Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Alinitupa Bila Majuto, Lakini Muda Mfupi Baadaye Alianza Kunisumbua Kila Siku Bila Mimi Kujitahidi

January 15, 2026

Nilikuwa Najaribu Kila Kitu Kupandisha Biashara Bila Mafanikio Siri Moja Iliyoniletea Mafanikio ya Haraka

January 15, 2026

Mwalunenge Aanza Kutatua Kero ya Barabara Iyela kwa Kumwaga Vifusi

January 15, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Alinitupa Bila Majuto, Lakini Muda Mfupi Baadaye Alianza Kunisumbua Kila Siku Bila Mimi Kujitahidi
  • Nilikuwa Najaribu Kila Kitu Kupandisha Biashara Bila Mafanikio Siri Moja Iliyoniletea Mafanikio ya Haraka
  • Mwalunenge Aanza Kutatua Kero ya Barabara Iyela kwa Kumwaga Vifusi
  • Iyela Yalia kwa Serikali, Barabara Muhimu Yageuka Mtego
  • Nilivyovutia Wateja Wengi Na Kila Siku Kuongeza Mapato Baada ya Hatua Moja Rahisi Ya Kienyeji Nilizofuata
  • Baada ya Kukwama Kuuza Mali Zangu, Hatua Niliyopata Ilibadilisha Kila Kitu Ndani ya Muda Mfupi Sana
  • MAKONDA KWA MARA YA KWANZA AUNGURUMA
  • Baada ya Miaka ya Kutokuwa na Hisia Kitandani, Hatimaye Nilipata Suluhisho la Kudumu
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WATANZANIA MILIONI 37 KUPIGA KURA TAREHE 29 OKTOBA, 2025
Habari za Kitaifa

WATANZANIA MILIONI 37 KUPIGA KURA TAREHE 29 OKTOBA, 2025

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJuly 26, 2025Updated:July 26, 2025No Comments19 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.

 

Sehemu ya viongozi kutoka vyama mbalimbali vya siasa vilivyohudhuria hafla ya uzinduzi wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.

 

 

Sehemu ya viongozi kutoka vyama mbalimbali vya siasa vilivyohudhuria hafla ya uzinduzi wa uzinduzi rasmi wa kalenda ya uchaguzi Mkuu 2025 katika hafla iliyofanyika Ofisi za Tume Njedengwa Jijini Dodoma Julai 26,2025. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani.

 

 

 

 

******

Na. Mwandishi Wetu
Tarehe 29 Oktoba, 2025 ndio siku ya
Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Madiwani
kwa Tanzania Bara. Jumla ya Wapiga Kura 37,655,559 wamejiandikisha.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume
Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele leo
tarehe 26 Julai, 2025 kwenye hafla ya uzinduzi wa ratiba ya uchaguzi
iliyofanyika kwenye makao makuu ya Tume, Njedengwa jijini Dodoma.

“Tarehe 09 Agosti, 2025 hadi tarehe 27
Agosti, 2025 itakuwa utoaji wa fomu za uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais na
Makamu wa Rais. Tarehe 14 Agosti, 2025 hadi tarehe 27 Agosti, 2025 itakuwa
utoaji wa fomu za uteuzi wa wagombea ubunge na udiwani na tarehe 27 Agosti,
2025 itakuwa siku ya uteuzi wa wagombea wa kiti cha Rais na Makamu wa Rais,
uteuzi wa wagombea ubunge na uteuzi wa wagombea udiwani,” amesema Jaji
Mwambegele na kuongeza…..

“Tarehe 28 Agosti, 2025 hadi tarehe 28
Oktoba, 2025 kitakuwa kipindi cha kampeni za uchaguzi kwa Tanzania Bara. Tarehe
28 Agosti, 2025 hadi 27 Oktoba, 2025 kitakuwa kipindi cha kampeni za Uchaguzi
kwa Tanzania Zanzibar ili kupisha kura ya mapema na Tarehe 29 Oktoba, 2025 siku
ya Jumatano itakuwa ndiyo Siku ya Kupiga Kura”.

