Author: Mbeya Yetu

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele leo Desemba 29,2025 amesoma risala maalum kuhusu uchaguzi wa ubunge katika jimbo la Siha lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Siha, Mkoa wa Kilimanjaro, Tanzania Bara na Jimbo la Fuoni lililopo Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, Tanzania Zanzibar unaotaraji kufanyika Desemba 30,2025. Jaji Mwambegele amesema, uchaguzi mdogo huo utahusisha pia, kata tano za Tanzania Bara. Kata hizo ni;            Chamwino iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Mkoa wa Morogoro; Mbagala Kuu iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Mkoa wa Dar es Salaam; na Nyakasungwa…

Read More

Wazee wanaoishi katika Makazi ya Wazee na wasiojiweza Bukumbi, wilayani Misungwi mkoani Mwanza, wameishukuru Serikali kwa kuimarisha huduma za ustawi wao, wakisema hatua hiyo imeleta faraja, heshima na matumaini mapya katika maisha yao ya uzeeni.

Mwenyekiti wa Wazee kituoni hapo, Mzee John Nguku amesema wazee wanathamini jitihada Serikali za kuwapatia huduma muhimu kwa wakati.

“Kwa niaba ya wazee wenzangu, tunaishukuru Serikali kwa kutukumbuka tunaishi kwa amani, tunahudumiwa kwa heshima na tunahisi bado tuna thamani katika jamii, tunaomba uangalizi huu uendelee ili wazee wengi zaidi wanufaike maana uzee siyo mzigo bali ni neema”. amesema Mzee John

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amesema Serikali inawatambua wazee kama tunu muhimu ya Taifa na itaendelea kuimarisha huduma za ustawi na ulinzi wao.

Mhe. Mahundi amesema pamoja na jitihada za Serikali, jamii ina wajibu wa msingi wa kuwatunza wazee, huku akiwataka vijana kutowasahau wazazi wao wanapofikia uzee na kuhakikisha wanapata upendo, heshima na msaada unaostahili.

“Nawasihi vijana na jamii kwa ujumla, msije mkawasahau wazazi wenu wanapofikia uzee. Kuwatunza wazee ni wajibu wa familia na ni sehemu ya maadili yetu ya Kitanzania, Serikali itaendelea kuhakikisha wazee wanathaminiwa, wanalindwa na wanapata huduma stahiki bila kubaguliwa. Tunazitaka familia, vijana na jamii kwa ujumla kutambua kuwa kuwajali wazee ni wajibu wa kimaadili na msingi wa ustawi wa Taifa letu” amesema Mhe. Mahundi.

Kwa upande wake, Mfawidhi wa Makazi ya Wazee na wasiojiweza Bukumbi, Vivian Kaiza amesema uangalizi wa Serikali na ushirikiano wa wadau umeendelea kuimarisha utoaji wa huduma kwa wazee waliopo kituoni hapo, Makazi yanaendelea kusimamiwa kwa weledi na kujali maslahi ya wazee, huku akiahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha wazee wanapata huduma stahiki na kuishi kwa amani.

Ziara hiyo ni mwendelezo wa dhamira ya Serikali katika kuimarisha ustawi wa wazee, huku jamii ikihimizwa kushirikiana na Serikali katika kuwatunza wazee ili waishi maisha yenye heshima, upendo na matumaini.

Read More

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (MNEC), Ndele Mwaselela, amewataka waandishi wa habari kuendelea kuzingatia maadili ya taaluma, kuandika habari za maendeleo na kuwasaidia wananchi kwa kuwaseemea, akisisitiza kuwa jamii inawategemea sana waandishi wa habari katika kusikika kwa sauti yao. Mwaselela ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kushtukiza katika Ofisi za Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya (Mbeya Press Club), ambapo alizungumza na baadhi ya waandishi wa habari aliowakuta wakiendelea na majukumu yao ya kila siku ofisini hapo. Akizungumza katika mazungumzo hayo ya ana kwa ana, Mwaselela alisema kuwa waandishi wa habari wana nafasi ya kipekee…

Read More

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Furaha Mwile Nyelele, mkazi
wa Kijiji cha Shilanga kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wa jirani yake
aliyekuwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Shilanga darasa la saba
aitwaye Boniventure Elia Lazaro [12] mkazi wa Shilanga.
Awali kabla ya tukio hilo tarehe 21.12.2025 saa 10:15 jioni huko Kijiji cha
Shilanga, Kata ya Ilembo, Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Mbeya Vijijini
mtuhumiwa Furaha Mwile Nyelele alimpiga kwa kipande cha mti kichwani
mtoto Boniventure Elia Lazaro [12] ambaye kwa sasa ni marehemu na
kumsababishia jeraha ambapo alikimbizwa katika Hospitali Teule ya Ifisi
kwa matibabu.
Tarehe 22.12.2025 saa 6:30 mchana akiwa anaendelea kupatiwa matibabu
katika Hospitali Teule ya Ifisi alifariki dunia. Uchunguzi wa awali umebaini
kuwa chanzo cha tukio hili ni kujichukulia sheria mkononi baada ya
mtuhumiwa kumtuhumu mtoto kuiba mayai ya kuku.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa kwa jamii kuacha tabia ya
kujichukulia sheria mkononi ili kuepuka madhara. Aidha, wazazi na walezi
wanakumbushwa kuzingatia suala la ulinzi na usalama wa mtoto kwa
kuhakikisha haki za mtoto zinaheshimiwa na kulindwa.

Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.

Read More

Serikali imesisitiza umuhimu wa jamii kuimarisha maadili na uzalendo miongoni mwa vijana nchini kwa kutumia taasisi za elimu ili kujenga taifa lenye misingi imara ya utu, uwajibikaji. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, akiwa mgeni rasmi katika Mdahalo wa maadili na uzalendo uliofanyika katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Buhare, mkoani Mara. Mhe. Mahundi amesema, Serikali ya Awamu ya Sita inaamini kuwa maendeleo ya kweli ya taifa hayawezi kupatıkana bila kujenga maadili ya wananchi wake, hususan vijana ambao ndiyo nguvu kazi na viongozi wa baadaye. “Huwezi kujenga…

Read More

Mbunge wa Jimbo la Uyole, Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson (@tulia.ackson), ameendelea kutoa sadaka kwa familia zisizo na uwezo katika kipindi cha kuelekea sikukuu ya Krismasi kwa kutoa chakula na fedha.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Dkt. Tulia amesema ushirikiano mzuri kati ya viongozi wa mitaa na wananchi ndiyo umefanikisha kuwatambua walengwa sahihi, akibainisha kuwa leo ilikuwa zamu ya Kata ya Ilemi, ambapo kaya 13 zimenufaika, huku jumla ya kaya 130 zikitarajiwa kupata msaada huo katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Uyole.

Ameongeza kuwa zoezi hilo ni endelevu na litaendelea katika kata nyingine kadri ratiba itakavyoruhusu, kwa lengo la kuwafikia wananchi wenye uhitaji mkubwa zaidi.

Read More