Author: Mbeya Yetu

Mbeya – Mwenyekiti wa Kongamano na Mgoda wa Kigoda cha Uprofesa cha Mwalimu J.K. Nyerere katika Taaluma za Umajumui wa Afrika, Profesa Alexander Makulilo, amezungumza na waandishi wa habari mkoani Mbeya akitoa mwito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika maandalizi ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Prof. Makulilo alizungumza leo wakati akitoa taarifa rasmi kuhusu Kongamano la Uchumi Jumuishi kuelekea Dira 2050, ambalo limeandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia Kigoda cha Uprofesa cha Mwalimu J.K. Nyerere kwa kushirikiana na Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP Centre). Kongamano hilo limepangwa…

Read More

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Jabiri Omari Makame leo tarehe 15/09/2025 amezindua rasmi huduma mkoba za Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia mkoani Songwe ikiwa ni juhudi za Serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhakikisha huduma bora za afya zinawafikia wananchi wote kwa ukamilifu. Katika hotuba yake, Mhe. Jabiri Makame ameeleza kuwa ujio wa kambi hiyo ya Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia ni ishara ya dhamira ya dhati ya Serikali ya kuimarisha huduma za afya mkoani Songwe. Amebainisha kuwa, kuanzia mwaka 2020 hadi 2025, mkoa umepata maendeleo makubwa ikiwa ni pamoja na…

Read More

Mbozi, Tanzania —  Na Mwandishi WETU 13/09/2023 Katika hatua muhimu ya kupunguza upofu unaepukika, Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) na Shirika Helen Keller International leo  wamewasili mkoani Songwe kwaajili ya kutoa Huduma Mkoba ya matibabu ya ugonjwa wa mtoto wa jicho “Cataract Management” kwa wananchi takribani 700 wa Songwe katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi (Vwawa). Akiongea na waandshi wa habari, Dkt. Jofrey Josephat Mratibu wa Huduma za macho Mkoa wa Songwe ameeleza kuwa kambi hiyo ya siku 6 imelenga kukabiliana na magonjwa ya mtoto wa jicho vilevile kusogeza huduma hizo adimu katika maeneo ya karibu na wanapoishi…

Read More