Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.
- DAS Mbeya: Kipato Kisiharibu Vyanzo vya Maji
- KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA
- Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji
- Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo
- TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya
- New Asante Mbeya Yapongeza TAKUKURU Mbeya kwa Elimu ya Uadilifu na Kufungua Uelewa wa Wanachama
- Utengule Usangu Yapata Jezi, Majiko ya Gesi na Msaada wa Kijamii Kutoka kwa Mbunge Ndingo
Author: Mbeya Yetu
Kuelekea Maadhimisho ya siku maalum ya familia ya Polisi Mbeya, 2026, Benki ya CRDB Mbeya imetoa msaada wa vifaa vya michezo kwa Jeshi la Polisi Mbeya. Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo, Meneja wa CRDB Mbeya ndugu Harrison Andrew amesema kuwa wao kama CRDB wanatekeleza kauli mbiu yao ya “ULIPO TUPO” kwa kuungana na jamii katika shughuli au matukio mbalimbali. Aliongeza kuwa, wanashirikiana katika mambo mbalimbali na Jeshi la Polisi ikiwemo jitihada za kuzuia na kutokomeza uhalifu hivyo kuelekea sikukuu maalum ya familia ya Polisi Mbeya watakuwepo kuungana na jamii. Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya…
Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Bw. Azizi Faki, ametoa onyo kali juu ya kuendelea kwa uharibifu wa vyanzo vya maji wilayani humo, akisema hali halisi ya uchafuzi na upungufu wa maji inaonekana wazi kutokana na shughuli za kibinadamu zisizozingatia sheria.
Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa chanzo cha maji cha Mtombalizi, kilichopo katika Kata za Utengule Usongwe na Nsalala, Bw. Faki alisema uchimbaji wa mchanga na mawe katikati ya mto pamoja na uharibifu wa kingo za maji umepelekea mto huo kupoteza mwelekeo wake wa asili, maji kuchafuka na kupungua kwa kiasi kikubwa.
Bw. Faki alisema licha ya kuwepo kwa maelekezo ya awali ya kulinda kingo za mito, kupanda miti na kuacha mita sitini kutoka kwenye chanzo cha maji bila shughuli za kibinadamu, hali bado ni mbaya kutokana na kuendelea kwa shughuli haramu, hali inayohatarisha vyanzo vya maji vinavyotegemewa na wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.
Alitoa wito kwa taasisi zote husika ikiwemo TFS, mamlaka za maji, mamlaka ya madini, Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Rukwa, pamoja na viongozi wa serikali za mitaa, kata na tarafa kushirikiana kikamilifu katika kulinda chanzo hicho. Alisisitiza kuwa jitihada za kutafuta kipato haziwezi kuwa sababu ya kuvunja sheria na kuharibu mazingira.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Mohamed Fakii, ametoa onyo dhidi ya uharibifu wa vyanzo vya maji unaotokana na ukataji miti ovyo na kilimo karibu na vyanzo vya maji.
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa Chanzo cha Maji cha Mbawe, kijiji cha Mbawe, Fakii alisema kuwa shughuli za kibinadamu zinaendelea kuhatarisha uendelevu wa vyanzo vya maji licha ya kuwepo kwa maji kwa sasa kutokana na mvua. Alisisitiza kuwa ni marufuku kufanya shughuli zozote ndani ya mita 60 kutoka chanzo cha maji.
Aliwaagiza wananchi wote wanaolima au kufanya shughuli karibu na vyanzo hivyo kuondoka mara moja, huku akizitaka serikali za vijiji na kata kushirikiana kikamilifu katika ulinzi wa vyanzo vya maji na kutoa elimu kwa wananchi.
Ziara hiyo ilifanywa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mheshimiwa Solomon Itunda, akiwa ameambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya.
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na Shirika la CARE wametoa mafunzo kwa wawezeshaji wa ngazi ya jamii kuhusu mabadiliko ya tabia nchi mkoani Mbeya kupitia Mradi wa Ustahimilivu Wake, Dunia Yetu unaotekelezwa katika vijiji 300 vya Mbeya, Njombe na Iringa.
Mafunzo hayo ya siku tatu yamefanyika kijiji cha Chimala, wilayani Mbarali, yakilenga kuwajengea wakulima na wafugaji uelewa wa masuala ya jinsia, utunzaji wa mazingira na mbinu za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Mbunge wa Jimbo la Mbarali, Bahati Ndingo, amegawa jezi, sufuria, majiko ya gesi pamoja na sabuni kwa wananchi na vikundi mbalimbali vya vijana katika Kata ya Utengule Usangu, wilayani Mbarali, mkoani Mbeya.
Msaada huo umetolewa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kuzaliwa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) yaliyofanyika kiwilaya, yakilenga kuimarisha michezo, matumizi ya nishati safi na ustawi wa jamii.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mbunge Ndingo amesisitiza umuhimu wa vijana kukuza vipaji vyao, akibainisha kuwa michezo, hususan soka, ni ajira. Aidha, ametangaza mpango wa kuanzisha mashindano ya soka yajulikanayo kama “Bahati Ndingo Cup” baada ya msimu wa mavuno.
Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na Aga Khan Health Service Tanzania zimeingia katika makubaliano ya ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuboresha utoaji wa huduma za afya kwa Watanzania. Akizungumza jijini Mbeya, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Dkt. Godlove Mbwanji, alisema ushirikiano huo utawezesha kubadilishana ujuzi na uzoefu kati ya sekta ya umma na binafsi kwa manufaa ya wananchi.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Aga Khan Health Service Tanzania, Sisawo Konteh, alisema makubaliano hayo yataimarisha huduma za kliniki, kujenga uwezo wa watumishi, kuboresha mifumo ya ubora na kusaidia hospitali hiyo kupata ithibati. Ushirikiano huo pia utahusisha mafunzo, tafiti na kuendeleza huduma bingwa ikiwemo saratani na magonjwa ya moyo, pamoja na kukuza utalii wa tiba katika mkoa wa Mbeya.
Diwani wa Kata ya Utengule Usangu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya, Ismail Matipa, ametoa sare za shule kwa wanafunzi 400 waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza, katika Shule ya Sekondari Utengule Usangu.
Hatua hiyo imelenga kuondoa changamoto ya baadhi ya wazazi kuchelewesha au kushindwa kuwapeleka watoto wao shule pindi msimu wa masomo unapoanza, hali inayosababishwa na ukosefu wa sare za shule.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Diwani Matipa amesema utoaji wa sare hizo ni sehemu ya jitihada zake za kuunga mkono elimu na kuhakikisha wanafunzi wote wanaanza masomo kwa wakati bila vikwazo vya kiuchumi.
Ameeleza kuwa tukio hilo limefanyika katika wiki ya maadhimisho ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutimiza miaka 49 tangu kuzaliwa kwake mwaka 1977, ikiwa ni ishara ya kuenzi mchango wa chama hicho katika maendeleo ya elimu na ustawi wa jamii.
