Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

WANAFUNZI WAFUNGWA WA GEREZA LA RUANDA MBEYA WAHITIMU MAFUNZO CHUO CHA UFUNDI MAGEREZA

June 18, 2025

WAKAZI KATA YA MAJENGO MBEYA WATANGAZA MITANO TENA KWA DIWANI WAO MAULIDI JAMADARI

June 17, 2025

MAMLAKA MAJI MBEYA YABAINI WIZI MKUBWA WA MAJI ENEO LA MAGEREJINI SOWETO MFUMO WA MITA WAHUJUMIWA

June 16, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • WANAFUNZI WAFUNGWA WA GEREZA LA RUANDA MBEYA WAHITIMU MAFUNZO CHUO CHA UFUNDI MAGEREZA
  • WAKAZI KATA YA MAJENGO MBEYA WATANGAZA MITANO TENA KWA DIWANI WAO MAULIDI JAMADARI
  • MAMLAKA MAJI MBEYA YABAINI WIZI MKUBWA WA MAJI ENEO LA MAGEREJINI SOWETO MFUMO WA MITA WAHUJUMIWA
  • T/PRISON YAICHIMBA MKWARA YANGA,MBEYA HAICHOMOKI INAHITAJI ALAMA 3 KUJIKWAMUA KUSHUKA
  • Utekelezaji wa Ilani ya CCM Wampa Heshima Meya Mbeya Kata ya Isanga
  • MAKALA MAALUMU: “Utekelezaji wa Miaka Mitano: Kazi, Matendo na Mafanikio ya Mhe. Mahundi”
  • VIJANA CCM MBEYA DC WAJIPANGA KUPIGA KURA OKTOBA 2025.
  • “Kasi Yaongezeka! CCM Mbeya Yajaza Nafasi Mbili Kamati ya Siasa mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu”
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TUME YA UCHAGUZI YAPONGEZWA MAANDALIZI UCHAGUZI MKUU 2025
Uncategorized

TUME YA UCHAGUZI YAPONGEZWA MAANDALIZI UCHAGUZI MKUU 2025

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJune 9, 2025No Comments13 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kilichokutana Mjini Unguja Zanzibar leo Juni 9,2025.

 
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume akizungumza mapema kabla ya ufunguzi wa kikao hicho.

 

 

 

 

 

Wajumbe wa Baraza hilo wakifuatilia mada katika Mkutano huo.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz (kulia) akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume, Ramadhani Kailima,  wakati Katibu Mkuu huyo alipofika kufungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi la Tume Mjini Unguja, Zanzibar leo Juni 9,2025.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz (kushoto)  na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume, Ramadhani Kailima,  pamoja na wajumbe wa baraza la Wafanyakazi la Tume wakiimba wimbo wa wafanyakazi wakati kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Wafanyakazi  Mjini Unguja, Zanzibar leo Juni 9,2025. 

Na. Mwandishi Wetu, Zanzibar

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge
na Uratibu), Dkt. Jim Yonaz ameipongeza Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa
kukamilisha zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na
kuendelea vyema na maandalizi ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Dkt. Yonazi ametoa pongezi hizo leo tarehe 09
Juni, 2025 Kisiwani Unguja, Zanzibar wakati wa kufungua kikao cha Baraza la
Wafanyakazi la INEC,  ambapo imewaasa
viongozi wa Tume kuendelea kuwa imara na kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano
ili kuhakikisha kuwa uchaguzi unakwenda vizuri.

“Kwanza niwapongeze sana kwa kukutekeleza
jukumu hili kubwa ambalo mmekabidhiwa na Taifa letu na kwa namna ya pekee
kabisa Mwenyekiti wa Baraza unifikishie salamu za pongezi kwa Mwenyekiti wa
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele pamoja na
wajumbe wa Tume kwa kazi kubwa ambayo mmeifanya katika kuhakikisha kuwa
shughuli za uchaguzi nchini kwetu zinakwenda vizuri,” amesema Dkt. Yonazi.

