Author: Mbeya Yetu

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Andrew Lentz, katika Ikulu ya Chamwino, kujadili maeneo muhimu ya ushirikiano na kuimarisha dhamira ya pamoja ya kujenga ushirikiano wa kisasa na wenye manufaa kwa pande zote mbili. Balozi Lentz—aliyefuatana na Mshauri wa Masuala ya Kisiasa na Uchumi—amesisitiza dhamira ya Washington kuhuisha mahusiano na kuongeza kina la ushirikiano wa kiuchumi, kisiasa na kiusalama kati ya mataifa haya mawili. “Marekani imejitolea kujenga ushirikiano usiotegemea misaada, bali unaojengwa juu ya ustawi wa pamoja,” alisema Balozi Lentz. Mazungumzo yamejikita katika hatua…

Read More

Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania, today held talks with the Acting United States Ambassador to Tanzania, Andrew Lentz, at Chamwino State House to advance key areas of bilateral cooperation and reaffirm the shared commitment to a modern, mutually beneficial partnership. Ambassador Lentz—accompanied by the Counselor for Political and Economic Affairs—underscored Washington’s determination to reset the relationship and deepen economic, political, and security collaboration with Tanzania. “The United States is committed to a partnership based not on aid dependency but on shared prosperity,” Ambassador Lentz said. The discussions centred on ongoing negotiations involving…

Read More

Mfanyakazi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, Dkt. Ekaristo Mwang’ande, ametunukiwa tuzo kubwa na sifa za kipekee kwa kuwa mwanafunzi bora wa Shahada ya Uzamili ya Udaktari Bingwa wa mpangilio wa meno, mataya na Uso (Master of Dentistry in Orthodontics and Dentofacial Orthopedics), kwenye mahafali yake ya 19 ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) jijini Da es Salaam. Akiwapongeza wanafunzi waliofanya vizuri wakati wa sherehe maalum iliyofanyika jijini Dar es Salaam Mkuu wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Prof. David Mwakyusa amewapongeza wanafunzi waliofanya vizuri katika fani mbalimbali ya afya na…

Read More

SERIKALI YA TANZANIA KUWAFUTIA HADHI YA UKIMBIZI WAKIMBIZI WANAOISHI NCHINI.

Serikali ya Tanzania imesema inaenda kuwafutia hadhi ya ukimbizi Wakimbizi wanaoishi nchini baada ya kurejea kwa hali ya amani katika nchi zao baada ya hapo awali kuwepo kwa machafuko.

Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene huku jumla ya Wakimbizi 238,956 wanahifadhiwa hapa nchini ambapo Warundi ni 152,019,Wakongo ni 86,256 na mataifa mengine yakichangia idadi ya 681.

“Katika mkutano wa mwisho tulikubaliana kurejesha Wakimbizi 3000 kwa wiki,hata hivyo hadi tunakutana hapa hii leo 2025 ni Wakimbizi 3000 pekee waliorejea nchini kwao.Hili ni jambo ambalo lingepaswa kukamilika ndani ya wiki moja lakini limechukua takribani mwaka mzima,hatuwezi kuruhusu Hali hii iendelee hivi.” Alisema Waziri Simbachawene

Read More

Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba (Mb) ameipongeza Wakala ya Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) kwa utendaji kazi mzuri katika kuhakikisha nchi inakuwa na akiba ya mafuta ya kutosha. Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Menejimenti ya PBPA leo Desemba 6,2025 jijini Dar es Salaam. “Nawapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya lakini hakikisheni mnatoa elimu kwa Watanzania kuhusu majukumu yenu na kazi zenu” amesema Mhe. Salome. Aidha, ametumia nafasi hiyo kuitaka PBPA kuwawezesha Watanzania wazawa kuingia kwenye biashara ya mafuta na kufanya kazi kwa ushirikiano. “Lazima tupate wawekezaji wa Tanzania, tuwawezeshe waingie kwenye hii…

Read More