Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya

February 16, 2026

TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA

February 16, 2026

AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI

February 15, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya
  • TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA
  • AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI
  • SHEIKH WA MKOA MBEYA ATOA UJUMBE KWA WAISLAMU KUELEKEA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN
  • EFTA YACHOCHEA UCHUMI KWA HATI FUNGANI YA BILIONI 50
  • Kanisa la Moravian Tanzania Lamkabidhi Yona Sonelo Tuzo Maalum Baada ya Shahada ya Heshima Australia
  • Beno Malisa Azindua Tawi la Strategies Insurance Mbeya, Akaribisha Wawekezaji
  • RC Malisa Afungua Mafunzo ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa Binafsi Mbeya
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » JK KWA MFALME MSWATI III KUJADILI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA KWA NCHI WANACHAMA WA ECSA
Habari za Kitaifa

JK KWA MFALME MSWATI III KUJADILI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA KWA NCHI WANACHAMA WA ECSA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 4, 2026No Comments9 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) ameshiriki Mkutano wa 67 wa Mawaziri wa Afya kutoka nchi 9 wanachama za Jumuiya ya Afya ya Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika (ECSA-HC) unaofanyika Ezulwini, Ufalme wa Eswatini tarehe 2-3 Februari, 2026.

Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo umejadili mikakati ya kuimarisha mifumo ya afya ya nchi wanachama wa ECSA-HC, hususan kwa kuzingatia mabadiliko yanayoendelea duniani kote yaliyopelekea kupungua au kusitishwa kabisa kwa upatikanaji wa fedha za kufadhili miradi ya afya kutoka kwa wafadhili waliozoeleka.

Katika hotuba akifungua Kikao cha Makatibu Wakuu na Maafisa Waandamizi wa ECSA-HC, Dkt. Kikwete alitoa rai kwa nchi hizo kuwa wabunifu katika kubuni na kutafuta vyanzo mbadala vya rasilimali za kifedha ili kuhakikisha kuwa miradi iliyokwishaanza kutekelezwa haitetereki au kufa kutokana na kukoma kwa fedha za wafadhili. “Kama Serikali huwezi kuwaambia wananchi kuwa tunasitisha huduma za afya kwa sababu wafadhili wameacha kutoa fedha. Hapana. Ni wajibu wenu kama watunga Sera kuumiza vichwa na kufanya juu chini kutafuta vyanzo mbadala vya fedha ili wananchi waendelee kupata huduma wanazostahili”, alieleza Dkt. Kikwete.

Alitumia pia fursa hiyo kutoa uzoefu wake jinsi walivyowahi kukabiliana na changamoto za aina hiyo wakati wa uongozi wake ambapo moja ya mbinu walizobuni ni kuimarisha ushirikiano wa kikanda baina ya nchi za Afrika ili kuongeza uhimilivu wa mifumo ya afya, ikiwemo uamuzi wa nchi za ukanda huu kufanya manunuzi ya pamoja ya jumla kwa bei nafuu (bulk-procurement) ya dawa, vifaa tisa na vitendanishi badala ya kila nchi kununua vifaa hivyo kivyake.

Rais Mstaafu Dkt. Kikwete alitumia pia fursa hiyo kueleza washiriki hao hatua kubwa za mafanikio zilizopigwa na Tanzania chini ya uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan katika sekta ya afya. Akitoa mfano, alieleza namna ushirikiano wa karibu kati ya Serikali ya Tanzania na wadau wa mashirika yasiyo ya kiserikali, ikiwemo Taasisi ya JMKF, ulivyoweza kushusha kiwango cha vifo vya wakinamama wanaojufungua kutoka vifo 560 kwa kila kinamama 100,000 wanaojifungua hadi kufikia vifo 104 na kuifanya Tanzania kuwa nchi inayoongoza barani Afrika katika kutimiza lengo la Umoja wa Mataifa la SDG 3.1 linalozitaka nchi zote duniani kushusha kiwango hicho hadi kufikia vifo 70 ifikapo mwaka 2030.

Akitoa mfano wa umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali mashirika binafsi katika kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya katika ngazi ya jamii, Dkt. Kikwete alieleza namna JMKF inavyotoa huduma za kliniki inayotembea (mobile outreach) kwa kinamama wajawazito wanaoishi maeneo ya mbali na vituo vya afya na magumu kufikika katika Wilaya za Uyui na Sikonge, Mkoani Tabora.

Kwa mujibu wa Taasisi ya JMKF, Mradi huo unaojulikana kama Jamii Salama umechangia kwa kiasi kikubwa kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga mkoani Tabora ambapo hadi sasa umewagusa zaidi ya wakina mama 1,500 kwa kuwapatia huduma za kliniki, ikiwemo huduma ya ultrasound, tiba ya malaria, pamoja na kuwafikia watoto wa shule zaidi ya 3,200 kwa elimu ya afya ya kinywa na malaria.

Kwa upande mwingine, Rais Mstaafu Dkt. Kikwete aliongoza washiriki wa Mkutano huo kuonana na Mfalme Mswati III wa Eswatini ambaye aliahidi kupokea ripoti itakayotokana na majadiliano ya Mkutano huo na kuifikisha kwa Viongozi wenzake wa nchi wanachana wa ECSA-HC na Jumuiya nyingine za Kikanda.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI

February 15, 2026

EFTA YACHOCHEA UCHUMI KWA HATI FUNGANI YA BILIONI 50

February 14, 2026

KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA

February 10, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025347

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024231

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Video Mpya

Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya

By Mbeya YetuFebruary 16, 20265

ZAIDI ya kaya 200 zimepata madhara ya kukosa makazi baada ya nyumba zao kuezuliwa na nyingine kubomoka kufuatia mvua kubwa zilizoambatana na upepo mkali zinazoendelea kunyesha katika Nyanda za Juu Kusini.

Mbali na makazi kuharibika, vyakula na mavazi pia vimeathirika baada ya maji kujaa kwenye nyumba na mali nyingi kufunikwa na tope.

Uharibifu huo umeripotiwa katika kata sita, ambazo ni Iganzo, Isanga, Karobe, Iyunga, Nzovwe na Iwambi, wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Patrick Mwalunenge, aliyefika kujionea hali halisi ya wananchi walioathirika.

Baadhi ya wakazi wamesema chanzo kikubwa cha mafuriko hayo ni mifereji kuziba, hali iliyosababisha maji kuingia moja kwa moja kwenye makazi yao.

Licha ya uharibifu mkubwa wa mali na makazi, hakuna madhara ya kibinadamu yaliyoripotiwa hadi sasa.

TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA

February 16, 2026

AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI

February 15, 2026

SHEIKH WA MKOA MBEYA ATOA UJUMBE KWA WAISLAMU KUELEKEA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN

February 15, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya

February 16, 2026

TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA

February 16, 2026

AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI

February 15, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025347

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024231
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.