Author: Mbeya Yetu

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Mhe. Patali Shida Patali, amesema Serikali imetoa zaidi ya shilingi milioni 250 kwa ajili ya matengenezo ya barabara ya Igyoma–Ilambo (takribani km 9), ambapo mkandarasi tayari ameanza kazi ili kuwezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za kiuchumi.

Amesema pia fedha zimetolewa kwa ajili ya ukarabati wa barabara ya Isionje–Kikondo ambayo imekuwa na changamoto kubwa wakati wa mvua, huku mkandarasi akiwa tayari eneo la kazi na hali ya barabara ikionekana kuimarika ikilinganishwa na miaka iliyopita.

Akizungumzia changamoto ya barabara iliyo karibu na Shule ya Maadilisho Irambo, Mhe. Patali amesema hakuna mgogoro bali kuna taratibu za kisheria zinazohitajika kufuatwa baada ya barabara hiyo kuhamishwa kutoka TARURA kwenda TANROADS, na kuomba mamlaka husika kuharakisha mchakato huo kwa manufaa ya wananchi.

Kauli hiyo ilitolewa wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, katika Shule ya Maadilisho Irambo mkoani Mbeya.

Read More

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewataka watoto waliopo katika Shule ya Maadilisho Irambo mkoani Mbeya kuchukulia uwepo wao chuoni hapo kama fursa ya mabadiliko chanya na maandalizi ya maisha bora ya baadaye. Akizungumza wakati wa ziara yake shuleni hapo, Mhe. Mahundi alisema watoto hao hawapaswi kujiona tofauti au waliopotea, bali wajione kama vijana wanaojengwa upya ili kuwa raia wema na viongozi wa kesho. “Kuwepo kwenu hapa siyo adhabu bali ni mpango wa Mwenyezi Mungu wa kuwajenga upya. Maadilisho ni mabadiliko ya kweli, na kesho yenu bado ni njema,” alisema Mhe.…

Read More

📌 Aagiza Bweni la Wasichana Chuo cha Maendeleo ya Jamii Uyole likamilishwe kwa wakati. Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amemtaka mkandarasi anayesimamia ujenzi wa bweni la wasichana katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Uyole, Jijini Mbeya, kuhakikisha anakamilisha mradi huo kwa wakati uliopangwa ili kuendana na malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuboresha mazingira ya elimu kwa watoto wa kike. Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi ametoa maagizo hayo wakati alipotembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mabweni hayo, ambayo yamefikia zaidi ya asilimia 90 ya utekelezaji wake huku akisisitiza…

Read More

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalum Mhe.Mhandisi Maryprisca Mahundi ametembelea Kituo cha Tumaini la Wazee kilichopo Kata ya Majengo Jijini Mbeya kwa lengo la kuwapa tabasamu na kuwatia moyo kwa kutoa zawadi mbalimbali. Akiongea na Wazee zaidi ya hamsini wa Kata ya Majengo Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan imeweka mkakati mzuri kwa ajili ya kuwasaidia wazee hususani katika huduma za afya. Kwa upande wake Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Mbeya Salum Manyendi amesema Serikali imedhamiria kuanza kutoa…

Read More

Mdau wa Maendeleo nchini Ndele Mwaselela amewataka Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya kuandika habari zitakazosaidia kutatua changamoto za wananchi ili serikali iweze kuzitatua kwa wakati. Ndele ameyasema hayo Jijini Mbeya katika kikao maalumu cha kutathimini mahusiano ya waandishi wa habari,wananchi,vyama na serikali kwa lengo la kujenga upendo na mshikamano. Katika hatua nyingine Mwaselela amewataka waandishi kuisaidia serikali kwa kufichua changamoto badala ya kuficha kero zinazowakabili wananchi. Waandishi wamesema kupitia taaluma yao wanaweza kuibua changamoto lakini maisha yao yanakuwa hatarini kutoka kwa wahusika wanaolalamikiwa. Amesema endapo Waandishi wataibua changamoto wataisaidia Serikali kuzitatua zikiwemo za afya,barabara,maji na elimu. Mwenyekiti wa Klabu…

Read More