Author: Mbeya Yetu

Mdau wa Maendeleo nchini Ndele Mwaselela amewataka Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya kuandika habari zitakazosaidia kutatua changamoto za wananchi ili serikali iweze kuzitatua kwa wakati. Ndele ameyasema hayo Jijini Mbeya katika kikao maalumu cha kutathimini mahusiano ya waandishi wa habari,wananchi,vyama na serikali kwa lengo la kujenga upendo na mshikamano. Katika hatua nyingine Mwaselela amewataka waandishi kuisaidia serikali kwa kufichua changamoto badala ya kuficha kero zinazowakabili wananchi. Waandishi wamesema kupitia taaluma yao wanaweza kuibua changamoto lakini maisha yao yanakuwa hatarini kutoka kwa wahusika wanaolalamikiwa. Amesema endapo Waandishi wataibua changamoto wataisaidia Serikali kuzitatua zikiwemo za afya,barabara,maji na elimu. Mwenyekiti wa Klabu…

Read More

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele leo Desemba 29,2025 amesoma risala maalum kuhusu uchaguzi wa ubunge katika jimbo la Siha lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Siha, Mkoa wa Kilimanjaro, Tanzania Bara na Jimbo la Fuoni lililopo Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, Tanzania Zanzibar unaotaraji kufanyika Desemba 30,2025. Jaji Mwambegele amesema, uchaguzi mdogo huo utahusisha pia, kata tano za Tanzania Bara. Kata hizo ni;            Chamwino iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Mkoa wa Morogoro; Mbagala Kuu iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Mkoa wa Dar es Salaam; na Nyakasungwa…

Read More

Wazee wanaoishi katika Makazi ya Wazee na wasiojiweza Bukumbi, wilayani Misungwi mkoani Mwanza, wameishukuru Serikali kwa kuimarisha huduma za ustawi wao, wakisema hatua hiyo imeleta faraja, heshima na matumaini mapya katika maisha yao ya uzeeni.

Mwenyekiti wa Wazee kituoni hapo, Mzee John Nguku amesema wazee wanathamini jitihada Serikali za kuwapatia huduma muhimu kwa wakati.

“Kwa niaba ya wazee wenzangu, tunaishukuru Serikali kwa kutukumbuka tunaishi kwa amani, tunahudumiwa kwa heshima na tunahisi bado tuna thamani katika jamii, tunaomba uangalizi huu uendelee ili wazee wengi zaidi wanufaike maana uzee siyo mzigo bali ni neema”. amesema Mzee John

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema Serikali inawatambua wazee kama tunu muhimu ya Taifa na itaendelea kuimarisha huduma za ustawi na ulinzi wao.

Mhe. Mahundi amesema pamoja na jitihada za Serikali, jamii ina wajibu wa msingi wa kuwatunza wazee, huku akiwataka vijana kutowasahau wazazi wao wanapofikia uzee na kuhakikisha wanapata upendo, heshima na msaada unaostahili.

“Nawasihi vijana na jamii kwa ujumla, msije mkawasahau wazazi wenu wanapofikia uzee. Kuwatunza wazee ni wajibu wa familia na ni sehemu ya maadili yetu ya Kitanzania, Serikali itaendelea kuhakikisha wazee wanathaminiwa, wanalindwa na wanapata huduma stahiki bila kubaguliwa. Tunazitaka familia, vijana na jamii kwa ujumla kutambua kuwa kuwajali wazee ni wajibu wa kimaadili na msingi wa ustawi wa Taifa letu” amesema Mhe. Mahundi.

Kwa upande wake, Mfawidhi wa Makazi ya Wazee na wasiojiweza Bukumbi, Vivian Kaiza amesema uangalizi wa Serikali na ushirikiano wa wadau umeendelea kuimarisha utoaji wa huduma kwa wazee waliopo kituoni hapo, Makazi yanaendelea kusimamiwa kwa weledi na kujali maslahi ya wazee, huku akiahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha wazee wanapata huduma stahiki na kuishi kwa amani.

Ziara hiyo ni mwendelezo wa dhamira ya Serikali katika kuimarisha ustawi wa wazee, huku jamii ikihimizwa kushirikiana na Serikali katika kuwatunza wazee ili waishi maisha yenye heshima, upendo na matumaini.

Read More

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (MNEC), Ndele Mwaselela, amewataka waandishi wa habari kuendelea kuzingatia maadili ya taaluma, kuandika habari za maendeleo na kuwasaidia wananchi kwa kuwaseemea, akisisitiza kuwa jamii inawategemea sana waandishi wa habari katika kusikika kwa sauti yao. Mwaselela ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika Ofisi za Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya (Mbeya Press Club), ambapo alizungumza na baadhi ya waandishi wa habari aliowakuta wakiendelea na majukumu yao ya kila siku ofisini hapo. Akizungumza katika mazungumzo hayo ya ana kwa ana, Mwaselela alisema kuwa waandishi wa habari wana nafasi ya kipekee…

Read More