Author: Mbeya Yetu

Maafisa Usafirishaji maarufu kama Bodaboda Mkoani Iringa wamelaani kitendo cha baadhi ya vijana kukubali kushawika na kushiriki kwenye vitendo vya uvunjifu wa amani kwa kisingizio cha kwamba ni maandamano ya amani.

Kauli hiyo imetolewa Desemba 11, 2025 na kundi hilo la vijana ambapo wameonyesha kutofurahishwa na vitendo viovu ikiwemo uchomaji wa miundombinu mbalimbali jambo ambalo linapelekea kudhorota kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Read More

Na Mwandishi Wetu, Mbeya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Benno Malisa amewaalika wawekezaji kuwekeza katika mkoa wa Mbeya kwenye fursa za Biashara, Usafirishaji, Viwanda, Ufugaji, Utalii na uwekezaji kwenye mifumo ya Kidijitali. RC Malisa ameyasema hayo kwenye mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu TIA Kampasi ya Mbeya kwenye kilele cha mahafali ya Taasisi hiyo. Jumla ya wahitimu 1480 wa ngazi mbalimbali ya vyeti, Astashahada na Shahada wamehitimu katika Taasisi hiyo. “Nitumie fursa hii kuwakaribisha wawekezaji kuwekeza mkoani kwetu kwenye miradi mikubwa ya kimkakati inayoendelea, imeongeza mvuto wa uwekezaji kutoka ndani na nje ya nchi” Amesema RC Malisa. Aidha RC…

Read More

Meya wa Jiji la Mbeya, Dourmohamed Issa, ameonyesha kukerwa na kasi ndogo ya ujenzi wa soko la Tandale na stendi, akisema mradi umesimama licha ya mkandarasi kuongezewa muda mara kadhaa.

Amesema mradi huo ulipaswa kukamilika mwezi Agosti, lakini hadi sasa — Desemba — kazi haijaonyesha maendeleo, huku mkandarasi akitoa sababu dhaifu kama ukosefu wa vifaa.

Meya Issa amesema serikali tayari imetoa zaidi ya bilioni 12, hivyo hakutakiwi kuwe na visingizio, na ametaka kasi iongezeke mara moja vinginevyo hatua kali zitachukuliwa.

Read More

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amewashukuru watanzania kwa kuonyesha utulivu na uzalendo katika kuilinda amani ya Tanzania na kudumisha utulivu wakati nchi ikienda kuazimisha miaka 64 ya Uhuru wa Tanzania Bara…..

Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa ukaguzi wa hali ya ulinzi na usalama katika mitaa mbalimbali ya jijini Dar es Salaam huku Vyombo vya Ulinzi na usalama vikiendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo tofauti nchini ambapo wananchi nao wametoa maoni yao.

Read More

Na WAF, Dar es Salaam.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepanga kuwatibu watu 760 wasio na uwezo wa kumudu gharama za matibabu ambapo shilingi Bilioni 6.7 zimetengwa kwa kazi hiyo kwa mwaka wa fedha 2025/26

Hayo yameibainishwa na Waziri wa Afya Mhe. Mohamed Mchengerwa Desemba 8, 2025 alipokuwa akizungumza na watumishi wa Sekta ya Afya ngazi ya Wizara waliopo mkoa wa Dar es Salaam kwenye kikao kazi kilichofanyika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

“Kutokana na faida kubwa iliyopatikana kwa mwaka 2024/25 ambapo jumla ya wagonjwa 677 walinufaika kwa huduma za kibobezi kama kupandikizwa Uloto watoto wenye Sikoseli, Kupandikizwa figo, upasuaji wa moyo, uapndikizaji wa vifaa vya usikivu kwa watoto, matibabu ya Saratani, upandikizaji wa nyonga, Rais Samia ameridhia kuwa na bajeti husika,” amefafanua Waziri Mchengerwa.

Waziri Mchengerwa amesema Rais Samia anadhamira ya dhati ya kuboresha Afya za wananchi kwakuhakikisha kila mwananchi uhitaji wa huduma za kibingwa anapata huduma hizo pasipo na kikwazo cha fedha. @wizara_afyatz @mohamed_mchengerwa

Read More