Author: Mbeya Yetu

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) ameshiriki Mkutano wa 67 wa Mawaziri wa Afya kutoka nchi 9 wanachama za Jumuiya ya Afya ya Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika (ECSA-HC) unaofanyika Ezulwini, Ufalme wa Eswatini tarehe 2-3 Februari, 2026. Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo umejadili mikakati ya kuimarisha mifumo ya afya ya nchi wanachama wa ECSA-HC, hususan kwa kuzingatia mabadiliko yanayoendelea duniani kote yaliyopelekea kupungua au kusitishwa kabisa kwa upatikanaji wa fedha za kufadhili miradi ya afya kutoka kwa wafadhili waliozoeleka.…

Read More

Mbunge wa Jimbo la Lupa, Mhe. Masache Kasaka, akichangia Mpango wa Maendeleo wa Serikali 2026/27 bungeni, amepongeza Serikali kwa mwelekeo mzuri wa mpango huo na kusisitiza umuhimu wa kuimarisha miundombinu ya usambazaji wa umeme, hususan Chunya. Ameshauri ujenzi wa kituo cha umeme (substation) na upanuzi wa umeme kwenye maeneo ya wachimbaji ili kupunguza gharama za uendeshaji, kuongeza uzalishaji, na kuchochea ukuaji wa sekta ya madini na sekta binafsi kwa ujumla.

Read More

Mbunge wa Jimbo la Mbarali, Mhe. Bahati Kenneth Ndingo, amekabidhi mashuka kwa Kituo cha Afya Utengule ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Maadhimisho hayo yamefanyika katika Kata ya Utengule Usongwe, wilayani Mbarali.

Hatua hiyo inalenga kuboresha mazingira na huduma kwa wagonjwa wanaofika kupata matibabu katika kituo hicho cha afya. Baadhi ya wananchi wameeleza kuwa msaada huo utasaidia kupunguza changamoto zilizokuwepo awali na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya.

Read More

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la CARE wametoa mafunzo kwa wawezeshaji wa ngazi ya jamii kuhusu mabadiliko ya tabia nchi katika mkoa wa Mbeya, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Ustahimilivu Wake, Dunia Yetu. Mradi huo unatekelezwa katika vijiji 300 vya mikoa ya Mbeya, Njombe na Iringa kwa lengo la kuimarisha uwezo wa jamii kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi pamoja na kuboresha utunzaji wa mazingira. Katika mkoa wa Mbeya, mafunzo hayo yamefanyika kwa siku tatu wilayani Mbarali, kijiji cha Chimala, yakilenga zaidi wakulima na wafugaji ili kuwajengea uelewa kuhusu…

Read More

Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Mjini imefanya matembezi ya amani leo, ikiwa ni sehemu ya ufunguzi rasmi wa maadhimisho ya miaka 49 tangu kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi, kilichoasisiwa Februari 5 mwaka 1977. Akizungumza mara baada ya matembezi hayo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mbeya Mjini, Emmanuel Mwalupindi, amewataka wanachama wa chama hicho kuondoa hofu na uoga katika kukitumikia chama chao, akisisitiza kuwa CCM ni chama chenye misingi imara na historia kubwa ya kulihudumia Taifa. Kwa upande wake, Katibu wa Shirikisho la Walimu wa CCM Mkoa wa Mbeya, Daud Siame, ametumia…

Read More