Author: Mbeya Yetu

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi Julai 1,2025 amefungua kambi ya matibabu bila gharama kwa wagonjwa wa macho Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya inayolenga kuwafikia wagonjwa zaidi ya mia mbili.

Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema gharama zote za uchunguzi,dawa na matibabu ni bure kupitia wadau wake kutoka Ujerumani na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

Dkt Fariji Kilewa Mkuu wa Kitengo cha macho Hospitali ya Mkoa wa Mbeya amesema lengo ni kuwafikia wagonjwa zaidi ya mia mbili waliopo Mkoa wa Mbeya na mikoa jirani.

Aidha amesema mbali ya upasuaji wa mtoto wa jicho pia wanawafanyia uchunguzi wa macho kwa matatizo mengine ya macho.

Hata hivyo Dkt Fariji Kilewa amesema gharama za upasuaji wa mtoto wa jicho zinagharimu zaidi ya shilingi laki tatu ambazo ni watu wachache wanaoweza kumudu gharama hizo.

Afisa uhusiano Hospitali ya Mkoa wa Mbeya Agrey Mwaijande amesema gharama zote zinatolewa bure hivyo wito umetolewa kwa wananchi kuitumia vizuri fursa hiyo.

Baadhi ya wagonjwa waliojitokeza kupatiwa watibabu wamepongeza huduma hiyo kutokana na wengi wao kushindwa kumudu gharama za matibabu ya macho.

Hii ni kambi ya pili kwa Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi kuandaa kambi ya macho iliyoanza juni 30,2025 itakayotamatika julai 5,2025kwa ushirikiano na Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.

Read More

#mbeyayetutv
Wakili Msomi na Kada wa Chama Cha Mapinduzi CCM Kapteni Sambwee Shitambala Mwalyego amejitokeza kuchukua fomu kuwania Ubunge Jimbo la Mbeya mjini.

Shitambala amesema ameguswa kuwania nafasi hiyo akitumia haki yake ya msingi, akidhamiria kuendeleza pale alipoishia Spika wa Bunge Dkt Tulia Ackson ambaye amehamia kuwania katika jimbo jipya la Uyole.

Read More

Kada wa Chama cha Mapinduzi, CPA (T) Ruth Hassani akisaini kitabu. Kada wa Chama cha Mapinduzi, CPA (T) Ruth Hassani  ametia nia ya kuwania kuteuliwa na Chama chake kuwania Ubunge katika Jimbo la Same Mashariki, Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro. Akiwa ameambatana na Mumewe Bw. Banyinga Majeshi, CPA Ruth ambaye ni Mhasibu wa Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mkoani Moprogoro alichukua fomu hiyo katika Ofisi za CCM Wilaya ya Same  na kukabidhiwa na Katibu wa CCM Wilaya, Ndg.Amos Kusakula leo Juni 29,2025. Ruth amesema nia yake si kutafuta nafasi ya uongozi katika jimbo la Same Mashariki bali kuwasemea Wanasame Mashariki…

Read More

Wananchi wa Jimbo la Uyole, Mkoani Mbeya, kwa moyo wa upendo na imani kubwa, wamemchukulia fomu ya kuwania tena Ubunge Dkt. Tulia Ackson @tulia.ackson kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 25 Oktoba 2025. Hatua hiyo inaonesha wazi dhamira ya wananchi kuendelea kumuunga mkono kiongozi huyu mahiri ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuleta maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa jimboni humo.

Wakizungumza baada ya kukabidhiwa fomu hiyo, baadhi ya wakazi wa Uyole wamesisitiza kuwa Dkt. Tulia ni chaguo sahihi kutokana na utendaji wake uliotukuka, uwezo mkubwa wa kiuongozi na ushirikiano wake wa karibu na wananchi katika kutatua changamoto mbalimbali.

Kwa kauli moja, wananchi hao wameahidi kuendelea kumpigania hadi ushindi, wakiamini kuwa uongozi wake utaendeleza kasi ya maendeleo na kuimarisha ustawi wa wananchi wa Uyole.

Read More