Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

MAZISHI YA SAMSON MWAMAKIMBULA

December 6, 2025

Mbinu aliyotumia kupata kazi ya udereva baada ya kusota sana

December 6, 2025

MHE. SALOME MAKAMBA AIPONGEZA PBPA KWA UTENDAJI KAZI MZURI

December 6, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • MAZISHI YA SAMSON MWAMAKIMBULA
  • Mbinu aliyotumia kupata kazi ya udereva baada ya kusota sana
  • MHE. SALOME MAKAMBA AIPONGEZA PBPA KWA UTENDAJI KAZI MZURI
  • Hofu yake zilianza kuathiri hata furaha ya ndoa yake
  • MASACHE AWATAKA WANANCHI KUENDELEA KUSHIKILIA AMANI
  • MH. MASACHE: TUENDELEE KUISIMAMIA MIRADI ILIYOKUWEPO NA KUIBUA MIPYA AWASHUKURU WANA CHUNYA
  • MH. NOAH MWAKISU AAPISHWA RASMI KUWA DIWANI KATA YA ILOMBA
  • Dourmohamed Issa ashinda kwa kishindo Umeya na kutetea nafasi yake
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA
Habari za Kitaifa

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuNovember 26, 2025Updated:November 26, 2025No Comments10 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Rungwe, Tanzania – Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe imekamilisha hatua ya awali ya mradi mkubwa wa Soko la Kisasa la Ndizi lenye thamani ya Shilingi bilioni 2.8, hatua inayofungua ukurasa mpya wa maendeleo kwa wakulima na wafanyabiashara wa eneo hilo na mikoa ya jirani.

Akizungumza wakati wa hafla ya leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, Bwana Renatus Mchau, amesema hatua hii ni kumkabidhi mkandarasi site pamoja na kuhakikisha taratibu zote za kimkataba zimekamilika.

“Leo hii tumekamilisha taratibu zote za kimkataba. Zoezi la leo ni kumkabidhi mkandarasi site, kuhakikisha kila kitu kipo sawa kabla ya kuanza ujenzi rasmi,” alisema Mchau.

Mkurugenzi Mtendaji aliishukuru Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wizara ya Tamisemi, Wizara ya Fedha, na Wizara ya Kilimo kwa mchango wao wa kitaalam katika hatua zote za maandalizi ya mradi. Alihakikisha kuwa wananchi, wafanyabiashara na wakulima ambao kwa muda mrefu wamepitia changamoto mbalimbali katika eneo hilo, wanapaswa kuwa wanufaika wakubwa wa mradi huu.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Kagwa General Supplies Limited, Bwana Emmanuel Madaffa, amesema serikali imeonyesha imani kubwa kwa kutoa fursa kwa wazawa kutekeleza mradi huo badala ya wageni.

“Naiishukuru sana Serikali chini ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutuamini sisi wazawa. Tunawaahidi kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha tunatimiza lengo la Serikali na kuondoa changamoto za muda mrefu kwa wananchi,” alisema Madaffa.

Amesema mradi huo utakuwa kichocheo muhimu cha maendeleo na utawanufaisha si tu wakulima wa Rungwe na Kyela, bali pia mikoa ya jirani. Kampuni tayari imekabidhiwa cheti cha kuanza kazi, hivyo shughuli zinaanza mara moja. Aidha, amewaasa wakandarasi kushirikiana na wahandisi na taasisi za kitaalamu, kuepuka ubadhirifu, na kutoa nafasi kwa vijana wa Rungwe kushiriki katika kazi ndogo zisizohitaji ujuzi.

Mbunge wa Jimbo la Rungwe, Mh. Mantona, amesema soko hilo ni mojawapo ya miradi mikubwa inayolenga kuboresha uchumi wa wakulima na wafanyabiashara wa eneo hilo, akibainisha kuwa litafungua fursa nyingi za kipato na kuongeza thamani ya mazao.

“Huu ni mradi mkubwa sana kwa watu wa Rungwe. Tukiuendeleza vizuri, manufaa yake yataonekana kwa wote—wakulima, wafanyabiashara, na jamii kwa ujumla,” alisema Mbunge Mantona.

Soko hili la kisasa linatarajiwa kuwa suluhu ya kudumu kwa changamoto ya masoko kwa wakulima wa ndizi, litakaloongeza thamani ya zao hilo, na kuvutia wanunuzi kutoka ndani na nje ya nchi.

Mwisho, Afisa Tawala Amimu Mwandelile, aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya Rungwe, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano, uwazi na kufuata taratibu zote za kiserikali katika utekelezaji wa mradi.

“Njia bora ya kutatua changamoto ni kupitia vikao na majadiliano ya pamoja. Viongozi, wafanyabiashara na wahandisi wanapaswa kushirikiana ili mradi uendelee bila matatizo,” alisema Mwandelile.

Amewaasa wakandarasi kushirikiana na taasisi za kitaalamu, kuzingatia mkataba, na kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa viwango vinavyotarajiwa. Pia alisisitiza kuepuka haraka isiyo na mpangilio, ubadhirifu au ubinafsi, akibainisha kuwa kila hatua inapaswa kufuata mpangilio thabiti ili kufanikisha mradi.

“Tukiongoza mradi huu vizuri na kushirikiana kwa uwazi, tutapata matokeo bora. Mradi ni mali ya wananchi na kila mmoja ana wajibu wa kulinda ubora wake,” aliongeza.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

MHE. SALOME MAKAMBA AIPONGEZA PBPA KWA UTENDAJI KAZI MZURI

December 6, 2025

MH. MAHUNDI: Serikali Yaendelea Kuimarisha Mazingira Wezeshi kwa Biashara za Wanawake Dodoma

November 28, 2025

MIKOPO IWE CHACHU YA KUKUA KIUCHUMI NA KUZITUNZA FAMILIA ZENU – MHE. MARYPRISCA

November 28, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025246

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025234

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024206

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025128
Don't Miss
Video Mpya

MAZISHI YA SAMSON MWAMAKIMBULA

By Mbeya YetuDecember 6, 20251

Mbinu aliyotumia kupata kazi ya udereva baada ya kusota sana

December 6, 2025

MHE. SALOME MAKAMBA AIPONGEZA PBPA KWA UTENDAJI KAZI MZURI

December 6, 2025

Hofu yake zilianza kuathiri hata furaha ya ndoa yake

December 6, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

MAZISHI YA SAMSON MWAMAKIMBULA

December 6, 2025

Mbinu aliyotumia kupata kazi ya udereva baada ya kusota sana

December 6, 2025

MHE. SALOME MAKAMBA AIPONGEZA PBPA KWA UTENDAJI KAZI MZURI

December 6, 2025
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025246

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025234

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024206
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.