Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Mbeya Zonal: Mafunzo ya Dharura Yaendelea Kuimarisha Uokozi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini

November 26, 2025

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA

November 26, 2025

*DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA*

November 26, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Mbeya Zonal: Mafunzo ya Dharura Yaendelea Kuimarisha Uokozi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini
  • WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA
  • *DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA*
  • WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI
  • Karejesha tabasamu la uso wake na ndoa yake
  • HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAANZA RASMI KUTOA MAFUNZO YA HUDUMA ZA DHARURA KWA LENGO LA KUOKOA MAISHA NA KUPUNGUZA ATHARI ZA AJALI NA DHARURA ZA KIAFYA NYANDA ZA JUU KUSINI
  • TANZANIA NA QATAR ZASAINI HATI YA MAKUBALIANO YA KUTAMBULIANA VYETI VYA MABAHARIA
  • EDEN KATININDA: ”MNUNUZI MASHUHURI WA PARETO NCHINI ATOA SOMO KWA WAKULIMA WA ZAO LA PARETO”
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » CHUO CHA SAYANSI ZA AFYA K’S ROYAL CHAPONGEZWA KWA JUHUDI ZA KUKUZA UJUZI KWA WANAFUNZI KUKIDHI SOKO LA AJIRA NCHINI
Afya na Ustawi

CHUO CHA SAYANSI ZA AFYA K’S ROYAL CHAPONGEZWA KWA JUHUDI ZA KUKUZA UJUZI KWA WANAFUNZI KUKIDHI SOKO LA AJIRA NCHINI

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 9, 2025Updated:February 9, 2025No Comments34 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Sayansi za Afya cha K’s Royal imepata nafasi ya kipekee ya kupongeza uongozi na wafanyakazi wa chuo kwa juhudi zao za kuhakikisha wanafunzi wanapata maarifa na ujuzi wa kisasa ili kuendana na mahitaji ya soko la ajira nchini. Katika kikao cha hivi karibuni, bodi hiyo ilibaini kwamba chuo kimejizatiti katika kuimarisha mitaala na mafunzo ambayo yanajibu moja kwa moja changamoto zinazokabili sekta ya afya nchini.

Akiongea katika kikao kwenye kikao cha uzinduzi wa bodi mpya ya Chuo, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri, Sr. Shukrani Ndumilla alisema, “Tuna furaha kubwa kuona kwamba chuo cha K’s Royal kinazingatia ubora wa elimu na mafunzo yanayotolewa kwa wanafunzi wake. Hii ni hatua muhimu sana katika kuimarisha sekta ya afya na kuandaa wanachuo kuwa viongozi wa baadaye.”

Nae Mkuu wa Chuo cha K’s Royal Edward Aloyce amesema Wafanyakazi wa chuo hicho wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu na wadau mbalimbali, ikiwa ni pamoja na hospitali, vituo vya afya na mashirika yasiyo ya kiserikali, ili kuhakikisha mafunzo yanayotolewa yanazingatia mahitaji halisi ya soko. Chuo pia kina programu za mafunzo kwa vitendo, ambapo wanafunzi wanapata nafasi ya kufanya kazi katika maeneo halisi ya huduma za afya.
Amesema kuwa wanafunzi wanaofuzu kutoka chuo hicho wamekuwa wakifanya vizuri katika soko la ajira, huku wengi wakiteuliwa katika nafasi muhimu katika taasisi mbalimbali za afya. Hii ni ishara tosha ya kazi nzuri inayoendelea kufanywa na chuo hicho.
“Tutendelea kufanya kila posible kuhakikisha kuwa wanafunzi wetu wanapokea elimu bora na mafunzo yanayowafanya wawe tayari kukabiliana na changamoto za sekta ya afya. Tunashirikiana na wadau mbalimbali ili kuboresha mazingira ya kujifunza na kuwapatia wanafunzi ujuzi wanaohitaji.” – Edward

Bodi ya Ushauri imeelekeza wito kwachuo hicho kuendelea kuwa mfano ili kuimarisha ubora wa mafunzo yanayotolewa nchini, na mwisho, kuimarisha sekta ya afya kwa faida ya jamii nzima

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAANZA RASMI KUTOA MAFUNZO YA HUDUMA ZA DHARURA KWA LENGO LA KUOKOA MAISHA NA KUPUNGUZA ATHARI ZA AJALI NA DHARURA ZA KIAFYA NYANDA ZA JUU KUSINI

