Author: Mbeya Yetu

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mzee Rashidi Mfaume Kawawa, mwanasiasa mashuhuri na mmoja wa viongozi waliokuwa karibu sans na xdwa Mwalimu Julius Nyerere katika harakati za uhuru na ujenzi wa taifa. Mzee Kawawa aliyesaliwa tarehe 27 Februari 1926 na kufariki 31 Desemba 2009, alikuwa Waziri Mkuu wa pili wa Tanganyika kuanzia tarehe 22 Januari 1962 hadi 9 Desemba 1962, akichukua nafasi baada ya Julius Nyerere kujiuzulu kwa muda ili kuimarisha chama cha TANU. Baada ya Tanganyika kupata uhuru kamili na kuwa Jamhuri, Mwalimu Nyerere alirejea madarakani kama Rais, ambspi baadaye Mzee Kawawa alikuja kuwa Waziri Mkuu wa…

Read More

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Wilaya ya Mbeya Mjini, Emmanuel Mwalupindi, amekabidhi tuzo na vitabu kwa walimu wa Shule ya Sekondari ya Sangu, shule inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), ikiwa ni sehemu ya pongezi kwa kufanya vizuri katika matokeo ya Kidato cha Nne mwaka 2025. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi tuzo hizo iliyofanyika shuleni hapo Mbeya Mjini, Mwalupindi amesema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mzuri kati ya walimu, wanafunzi na wazazi, na ni jambo la kujivunia kuona shule ikiendelea kufanya vizuri kitaaluma. Ameeleza kuwa katika matokeo ya mwaka 2025, shule hiyo haikuwa na mwanafunzi mwenye daraja la…

Read More

Naibu  Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mbeya, Jasper H. Luoga, ametoa taarifa kwa waandishi wa habari mkoani Mbeya akieleza mafanikio na hatua zilizochukuliwa na taasisi hiyo katika kudhibiti rushwa na kulinda rasilimali za umma. Akizungumza katika mkutano huo na vyombo vya habari, alisema TAKUKURU imefanikiwa kuokoa shilingi 107,450,300 kati ya shilingi 125,431,000 ambazo hazikuwasilishwa kwenye akaunti ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali baada ya kukusanywa na watoza ushuru wa halmashauri hiyo. Alisema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha mapato ya umma yanakusanywa na kuwasilishwa kwa usahihi pamoja na kudhibiti ubadhirifu wa…

Read More

Mfumo wa kidigitali wa utoaji wa Vyeti vya Uasili kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP) unaopatikana kupitia tovuti ya tcp.tncc.or.tz unatarajiwa kuanza kutumika rasmi kuanzia Machi 2, 2026, hatua inayolenga kurahisisha na kuharakisha huduma za biashara za kimataifa nchini. Akizungumza mkoani Mbeya wakati wa mafunzo kwa wasafirishaji wa bidhaa kwenda nje (exporters), Makamu wa Rais Kilimo wa Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC), Bw. Swallah Swallah, amewahimiza wafanyabiashara kujiandaa na kuutumia kikamilifu mfumo huo kwa kujisajili na kuwasilisha maombi yao kupitia tcp.tncc.or.tz, ili kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kila siku. Alisema kuanza kwa kutumika kwa mfumo huo wa kidigitali…

Read More

Serikali imesema itaendelea kuimarisha malezi ya watoto na utoaji wa mafunzo ya ustawi wa jamii kwa wananchi ili kupunguza changamoto za misongo ya mawazo, migogoro ya kifamilia na matatizo ya kisaikolojia, sambamba na kujenga jamii yenye maadili mema, ustawi imara na uwezo wa kukabiliana na changamoto za maisha ya kila siku. Akizungumza wakati wa ziara yake katika Taasisi ya Ustawi wa Jamii Kampasi ya Kisangara wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali inatambua umuhimu wa taasisi hiyo katika kutoa wataalamu na elimu kwa jamii kuhusu malezi,…

Read More

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa kushirikiana na NHIF Mkoa wa Mbeya wamekutana na kundi la watu wenye ulemavu mkoani Mbeya kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kujiunga na Bima ya Afya kwa wote.

Akifungua kikao hicho Februari 25, 2026, Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo Dkt. Godlove Mbwanji alisema lengo ni kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata uelewa wa bima hiyo, kwani ni miongoni mwa makundi maalumu yaliyopewa kipaumbele na Serikali ya Awamu ya Sita katika utekelezaji wa sheria ya Bima ya Afya kwa wote.

Msimamizi wa NHIF mkoa wa Mbeya, Bw. Nicolaus Mwangomo, alieleza kuwa washiriki walipatiwa elimu kuhusu utaratibu wa uchangiaji, faida na dhana ya bima hiyo, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya Bima ya Afya kwa wote.

Kwa niaba ya washiriki, Bi. Rebecca Ramadhani alishukuru kwa elimu hiyo akisema itasaidia watu wenye ulemavu kukabiliana na changamoto za matibabu na kuboresha upatikanaji wa huduma za afya.

Read More

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato Mbeya-Katika hatua kubwa ya mapinduzi ya kidigitali, Serikali iko katika hatua za mwisho kukamilisha zoezi la kuunganisha mifumo yake ili iweze kusomana na kubadilishana taarifa kwa ufanisi nchi nzima. Hatua hiyo inalenga kuimarisha mazingira ya biashara kupitia maboresho ya teknolojia na kupunguza urasimu katika utoaji wa huduma. Kuunga mkono mageuzi hayo, Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) imezindua mafunzo ya wiki moja mkoani Mbeya kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa utoaji wa Vyeti vya Usaili (Certificate of Origin) kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP). Mafunzo hayo yanahusisha mikoa 14 ikiwemo…

Read More

 Na Mwandishi wetu, Ruvuma Wapiga Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe.Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika. “Kati yao…

Read More

Dar Es Salaam Serikali itaendelea kukiimarisha Chuo cha Ustawi wa Jamii ili kiendelee kuzalisha wataalamu wenye uwezo wa kukabiliana na changamoto za kijamii na kuchangia maendeleo ya taifa, sambamba na kuboresha miundombinu na mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi. Akizungumza wakati wa ziara yake katika Chuo hicho mkoani Dar Es Salaam, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema, Serikali inatambua nafasi ya Chuo hicho katika kuandaa wataalamu wa ustawi wa jamii watakaosaidia kuimarisha huduma za kijamii nchini ambapo Serikali itaendelea kushirikiana na uongozi wa Chuo hicho pamoja na wadau mbalimbali kuhakikisha changamoto…

Read More