Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Beno Malisa Azindua Tawi la Strategies Insurance Mbeya, Akaribisha Wawekezaji

February 13, 2026

RC Malisa Afungua Mafunzo ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa Binafsi Mbeya

February 11, 2026

CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.

February 11, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Beno Malisa Azindua Tawi la Strategies Insurance Mbeya, Akaribisha Wawekezaji
  • RC Malisa Afungua Mafunzo ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa Binafsi Mbeya
  • CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.
  • DAS Mbeya: Kipato Kisiharibu Vyanzo vya Maji
  • KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA
  • Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji
  • Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo
  • TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MH. MAHUNDI: SERIKALI YABORESHA MAWASILIANO KATA YA MKWAMBA RUKWA KUPITIA MIRADI YA UCSAF
Habari za Kitaifa

MH. MAHUNDI: SERIKALI YABORESHA MAWASILIANO KATA YA MKWAMBA RUKWA KUPITIA MIRADI YA UCSAF

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJune 8, 2025Updated:June 8, 2025No Comments17 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprsca Mahundi, amewatoa hofu wananchi kuwa Serikali inaendelea kuhakikisha kuwa wananchi wote wanapata huduma bora za mawasiliano hasa maeneo ya vijijini.

Katika kutekeleza hilo, kata ya Mkwamba iliyopo mkoani Rukwa yenye jumla ya vijiji vinne—Swaila, Tambaruka, Itindi na Lyele—imepata mafanikio makubwa kupitia miradi ya Serikali inayolenga kuboresha mawasiliano.

Kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Serikali imefanikiwa kujenga minara ya mawasiliano kwa kushirikiana na makampuni ya mawasiliano ya VODACOM na HALOTEL.

Mnara wa Vodacom umejengwa katika Kijiji cha Tambaruka kupitia mradi wa Tanzania ya Kidijitali (DTP), huku mnara wa Halotel ukijengwa katika Kijiji cha Itindi chini ya awamu ya tatu ya mradi wa mawasiliano vijijini.

Minara yote imewashwa na inatoa huduma kwa wananchi, hatua inayowezesha kuimarika kwa shughuli za kijamii na kiuchumi kupitia mawasiliano ya uhakika.

Meneja wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Mkoa wa Rukwa, Bw. Ching’uli, amesema utekelezaji wa miradi ya UCSAF umeleta mabadiliko makubwa katika maisha ya wananchi wa Wilaya ya Nkasi kwa kuwaunganisha na huduma muhimu za mawasiliano.

Amesema kuwa kupitia minara iliyojengwa katika maeneo kama Kala, Izinga na Mlambo, wananchi wameweza kuwasiliana kwa urahisi zaidi, kupata taarifa kwa haraka, pamoja na kuendesha shughuli zao za biashara na kijamii kwa ufanisi.

“Huduma hizi zimefungua dunia kwa wananchi waliokuwa hawajawahi kupata mawasiliano kabisa,” alisema Ching’uli.

Aidha, Bw. Ching’uli ameongeza kuwa TTCL kama mtoa huduma wa ndani inaendelea kushirikiana na serikali katika kuhakikisha huduma zinafika hadi maeneo ya pembezoni ambayo bado hayajafikiwa.

Amesema kuwa pamoja na changamoto za miundombinu na jiografia ya maeneo mengi ya Nkasi, shirika lao limejipanga kuhakikisha kuwa kila mnara unaojengwa unatoa huduma bora na za uhakika kwa wananchi.

Aliwataka wananchi kutumia miundombinu hiyo kwa tija ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika jamii zao.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Makongolo Nyerere ametumia wasaa huo kuishukuru serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote UCSAF kwa kupeleka huduma ya mawasiliano katika mkoa huo.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA

February 10, 2026

JK KWA MFALME MSWATI III KUJADILI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA KWA NCHI WANACHAMA WA ECSA

February 4, 2026

TGNP na CARE Watoa Mafunzo ya Mabadiliko ya Tabia Nchi kwa Jamii Mbeya

January 31, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025342

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024229

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025139
Don't Miss
Video Mpya

Beno Malisa Azindua Tawi la Strategies Insurance Mbeya, Akaribisha Wawekezaji

By Mbeya YetuFebruary 13, 20263

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Region, Beno Malisa, amesema Serikali ipo tayari kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wote wanaotaka kuwekeza mkoani humo ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kwa wananchi.

Amesema hayo wakati wa uzinduzi wa tawi la Strategies Insurance, kampuni inayotoa huduma za bima, uliofanyika jijini Mbeya. Amepongeza uamuzi wa kampuni hiyo kufungua tawi katika mkoa huo, akieleza kuwa hatua hiyo itarahisisha upatikanaji wa huduma za bima kwa wananchi na wafanyabiashara.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Strategies Tanzania, Jabiri Kigoda, amesema kampuni hiyo imejipanga kutoa huduma bora, za haraka na zinazoendana na mahitaji ya wateja.

Aidha, baadhi ya viongozi wa taasisi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo wamewahimiza wananchi kujiunga na huduma za bima ili kujikinga na athari za majanga yanayoweza kujitokeza, pamoja na kulinda mali na maisha yao.

RC Malisa Afungua Mafunzo ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa Binafsi Mbeya

February 11, 2026

CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.

February 11, 2026

DAS Mbeya: Kipato Kisiharibu Vyanzo vya Maji

February 10, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Beno Malisa Azindua Tawi la Strategies Insurance Mbeya, Akaribisha Wawekezaji

February 13, 2026

RC Malisa Afungua Mafunzo ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa Binafsi Mbeya

February 11, 2026

CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.

February 11, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025342

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024229
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.