Author: Mbeya Yetu

Maafisa Usafirishaji maarufu kama Bodaboda Mkoani Iringa wamelaani kitendo cha baadhi ya vijana kukubali kushawika na kushiriki kwenye vitendo vya uvunjifu wa amani kwa kisingizio cha kwamba ni maandamano ya amani.

Kauli hiyo imetolewa Desemba 11, 2025 na kundi hilo la vijana ambapo wameonyesha kutofurahishwa na vitendo viovu ikiwemo uchomaji wa miundombinu mbalimbali jambo ambalo linapelekea kudhorota kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Read More

Na Mwandishi Wetu, Mbeya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Benno Malisa amewaalika wawekezaji kuwekeza katika mkoa wa Mbeya kwenye fursa za Biashara, Usafirishaji, Viwanda, Ufugaji, Utalii na uwekezaji kwenye mifumo ya Kidijitali. RC Malisa ameyasema hayo kwenye mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu TIA Kampasi ya Mbeya kwenye kilele cha mahafali ya Taasisi hiyo. Jumla ya wahitimu 1480 wa ngazi mbalimbali ya vyeti, Astashahada na Shahada wamehitimu katika Taasisi hiyo. “Nitumie fursa hii kuwakaribisha wawekezaji kuwekeza mkoani kwetu kwenye miradi mikubwa ya kimkakati inayoendelea, imeongeza mvuto wa uwekezaji kutoka ndani na nje ya nchi” Amesema RC Malisa. Aidha RC…

Read More