Ameeleza kuridhishwa na jinsi Tume ilivyotekeleza
kwa ufanisi zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuongeza
kuwa ni matarajio ya Serikali kuwa utendaji huo mzuri wa Tume utaendelea kwa
viwango vya juu kwa mujibu wa katiba, sheria na taratibu mbalimbali ambazo zimewekwa.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti
wa Baraza la Wafanyakazi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya
Taifa ya Uchaguzi, Ndugu. Kailima Ramadhan amesema tayari Tume imekamilisha
awamu ya kwanza ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambapo kwa
sasa inaendelea na uboreshaji wa awamu ya pili.

“Tume imeshakamilisha uboreshaji wa awamu ya
kwanza na imeshachakata na kutoa daftari la awali na imeshakamilisha uboreshaji
wa awamu ya pili mzunguko wa kwanza na mzunguko wa pili. Tunategemea kuanzia
tarehe 28 mwezi huu (tarehe 28 Juni, 2025) tutaanza mzunguko wa tatu wa
uboreshaji katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar na Magereza Tanzania Bara
kwa wanafunzi na wafungwa waliohukumiwa kifungo chini ya miezi sita,” amesema
Kailima.

Katibu huyo wa Baraza amesema mzunguko huo wa
tatu utahusisha vituo 140 vya kuandikisha wapiga kura ambapo 130 vipo kwenye
magereza Tanzania Bara na vituo 10 vipo kwenye vyuo vya mafunzo Tanzania
Zanzibar. Zoezi hilo linatarajiwa kufanyika kwa siku saba hadi tarehe 04 Julai,
2025.

Ameongeza kuwa Tume imekamilisha maandalizi
ya nyaraka mbalimbli kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ikiwa ni pamoja
na Kanuni za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025, Kanuni za
Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025 na maelekezo
mbalimbali kwa ajili ya watendaji wa uchaguzi na wadau wa uchaguzi kupata
miongozo kwa ajili ya utekelezaji wa uchaguzi.

Alimkumbusha mgeni rasmi kuwa tayari Tume
imekamilisha zoezi la ugawaji wa majimbo na kwamba kwenye uchaguzi mkuu wa
mwaka 2025 kutakuwa na jumla ya majimbo 272 yatakayofanya uchaguzi wa wabunge
katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kata 3960 kwa ajili ya uchaguzi wa
madiwani kwa Tanzania Bara.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

AFISA MTENDAJI MKUU WA AfD AZUNGUMZA NA WAJUMBE WA BODI YA GPE MJINI PARIS LEO

June 4, 2025

Wizi wa Bima Wafumuliwa, Serikali Yapanga Mashambulizi

May 16, 2025

WATENDAJI UBORESHAJI WA DAFTARI AWAMU YA PILI WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA

May 1, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024171

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202482

UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA

May 12, 202566

DKT. TULIA ATOA MSAADA WA VIPAZA SAUTI MSIKITI WA MASJID BI FATMA NZOVWE JIJINI MBEYA

March 29, 202458
Don't Miss
Video Mpya

WANAFUNZI WAFUNGWA WA GEREZA LA RUANDA MBEYA WAHITIMU MAFUNZO CHUO CHA UFUNDI MAGEREZA

By Mbeya YetuJune 18, 20250

#mbeyayetutv

WAKAZI KATA YA MAJENGO MBEYA WATANGAZA MITANO TENA KWA DIWANI WAO MAULIDI JAMADARI

June 17, 2025

MAMLAKA MAJI MBEYA YABAINI WIZI MKUBWA WA MAJI ENEO LA MAGEREJINI SOWETO MFUMO WA MITA WAHUJUMIWA

June 16, 2025

T/PRISON YAICHIMBA MKWARA YANGA,MBEYA HAICHOMOKI INAHITAJI ALAMA 3 KUJIKWAMUA KUSHUKA

June 16, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

WANAFUNZI WAFUNGWA WA GEREZA LA RUANDA MBEYA WAHITIMU MAFUNZO CHUO CHA UFUNDI MAGEREZA

June 18, 2025

WAKAZI KATA YA MAJENGO MBEYA WATANGAZA MITANO TENA KWA DIWANI WAO MAULIDI JAMADARI

June 17, 2025

MAMLAKA MAJI MBEYA YABAINI WIZI MKUBWA WA MAJI ENEO LA MAGEREJINI SOWETO MFUMO WA MITA WAHUJUMIWA

June 16, 2025
Most Popular

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024171

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202482

UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA

May 12, 202566
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.