Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- KAILIMA AFUNGA KIKAO CHA UPANGAJI WA RATIBA YA KAMPENI ZA WAGOMBEA URAIS
- Pastor akimbia baada ya mke wake kuvamia madhabahu akilia
- MAHUNDI Atamka Hadharani: Samia na Tulia Ushindi wa Kishindo 2025
- Jinsi ya Kumkamata Mpenzi Wako Akiwa na Mpango wa Kando Bila Stress
- Masache Kasaka achukua fomu ya Ubunge Lupa Chunya aingia site kibabe
- MAHUNDI: CHAMA CHA MAPINDUZI NA MPEPERUSHA BENDERA MWALUNENGE NDIYO HABARI YA MBEYA MJINI
- “Nguvu ya Umoja: Mwakipesile Amuunga Mkono Patric Mwalunenge kuanzia Kampeni Hadi Ushindi”
- Ipyana Samson Ajitosa Rasmi Uyole, CHAUMMA Yataka Kuandika Historia Mpya
Author: Mbeya Yetu
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Beno Malisa Agosti 22, 2025 amemkabidhi boti moja mpya PB.44 ULINZI Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga. Akikabidhi boti hiyo kwa Jeshi Mkoa wa Mbeya, Mhe Malisa amelitaka Jeshi hilo kulitumia vizuri boti hilo katika kuimarisha doria za ziwa nyasa Wilayani Kyela na kutokomeza uhalifu. nipe vichwa vitano vya habari Aidha, Mhe.Malisa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura kwa kutimiza ahadi ya kutoa boti kwa ajili ya kuimarisha ulinzi Ziwa Nyasa na kuahidi kuitunza na kuitumia vizuri kwa malengo yaliyokusudiwa. Naye, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya SACP Benjamin Kuzaga amesema kuwa Boti hiyo inakwenda kuimarisha ulinzi Ziwa Nyasa kupitia doria za pamoja za Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, JWTZ, Uhamiaji na TRA. Ziwa nyasa ni miongoni mwa maziwa makuu nchini ambalo sehemu ya Ziwa hilo ni nchi jirani ya Malawi na Mkoa wa Njombe na Ruvuma hivyo uwepo wa Boti hiyo ni mikakati ya kuimarisha ulinzi na kudhibiti uhalifu wa majini.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Askari Wanyama pori [TAWA] kutoka Mpanga Kipengele linamshikilia Frank Alon [49] mkazi wa Uyole – Nsalaga Jijini Mbeya kwa tuhuma za kupatikana na nyara za serikali meno nane [08] ya Tembo yenye uzito wa kilogram 31.6 bila kibali.
Mtuhumiwa alikamatwa Agosti 17, 2025 saa 9:00 alasiri Kijiji cha Nsonyanga kilichopo Kata ya Mahongole, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali katika muendelezo wa Misako na Doria za pamoja zinazofanywa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Askari Wanyama Pori [TAWA].
Mtuhumiwa alikuwa akisafirisha meno hayo ya Tembo kwa kutumia usafiri wa Pikipiki yenye namba za usajili MC 165 DDF aina ya TVS akiwa katika harakati za kutafuta mteja. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa mtuhumiwa ni mwindaji haramu katika hifadhi za Taifa.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Maafisa wa Shirika la Umeme [TANESCO] Tawi la Mbeya linamshikilia Ikupa Mwakibibi [32] mjasilimali na mkazi wa Sae Jijini Mbeya kwa tuhuma za kuhujumu miundombinu ya Shirika la Umeme kwa kujiunganishia umeme kinyume na utaratibu wa shirika hilo.
Mtuhumiwa alikamatwa Agosti 18, 2025 saa 9:30 alasiri Mtaa wa Sae uliopo Kata ya Ilomba Jijini Mbeya katika oparesheni za pamoja za Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Shirika la Umeme [TANESCO] ambapo baada ya kupekuliwa katika nyumba yake mtuhumiwa alikutwa akiwa na mita za umeme 19, rimoti za TANESCO 45 pamoja na waya rola 25 vyote vikiwa ni mali ya shirika la TANESCO.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watuhumiwa saba [09] kwa tuhuma za utapeli na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na WhatsApp. Watuhumiwa hao walikamatwa kwa nyakati tofauti katika Misako inayofanywa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya ambapo Agosti 18, 2025 saa 6:00 mchana huko Kitongoji na Kata ya Nsalala, Tarafa ya Usongwe, walikamatwa watuhumiwa 04 wanaojishughulisha na utapeli wa fedha kupitia mitandao ya Facebook na WhatsApp kwa kudanganya wanatafuta wafanyakazi wa kuuza Supermarket iitwayo Kajala iliyopo Jijini Dar es salaam.
Watuhumiwa waliokamatwa ni Nemia Japhet Njonga [23] fundi rangi, mkazi wa mwakapangala, Ombeni Asangalwisye Ambilikile [22] Bodaboda, mkazi wa Nsalala, Jacob Peter Hamis [23] fundi rangi, mkazi wa mwakapangala, Baraka Joniphat Mgala [22] Bodaboda, mkazi wa mtaa wa Ndola Mbalizi.
Watuhumiwa wamekuwa wakitengeneza link za kughushi kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook na WhatsApp ambapo mtu anayeomba ajira hutumia kujiunga kwenye kundi hilo na kisha hutumiwa ujumbe unaomtaka kutuma CV yake na kumuomba mtume fedha za kujaziwa fomu na kulipia sare za kufanyia kazi. Watuhumiwa wamekutwa wakiwa na simu mbalimbali pamoja na laini za simu za mitandao mbalimbali zilizosajiliwa kwa majina ya watu tofauti ambazo hutumika kupokelea fedha na kufanyia mawasiliano
Mbeya, Agosti 2025 – Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mbeya imetangaza kufanikisha uokoaji wa zaidi ya shilingi milioni 47 na kuziwezesha Halmashauri kuongeza mapato ya ndani kwa zaidi ya shilingi milioni 200 kupitia ufuatiliaji na udhibiti wa mianya ya rushwa na upotevu wa fedha za umma. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mbeya, Maghela P. Ndimbo, mafanikio hayo yametokana na kazi za ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo, uchambuzi wa mifumo ya ukusanyaji mapato, na kudhibiti matumizi yasiyo sahihi ya fedha katika kipindi cha Aprili hadi Juni 2025. Miradi ya Maendeleo…
*Katibu Wa Siasa na Wenezi Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Mbeya Mjini Ndugu, Philimon Mng’ong’o Chatangaza Majina ya Madiwani Wateule Jimbo la Mbeya Mjini*
*#Oktoba Tunatiki*
*#Kazi na Utu Tunasonga Mbele*