Author: Mbeya Yetu

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mhe. Patrick Mwalunenge, ameendelea kuwawezesha vijana wa bodaboda jijini Mbeya kwa kutoa msaada katika vijiwe mbalimbali.

Katika ziara hiyo, ametoa bodaboda moja kwa vijana wa kijiwe cha Nzovwe, pamoja na mtaji wa mafuta wa shilingi 40,000 kwa kila kikundi alichotembelea. Aidha, ameacha shilingi 400,000 kwa ajili ya kuwaendeleza vijana wengine.

Mhe. Mwalunenge amewahimiza vijana kuwa watulivu na wavumilivu wakati serikali ikiendelea kuweka mikakati madhubuti ya kuwawezesha kupitia fursa za kiuchumi.

Read More

Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkoa wa Dodoma itaendelea kushirikiana kwa karibu na jukwaa la viongozi la uwezeshaji wanawake kiuchumi jijini Dodoma, kwa kuhakikisha mazingira wezeshi ya biashara yanaimarishwa, Sera na Miongozo rafiki inatekelezwa na fursa zaidi za maendeleo zinapatikana kwa wanawake wote bila ubaguzi. Akizungumza na viongozi pamoja na wajumbe wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Jiji la Dodoma Novemba 28,2025 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi. MaryPrisca Mahundi amesema Majukwaa hayo yamekuwa chachu ya mabadiliko katika maisha ya wanawake wa jiji la Dodoma ambapo yameongeza uelewa wa masuala ya fedha,…

Read More

Wadau wa kilimo kutoka taasisi za Serikali na sekta binafsi wamepatiwa mafunzo juu ya matumizi ya mashine za kisasa za kukaushia na kupima unyevu wa mazao ya nafaka, katika warsha iliyoandaliwa na Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na JICA jijini Mbeya.

Warsha hiyo imefanyika tarehe 26 Novemba 2025 katika shamba la Raphael Group Ltd, ambapo mashine ya Batch Circulating Dryer yenye uwezo wa kukaushia hadi tani 8 za mpunga ndani ya saa 4 imeoneshwa kwa vitendo. Teknolojia hii inatarajiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa upotevu wa mazao baada ya mavuno.

Akizungumza katika mafunzo hayo, Mhandisi Sekela Mwakihaba kutoka Idara ya Zana za Kilimo na Uongezaji Thamani alisema ushiriki wa wadau unaonesha dhamira ya Serikali ya awamu ya sita kuboresha mnyororo wa thamani wa mazao na kupunguza uharibifu wa nafaka wakati wa uvunaji. Alibainisha pia kuwa Serikali inaendelea kusukuma matumizi ya teknolojia kupitia utekelezaji wa Agenda 10/30 ili kuongeza tija na kipato cha wakulima.

Kwa upande wake, Meneja wa Uzalishaji wa Raphael Group Ltd – Kituo cha Uyole, Bw. Maisha Ambangile, alisema mashine hiyo itasaidia wakulima kupata nafaka kavu kwa ubora wa soko na kwa muda mfupi, huku gharama ya mashine moja ikiwa takriban shilingi milioni 188.

Warsha hiyo imeratibiwa na JICA kwa kushirikiana na kampuni za YAMAMOTO (watengenezaji wa mashine za kukaushia nafaka) na Kett Electric Laboratory (watengenezaji wa mashine za kupima unyevu), ikiwakutanisha maafisa wa Serikali, wataalamu wa JICA, wamiliki wa mitambo ya ukavu na wakulima kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya.

Read More

Serikali imeendelea kuanzisha Majukwaa ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi kuanzia ngazi ya Vijiji/Mtaa, Kata, Wilaya na Mkoa ambapo Katika kipindi cha mwaka 2020 hadi 2025, jumla ya Majukwaa 15,147 yameanzishwa, ambayo yameleta chachu kwa wanawake ya kujifunza masuala ya ujasiriamali, elimu ya fedha na uwekezaji. Hayo yamesemwa na Naibu wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi MaryPrisca Mahundi wakati akizungumza na wanavikundi vya malezi na matunzo ya watoto Kata ya lhumwa Jijini Dodoma. Mahundi amesema katika eneo la fursa za kiuchumi, Wizara inaratibu na kusimamia jukumu la kuwezesha kiuchumi wafanyabiashara ndogondogo na wao wakiwa miongoni mwao watatambuliwa…

Read More

Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mwenyekiti Mstaafu wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, ametunuku Shahada kwa wahitimu wa Chuo Kikuu Mzumbe, Ndaki ya Mbeya, katika Mahafali ya 24 yaliyofanyika leo, tarehe 27 Novemba 2025.

