Author: Mbeya Yetu

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imeanza rasmi kutoa mafunzo ya magonjwa ya Dharura na Mahututi kwa watoa huduma za afya, wanafunzi wa kada za Afya pamoja Jamii Nyanda za Juu Kusini kwa lengo la kuokoa maisha na kupunguza athari za ajali na dharura za kiafya. Akiongea wakati wa kufungua mafunzo hayo leo tarehe 26 novemba,2025 katika kituo cha kutolea mafunzo hayo kwa vitendo kilichojengwa chini ya udhamini wa taasisi ya Abbott Fund, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji amesema, kuanzishwa kwa mafunzo hayo kutasaidia upatikanaji wa wataalamu wenye weredi kwani kumekuwa na ongezeko…

Read More

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Bw. Mohamed Malick Salum na Mhandisi Abdulaziz Abdullah Al-Sulait, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi wa Qatar, akisaini kwa niaba ya nchi yake wakisaini Hati ya kutambuliana vyeti vya Mabaharia na Qatar katika hafla iliyofanyika London Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Bw. Mohamed Malick Salum na Mhandisi Abdulaziz Abdullah Al-Sulait, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi wa Qatar wakiwa wameshikana mkono mara baada kusaini Hati ya Makubaliano ya kutambuliana vyeti vya Mabaharia na Qatar katika hafla iliyofanyika London Na Mwandishi Wetu London Serikali…

Read More

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Tanzania ni mali ya Watanzania wote wala si ya Serikali au chama cha siasa na hivyo kila mmoja anapaswa kuilinda. “Tanzania si mali ya Serikali, Tanzania si mali ya chama cha siasa na vyama vya siasa vipo kwa sababu nchi ipo. Tuilinde nchi yetu. Mungu ametupa nchi nzuri na kila mmoja ana wajibu wa kuilinda,” amesisitiza. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo jioni (Jumanne, Novemba 25, 2025) wakati akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali nchini katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Amesema…

Read More

– Azungumza na vijana Tunduma, Mkoa wa Songwe Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka leo Novemba 25, 2025 amewasili mkoani Songwe kwa lengo la ziara ya kukutana na kuzungumza na vijana kuhusu masuala mbalimbali ya ustawi wa kundi hilo ikiwemo shughuli za Ajira, Uwezeshwaji kiuchumi, Elimu, Afya na Miundombinu kwa ajili ya ustawi wa maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla. Mhe. Waziri Nanauka ametembelea kwenye vijiwe pamoja na miradi ya vijana katika eneo la Sogea stendi, Kilimanjaro, Kisimani, Stendi ya zamani ya Majengo na Mpemba. Akizungumza mara baada ya kukutana na vijana…

Read More