Akazingumza kuhusu idadi ya wapiga kura
waliojiandikisha kupiga kura kwenye uchaguzi huo, Jaji Mwambegele amesema jumla
ya wapiga kura 37,655,559 wamejiandikisha na kuongeza kuwa idadi hiyo ni sawa
na ongezeko la asilimia 26.55 kutoka idadi ya wapiga kura 29,754,699 waliokuwa
kwenye daftari, mwaka 2020.

Ameongeza kuwa kwa upande wa Zanzibar,
Wapiga Kura 725,876 wapo katika Daftari la Wapiga Kura la Tume ya Uchaguzi ya
Zanzibar (ZEC) na wapiga kura 278,751 wameandikishwa na INEC kwa kuwa hawakuwa
na sifa za kuandikishwa na ZEC.

“Katika idadi ya wapiga kura 37,655,559
waliopo katika daftari, wapiga kura 36,650,932 wapo Tanzania Bara na wapiga kura
1,004,627 wapo Tanzania Zanzibar,” amesema Jaji Mwambegele.

Ameongeza kuwa kati ya wapiga kura hao,
18,943,455 ni wanawake sawa na asilimia 50.31 na wapiga kura 18,712,104 ni
wanaume sawa na asilimia 49.69 na wapiga kura 49,174 ni watu wenye ulemavu.

Amesema jumla ya vituo 99,911
vitatumika kupigia kura ambapo vituo 97,349 vitatumika kwa ajili ya kupigia
kura kwa Tanzania Bara na vituo 2,562 vitatumika kwa ajili ya kupigia kura kwa
Tanzania Zanzibar.

“Idadi hii ya vituo 99,911 ni sawa na
ongezeko la asilimia 22.49 ya vituo vya kupigia kura 81,567 vilivyotumika
katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020,” amesema.

Jaji Mwambegele ametoa wito kwa wadau
wote ikiwa ni pamoja na wananchi kushiriki kikamilifu katika mchakato wa
uchaguzi kwa kuzingatia sheria, kanuni, miongozo na maelekezo yatakayotolewa na
Tume.

 

 

 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Child Support Tanzania Yawawezesha Madiwani Mbeya Kuhusu Elimu Jumuishi

January 8, 2026

NMB Yaimarisha Ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya

January 7, 2026

MHE. MAHUNDI AWASISITIZA WATOTO WA SHULE YA MAADILISHO IRAMBO KUBADILIKA NA KUJENGA MUSTAKABALI MWEMA

January 6, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025302

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025243

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024216

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025135
Don't Miss
Uncategorized

Alinitupa Bila Majuto, Lakini Muda Mfupi Baadaye Alianza Kunisumbua Kila Siku Bila Mimi Kujitahidi

By Mbeya YetuJanuary 15, 20260

Nilikuwa nikiwa na uhusiano wa miaka miwili na mpenzi wangu wa zamani. Kila kitu kilionekana…

Nilikuwa Najaribu Kila Kitu Kupandisha Biashara Bila Mafanikio Siri Moja Iliyoniletea Mafanikio ya Haraka

January 15, 2026

Mwalunenge Aanza Kutatua Kero ya Barabara Iyela kwa Kumwaga Vifusi

January 15, 2026

Iyela Yalia kwa Serikali, Barabara Muhimu Yageuka Mtego

January 15, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Alinitupa Bila Majuto, Lakini Muda Mfupi Baadaye Alianza Kunisumbua Kila Siku Bila Mimi Kujitahidi

January 15, 2026

Nilikuwa Najaribu Kila Kitu Kupandisha Biashara Bila Mafanikio Siri Moja Iliyoniletea Mafanikio ya Haraka

January 15, 2026

Mwalunenge Aanza Kutatua Kero ya Barabara Iyela kwa Kumwaga Vifusi

January 15, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025302

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025243

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024216
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.