Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

“Ndingo: Uongozi wa Samia Ni Ukombozi Mkubwa kwa Wanawake Tanzania.”

March 8, 2026

WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

March 7, 2026

Mwalunenge Achangia Milioni 3 Baada ya Wanawake MZRH Kutoa Mashine ya EEG

March 7, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • “Ndingo: Uongozi wa Samia Ni Ukombozi Mkubwa kwa Wanawake Tanzania.”
  • WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM
  • Mwalunenge Achangia Milioni 3 Baada ya Wanawake MZRH Kutoa Mashine ya EEG
  • Comfy Mum na TNCC Wawafariji Wakinamama Wodi ya Wanawake Hospitali ya Sinza
  • Mbunge CCM,wapinzani waimarisha umoja,wajadili maendeleo ya wana Mbeya
  • Dkt. Tulia Aunga Mkono Ujenzi wa Barabara Bombambili kwa Mifuko 100 ya Saruji na tripu 10 za mawe
  • SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
  • Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.
Biashara na Uchumi

CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 11, 2026No Comments20 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Kuelekea Maadhimisho ya siku maalum ya familia ya Polisi Mbeya, 2026, Benki ya CRDB Mbeya imetoa msaada wa vifaa vya michezo kwa Jeshi la Polisi Mbeya.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo, Meneja wa CRDB Mbeya ndugu Harrison Andrew amesema kuwa wao kama CRDB wanatekeleza kauli mbiu yao ya “ULIPO TUPO” kwa kuungana na jamii katika shughuli au matukio mbalimbali.

Aliongeza kuwa, wanashirikiana katika mambo mbalimbali na Jeshi la Polisi ikiwemo jitihada za kuzuia na kutokomeza uhalifu hivyo kuelekea sikukuu maalum ya familia ya Polisi Mbeya watakuwepo kuungana na jamii.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga ameshukuru kwa msaada wa jezi za michezo (mpira wa miguu na riadha) zilizotolewa na Benki hiyo.

Aidha, Kamanda Kuzaga amewakaribisha wakazi wa Mkoa wa Mbeya kuungana na Jeshi hilo katika Maadhimisho ya siku maalum ya familia ya Polisi Mbeya itakayojumuisha michezo mbalimbali, burudani na utoaji wa elimu ya masuala ya ulinzi na usalama.

Siku Maalum ya Familia ya Polisi uadhimishwa kila mwaka ambapo kwa mwaka huu itaadhimishwa siku ya jumamosi Februari 14, 2026 kama sehemu ya Jeshi hilo kufanya tathmini ya utendaji kazi, kutoa zawadi kwa Askari waliofanya vizuri zaidi katika utendaji kazi, kuungana na wadau mbalimbali wa ulinzi na usalama pamoja na Wananchi.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026

February 26, 2026

KIKWETE AIPONGEZA BENKI YA NMB

October 8, 2025

Ujenzi barabara ya Lupeta-Wimba-Izumbwe kuinua Uchumi wa wananchi Mbeya.

January 12, 2024

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025364

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025141
Don't Miss
Video Mpya

“Ndingo: Uongozi wa Samia Ni Ukombozi Mkubwa kwa Wanawake Tanzania.”

By Mbeya YetuMarch 8, 20260

Mbunge wa Jimbo la Mbarali mkoani Mbeya, Bahati Ndingo, amesema maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni fursa ya kutathmini hatua zilizopigwa katika kuimarisha usawa wa kijinsia na kuhamasisha jamii kuendelea kuwapa wanawake na wasichana nafasi ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Akizungumza Machi 6, 2026 katika maadhimisho ya siku hiyo yaliyofanyika kiwilaya katika Kata ya Igurusi, Ndingo alisema Tanzania imepiga hatua kubwa kwa kumpa mwanamke nafasi ya juu ya uongozi nchini, akimtaja Rais Samia Suluhu Hassan kama mfano wa mafanikio ya wanawake katika uongozi.

Aidha, alisisitiza kuwa maadhimisho hayo hayalengi kujisifia bali kutambua mchango wa wanaume na wanawake katika kubadilisha mtazamo wa jamii kuhusu uwezo wa mtoto wa kike. Aliongeza kuwa mtoto wa kike ana uwezo wa kufanya kazi na majukumu yoyote kama ilivyo kwa mwanaume.

Maadhimisho hayo ni sehemu ya maandalizi ya kilele cha Siku ya Wanawake Duniani kinachoadhimishwa kila mwaka Machi 8.

WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

March 7, 2026

Mwalunenge Achangia Milioni 3 Baada ya Wanawake MZRH Kutoa Mashine ya EEG

March 7, 2026

Comfy Mum na TNCC Wawafariji Wakinamama Wodi ya Wanawake Hospitali ya Sinza

March 6, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

“Ndingo: Uongozi wa Samia Ni Ukombozi Mkubwa kwa Wanawake Tanzania.”

March 8, 2026

WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

March 7, 2026

Mwalunenge Achangia Milioni 3 Baada ya Wanawake MZRH Kutoa Mashine ya EEG

March 7, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025364

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.