Author: Mbeya Yetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Furaha Mwile Nyelele, mkazi
wa Kijiji cha Shilanga kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wa jirani yake
aliyekuwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Shilanga darasa la saba
aitwaye Boniventure Elia Lazaro [12] mkazi wa Shilanga.
Awali kabla ya tukio hilo tarehe 21.12.2025 saa 10:15 jioni huko Kijiji cha
Shilanga, Kata ya Ilembo, Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Mbeya Vijijini
mtuhumiwa Furaha Mwile Nyelele alimpiga kwa kipande cha mti kichwani
mtoto Boniventure Elia Lazaro [12] ambaye kwa sasa ni marehemu na
kumsababishia jeraha ambapo alikimbizwa katika Hospitali Teule ya Ifisi
kwa matibabu.
Tarehe 22.12.2025 saa 6:30 mchana akiwa anaendelea kupatiwa matibabu
katika Hospitali Teule ya Ifisi alifariki dunia. Uchunguzi wa awali umebaini
kuwa chanzo cha tukio hili ni kujichukulia sheria mkononi baada ya
mtuhumiwa kumtuhumu mtoto kuiba mayai ya kuku.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa kwa jamii kuacha tabia ya
kujichukulia sheria mkononi ili kuepuka madhara. Aidha, wazazi na walezi
wanakumbushwa kuzingatia suala la ulinzi na usalama wa mtoto kwa
kuhakikisha haki za mtoto zinaheshimiwa na kulindwa.

Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.

Read More

Serikali imesisitiza umuhimu wa jamii kuimarisha maadili na uzalendo miongoni mwa vijana nchini kwa kutumia taasisi za elimu ili kujenga taifa lenye misingi imara ya utu, uwajibikaji. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, akiwa mgeni rasmi katika Mdahalo wa maadili na uzalendo uliofanyika katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare, mkoani Mara. Mhe. Mahundi amesema, Serikali ya Awamu ya Sita inaamini kuwa maendeleo ya kweli ya taifa hayawezi kupatıkana bila kujenga maadili ya wananchi wake, hususan vijana ambao ndiyo nguvu kazi na viongozi wa baadaye. “Huwezi kujenga…

Read More

Mbunge wa Jimbo la Uyole, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson (@tulia.ackson), ameendelea kutoa sadaka kwa familia zisizo na uwezo katika kipindi cha kuelekea sikukuu ya Krismasi kwa kutoa chakula na fedha.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Dkt. Tulia amesema ushirikiano mzuri kati ya viongozi wa mitaa na wananchi ndiyo umefanikisha kuwatambua walengwa sahihi, akibainisha kuwa leo ilikuwa zamu ya Kata ya Ilemi, ambapo kaya 13 zimenufaika, huku jumla ya kaya 130 zikitarajiwa kupata msaada huo katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Uyole.

Ameongeza kuwa zoezi hilo ni endelevu na litaendelea katika kata nyingine kadri ratiba itakavyoruhusu, kwa lengo la kuwafikia wananchi wenye uhitaji mkubwa zaidi.

Read More

Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Uyole, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ameanza zoezi maalum la kuwafikia kaya zenye uhitaji zaidi katika Jimbo la Uyole ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya. Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Mhe. Dkt. Tulia amesema kuwa mwezi wa Desemba umechaguliwa mahsusi kwa ajili ya kuwafikia wananchi walio katika uhitaji mkubwa zaidi, akibainisha kuwa ingawa wahitaji ni wengi katika jamii, lengo ni kuanza na wale walio katika mazingira magumu zaidi. Amesema kwa…

Read More

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhandisi Maryprisca Mahundi, ameagiza Chuo cha Maendeleo ya jamii Uyole kupitia dhana ya ushirikishwaji jamii kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia na kutaka kazi hiyo kuwa endelevu ndani na nje ya chuo Mahundi amezungumza hayo wakati wa mahafali ya kumi na sita ya chuo cha maendeleo ya jamii CDTI uyole yaliofanyika viwanja vya michezo chuo cha maendeleo ya jamii Uyole na kusema licha ya siku kumi na sita za kupinga ukatili kufanyika lazima zoezi hilo likawe endelevu Ameitaka jamii inayozunguka Chuo na kila mwanafunzi ni vema kila mmoja akawa…

Read More