Author: Mbeya Yetu

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Ndugu Kailima R.K, amefunga kikao cha siku mbili cha Tume na Vyama vya Siasa 18 vyenye usajili kamili na ambavyo vimependekeza wagombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania  na Makamu wa Rais, kwa lengo la kujadili na kupanga kwa pamoja ratiba ya kampeni za vyama hivyo.    Kikao hicho kilichoketi Agosti 25 na 26, 2025  kilishirikisha vyama vya Civic United Front (CUF), National Convention for Construction and Reform (NCCR-Mageuzi), Union for Multiparty Democracy (UMD), Chama cha Mapinduzi (CCM), National League for Democracy (NLD), United Peoples’…

Read More

Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma Taifa, Ipyana Samson Njiku, leo Tarehe 25/08/2025 amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia chama hicho.
Ipyana amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Uyole kwa uadilifu, uwajibikaji na kusimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amesisitiza kuwa chama chake kimejipanga kutoa mbadala mpya wa kiuongozi unaolenga kuleta matumaini mapya kwa wananchi.

Read More

Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini mkoani Mbeya, Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 25 Agosti 2025, amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya wananchi wa Jimbo jipya la Uyole katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu. Dkt. Tulia amechukua fomu hiyo katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya, huku akipokelewa na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), viongozi wa ngazi mbalimbali pamoja na wafuasi wake waliokuwa na shauku kubwa ya kumuona akiendelea kulitumikia Taifa kupitia jimbo hilo jipya. Aidha, amewataka wananchi wa Uyole kuungana naye katika safari ya maendeleo,…

Read More