Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

“KUNUNA MWISHO – MWALUNENGE AWAPA MOTISHA VIJANA WA KIWIRA: PESA IPO, CHANGAMKIA FURSA”

December 10, 2025

Alivyovutia fursa kubwa katika kutengeneza samani na kuuza

December 10, 2025

MEYA ISSA ACHARUKA—AMLIPUA MKANDARASI WA SOKO MATOLA NA STENDI KUU KWA KUCHELEWESHA UJENZI

December 10, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • “KUNUNA MWISHO – MWALUNENGE AWAPA MOTISHA VIJANA WA KIWIRA: PESA IPO, CHANGAMKIA FURSA”
  • Alivyovutia fursa kubwa katika kutengeneza samani na kuuza
  • MEYA ISSA ACHARUKA—AMLIPUA MKANDARASI WA SOKO MATOLA NA STENDI KUU KWA KUCHELEWESHA UJENZI
  • Mama Ashikiliwa Kwa Tuhuma za Mauaji ya Mtoto Wake wa Miaka 10
  • Baada ya hapo ndipo akapata kazi kubwa zaidi!
  • SIMBACHAWENE ATEMBEA MITAANI KUANGALIA USALAMA—AWAPA HONGERA WANANCHI KWA UTULIVU
  • Taarifa nyingine Tena Toka jeshi la polisi
  • 2021 11 26 14 36 44
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TANZANIA WENYEJI WA WARSHA YA WAKUU WA TAASISI ZA KUPAMBANA NA RUSHWA KUTOKA NCHI ZA SADC
Habari za Kitaifa

TANZANIA WENYEJI WA WARSHA YA WAKUU WA TAASISI ZA KUPAMBANA NA RUSHWA KUTOKA NCHI ZA SADC

Mbeya YetuBy Mbeya YetuAugust 4, 2025No Comments23 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Arusha, Agosti 4, 2025

Tanzania imepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa Warsha ya Wakuu wa Taasisi za Kuzuia na Kupambana na Rushwa kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), itakayofanyika kwa siku tatu kuanzia Agosti 4 hadi 6, 2025, katika Hoteli ya Gran Melia, jijini Arusha.

Warsha hii ya kimataifa inafanyika wakati Tanzania ikiwa na jukumu la Uenyekiti wa Kamati ya Kupambana na Rushwa ya SADC (SADC Anti-Corruption Committee – SACC) kupitia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), nafasi ambayo ilianza rasmi Oktoba 2, 2024.

Hii ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya nchi wanachama chini ya Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC ambayo kwa sasa inaongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, tangu Agosti 17, 2024.

Warsha hiyo pia itaambatana na maadhimisho ya miaka 20 ya utekelezaji wa Itifaki ya SADC Dhidi ya Rushwa, itifaki ambayo ilianza kutekelezwa rasmi Julai 2005 kwa lengo la kuimarisha mifumo ya kuzuia, kugundua, kuadhibu na kutokomeza rushwa katika sekta za umma na binafsi ndani ya nchi wanachama.

Malengo mahsusi ya warsha hii ni pamoja na:

  1. Kutafakari miaka 20 ya utekelezaji wa Itifaki ya SADC Dhidi ya Rushwa – mafanikio na changamoto.

  2. Kutathmini mafanikio yaliyopatikana na kubaini mapungufu katika sheria, uwezo wa taasisi na ushirikiano wa kikanda.

  3. Kuweka vipaumbele vya kimkakati kwa mustakabali wa mapambano dhidi ya rushwa katika ukanda wa SADC.

Katika warsha hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Crispin Francis Chalamila, ambaye pia ni Mwenyekiti anayemaliza muda wake wa SACC, atakabidhi rasmi kijiti cha Uenyekiti kwa mwakilishi kutoka nchi ya Malawi.

Ni muhimu kukumbusha kwamba Tanzania ilipongezwa na Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa SADC katika mkutano wao wa 27 uliofanyika Julai 21–25, 2025 jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo, Katibu Mtendaji wa SADC, Elias Magosi, alisifu juhudi za Tanzania katika mapambano dhidi ya rushwa, akieleza kuwa nchi imeonesha mafanikio makubwa katika maeneo ya mifumo ya kisheria, dhamira ya kisiasa na ushiriki wa wadau.

Kupata heshima ya kuwa mwenyeji wa warsha hii ni ushahidi wa nafasi ya Tanzania katika juhudi za kimataifa za kupambana na rushwa, kuimarisha utawala bora, kuendeleza amani na kukuza maendeleo ya kiuchumi katika kanda.

TAKUKURU imesisitiza kuwa imejipanga kuhakikisha kuwa maazimio ya warsha hii yatakuwa na mchango chanya kwa taifa na ukanda wa SADC kwa ujumla.


Mwisho
Imetolewa na: Kitengo cha Mawasiliano – TAKUKURU
Arusha, Tanzania

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

TANZANIA NA MAREKANI ZASONGA MBELE KUKAMILISHA MAKUBALIANO MAKUBWA YA UWEKEZAJI

December 9, 2025

TANZANIA AND U.S. MOVE TO FINALISE MAJOR INVESTMENT AGREEMENTS

December 8, 2025

MHE. SALOME MAKAMBA AIPONGEZA PBPA KWA UTENDAJI KAZI MZURI

December 6, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025249

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025234

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024207

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025130
Don't Miss
Video Mpya

“KUNUNA MWISHO – MWALUNENGE AWAPA MOTISHA VIJANA WA KIWIRA: PESA IPO, CHANGAMKIA FURSA”

By Mbeya YetuDecember 10, 20252

Alivyovutia fursa kubwa katika kutengeneza samani na kuuza

December 10, 2025

MEYA ISSA ACHARUKA—AMLIPUA MKANDARASI WA SOKO MATOLA NA STENDI KUU KWA KUCHELEWESHA UJENZI

December 10, 2025

Mama Ashikiliwa Kwa Tuhuma za Mauaji ya Mtoto Wake wa Miaka 10

December 10, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

“KUNUNA MWISHO – MWALUNENGE AWAPA MOTISHA VIJANA WA KIWIRA: PESA IPO, CHANGAMKIA FURSA”

December 10, 2025

Alivyovutia fursa kubwa katika kutengeneza samani na kuuza

December 10, 2025

MEYA ISSA ACHARUKA—AMLIPUA MKANDARASI WA SOKO MATOLA NA STENDI KUU KWA KUCHELEWESHA UJENZI

December 10, 2025
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025249

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025234

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024207
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.