Author: Mbeya Yetu

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa na baadhi ya Wadhamini wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yaliyozinduliwa Oktoba 10,2025 akiwemo Meneja Mahusiano Mwandamizi wa NMB Josephine Kulwa wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Vijana katika Soko la Uhindini jijini Mbeya. Baadhi ya wanafunzi na wananchi waliohudhuria ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana Oktoba 10,2025 katika Viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya wakifuatilia kwa karibu hotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa aliyekuwa mgeni rasmi. Wanafunzi wa shule ya Sekondari wasichana Loleza waliotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya Vijana viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya.…

Read More

Mgombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Ipyana Samson Njiku, ameendelea na kampeni zake za mguu kwa mguu kwa  wananchi wa Jimbo la Uyole, ambapo leo ametembelea maeneo ya Kata ya Itezi na Igawilo akiwahamasisha wananchi kujiandaa kwa mabadiliko chanya kupitia uongozi makini na wenye dira ya maendeleo. Akizungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali , Njiku amesema kuwa endapo atapata ridhaa ya wananchi wa Uyole, ataweka kipaumbele katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo: Ujenzi wa Soko la Kisasa na Kimataifa litakalowezesha wakulima na wafanyabiashara kuuza mazao yao ndani na nje ya nchi…

Read More

Shirika la Posta Tanzania (TPC) kupitia Ofisi yake ya Mkoa wa Mbeya, limeadhimisha Wiki ya Posta Duniani kwa kufanya shughuli za kijamii ikiwemo kukabidhi msaada wa vyandarua katika Hospitali ya Wilaya ya Igawilo, Jijini Mbeya. Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Meneja wa Shirika la Posta Mkoa wa Mbeya, Amos Millinga, alisema kuwa wiki hiyo imelenga kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma mbalimbali za Posta, sambamba na kuadhimisha Siku ya Posta Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 9 Oktoba. “Wiki hii tumeendesha programu maalum inayolenga kutoa uelewa wa huduma zetu za Posta. Lakini sambamba na hilo, tunasherehekea Siku ya Posta Duniani…

Read More

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Meneja Mahusiano Idara ya Wateja Binafsi – Luiana Keenja, alipotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya Vijana katika viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya katikati ni Meneja Mauzo Kanda Nyanda za Juu Ungandeka Mwakatage. WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete ameipongeza Benki ya NMB kwa kuendelea kuwa karibu na Wananchi kwa kusogeza huduma kwa watu wa maeneo ya pembezoni. Kikwete ameongea hayo alipotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya…

Read More