Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilihofia Usalama wa Familia Yangu Kuingia Mwaka Mpya Hatua Nilizochukua Kuweka Kinga

January 1, 2026

Nilikuwa Naogopa Kuanza Mwaka Mpya Kwa Bahati Mbaya—Maamuzi Yaliyobadili Mwelekeo Wangu

January 1, 2026

HUPASWI KUJIULIZA MARA MBILI KWANINI USIMPELEKE MWANAO PARADISE MISSION PRE & PRIMARY SCHOOL MBEYA

January 1, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilihofia Usalama wa Familia Yangu Kuingia Mwaka Mpya Hatua Nilizochukua Kuweka Kinga
  • Nilikuwa Naogopa Kuanza Mwaka Mpya Kwa Bahati Mbaya—Maamuzi Yaliyobadili Mwelekeo Wangu
  • HUPASWI KUJIULIZA MARA MBILI KWANINI USIMPELEKE MWANAO PARADISE MISSION PRE & PRIMARY SCHOOL MBEYA
  • MDAU WA MAENDELEO NDELE MWASELELA AYAJENGA NA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MBEYA
  • LIVE: TUKIO LA KUFUNGA MWAKA JIJINI MBEYA
  • NDELE MWASELELA AFICHUA SIRI YA MAFANIKIO YA SHULE PARADISE MISION PRE & PRIMARY SCHOOL MBEYA
  • Nilitumia Zaidi ya Uwezo Wangu Sikukuu Njia Rahisi ya Kujipanga Upya Kabla ya Shule Kufunguliwa
  • Familia Ilitegemea Mimi Baada ya Sikukuu Hatua Nilizochukua Kurejesha Utulivu wa Nyumbani
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » KUUNDWA KWA JAB NI HATUA YA KUIMARISHA NA KUBORESHA SEKTA YA HABARI – MAJALIWA
Habari za Kitaifa

KUUNDWA KWA JAB NI HATUA YA KUIMARISHA NA KUBORESHA SEKTA YA HABARI – MAJALIWA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuApril 29, 2025No Comments10 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Na Mwandishi Wetu, JAB

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amesema Serikali ya Awamu ya Sita imechukua hatua kadhaa katika kuimarisha na kuboresha sekta ya habari nchini ikiwa ni pamoja na kuunda Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari.

Waziri Mkuu amesema hayo leo tarehe 29 Aprili, 2025 wakati akifunga Kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari lililofanyika jijini Arusha kwa siku mbili.

“Kwenye sekta ya habari na utangazaji, falsafa ya “4Rs” za Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, alizozibainisha baada ya kuingia madarakani mwezi Machi 2021, imetekelezwa kwa vitendo hususani kwenye eneo la “Reforms” (Mageuzi),” amesema Waziri Mkuu na kuongeza;

“Serikali ya Awamu ya Sita katika kutekeleza falsafa hii imechukuwa hatua mbalimbali kuimarisha sekta ya habari na utangazaji nchini kwa kuunda chombo kipya cha kushughulikia usajili wa taaluma ya waandishi wa habari yaani Bodi ya Ithibati”.

Waziri Mkuu Majaliwa amesema Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari iliyozinduliwa mwaka huu ina jukumu la kusimamia viwango vya kitaaluma kwa wanahabari ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa matakwa ya kisheria chini ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229.

Amesema hatua nyingine zilizochukuliwa na Serikali ni kuhakikisha inawezesha shirika la Habari la utangazaji kuwepo kisheria pamoja na kuimarisha Idara ya Habari Maelezo kwa kununua vitendea kazi vikiwemo Magari na vifaa vya kurushia matangazo mbashara.

Aidha, Waziri Mkuu Majaliwa amesema kauli mbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu inayosema “Uhabarishaji kwenye Dunia Mpya: Mchango wa Akili Mnemba katika uhuru wa vyombo vya habari” inalenga kujadili athari za teknolojia ya akili mnemba katika uendeshaji wa vyombo vya Habari na uhuru wake.

Amesema Serikali katika kuhakikisha Akili Mnemba (AI) inatumika kwa njia inayowezesha badala ya kudhibiti uhuru wa vyombo vya habari, imeanzisha mchakato wa kuandaa sera maalum ya AI na waandishi wanaowajibu wa kuchangia ili kupata sera nzuri.

“Sera hii itatoa mwongozo wa matumizi ya AI katika vyombo vya habari, ili kuhakikisha kwamba teknolojia mpya zinaendana na misingi ya uhuru wa vyombo vya habari, uwazi, na uadilifu wa uandishi wa Habari, hivyo mtumie muda wenu hapa kujadili na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuboresha sera hiyo,” amesema Waziri Mkuu.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

MDAU WA MAENDELEO NDELE MWASELELA AYAJENGA NA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MBEYA

January 1, 2026

WANANCHI HAI, FUONI , KATA TANO KUPIGA KURA KUCHAGUA WABUNGE NA MADIWANI KESHO

December 29, 2025

NDELE MWASELELA AWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUZINGATIA MAADILI, KUANDIKA HABARI ZA MAENDELEO NA KUWASEMEA WANANCHI

December 29, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025286

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025239

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024212

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025132
Don't Miss
Uncategorized

Nilihofia Usalama wa Familia Yangu Kuingia Mwaka Mpya Hatua Nilizochukua Kuweka Kinga

By Mbeya YetuJanuary 1, 20264

Mwaka mpya ulikaribia na moyo wangu ulikuwa mzito kwa hofu. Nilihofia usalama wa familia yangu,…

Nilikuwa Naogopa Kuanza Mwaka Mpya Kwa Bahati Mbaya—Maamuzi Yaliyobadili Mwelekeo Wangu

January 1, 2026

HUPASWI KUJIULIZA MARA MBILI KWANINI USIMPELEKE MWANAO PARADISE MISSION PRE & PRIMARY SCHOOL MBEYA

January 1, 2026

MDAU WA MAENDELEO NDELE MWASELELA AYAJENGA NA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MBEYA

January 1, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilihofia Usalama wa Familia Yangu Kuingia Mwaka Mpya Hatua Nilizochukua Kuweka Kinga

January 1, 2026

Nilikuwa Naogopa Kuanza Mwaka Mpya Kwa Bahati Mbaya—Maamuzi Yaliyobadili Mwelekeo Wangu

January 1, 2026

HUPASWI KUJIULIZA MARA MBILI KWANINI USIMPELEKE MWANAO PARADISE MISSION PRE & PRIMARY SCHOOL MBEYA

January 1, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025286

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025239

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024212
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.