Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

TAASISI ZA PICTERUS AS NA GOAL 3 KUANZISHA TEKNOLOJIA YA KISASA YA KUPIMA MANJANO KWA WATOTO WACHANGA TANZANIA

January 28, 2026

MAHUNDI: SERIKALI YAELEZA SABABU ZA KUTOWALAZIMISHA WATOTO KUWAHUDUMIA WAZAZI.

January 28, 2026

WAZEE WASHIRIKIANA NA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII ZOEZI LA UPANDAJI MITI DODOMA.

January 27, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • TAASISI ZA PICTERUS AS NA GOAL 3 KUANZISHA TEKNOLOJIA YA KISASA YA KUPIMA MANJANO KWA WATOTO WACHANGA TANZANIA
  • MAHUNDI: SERIKALI YAELEZA SABABU ZA KUTOWALAZIMISHA WATOTO KUWAHUDUMIA WAZAZI.
  • WAZEE WASHIRIKIANA NA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII ZOEZI LA UPANDAJI MITI DODOMA.
  • Wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Waadhimisha Kuzaliwa Rais Samia kwa Mshikamano
  • MADAKTARI BINGWA WA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA MKOANI MANYARA
  • Serikali Yakabidhi Vifaa vya Kujifunzia kwa Wanafunzi Wenye Mahitaji Maalum Nsalala
  • Nilipata Miscarriage Mara Tano Hadi Nikapoteza Ndoto Zangu Za Kuwa Mama Mpaka Nilipopata Usaidizi Usio na Madhara
  • Nilifanya Kazi Kwa Miaka Miwili Bila Kupata Promotion Ila Nilijitafutia Hiyo Promotion Mwenyewe
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MKURUGENZI MOSHI ATOKWA MACHOZI, CCM NA CHADEMA WAKIMPA ZAWADI
Habari za Kitaifa

MKURUGENZI MOSHI ATOKWA MACHOZI, CCM NA CHADEMA WAKIMPA ZAWADI

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 17, 2025Updated:February 17, 2025No Comments7 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email
Mkurugenzi wa Halmashauriya Manispaa ya Moshi Mwajuma NAsombe akizungumza wakati wa kikao cha mwisho cha Bajeti cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri .
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo akizungumza jambo katika kikao hicho ,kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe .
Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Moshi wakikabidhi keki kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe kama zawadi kutokana na namna alivyosimamia manispaa hiyo pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo kufanikisha kupaa kwa mapato ya halmashauri.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akipokea zawadi ya seti ya vyombo kwa ajili ya chakula kutoka kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Moshi kutokana na namna alivyosimamia manispaa hiyo pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo kufanikisha kupaa kwa mapato ya halmashauri.
Diwani wa kata ya Kiboriloni Frank Kagoma (Chadema)  akiwaamebeba zawadi ya jagi la kuchemshia chai ikiwa ni zawadi aliyotoa kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kutokana na utendajikazi wake .
Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akifurahia zawadi ya JAgi alilopewa na Diwani wa kata ya Kiboriloni Frank Kagoma (Chadema) kama zawadi .

 

 

 

Na Dixon Hussein – Moshi 

Katika hatua isiyo ya kawaida katika siasa za Tanzania,
diwani pekee wa upinzani katika baraza la madiwani wa Halmashauri ya Manispaa
ya Moshi Frank Kagoma (Chadema) ameungana na Chama cha  Mapinduzi (CCM) kutoa pongezi kwa Mkurugenzi
wa Manispaa ya Moshi kwa usimamizi thabiti wa mapato na miradi ya maendeleo.

Mh Kagoma ambaye ni diwani wa kata ya Kiboriloni na viongozi
wa CCM wilaya ya Moshi wametoa pongezi hizo wakati wa kikao cha Baraza la
Madiwani kilichofanyika mjini Moshi, ambapo viongozi wa halmashauri hiyo
walitangaza ongezeko kubwa la mapato kutoka bilioni 41.7 hadi bilioni 53.2
katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/24.

