Author: Mbeya Yetu

*SAFARI YENYE TABASAMU KATA YA ILEMI.*

Kazi inaendelea pale ilipoishia katika kusambaza Tabasamu Kwa Wananchi wa Jimbo la Uyole Ndani ya kata Ya Ilemi Mkoani Mbeya.

Familia ya Anyomwisye Mwalyaje inaenda Kutabasamu, hii ni baada ya kukutana na changamoto ya nyumba ambayo walikuwa wakiishi kupata ajali ya Moto Septemba 05, 2025.

Kama kawaida ya Taasisi ya Tulia Trust chini ya mkurugenzi wake ambae ni Mbunge Jimbo la Uyole na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani(IPU) Mh. Dkt. Tulia Ackson imedhamiria kurudisha Tabasamu Kwa familia hiyo.

@tuliatrust_tz
@tulia.ackson

#TuliaTrustNaJamii
#TabasamishaNaTuliaTrust
#TuliaTrustMtaaniKwetu

Read More

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mhe. Patrick Mwalunenge, ameendelea kuwawezesha vijana wa bodaboda jijini Mbeya kwa kutoa msaada katika vijiwe mbalimbali.

Katika ziara hiyo, ametoa bodaboda moja kwa vijana wa kijiwe cha Nzovwe, pamoja na mtaji wa mafuta wa shilingi 40,000 kwa kila kikundi alichotembelea. Aidha, ameacha shilingi 400,000 kwa ajili ya kuwaendeleza vijana wengine.

Mhe. Mwalunenge amewahimiza vijana kuwa watulivu na wavumilivu wakati serikali ikiendelea kuweka mikakati madhubuti ya kuwawezesha kupitia fursa za kiuchumi.

Read More