Akizungumza katika mahafali hayo, Dkt. Shein amewataka wahitimu kuwa na nidhamu, uadilifu, na bidii ya kazi wanapoingia kwenye soko la ajira na katika nafasi zao za kulitumikia taifa. Ameeleza kuwa dunia ya sasa inahitaji viongozi na wataalamu wanaojituma, wabunifu, na wenye maadili mema.

Amesisitiza kuwa elimu waliyoipata Mzumbe ni nguzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya nchi, hivyo ni wajibu wa kila mhitimu kujiandaa kikamilifu na kutumia taaluma yao kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla.

Mahafali hayo yamehudhuriwa na viongozi wa Chuo Kikuu Mzumbe, wadau wa elimu, wazazi, na ndugu wa wahitimu kutoka maeneo mbalimbali.

Read More

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imeanza rasmi kutoa mafunzo ya magonjwa ya Dharura na Mahututi kwa watoa huduma za afya, wanafunzi wa kada za Afya pamoja Jamii Nyanda za Juu Kusini kwa lengo la kuokoa maisha na kupunguza athari za ajali na dharura za kiafya.

Akiongea wakati wa kufungua mafunzo hayo leo tarehe 26 novemba,2025 katika kituo cha kutolea mafunzo hayo kwa vitendo kilichojengwa chini ya udhamini wa taasisi ya Abbott Fund, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji amesema, kuanzishwa kwa mafunzo hayo kutasaidia upatikanaji wa wataalamu wenye weredi kwani kumekuwa na ongezeko la wanafunzi wengi kuliko miundo mbinu ya kufundishia mafunzo haya kwa vitendo.

“…wote tunajua kwamba miaka ya karibuni kumekuwa na ongezeko la wanafunzi kwenye vyuo vyetu ambalo haliendi sambamba na miundombinu ya kufundishia kwa vitendo.” – Dkt. Mbwanji

Aidha Dkt. Mbwanji ameishukuru taasisi ya Abbott Fund Tanzania, Wizara ya Afya pamoja (EMAT) kwa ushirikiano katika ujenzi wa kituo hicho cha kutolea mafunzo hayo.

“…lilianza kama wazo na sasa linaonekana hivyo niwashukuru sana Abbott Fund Tanzania, Wizara ya afya pamoja na (EMAT) kwa kuratibu upatikanaji wa kituo hiki”. – Dkt. Mbwanji

Kwa upande wake Dkt. Raya Mussa, Meneja Mradi huduma za dharura akiongea kwa niaba ya Taasisi ya Abbott Fund Tanzania ameishukuru Wizara ya Afya kupitia Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa ushirikiano waliouonyesha kwa kukubali ujenzi wa kituo ambacho kitawanufaisha watoa huduma za afya, wanafunzi pamoja wataalamu wote wanapatikana Kanda ya Nyanda za Juu Kusini katika idara za Magonjwa ya Dharura na Ajali kutokana na miundombinu pamoja na vifaa ya kisasa vinavyopatikana katika kituo hicho.

“…lengo la kituo hiki si kunufaisha watu wa ndani tu lakini pia itanufaisha wanafunzi pamoja na watu wengine watakaohitaji kujifunza mafunzo haya hata kama si watoa huduma za afya”. – Dkt. Raya Mussa

Dkt. Prosper Bashaka ni Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya amesema, maboresho ya upatikanaji wa huduma za dharura imekuwa ni kipaumbele kikubwa cha serikali, hivyo amewapongeza wadau wote walioshiriki katika jitihada za uanzishwaji wa kituo hicho cha kutolea mafunzo ya Magonjwa ya Dharura na Mahututi kwani kitaleta tija kwa hospitali na jamii hasa kwa wakazi wa Nyanda za Juu Kusini.

“…nitoe pongezi kwa wadau wote walioshiriki katika ujenzi wa kituo hiki kwani kitaleta tija kwa hospitali na zaidi wakazi wa Nyanda za Juu Kusini”. – Dkt. Prosper Bashaka.

Hadi sasa vituo hivyo vya kutolea mafunzo ya Magonjwa ya Dharura na Mahututi vimejengwa zaidi ya 6 nchi nzima kwa ushirikiano wa taasisi ya Abott Fund, Wizara ya Afya pamoja na EMART.

Read More