Katika kikao hicho,Mh Kagoma amekiri kuwa licha ya tofauti
za kisiasa, hawezi kupuuza ukweli kwamba usimamizi mzuri wa halmashauri umeleta
matokeo chanya kwa wananchi wa Moshi.

“Mimi ni mpinzani lakini siwezi kupinga maendeleo
yanayoonekana. Tumeona miradi ya halmashauri ikitekelezwa kwa wakati, mapato
yakiongezeka,hii ni hatua nzuri kwa wananchi,” alisema.

Viongozi wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Moshi wakiongozwa
na Mwenyekiti wake Faraji Swai pamoja na Madiwani wa CCM wameonyesha furaha yao
kwa ufanisi huo, wakisema kuwa halmashauri inatekeleza kwa vitendo ilani ya
chama chao kwa kuhakikisha rasilimali zinatumika ipasavyo kwa maendeleo ya
wananchi.

Mstahiki meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo alisisitiza
kuwa mafanikio haya ni matokeo ya mshikamano kati ya baraza la madiwani, timu
ya wataalamu wa halmashauri, na wananchi.

“Sisi tumejifunza kuwa maendeleo hayana chama.
Mkurugenzi wetu amesimamia vyema ukusanyaji wa mapato na utekelezaji wa miradi,
na leo tuna bajeti inayotekelezeka kwa zaidi ya asilimia 60, kitu ambacho
hakijawahi kutokea katika miaka ya nyuma,” alisema Mwenyekiti huyo.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akitokwa na machozi amewashukuru
viongozi wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Moshi kwa kutambua mchango ambao watendaji
wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wafanya kwa niaba ya wananchi .

Hatua hii ya mshikamano wa kisiasa imeibua mjadala mpana
kuhusu umuhimu wa kushirikiana kwa ajili ya maendeleo ya wananchi, huku wadau
wa siasa wakisema kuwa inaweza kuwa mfano kwa halmashauri nyingine nchini.

Mwisho 

 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

MAHUNDI: SERIKALI YAELEZA SABABU ZA KUTOWALAZIMISHA WATOTO KUWAHUDUMIA WAZAZI.

January 28, 2026

WAZEE WASHIRIKIANA NA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII ZOEZI LA UPANDAJI MITI DODOMA.

January 27, 2026

MADAKTARI BINGWA WA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA MKOANI MANYARA

January 26, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025316

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025244

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024222

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025136
Don't Miss
Afya na Ustawi

TAASISI ZA PICTERUS AS NA GOAL 3 KUANZISHA TEKNOLOJIA YA KISASA YA KUPIMA MANJANO KWA WATOTO WACHANGA TANZANIA

By Mbeya YetuJanuary 28, 202626

Taasisi za Picterus AS (Norway) na GOAL 3 (Uholanzi) pamoja wameshinda ruzuku ya Eurostars ya…

MAHUNDI: SERIKALI YAELEZA SABABU ZA KUTOWALAZIMISHA WATOTO KUWAHUDUMIA WAZAZI.

January 28, 2026

WAZEE WASHIRIKIANA NA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII ZOEZI LA UPANDAJI MITI DODOMA.

January 27, 2026

Wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Waadhimisha Kuzaliwa Rais Samia kwa Mshikamano

January 27, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

TAASISI ZA PICTERUS AS NA GOAL 3 KUANZISHA TEKNOLOJIA YA KISASA YA KUPIMA MANJANO KWA WATOTO WACHANGA TANZANIA

January 28, 2026

MAHUNDI: SERIKALI YAELEZA SABABU ZA KUTOWALAZIMISHA WATOTO KUWAHUDUMIA WAZAZI.

January 28, 2026

WAZEE WASHIRIKIANA NA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII ZOEZI LA UPANDAJI MITI DODOMA.

January 27, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025316

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025244

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024222
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.