Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kwa namna moja au nyingine kuna baadhi ya taasisi za dini zimejiingiza kwenye mkumbo ambao unaendelea wenye nia ovu ndani yake. Akieleza juu ya uongozi wa nchi katika kufuata misingi ya katiba na sheria, Rais Dkt. Samia amesema Tanzania haina dini lakini Watanzania wana dini za madhehebu mbalimbali huku akisisitiza kuwa kikatiba na sheria za nchi hakuna dini na dhehebu lolote lenye uwezo wa’kuover ride’ madhehebu mengine. Akizungumza na Wazee wa mkoa wa Dar es salaam leo tarehe 2 Disemba 2025, Rais DKt. Samia ameyasema na kuyasisitizia haya kuhusu taasisi za dini nchini “Viongozi wa dini msijivishe majoho ya kwamba nyinyi ndio mnaweza ‘kuover run’ nchi hii, hakuna. Tutakwenda kwa kwa Katiba na Sheria ya Nchi hii.” “Hatutaendeshwa na madhehebu yoyote ya dini, madhehebu ya dini na wafuasi wao” “ubora wa dini upo miyoyoni kwetu, wale wanaoamini ndio wanajua ubora wa dini yao..” “hakuna ‘over riding’ hapa! Kwamba “mimi dini yangu ndio itaover ride Tanzania na tamko nikilitoa ndio hilo hilo”. “…hata wenyewe wanatofautiana, mimi toka nimekaa matamko 8 yametolewa na TEC, lakini ukienda chini chini wenyewe wanapingana, matamko yale hayafanyi kazi…waliosimama kwenye mstari wa haki wanaona ni batili iliyofanyika..hawaungani nao..” “Tanzania yetu ni nchi ya umoja na mshikamano, amani na utulivu ndio ngazo zetu, tusivurugwe ndugu zangu
Trending
- MAZISHI YA SAMSON MWAMAKIMBULA
- Mbinu aliyotumia kupata kazi ya udereva baada ya kusota sana
- MHE. SALOME MAKAMBA AIPONGEZA PBPA KWA UTENDAJI KAZI MZURI
- Hofu yake zilianza kuathiri hata furaha ya ndoa yake
- MASACHE AWATAKA WANANCHI KUENDELEA KUSHIKILIA AMANI
- MH. MASACHE: TUENDELEE KUISIMAMIA MIRADI ILIYOKUWEPO NA KUIBUA MIPYA AWASHUKURU WANA CHUNYA
- MH. NOAH MWAKISU AAPISHWA RASMI KUWA DIWANI KATA YA ILOMBA
- Dourmohamed Issa ashinda kwa kishindo Umeya na kutetea nafasi yake