November 26, 2025

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025

“Serikali yajizatiti kumaliza Fistula — Huduma bora kwa mama na mtoto yazidi kupewa kipaumbele”

May 21, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025236

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025230

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024201

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025128
Don't Miss
Video Mpya

Mbeya Zonal: Mafunzo ya Dharura Yaendelea Kuimarisha Uokozi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini

By Mbeya YetuNovember 26, 20251

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imeanza rasmi kutoa mafunzo ya magonjwa ya Dharura na Mahututi kwa watoa huduma za afya, wanafunzi wa kada za Afya pamoja Jamii Nyanda za Juu Kusini kwa lengo la kuokoa maisha na kupunguza athari za ajali na dharura za kiafya.

Akiongea wakati wa kufungua mafunzo hayo leo tarehe 26 novemba,2025 katika kituo cha kutolea mafunzo hayo kwa vitendo kilichojengwa chini ya udhamini wa taasisi ya Abbott Fund, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji amesema, kuanzishwa kwa mafunzo hayo kutasaidia upatikanaji wa wataalamu wenye weredi kwani kumekuwa na ongezeko la wanafunzi wengi kuliko miundo mbinu ya kufundishia mafunzo haya kwa vitendo.

“…wote tunajua kwamba miaka ya karibuni kumekuwa na ongezeko la wanafunzi kwenye vyuo vyetu ambalo haliendi sambamba na miundombinu ya kufundishia kwa vitendo.” – Dkt. Mbwanji

Aidha Dkt. Mbwanji ameishukuru taasisi ya Abbott Fund Tanzania, Wizara ya Afya pamoja (EMAT) kwa ushirikiano katika ujenzi wa kituo hicho cha kutolea mafunzo hayo.

“…lilianza kama wazo na sasa linaonekana hivyo niwashukuru sana Abbott Fund Tanzania, Wizara ya afya pamoja na (EMAT) kwa kuratibu upatikanaji wa kituo hiki”. – Dkt. Mbwanji

Kwa upande wake Dkt. Raya Mussa, Meneja Mradi huduma za dharura akiongea kwa niaba ya Taasisi ya Abbott Fund Tanzania ameishukuru Wizara ya Afya kupitia Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa ushirikiano waliouonyesha kwa kukubali ujenzi wa kituo ambacho kitawanufaisha watoa huduma za afya, wanafunzi pamoja wataalamu wote wanapatikana Kanda ya Nyanda za Juu Kusini katika idara za Magonjwa ya Dharura na Ajali kutokana na miundombinu pamoja na vifaa ya kisasa vinavyopatikana katika kituo hicho.

“…lengo la kituo hiki si kunufaisha watu wa ndani tu lakini pia itanufaisha wanafunzi pamoja na watu wengine watakaohitaji kujifunza mafunzo haya hata kama si watoa huduma za afya”. – Dkt. Raya Mussa

Dkt. Prosper Bashaka ni Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya amesema, maboresho ya upatikanaji wa huduma za dharura imekuwa ni kipaumbele kikubwa cha serikali, hivyo amewapongeza wadau wote walioshiriki katika jitihada za uanzishwaji wa kituo hicho cha kutolea mafunzo ya Magonjwa ya Dharura na Mahututi kwani kitaleta tija kwa hospitali na jamii hasa kwa wakazi wa Nyanda za Juu Kusini.

“…nitoe pongezi kwa wadau wote walioshiriki katika ujenzi wa kituo hiki kwani kitaleta tija kwa hospitali na zaidi wakazi wa Nyanda za Juu Kusini”. – Dkt. Prosper Bashaka.

Hadi sasa vituo hivyo vya kutolea mafunzo ya Magonjwa ya Dharura na Mahututi vimejengwa zaidi ya 6 nchi nzima kwa ushirikiano wa taasisi ya Abott Fund, Wizara ya Afya pamoja na EMART.

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA

November 26, 2025

*DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA*

November 26, 2025

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI

November 26, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Mbeya Zonal: Mafunzo ya Dharura Yaendelea Kuimarisha Uokozi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini

November 26, 2025

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA

November 26, 2025

*DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA*

November 26, 2025
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025236

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025230

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024201
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.