Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nyota Yangu Ilibiwa na Rafiki Yangu Wa Karibu Lakini Nilipata Mtaalam Aliyerejesha Kila Kitu Nilichopoteza

January 21, 2026

Alinitumia Uchawi Mbaya Nilijaribu Kujilinda Lakini Nilishindwa, Nilihisi Hakuna Njia Suluhisho Hili Lilirudisha Amani Yangu

January 21, 2026

Nilipoteza Kazi, Biashara na Marafiki Lakini Bahati Iliporudi Kila Kitu Kilifuata

January 20, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nyota Yangu Ilibiwa na Rafiki Yangu Wa Karibu Lakini Nilipata Mtaalam Aliyerejesha Kila Kitu Nilichopoteza
  • Alinitumia Uchawi Mbaya Nilijaribu Kujilinda Lakini Nilishindwa, Nilihisi Hakuna Njia Suluhisho Hili Lilirudisha Amani Yangu
  • Nilipoteza Kazi, Biashara na Marafiki Lakini Bahati Iliporudi Kila Kitu Kilifuata
  • Walinitakia Mabaya Kwenye Giza Lakini Nuru Ilipowaka Walikimbia
  • Tuligombana Kila Siku Ndani ya Ndoa Nilipoondoa Kitu Kimoja Kisichoonekana, Amani Ilirudi Nyumbani
  • Duka Langu Halikuwa Linapata Wateja Siku Nilipobadili Njia, Foleni Ilianza Asubuhi
  • Nilinunulia Mtoto Doli Ambayo Ilirudi Kutuhangaisha Sisi Wote, Njia Hii Ndio Iliyotuokoa
  • Niliona Watu Wakigeuka Dhidi Yangu Bila Sababu Baadaye Nikagundua Chanzo cha Chuki Isiyoelezeka
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » RAIS SAMIA NA RAIS MSTAAFU KIKWETE WAPONGEZWA KWA KUFANIKISHA USHINDI WA PROFESA JANABI KATIKA UCHAGUZI WA MKURUGENZI WA WHO KANDA YA AFRIKA
Habari za Kitaifa

RAIS SAMIA NA RAIS MSTAAFU KIKWETE WAPONGEZWA KWA KUFANIKISHA USHINDI WA PROFESA JANABI KATIKA UCHAGUZI WA MKURUGENZI WA WHO KANDA YA AFRIKA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMay 19, 2025Updated:May 19, 2025No Comments7 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Na Mwandishi `Maalumu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepongezwa kwa maono yake ya mbali na uamuzi wa busara wa kumpendekeza Profesa Mohamed Yakub Janabi kugombea nafasi ya Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirika la Afya Duniani (WHO).

Wananchi mbalimbali waliohojiwa wametaja hatua hiyo ya Rais Samia kama ishara ya kujiamini kama taifa, na uthibitisho kuwa Watanzania wanao uwezo wa kushika nafasi nyeti katika taasisi kubwa za kimataifa, wakielezea faraja yao kwa jinsi Tanzania inavyozidi kung’ara kwenye majukwaa ya kidiplomasia duniani.

Aidha, Rais Samia amesifiwa kwa kuunda kikosi kazi maalum kilichoongozwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, kwa ajili ya kuratibu na kusimamia kampeni ya kidiplomasia ya Profesa Janabi.

Ushirikiano huo umeibuka na matokeo chanya, ambapo Profesa Janabi ameibuka mshindi kwa kishindo kupitia mchakato wa uchaguzi uliopigiwa kura na nchi wanachama wa WHO Kanda ya Afrika.

Dkt. Kikwete, ambaye ana uzoefu mkubwa katika medani za kimataifa, amepongezwa kwa kutumia umahiri na uhusiano wake wa kidiplomasia kuhakikisha kampeni hiyo inafanikiwa. Mchango wake umetajwa kama kichocheo muhimu kilichowezesha Tanzania kupata ushindi dhidi ya wagombea kutoka Côte d’Ivoire, Guinea na Togo.

Katika picha iliyopigwa wakati wa harakati za kampeni hiyo, Dkt. Kikwete anaonekana akiongoza moja ya vikao vya kikosi kazi hicho, ambacho hatimaye kilitimiza azma yake mnamo Jumapili, Mei 18, 2025, kwa ushindi mkubwa wa Profesa Janabi.

Mgombea huyo wa Tanzania alipata kura 32 kati ya 47 zilizopigwa kwa siri na wajumbe wa nchi wanachama wa WHO Afrika, kabla ya kuanza kwa Mkutano Mkuu wa WHO.

Uchaguzi huo umefanyika kufuatia kifo cha ghafla cha aliyekuwa Mkurugenzi mteule, Dkt. Faustine Ndugulile, mnamo Novemba 2024. Nafasi hiyo ilivuta wagombea mahiri kutoka mataifa kadhaa, lakini Profesa Janabi alifanikiwa kuungwa mkono kwa wingi, akionesha kuwa jina la Tanzania bado lina nguvu katika diplomasia ya afya barani Afrika.

Kwa mujibu wa taratibu za Shirika la Afya Duniani, jina la Profesa Janabi sasa litawasilishwa kwa ajili ya kuthibitishwa rasmi na Bodi ya Utendaji ya WHO katika kikao chake cha 157 kitakachofanyika Mei 28–29, 2025, mjini Geneva, Uswisi.

Iwapo atathibitishwa, Profesa Janabi ataapishwa na kuanza kutekeleza rasmi majukumu yake kwa kipindi cha miaka mitano, huku akiwa na fursa ya kuongezewa muhula mmoja zaidi kulingana na kanuni za taasisi hiyo.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Child Support Tanzania Yawawezesha Madiwani Mbeya Kuhusu Elimu Jumuishi

January 8, 2026

NMB Yaimarisha Ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya

January 7, 2026

MHE. MAHUNDI AWASISITIZA WATOTO WA SHULE YA MAADILISHO IRAMBO KUBADILIKA NA KUJENGA MUSTAKABALI MWEMA

January 6, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025309

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025243

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024217

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025136
Don't Miss
Uncategorized

Nyota Yangu Ilibiwa na Rafiki Yangu Wa Karibu Lakini Nilipata Mtaalam Aliyerejesha Kila Kitu Nilichopoteza

By Mbeya YetuJanuary 21, 20262

Kwa muda mrefu nilishangaa kwa nini maisha yangu yalibadilika ghafla. Nilikuwa nafanya kazi kwa bidii,…

Alinitumia Uchawi Mbaya Nilijaribu Kujilinda Lakini Nilishindwa, Nilihisi Hakuna Njia Suluhisho Hili Lilirudisha Amani Yangu

January 21, 2026

Nilipoteza Kazi, Biashara na Marafiki Lakini Bahati Iliporudi Kila Kitu Kilifuata

January 20, 2026

Walinitakia Mabaya Kwenye Giza Lakini Nuru Ilipowaka Walikimbia

January 20, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nyota Yangu Ilibiwa na Rafiki Yangu Wa Karibu Lakini Nilipata Mtaalam Aliyerejesha Kila Kitu Nilichopoteza

January 21, 2026

Alinitumia Uchawi Mbaya Nilijaribu Kujilinda Lakini Nilishindwa, Nilihisi Hakuna Njia Suluhisho Hili Lilirudisha Amani Yangu

January 21, 2026

Nilipoteza Kazi, Biashara na Marafiki Lakini Bahati Iliporudi Kila Kitu Kilifuata

January 20, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025309

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025243

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024217
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.