Author: Mbeya Yetu

DKT TULIA ACKSON:”Kwanza kabisa nichukue fursa hii kutoa pole kwa dhati. Sisi ni sehemu ya wananchi ambao tuliathirika na tukio lililotokea, na kama ilivyoelezwa vizuri na Sheikh wa Mkoa, sitarudia kwa kirefu. Lakini nitoe pole zangu za dhati kwa wananchi wenzangu wa Mbeya, Uyole, na Watanzania wote kwa ujumla, kufuatia tukio lililolikumba Taifa letu tarehe 29 Oktoba”.

”Wakati huohuo, baada ya dua na maelezo yaliyotolewa, nitoe pole pia kwa wananchi wenzetu waliopoteza maisha, na niwatakie uponaji wa haraka wale wote waliojeruhiwa.

Nichukue fursa hii pia, Mheshimiwa Waziri Mkuu, kukukaribisha mkoani Mbeya, lakini kwa ziara hii maalum, nitoe pole kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa changamoto iliyotokea, ambayo pia imekupa fursa ya kutembelea miundombinu mbalimbali ya umma na mali za wananchi zilizopata athari”.

Read More

*DKT. MWIGULU AMBANA MKANDARASI UJENZI WA BARABARA YA KITAI-RUANDA*

_Aaagiza kukamatwa kwa hati yake ya kusafiria hadi atakapokamilisha ujenzi_

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma kumsimamia vema mkandarasi anayejenga barabara ya Kitai hadi Ruanda ili aweze kuendana na kasi iliyotarajiwa.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema tayari Serikali ilikwishalipa fedha za ujenzi wa barabara hiyo kwa kutambua umuhimu wake kwenye uchumi wa mkoa huo na Taifa kwa ujumla.

📍Songea-Tanzania
🗓️Desemba 16, 2025

Read More

Mbeya. Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Eng. Kundo A. Mathew, amesema Serikali imejipanga kuhakikisha miradi yote ya maji mkoani Mbeya na Chunya inakamilishwa kwanza kabla ya kuanzisha mingine, ili wananchi wapate huduma ya maji safi na salama. Akizungumza katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili, Mhe. Kundo alisema miradi ya kimkakati ikiwemo Mradi wa Maji Chunya inakidhi vigezo vya upatikanaji wa maji, wingi wa maji na gharama nafuu. Pia ameeleza kuwa chanzo cha maji kilibadilishwa baada ya visima awali kubainika kuwa na maji kidogo na chumvi nyingi, huku mazungumzo ya…

Read More