Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
- WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI
- SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA
- INEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO
- INEC YAWAPIGA MSASA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA PERAMIHO, SHIWINGA
- MAHUNDI AONYA VIJANA KUTELEKEZA WAZAZI WAO
- NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATEMBELEA MAKAZI YA WAZEE, ASISITIZA UPENDO NA MATUNZO KWAKUWA WAZEE NI TUNU YA TAIFA.
- DKT. MARY MWANJELWA ATOA USHUHUDA MZITO KWENYE MAZISHI YA ULIMBOKA MWAKILILI
Author: Mbeya Yetu
Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato Mbeya-Katika hatua kubwa ya mapinduzi ya kidigitali, Serikali iko katika hatua za mwisho kukamilisha zoezi la kuunganisha mifumo yake ili iweze kusomana na kubadilishana taarifa kwa ufanisi nchi nzima. Hatua hiyo inalenga kuimarisha mazingira ya biashara kupitia maboresho ya teknolojia na kupunguza urasimu katika utoaji wa huduma. Kuunga mkono mageuzi hayo, Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) imezindua mafunzo ya wiki moja mkoani Mbeya kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa utoaji wa Vyeti vya Usaili (Certificate of Origin) kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP). Mafunzo hayo yanahusisha mikoa 14 ikiwemo…
Na Mwandishi wetu, Ruvuma Wapiga Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe.Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika. “Kati yao…
Dar Es Salaam Serikali itaendelea kukiimarisha Chuo cha Ustawi wa Jamii ili kiendelee kuzalisha wataalamu wenye uwezo wa kukabiliana na changamoto za kijamii na kuchangia maendeleo ya taifa, sambamba na kuboresha miundombinu na mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi. Akizungumza wakati wa ziara yake katika Chuo hicho mkoani Dar Es Salaam, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema, Serikali inatambua nafasi ya Chuo hicho katika kuandaa wataalamu wa ustawi wa jamii watakaosaidia kuimarisha huduma za kijamii nchini ambapo Serikali itaendelea kushirikiana na uongozi wa Chuo hicho pamoja na wadau mbalimbali kuhakikisha changamoto…
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 23, 2026 ametembelea mafunzo ya Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma na kuzungumza nao ambapo amewasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa weledi kwa kufuata Sheria, Kanuni na maelekezo ya Tume. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 23, 2026 ametembelea mafunzo ya Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma…
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza leo Februari 22, 2026 na washiriki wa mafunzo ya makarani waongozaji wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Peramiho unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026. Na Waandishi wetu, Ruvuma na Songwe Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewataka Makarani Waongozaji wapiga kura katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma kutekeleza majukumu yao bila woga kwa kufuata Sheria, Kanuni, maelekezo ya Tume. Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC),…
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amewasihi watu wenye uwezo kuwatunza wazazi na ndugu ili kuenzi mchango wao katika jamii. Mhandisi Mahundi amesema hayo wakati wa ziara ya kutembelea makazi ya wazee yanayomilikiwa na taasisi binafsi ya Tushikamane Pamoja Foundation,Kwembe, Manispaa ya Ubungo Jijini Dar Es Salaam ambapo amesema jamii inapaswa kubadili mtazamo na kuhakikisha wazee wanapewa upendo, ulinzi na matunzo wanayostahili bila kujali changamoto zilizopita. Ameeleza kwamba hata kama walipitia changamoto au walikosewa, ni muhimu kulipa kwa wema na si kwa mabaya, kwa sababu wazee ni tunu ya taifa na…
