Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya

February 16, 2026

TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA

February 16, 2026

AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI

February 15, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya
  • TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA
  • AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI
  • SHEIKH WA MKOA MBEYA ATOA UJUMBE KWA WAISLAMU KUELEKEA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN
  • EFTA YACHOCHEA UCHUMI KWA HATI FUNGANI YA BILIONI 50
  • Kanisa la Moravian Tanzania Lamkabidhi Yona Sonelo Tuzo Maalum Baada ya Shahada ya Heshima Australia
  • Beno Malisa Azindua Tawi la Strategies Insurance Mbeya, Akaribisha Wawekezaji
  • RC Malisa Afungua Mafunzo ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa Binafsi Mbeya
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TGNP na CARE Watoa Mafunzo ya Mabadiliko ya Tabia Nchi kwa Jamii Mbeya
Habari za Kitaifa

TGNP na CARE Watoa Mafunzo ya Mabadiliko ya Tabia Nchi kwa Jamii Mbeya

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJanuary 31, 2026Updated:January 31, 2026No Comments37 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la CARE wametoa mafunzo kwa wawezeshaji wa ngazi ya jamii kuhusu mabadiliko ya tabia nchi katika mkoa wa Mbeya, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Ustahimilivu Wake, Dunia Yetu.

Mradi huo unatekelezwa katika vijiji 300 vya mikoa ya Mbeya, Njombe na Iringa kwa lengo la kuimarisha uwezo wa jamii kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi pamoja na kuboresha utunzaji wa mazingira.

Katika mkoa wa Mbeya, mafunzo hayo yamefanyika kwa siku tatu wilayani Mbarali, kijiji cha Chimala, yakilenga zaidi wakulima na wafugaji ili kuwajengea uelewa kuhusu masuala ya jinsia, uhifadhi wa mazingira na mbinu za kuielimisha jamii juu ya mabadiliko ya tabia nchi. TGNP na CARE wameeleza kuwa wataendelea kutoa elimu katika vijiji vyote vinavyonufaika na mradi huo.

Hatua hiyo imekuja kufuatia kubainika kwa changamoto ya upungufu wa maji inayochochea migogoro kati ya wakulima na wafugaji, huku wanawake, vijana na makundi maalum wakiwa miongoni mwa waathirika wakubwa.

Aidha, kupungua kwa mvua kumesababisha wakulima kukosa mavuno na wafugaji kukabiliwa na uhaba wa malisho, hali inayochangia vifo vya mifugo pamoja na kushuka kwa thamani yake.

Mkufunzi kutoka TGNP, Rose Ngunangwa, amesema taasisi hiyo inaendelea kutoa mafunzo kwa jamii mbalimbali chini ya mradi huo ili kuongeza uelewa na kuchochea ushiriki wa wananchi katika kulinda mazingira.

Baadhi ya wawezeshaji walioshiriki mafunzo hayo wameeleza kuwa ukame unaotokana na ukosefu wa elimu ya utunzaji wa mazingira umeathiri kwa kiwango kikubwa shughuli zao za kila siku.

Kwa upande wake, Rubeni Mwale, mkazi wa kijiji cha Kamwale na mmoja wa washiriki, amesema mafunzo hayo yamewapa uelewa mpya na yatawasaidia kuleta mabadiliko chanya katika jamii kwa kueneza elimu kuhusu athari na namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Kupitia mpango huo, TGNP na CARE Tanzania wanaendelea kuiwezesha jamii kujenga ustahimilivu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa ajili ya maendeleo endelevu.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI

February 15, 2026

EFTA YACHOCHEA UCHUMI KWA HATI FUNGANI YA BILIONI 50

February 14, 2026

KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA

February 10, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025347

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024231

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Video Mpya

Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya

By Mbeya YetuFebruary 16, 20265

ZAIDI ya kaya 200 zimepata madhara ya kukosa makazi baada ya nyumba zao kuezuliwa na nyingine kubomoka kufuatia mvua kubwa zilizoambatana na upepo mkali zinazoendelea kunyesha katika Nyanda za Juu Kusini.

Mbali na makazi kuharibika, vyakula na mavazi pia vimeathirika baada ya maji kujaa kwenye nyumba na mali nyingi kufunikwa na tope.

Uharibifu huo umeripotiwa katika kata sita, ambazo ni Iganzo, Isanga, Karobe, Iyunga, Nzovwe na Iwambi, wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Patrick Mwalunenge, aliyefika kujionea hali halisi ya wananchi walioathirika.

Baadhi ya wakazi wamesema chanzo kikubwa cha mafuriko hayo ni mifereji kuziba, hali iliyosababisha maji kuingia moja kwa moja kwenye makazi yao.

Licha ya uharibifu mkubwa wa mali na makazi, hakuna madhara ya kibinadamu yaliyoripotiwa hadi sasa.

TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA

February 16, 2026

AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI

February 15, 2026

SHEIKH WA MKOA MBEYA ATOA UJUMBE KWA WAISLAMU KUELEKEA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN

February 15, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya

February 16, 2026

TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA

February 16, 2026

AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI

February 15, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025347

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024231
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.