ilisema sehemu ya hotuba hiyo.
 
Pia Tume imewataka watendaji hao kuwa makini katika kila eneo la usambazaji na utunzaji wa vifaa na muda sahihi wa ufunguaji na ufungaji wa vituo vya kuandikishia wapiga kura.
 
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unataraji kuanza Januari 12 hadi 18, 2025 katika mikoa ya Songwe, Njombe, Rukwa na Ruvuma kwenye Halmashauri za Wilaya ya Nyasa, Mbinga, Mbinga Mji, Wilaya ya Songea na Manispaa ya Songea ambapo vituo vitakuwa vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
 
Mafunzo hayo yaliwahusisha Maafisa Waandikishaji,Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi, Maafisa TEHAMA wa Halmashauri.

 

 

Washiriki wakisikiliza hotuba ya kufunga mafunzo hayo. 
Mafunzo yakiendelea 

 

mmoja wa wakufunzi akitoa maelekezo wakati wa mafunzo kwa vitendo. 

 

 

Washiriki wakifanya mafunzo kwa vitendo. 

 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri

September 17, 2025

Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake

September 17, 2025

Tajiri wa madini aliyefilisika arejea tena katika biashara kwa kishindo

September 17, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025210

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024184

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025126

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025125
Don't Miss
Uncategorized

Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri

By Mbeya YetuSeptember 17, 20251

Baadhi yao waliniambia waziwazi kuwa hawawezi kuwa na mwanamke mwenye ulemavu. Nilipita katika aibu nyingi…

Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake

September 17, 2025

Kongamano la Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050 Kufanyika Mbeya

September 17, 2025

Prof. Makulilo: Watanzania Wajiandae kwa Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050

September 17, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri

September 17, 2025

Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake

September 17, 2025

Kongamano la Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050 Kufanyika Mbeya

September 17, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025210

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024184

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025126
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.