Author: Mbeya Yetu

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewataka wadau mbalimbali mkoani Mbeya kuendelea kushirikiana na kituo cha kulea watoto wenye usonji cha Funguka Foundation kilichopo Kata ya Ilomba, ili kusaidia juhudi za malezi na huduma kwa watoto wenye mahitaji maalum. Mhe. Mahundi ametoa wito huo alipofanya ziara katika kituo hicho Machi 07, 2026. Amesema kazi ya kulea na kuwahudumia watoto wenye mahitaji maalum ni jukumu la pamoja la jamii, hivyo kuna umuhimu wa wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia vituo vinavyotoa huduma hizo. “Ni muhimu kwa wadau na jamii kwa ujumla kushirikiana kusaidia vituo…

Read More

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya na Mbunge, Patrick Mwalunenge, amepongeza juhudi za Jumuiya ya Wanawake wa Mbeya Zonal Referral Hospital (MZRH) kwa kutoa zawadi ya mashine ya kisasa ya kupima umeme wa kichwa (EEG) yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 67, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Samia Suluhu Hassan katika kuboresha huduma za afya nchini. Akizungumza kama Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika hospitalini hapo, Mwalunenge alisema hatua ya wanawake hao ni mfano wa uzalendo na mshikamano katika kuunga mkono maendeleo ya sekta ya afya. Amesema mchango huo…

Read More

Dar es Salaam-Wakinamama waliolazwa katika wodi ya wanawake ya Hospitali ya Sinza jijini Dar es Salaam wamepatiwa msaada wa Comfy Mum pants uliotolewa na kampuni ya Comfy Mum kwa kushirikiana na Chemba ya Taifa ya Biashara (TNCC), ikiwa ni sehemu ya kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani na kuonyesha upendo na kujali afya ya wanawake katika jamii. Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa Comfy Mum, Bi. Irene Mville alisema kampuni hiyo imeona umuhimu wa kushiriki katika kuunga mkono wanawake, hususan waliotoka kujifungua na wanaokabiliwa na changamoto ya hedhi nyingi. “Katika kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani,…

Read More

MBUNGE wa Jimbo la Mbeya Mjini (CCM), Mhe. Patrick Mwalunenge amekutana na viongozi wa vyama vya upinzani kwa ajili ya kujadili masuala ya kisiasa mkoani Mbeya na maendeleo ya wananchi wa mkoa huo. Katika kikao hicho kimefanyika leo Machi 5,2026 katika ukumbi wa Mkulu ambapo viongozi hao walibadilishana mawazo kuhusu hali ya kisiasa mkoani Mbeya, pamoja na namna bora ya kuimarisha ushirikiano miongoni mwa vyama vya upinzani. Lengo kuu ni kusukuma mbele ajenda za maendeleo na ustawi wa wananchi. Akizungumza katika kikao hicho, Mbunge Mwalunenge amesisitiza umuhimu wa viongozi wa vyama vya siasa kuweka mbele maslahi ya wananchi badala ya…

Read More

Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Uyole, Dkt. Tulia Ackson, ameunga mkono juhudi za wananchi wa Mtaa wa Bombambili, Kata ya Mwakibete mkoani Mbeya, kwa kuchangia mifuko 100 ya saruji na tripu 10 za mawe kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya zege iliyoanzishwa na wananchi kwa nguvu zao.

Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, vipande viwili vya barabara inayounganisha Kata za Iyela, Mwakibete na Mwasanga vinatarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi milioni 41, ambapo kipande kimoja kimegharimu zaidi ya milioni 23 na cha pili kinakadiriwa kugharimu zaidi ya milioni 18.

Diwani wa Kata ya Mwakibete, Lucas Mwampiki, alimshukuru Dkt. Tulia kwa kuendelea kuunga mkono maendeleo ya kata hiyo, huku akitaja pia msaada wake katika ujenzi wa nyumba inayotarajiwa kukabidhiwa Machi 7, 2026 katika Mtaa wa Itongo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Bombambili, Saidi George Kumbemba, alimpongeza Dkt. Tulia kwa kusaidia wananchi na wadau wanaojitolea kujenga barabara hiyo inayoelekea Makaburi ya Iyela, pamoja na kuendelea kuwatetea katika maendeleo ya miundombinu ya barabara.

Read More

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mzee Rashidi Mfaume Kawawa, mwanasiasa mashuhuri na mmoja wa viongozi waliokuwa karibu sans na xdwa Mwalimu Julius Nyerere katika harakati za uhuru na ujenzi wa taifa. Mzee Kawawa aliyesaliwa tarehe 27 Februari 1926 na kufariki 31 Desemba 2009, alikuwa Waziri Mkuu wa pili wa Tanganyika kuanzia tarehe 22 Januari 1962 hadi 9 Desemba 1962, akichukua nafasi baada ya Julius Nyerere kujiuzulu kwa muda ili kuimarisha chama cha TANU. Baada ya Tanganyika kupata uhuru kamili na kuwa Jamhuri, Mwalimu Nyerere alirejea madarakani kama Rais, ambspi baadaye Mzee Kawawa alikuja kuwa Waziri Mkuu wa…

Read More

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Wilaya ya Mbeya Mjini, Emmanuel Mwalupindi, amekabidhi tuzo na vitabu kwa walimu wa Shule ya Sekondari ya Sangu, shule inayomilikiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), ikiwa ni sehemu ya pongezi kwa kufanya vizuri katika matokeo ya Kidato cha Nne mwaka 2025. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi tuzo hizo iliyofanyika shuleni hapo Mbeya Mjini, Mwalupindi amesema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mzuri kati ya walimu, wanafunzi na wazazi, na ni jambo la kujivunia kuona shule ikiendelea kufanya vizuri kitaaluma. Ameeleza kuwa katika matokeo ya mwaka 2025, shule hiyo haikuwa na mwanafunzi mwenye daraja la…

Read More

Naibu  Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mbeya, Jasper H. Luoga, ametoa taarifa kwa waandishi wa habari mkoani Mbeya akieleza mafanikio na hatua zilizochukuliwa na taasisi hiyo katika kudhibiti rushwa na kulinda rasilimali za umma. Akizungumza katika mkutano huo na vyombo vya habari, alisema TAKUKURU imefanikiwa kuokoa shilingi 107,450,300 kati ya shilingi 125,431,000 ambazo hazikuwasilishwa kwenye akaunti ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali baada ya kukusanywa na watoza ushuru wa halmashauri hiyo. Alisema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kuhakikisha mapato ya umma yanakusanywa na kuwasilishwa kwa usahihi pamoja na kudhibiti ubadhirifu wa…

Read More

Mfumo wa kidigitali wa utoaji wa Vyeti vya Uasili kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP) unaopatikana kupitia tovuti ya tcp.tncc.or.tz unatarajiwa kuanza kutumika rasmi kuanzia Machi 2, 2026, hatua inayolenga kurahisisha na kuharakisha huduma za biashara za kimataifa nchini. Akizungumza mkoani Mbeya wakati wa mafunzo kwa wasafirishaji wa bidhaa kwenda nje (exporters), Makamu wa Rais Kilimo wa Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC), Bw. Swallah Swallah, amewahimiza wafanyabiashara kujiandaa na kuutumia kikamilifu mfumo huo kwa kujisajili na kuwasilisha maombi yao kupitia tcp.tncc.or.tz, ili kuongeza ufanisi katika shughuli zao za kila siku. Alisema kuanza kwa kutumika kwa mfumo huo wa kidigitali…

Read More