Author: Mbeya Yetu

Kijana dereva wa bodaboda Brown Anthony amevunja rekodi baada ya kusafiri kutoka Mbeya hadi Dar es Salaam kwa saa 10 tu akitumia pikipiki aina ya Boxer 150 HD (MC 473 FKT).

Safari hii ilianza kama ubishani wa kawaida kati yake na bodaboda mwenzake Alex Ndile tarehe 14 Januari 2026, wakibishana kama inawezekana kufika Dar ndani ya masaa 13. Ubishi ukawekwa kwenye makubaliano rasmi, na Brown akaamua kuthibitisha kwa vitendo.

Read More

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mhe. Patrick Mwalunenge, ameanza kutatua kero ya barabara katika Kata ya Iyela, mitaa ya Iyela na Pambogo, kwa kuagiza kumwagwa kwa vifusi kufuatia malalamiko ya muda mrefu ya wakazi wa maeneo hayo. Hatua hiyo inalenga kuboresha hali ya barabara na kurahisisha shughuli za kijamii na kiuchumi za wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mbunge, Katibu wa Mbunge Hakimu Edward alisema zoezi la kumwaga vifusi ni utekelezaji wa maelekezo ya moja kwa moja ya Mbunge Mwalunenge, ikiwa ni sehemu ya ahadi zake za kisiasa na mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi kwa vitendo.

Read More

Wananchi wa Kata ya Iyela, Jijini Mbeya, wameiomba Serikali kuangalia kwa jicho la huruma barabara ya eneo la Hali ya Hewa hadi Kituo cha Afya Iyela, wakieleza kuwa barabara hiyo imekuwa katika hali mbaya kwa zaidi ya miaka kumi. Wamesema barabara imejaa mashimo makubwa yanayosababisha vyombo vya usafiri ikiwemo bajaji na pikipiki kushindwa kupita kwa urahisi, hali inayowaathiri wananchi hususan wagonjwa wanaoelekea kupata huduma za afya katika kituo hicho.

Read More

Child Support Tanzania imeendesha kikao na madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya kupitia Kamati ya Elimu, Afya na Maendeleo ya Jamii kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wa Elimu Jumuishi, hususan kwa watoto na watu wenye ulemavu.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa Child Support Tanzania, Bi. Noela Msuya Shawa, amesema kupitia mradi wa Sauti Zetu unaofadhiliwa na Oxfam na kutekelezwa kwa ushirikiano na AkiElimu, madiwani wamepatiwa mafunzo kuhusu Mpango Mkakati wa Taifa wa Elimu Jumuishi, miongozo yake na wajibu wao katika kuhakikisha utekelezaji wake kwa ubora katika shule za kata zao.

Kwa upande wao, madiwani wamesema mafunzo hayo yamewajengea uelewa mpana kuhusu masuala ya watoto na watu wenye ulemavu. Mh. Juma Samson Simbeange, Diwani wa Kata ya Nsoho, amesema atahakikisha masuala ya watoto yanapewa kipaumbele wakati wa kupitisha bajeti za Halmashauri ili kuwasaidia watoto wanaohitaji msaada maalum.

Read More