Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilikuwa Mwembamba Kupita Kiasi Licha ya Kula Vizuri Hatua Nilizochukua Kuanza Kuongeza Uzito kwa Afya

January 4, 2026

Nilikuwa Nakunjamana kwa Maumivu Kila Nikifika Siku Zangu Njia Nilizojifunza Kudhibiti Maumivu ya Hedhi Bila Kukata Tamaa

January 4, 2026

NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATOA TABASAMU KWA KITUO CHA TUMAINI LA WAZEE JIJINI MBEYA.

January 4, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilikuwa Mwembamba Kupita Kiasi Licha ya Kula Vizuri Hatua Nilizochukua Kuanza Kuongeza Uzito kwa Afya
  • Nilikuwa Nakunjamana kwa Maumivu Kila Nikifika Siku Zangu Njia Nilizojifunza Kudhibiti Maumivu ya Hedhi Bila Kukata Tamaa
  • NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATOA TABASAMU KWA KITUO CHA TUMAINI LA WAZEE JIJINI MBEYA.
  • LIVE: JUBILEE YA MIAKA 25 KATIKA NDOA. YA MR. & MRS. PATRICK ADKIN MWALUNENGE
  • Alinilikataa Kimapenzi Mara Kadhaa Hatua Moja Iliyobadilisha Mtazamo Wake
  • Hatua Moja Iliyanifanya Nimepata Mali Yangu
  • Mtoto Wangu Alichelewa Kutembea na Kuongea Hatua Moja Iliibua Maendeleo Yake
  • Nilianza Januari Bila Pesa ya Mahitaji Hatua Moja Ilinisaidia Kusimama Tena
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WATENDAJI UBORESHAJI WATAKIWA KUHAMASISHA WANACHI KUJIANDIKISHA
Uncategorized

WATENDAJI UBORESHAJI WATAKIWA KUHAMASISHA WANACHI KUJIANDIKISHA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJanuary 4, 2025Updated:January 4, 2025No Comments1 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura (Elimu)  Dkt. Rose Likangaga akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mjumbe wa Tume, Dkt. Zakia Mohamed Abubakar. 

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura (Elimu)  Dkt. Rose Likangaga akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mjumbe wa Tume, Dkt. Zakia Mohamed Abubakar. 

Mwenyekiti wa Mafunzo, Bw. Khalid Khalif akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo. 
Na Mwandishi wetu, Songea
Watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura mkoani Ruvuma wametakiwa kuhamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao baadae mwaka huu.
 
Hayo yamesemwa na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Dkt. Zakia Mohamed Abubakar kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura (Elimu)  Dkt. Rose Likangaga wakati akifunga mafunzo ya siku mbili kwa watendaji hao mkoani Ruvuma.
 
“Mnahimizwa kuhamasisha wananchi wenye sifa ili wajitokeze kujiandikisha na kupata haki yao ya kikatiba itakayowawezesha kushiriki katika kuchagua viongozi wao,” ilisema sehemu ya hotuba hiyo.
 
Dkt Likangaga akisoma hotuba hiyo alisema ni matarajio ya Tume kuwa, mara baada ya zoezi hili lililopo mbele yao kukamilika watu watakaokuwa wamepatiwa kadi watakuwa ni Wapiga Kura Halali.
 
Aidha alisema, jukumu la uhamasishaji linawahusu moja kwa moja wao watendaji kwa kushirikiana na wadau wengine katika maeneo yao kupitia nyenzo walizonazo.
 
“Ninasisitiza kwamba, mabango na vipeperushi mtakavyopewa na Tume mvisambaze mapema katika kata zote zilizopo katika halmashauri zenu. Kazi yenu kubwa ni kusimamia na kuendesha shughuli zote za uboreshaji katika halmashauri zenu,”ilisisitiza hotuba hiyo.
 
 Watendaji hao wameatakiwa kuisoma kwa umakini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, Sheria za Uchaguzi, Kanuni za Uboreshaji, Maelekezo na Miongozo yote inayotolewa na Tume ili kazi yao ifanyike kwa uadilifu na haki.
 
Pia wametakiwa kuwasiliana na Tume kwa ajili ya ufafanuzi wa masuala yote yanayohusiana na utekelezaji wa majukumu yao pindi wanapokutana na changamoto zozote.
 
“Tume imetekeleza jukumu lake katika hatua ya mafunzo na hivyo nanyi mna wajibu wa kuhakikisha kuwa mnatekeleza kikamilifu majukumu yote mliyokasimiwa,” ilisema sehemu ya hotuba hiyo.
 
Pia Tume imewataka watendaji hao kuwa makini katika kila eneo la usambazaji na utunzaji wa vifaa na muda sahihi wa ufunguaji na ufungaji wa vituo vya kuandikishia wapiga kura.
 
Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unataraji kuanza Januari 12 hadi 18, 2025 katika mikoa ya Songwe, Njombe, Rukwa na Ruvuma kwenye Halmashauri za Wilaya ya Nyasa, Mbinga, Mbinga Mji, Wilaya ya Songea na Manispaa ya Songea ambapo vituo vitakuwa vinafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni.
 
Mafunzo hayo yaliwahusisha Maafisa Waandikishaji,Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi, Maafisa TEHAMA wa Halmashauri.

 

 

Washiriki wakisikiliza hotuba ya kufunga mafunzo hayo. 
Mafunzo yakiendelea 

 

mmoja wa wakufunzi akitoa maelekezo wakati wa mafunzo kwa vitendo. 

 

 

Washiriki wakifanya mafunzo kwa vitendo. 

 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Nilikuwa Mwembamba Kupita Kiasi Licha ya Kula Vizuri Hatua Nilizochukua Kuanza Kuongeza Uzito kwa Afya

January 4, 2026

Nilikuwa Nakunjamana kwa Maumivu Kila Nikifika Siku Zangu Njia Nilizojifunza Kudhibiti Maumivu ya Hedhi Bila Kukata Tamaa

January 4, 2026

Alinilikataa Kimapenzi Mara Kadhaa Hatua Moja Iliyobadilisha Mtazamo Wake

January 3, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025291

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025239

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024213

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025132
Don't Miss
Uncategorized

Nilikuwa Mwembamba Kupita Kiasi Licha ya Kula Vizuri Hatua Nilizochukua Kuanza Kuongeza Uzito kwa Afya

By Mbeya YetuJanuary 4, 20263

Kwa muda mrefu nilikuwa mtu wa kuonewa huruma. Nilikuwa nakula kama wengine, wakati mwingine hata…

Nilikuwa Nakunjamana kwa Maumivu Kila Nikifika Siku Zangu Njia Nilizojifunza Kudhibiti Maumivu ya Hedhi Bila Kukata Tamaa

January 4, 2026

NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATOA TABASAMU KWA KITUO CHA TUMAINI LA WAZEE JIJINI MBEYA.

January 4, 2026

LIVE: JUBILEE YA MIAKA 25 KATIKA NDOA. YA MR. & MRS. PATRICK ADKIN MWALUNENGE

January 3, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilikuwa Mwembamba Kupita Kiasi Licha ya Kula Vizuri Hatua Nilizochukua Kuanza Kuongeza Uzito kwa Afya

January 4, 2026

Nilikuwa Nakunjamana kwa Maumivu Kila Nikifika Siku Zangu Njia Nilizojifunza Kudhibiti Maumivu ya Hedhi Bila Kukata Tamaa

January 4, 2026

NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATOA TABASAMU KWA KITUO CHA TUMAINI LA WAZEE JIJINI MBEYA.

January 4, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025291

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025239

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024213
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.