Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

“Ndingo: Uongozi wa Samia Ni Ukombozi Mkubwa kwa Wanawake Tanzania.”

March 8, 2026

WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

March 7, 2026

Mwalunenge Achangia Milioni 3 Baada ya Wanawake MZRH Kutoa Mashine ya EEG

March 7, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • “Ndingo: Uongozi wa Samia Ni Ukombozi Mkubwa kwa Wanawake Tanzania.”
  • WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM
  • Mwalunenge Achangia Milioni 3 Baada ya Wanawake MZRH Kutoa Mashine ya EEG
  • Comfy Mum na TNCC Wawafariji Wakinamama Wodi ya Wanawake Hospitali ya Sinza
  • Mbunge CCM,wapinzani waimarisha umoja,wajadili maendeleo ya wana Mbeya
  • Dkt. Tulia Aunga Mkono Ujenzi wa Barabara Bombambili kwa Mifuko 100 ya Saruji na tripu 10 za mawe
  • SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
  • Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » Waziri Aweso Aagiza Mabomba Yote ya Mto Kiwira Yatengenezwe Mara Moja
Habari za Kitaifa

Waziri Aweso Aagiza Mabomba Yote ya Mto Kiwira Yatengenezwe Mara Moja

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJuly 24, 2025No Comments10 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb), amemtaka Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji kushirikiana na mkandarasi anayetekeleza mradi wa maji wa chanzo cha Mto Kiwira kuweka makubaliano maalum na kiwanda kinachotengeneza mabomba yatakayotumika katika zaidi ya kilomita 30 za mradi huo, ili kuhakikisha mabomba yote yanatengenezwa kwa wakati mmoja.

Mhe. Aweso ametoa maelekezo hayo leo alipofanya ziara kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo, ambapo alieleza kuridhishwa na kazi kubwa iliyofanyika chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (MBEYAUWSA). Hata hivyo, alieleza kuwa changamoto kubwa iliyobainika ni ucheleweshaji wa ulazaji wa mabomba kutoka kwenye chanzo cha maji hadi kwenye tanki kuu — tatizo linalosababishwa na uchelewaji wa upatikanaji wa mabomba katika eneo la mradi.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa MBEYAUWSA, CPA Gilbert Kayange, alisema kuwa mradi huo ni wa kimkakati na utakapokamilika utaongeza upatikanaji wa huduma ya maji kwa wakazi wa Jiji la Mbeya na maeneo jirani kwa kipindi cha zaidi ya miaka 20 ijayo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa MBEYAUWSA, Bi. Edna Mwaigomole, aliipongeza Serikali kwa utayari wake wa kutoa fedha zinazohitajika kukamilisha mradi huo kwa wakati, akisema hatua hiyo inaonesha dhamira ya dhati ya kuwaletea wananchi maendeleo.

Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Beno Malisa, amemuomba Waziri Aweso kuisaidia taasisi ya Wakala wa Majisafi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mbeya kwa kuiwezesha kifedha ili kukamilisha zaidi ya miradi 10 ya maji inayosuasua kutokana na ukosefu wa fedha kwa wakati.

default
default

“RUWASA imekuwa ikikumbwa na changamoto ya fedha, jambo ambalo linaathiri kasi ya utekelezaji wa miradi ya maji vijijini. Tunaomba Wizara itazame hili kwa jicho la huruma,” alisisitiza Mhe. Malisa.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

March 7, 2026

Comfy Mum na TNCC Wawafariji Wakinamama Wodi ya Wanawake Hospitali ya Sinza

March 6, 2026

Mbunge CCM,wapinzani waimarisha umoja,wajadili maendeleo ya wana Mbeya

March 5, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025364

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025141
Don't Miss
Video Mpya

“Ndingo: Uongozi wa Samia Ni Ukombozi Mkubwa kwa Wanawake Tanzania.”

By Mbeya YetuMarch 8, 20260

Mbunge wa Jimbo la Mbarali mkoani Mbeya, Bahati Ndingo, amesema maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni fursa ya kutathmini hatua zilizopigwa katika kuimarisha usawa wa kijinsia na kuhamasisha jamii kuendelea kuwapa wanawake na wasichana nafasi ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Akizungumza Machi 6, 2026 katika maadhimisho ya siku hiyo yaliyofanyika kiwilaya katika Kata ya Igurusi, Ndingo alisema Tanzania imepiga hatua kubwa kwa kumpa mwanamke nafasi ya juu ya uongozi nchini, akimtaja Rais Samia Suluhu Hassan kama mfano wa mafanikio ya wanawake katika uongozi.

Aidha, alisisitiza kuwa maadhimisho hayo hayalengi kujisifia bali kutambua mchango wa wanaume na wanawake katika kubadilisha mtazamo wa jamii kuhusu uwezo wa mtoto wa kike. Aliongeza kuwa mtoto wa kike ana uwezo wa kufanya kazi na majukumu yoyote kama ilivyo kwa mwanaume.

Maadhimisho hayo ni sehemu ya maandalizi ya kilele cha Siku ya Wanawake Duniani kinachoadhimishwa kila mwaka Machi 8.

WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

March 7, 2026

Mwalunenge Achangia Milioni 3 Baada ya Wanawake MZRH Kutoa Mashine ya EEG

March 7, 2026

Comfy Mum na TNCC Wawafariji Wakinamama Wodi ya Wanawake Hospitali ya Sinza

March 6, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

“Ndingo: Uongozi wa Samia Ni Ukombozi Mkubwa kwa Wanawake Tanzania.”

March 8, 2026

WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

March 7, 2026

Mwalunenge Achangia Milioni 3 Baada ya Wanawake MZRH Kutoa Mashine ya EEG

March 7, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025364

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.