Author: Mbeya Yetu

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya, Ndg. Patrick Mwalunenge, amelalamikia uamuzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na Bodi ya Ligi kuufungia mara kwa mara Uwanja wa Sokoine licha ya kufanyiwa maboresho.

Amesema hatua hiyo inawanyima wananchi wa Mbeya burudani ya mpira pamoja na kuathiri fursa za kiuchumi kwa wafanyabiashara wadogo wanaotegemea mechi kubwa, hususan zinazohusisha timu za Simba SC na Young Africans S.C..

Mwalunenge ameitaka TFF kutoa maelezo ya wazi kuhusu sababu za kuendelea kuufungia uwanja huo ili kuondoa sintofahamu kwa wananchi.

Read More

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma, Machi 8, 2026 amemtembelea na kumjulia hali mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi, Zahir Ally Zorro, nyumbani kwake Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Katika ziara hiyo, Mhe. Mwinjuma alimkabidhi Mzee Zorro shilingi milioni 10 taslimu ikiwa ni salamu za pole na faraja kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akimtakia apone haraka.

Read More

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Maryprisca Mahundi amewahimiza wanawake Mkoani Mbeya kuendelea kusimama imara kupinga vitendo vya ukatili na kuimarisha malezi bora ya watoto. Mhe, Mahundi amesema hayo Machi 08, 2026 katika sherehe iliyoandaliwa na kundi la Wanawake wa Dhahabu kutoka Wilaya ya Chunya ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya wanawake. Mhe. Mahundi amesema siku hiyo iwe ukumbusho kwa wanawake juu ya wajibu wao wa kulea na kuwajenga watoto katika misingi sahihi ya maadili, mila na tamaduni za Kitanzania ili waweze kukua wakiwa raia wema na wenye mchango chanya katika jamii. Katika…

Read More

Wanawake wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Mbeya wameadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa kutembelea kituo cha kulea watoto wenye mahitaji maalum cha Funguka Foundation kilichopo Mtaa wa Wasai, Kata ya Ilomba, na kukabidhi msaada wa mashine ya kufulia nguo ili kusaidia shughuli za malezi ya watoto wanaolelewa katika kituo hicho. Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Kisa Ngoloke alisema waliguswa na juhudi za mama mlezi wa kituo hicho anayewahudumia watoto wenye ulemavu wa akili, viungo na usonji, akieleza kuwa kazi anayofanya ni kubwa na inahitaji moyo wa kujitoa. Alisema waliona ni vyema kufika kituoni hapo ili…

Read More

Wanawake wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoa wa Mbeya wameadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa kutembelea kituo cha kulea watoto wenye mahitaji maalum cha Funguka Foundation kilichopo Mtaa wa Wasai, Kata ya Ilomba, na kukabidhi msaada wa mashine ya kufulia nguo ili kusaidia shughuli za malezi ya watoto wanaolelewa katika kituo hicho.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Kisa Ngoloke alisema waliguswa na juhudi za mama mlezi wa kituo hicho anayewahudumia watoto wenye ulemavu wa akili, viungo na usonji, akieleza kuwa kazi anayofanya ni kubwa na inahitaji moyo wa kujitoa. Alisema waliona ni vyema kufika kituoni hapo ili kushirikiana na watoto hao pamoja na kumpa moyo mlezi huyo, huku wakiamini kuwa msaada walioutoa utasaidia kurahisisha kazi ya kuwahudumia watoto hao.

Kwa upande wake Meneja wa kituo hicho, Nelly Elisha, aliwashukuru wanawake hao kwa msaada huo akisema utasaidia kupunguza changamoto aliyokuwa akikabiliana nayo ya kufua nguo nyingi za watoto, kazi ambayo mara nyingi alikuwa akiifanya mwenyewe. Alisema kituo hicho kinahudumia jumla ya watoto 78 wakiwemo yatima pamoja na wenye ulemavu wa akili, viungo na usonji, ambapo baadhi yao hulala kituoni huku wengine wakiletwa asubuhi na kurudishwa nyumbani jioni.

