Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Dkt. Tulia Aunga Mkono Ujenzi wa Barabara Bombambili kwa Mifuko 100 ya Saruji na tripu 10 za mawe

March 5, 2026

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Dkt. Tulia Aunga Mkono Ujenzi wa Barabara Bombambili kwa Mifuko 100 ya Saruji na tripu 10 za mawe
  • SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
  • Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
  • VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII
  • TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
  • Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
  • MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MKURUGENZI MOSHI ATOKWA MACHOZI, CCM NA CHADEMA WAKIMPA ZAWADI
Habari za Kitaifa

MKURUGENZI MOSHI ATOKWA MACHOZI, CCM NA CHADEMA WAKIMPA ZAWADI

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 17, 2025Updated:February 17, 2025No Comments7 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email
Mkurugenzi wa Halmashauriya Manispaa ya Moshi Mwajuma NAsombe akizungumza wakati wa kikao cha mwisho cha Bajeti cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri .
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo akizungumza jambo katika kikao hicho ,kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe .
Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Moshi wakikabidhi keki kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe kama zawadi kutokana na namna alivyosimamia manispaa hiyo pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo kufanikisha kupaa kwa mapato ya halmashauri.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akipokea zawadi ya seti ya vyombo kwa ajili ya chakula kutoka kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Moshi kutokana na namna alivyosimamia manispaa hiyo pamoja na watendaji wa halmashauri hiyo kufanikisha kupaa kwa mapato ya halmashauri.
Diwani wa kata ya Kiboriloni Frank Kagoma (Chadema)  akiwaamebeba zawadi ya jagi la kuchemshia chai ikiwa ni zawadi aliyotoa kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kutokana na utendajikazi wake .
Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akifurahia zawadi ya JAgi alilopewa na Diwani wa kata ya Kiboriloni Frank Kagoma (Chadema) kama zawadi .

 

 

 

Na Dixon Hussein – Moshi 

Katika hatua isiyo ya kawaida katika siasa za Tanzania,
diwani pekee wa upinzani katika baraza la madiwani wa Halmashauri ya Manispaa
ya Moshi Frank Kagoma (Chadema) ameungana na Chama cha  Mapinduzi (CCM) kutoa pongezi kwa Mkurugenzi
wa Manispaa ya Moshi kwa usimamizi thabiti wa mapato na miradi ya maendeleo.

Mh Kagoma ambaye ni diwani wa kata ya Kiboriloni na viongozi
wa CCM wilaya ya Moshi wametoa pongezi hizo wakati wa kikao cha Baraza la
Madiwani kilichofanyika mjini Moshi, ambapo viongozi wa halmashauri hiyo
walitangaza ongezeko kubwa la mapato kutoka bilioni 41.7 hadi bilioni 53.2
katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/24.

Katika kikao hicho,Mh Kagoma amekiri kuwa licha ya tofauti
za kisiasa, hawezi kupuuza ukweli kwamba usimamizi mzuri wa halmashauri umeleta
matokeo chanya kwa wananchi wa Moshi.

“Mimi ni mpinzani lakini siwezi kupinga maendeleo
yanayoonekana. Tumeona miradi ya halmashauri ikitekelezwa kwa wakati, mapato
yakiongezeka,hii ni hatua nzuri kwa wananchi,” alisema.

Viongozi wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Moshi wakiongozwa
na Mwenyekiti wake Faraji Swai pamoja na Madiwani wa CCM wameonyesha furaha yao
kwa ufanisi huo, wakisema kuwa halmashauri inatekeleza kwa vitendo ilani ya
chama chao kwa kuhakikisha rasilimali zinatumika ipasavyo kwa maendeleo ya
wananchi.

Mstahiki meya wa Manispaa ya Moshi Zuberi Kidumo alisisitiza
kuwa mafanikio haya ni matokeo ya mshikamano kati ya baraza la madiwani, timu
ya wataalamu wa halmashauri, na wananchi.

“Sisi tumejifunza kuwa maendeleo hayana chama.
Mkurugenzi wetu amesimamia vyema ukusanyaji wa mapato na utekelezaji wa miradi,
na leo tuna bajeti inayotekelezeka kwa zaidi ya asilimia 60, kitu ambacho
hakijawahi kutokea katika miaka ya nyuma,” alisema Mwenyekiti huyo.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe akitokwa na machozi amewashukuru
viongozi wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Moshi kwa kutambua mchango ambao watendaji
wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi wafanya kwa niaba ya wananchi .

Hatua hii ya mshikamano wa kisiasa imeibua mjadala mpana
kuhusu umuhimu wa kushirikiana kwa ajili ya maendeleo ya wananchi, huku wadau
wa siasa wakisema kuwa inaweza kuwa mfano kwa halmashauri nyingine nchini.

Mwisho 

 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

February 27, 2026

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025361

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Video Mpya

Dkt. Tulia Aunga Mkono Ujenzi wa Barabara Bombambili kwa Mifuko 100 ya Saruji na tripu 10 za mawe

By Mbeya YetuMarch 5, 20260

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Uyole, Dkt. Tulia Ackson, ameunga mkono juhudi za wananchi wa Mtaa wa Bombambili, Kata ya Mwakibete mkoani Mbeya, kwa kuchangia mifuko 100 ya saruji na tripu 10 za mawe kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya zege iliyoanzishwa na wananchi kwa nguvu zao.

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, vipande viwili vya barabara inayounganisha Kata za Iyela, Mwakibete na Mwasanga vinatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi milioni 41, ambapo kipande kimoja kimegharimu zaidi ya milioni 23 na cha pili kinakadiriwa kugharimu zaidi ya milioni 18.

Diwani wa Kata ya Mwakibete, Lucas Mwampiki, alimshukuru Dkt. Tulia kwa kuendelea kuunga mkono maendeleo ya kata hiyo, huku akitaja pia msaada wake katika ujenzi wa nyumba inayotarajiwa kukabidhiwa Machi 7, 2026 katika Mtaa wa Itongo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Bombambili, Saidi George Kumbemba, alimpongeza Dkt. Tulia kwa kusaidia wananchi na wadau wanaojitolea kujenga barabara hiyo inayoelekea Makaburi ya Iyela, pamoja na kuendelea kuwatetea katika maendeleo ya miundombinu ya barabara.

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Dkt. Tulia Aunga Mkono Ujenzi wa Barabara Bombambili kwa Mifuko 100 ya Saruji na tripu 10 za mawe

March 5, 2026

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025361

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.