Author: Mbeya Yetu

Na Woinde Shizza, Arusha Serikali imepiga kengele ya tahadhari kufuatia ongezeko la madai feki ya bima yanayodaiwa kuisababishia nchi hasara ya mabilioni, huku ikiweka wazi kuwa asilimia 10 hadi 15 ya madai hayo duniani yana chembechembe za udanganyifu. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Dk. Sada Mkuya, amesema hali hiyo imeifanya sekta ya bima kupoteza uaminifu wa umma na kuathiri utoaji wa huduma kwa wateja wa kweli wanaohitaji msaada halali. Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, wakati wa mkutano wa wataalamu wa udhibiti wa udanganyifu wa bima (IASIU), Dk. Sada alisema baadhi…

Read More

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza na Watendaji wa Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wakati alipotembelea mafunzo ya siku moja ya watendaji hao ambayo yanahusisha waandikishaji wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki kutoka Kata zote za Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani. Zoezi la uboreshaji awamu ya pili linataraji kuanza Mei 16 hadi 22, 2025 sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali la Wapiga Kura na vituo vitafunguliwa kuanzia Saa 2:00 asubuhi hadi Saa 12:00 jioni.  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe.…

Read More

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amesema kuwa Wizara inaendelea kushirikiana kwa karibu na Jeshi la Polisi katika kukabiliana na vitendo vya utapeli mtandaoni, hasa vinavyofanyika kupitia huduma za simu na miamala ya kifedha (SimBanking). Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Fakharia Shomari Khamisi (Mb.), katika kikao cha Bunge kilichofanyika jijini Dodoma, Mhandisi Mahundi alisema ongezeko la matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) limeleta manufaa makubwa kwa taifa katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa, huku pia likizua changamoto mbalimbali ikiwemo uhalifu wa mtandaoni. Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka…

Read More

Lusaka, Zambia – Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Mhe. Lt Gen Mathew Edward Mkingule, amekutana na kufanya mazungumzo na timu ya wataalamu kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, waliofika Ubalozini leo tarehe 12 Mei, 2025 asubuhi kwa ajili ya kujitambulisha. Wataalamu hao wapo nchini Zambia kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu na wataalamu wa Hospitali ya Kufundishia ya Zambia (University Teaching Hospital – UTH) kuhusu huduma ya uchujaji wa damu kwa njia tumbo (Peritoneal Dialysis). Katika mazungumzo yake na ujumbe huo Mhe. Balozi Lt Gen Mathew Edward Mkingule aliwakaribisha wataalamu hao waliobeba bendera ya Tanzania, akisema kuwa ni…

Read More

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma leo Mei 12, 2025 ambapo Tume imetangaza kugawanywa kwa majimbo na kubadilisha majimbo. Na. Mwandishi Wetu, Dodoma Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imeanzisha majimbo mapya nane na kubadilisha majina ya majimbo 12 ya uchaguzi yatakayotumika kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika oktoba mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo tarehe 12 Mei, 2025 Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele amesema Tume imefikia uamuzi huo…

Read More