Naye Afisa Mtendaji wa Kata ya Ilomba, Regina Kichwika, aliishukuru taasisi hiyo kwa msaada huo na kueleza kuwa kituo hicho bado kina mahitaji mbalimbali, hivyo akatoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kusaidia ili kuboresha huduma kwa watoto hao.

Aidha, Kichwika aliwataka wazazi kuacha tabia ya kuwaficha watoto wenye ulemavu majumbani, akisisitiza kuwa kuwatoa na kuwaonesha kwenye jamii kunasaidia kupata msaada pamoja na kuhakikisha wanapata haki zao za msingi.

Read More

Sheikh Ibrahim Bombo amempongeza Mbunge wa Jimbo la Uyole na Rais wa Inter‑Parliamentary Union (IPU) Tulia Ackson kwa kuandaa futari iliyowakutanisha wananchi mbalimbali nyumbani kwake.

Akizungumza wakati wa futari hiyo, Sheikh Bombo alimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwakutanisha watu wa makundi tofauti na kueleza kuwa kitendo cha kuwakaribisha wananchi kufuturu pamoja ni ishara ya moyo wa kujitolea na kuwajali wananchi.

Alisema watu waliopata futari hiyo wakiwemo wazee, wanawake, watoto na viongozi wa dini wanapoendelea kusema “Alhamdulillah”, baraka zake humrudia pia aliyeandaa futari hiyo.

Sheikh Bombo alimuombea Tulia Ackson aendelee kupewa nguvu, afya na ulinzi ili kuendelea kuwahudumia wananchi, huku akiwataka viongozi wengine kuiga moyo wa ukarimu na huduma kwa jamii.

Read More

Mbunge wa Jimbo la Mbarali mkoani Mbeya, Bahati Ndingo, amesema maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni fursa ya kutathmini hatua zilizopigwa katika kuimarisha usawa wa kijinsia na kuhamasisha jamii kuendelea kuwapa wanawake na wasichana nafasi ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Akizungumza Machi 6, 2026 katika maadhimisho ya siku hiyo yaliyofanyika kiwilaya katika Kata ya Igurusi, Ndingo alisema Tanzania imepiga hatua kubwa kwa kumpa mwanamke nafasi ya juu ya uongozi nchini, akimtaja Rais Samia Suluhu Hassan kama mfano wa mafanikio ya wanawake katika uongozi.

Aidha, alisisitiza kuwa maadhimisho hayo hayalengi kujisifia bali kutambua mchango wa wanaume na wanawake katika kubadilisha mtazamo wa jamii kuhusu uwezo wa mtoto wa kike. Aliongeza kuwa mtoto wa kike ana uwezo wa kufanya kazi na majukumu yoyote kama ilivyo kwa mwanaume.

Maadhimisho hayo ni sehemu ya maandalizi ya kilele cha Siku ya Wanawake Duniani kinachoadhimishwa kila mwaka Machi 8.

Read More

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewataka wadau mbalimbali mkoani Mbeya kuendelea kushirikiana na kituo cha kulea watoto wenye usonji cha Funguka Foundation kilichopo Kata ya Ilomba, ili kusaidia juhudi za malezi na huduma kwa watoto wenye mahitaji maalum. Mhe. Mahundi ametoa wito huo alipofanya ziara katika kituo hicho Machi 07, 2026. Amesema kazi ya kulea na kuwahudumia watoto wenye mahitaji maalum ni jukumu la pamoja la jamii, hivyo kuna umuhimu wa wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia vituo vinavyotoa huduma hizo. “Ni muhimu kwa wadau na jamii kwa ujumla kushirikiana kusaidia vituo…

Read More

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya na Mbunge, Patrick Mwalunenge, amepongeza juhudi za Jumuiya ya Wanawake wa Mbeya Zonal Referral Hospital (MZRH) kwa kutoa zawadi ya mashine ya kisasa ya kupima umeme wa kichwa (EEG) yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 67, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Samia Suluhu Hassan katika kuboresha huduma za afya nchini. Akizungumza kama Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika hospitalini hapo, Mwalunenge alisema hatua ya wanawake hao ni mfano wa uzalendo na mshikamano katika kuunga mkono maendeleo ya sekta ya afya. Amesema mchango huo…

Read More