Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- RC Malisa Afungua Mafunzo ya Maafisa Ulinzi wa Taarifa Binafsi Mbeya
- CRDB YAUNGANA NA JESHI LA POLISI MBEYA KUELEKEA SIKU MAALUM YA POLISI.
- DAS Mbeya: Kipato Kisiharibu Vyanzo vya Maji
- KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA
- Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji
- Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo
- TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya
- New Asante Mbeya Yapongeza TAKUKURU Mbeya kwa Elimu ya Uadilifu na Kufungua Uelewa wa Wanachama
Author: Mbeya Yetu
Diwani wa Kata ya Utengule Usangu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya, Ismail Matipa, ametoa sare za shule kwa wanafunzi 400 waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza, katika Shule ya Sekondari Utengule Usangu.
Hatua hiyo imelenga kuondoa changamoto ya baadhi ya wazazi kuchelewesha au kushindwa kuwapeleka watoto wao shule pindi msimu wa masomo unapoanza, hali inayosababishwa na ukosefu wa sare za shule.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Diwani Matipa amesema utoaji wa sare hizo ni sehemu ya jitihada zake za kuunga mkono elimu na kuhakikisha wanafunzi wote wanaanza masomo kwa wakati bila vikwazo vya kiuchumi.
Ameeleza kuwa tukio hilo limefanyika katika wiki ya maadhimisho ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutimiza miaka 49 tangu kuzaliwa kwake mwaka 1977, ikiwa ni ishara ya kuenzi mchango wa chama hicho katika maendeleo ya elimu na ustawi wa jamii.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Ndg. Salim Abri Asas, ameonyesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Mradi wa Soko la Matola jijini Mbeya, akieleza kuwa haiwezekani kukamilika mwezi Mei kama ilivyopangwa.
Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi katika maadhimisho ya miaka 49 ya CCM, Asas alisema mradi unasuasua licha ya fedha kuwepo. Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya, Mhe. Dk. Mohamed Issa, alimweleza kuwa mkandarasi ameshindwa kusimamia fedha za mradi ipasavyo.
Kwa upande wake, MNEC Ndg. Ndele Mwaselela alisema idadi ndogo ya wafanyakazi na kasi ndogo ya ujenzi ni sababu kuu zinazoathiri ukamilishaji wa mradi.
Ndg. Asas alisema atawasilisha taarifa ya kweli kwa mamlaka husika, akisisitiza kuwa hatakubali kutoa taarifa ya kukamilika kwa mradi wakati hali halisi ni tofauti.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi Jakaya Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) ameshiriki Mkutano wa 67 wa Mawaziri wa Afya kutoka nchi 9 wanachama za Jumuiya ya Afya ya Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika (ECSA-HC) unaofanyika Ezulwini, Ufalme wa Eswatini tarehe 2-3 Februari, 2026. Pamoja na mambo mengine, Mkutano huo umejadili mikakati ya kuimarisha mifumo ya afya ya nchi wanachama wa ECSA-HC, hususan kwa kuzingatia mabadiliko yanayoendelea duniani kote yaliyopelekea kupungua au kusitishwa kabisa kwa upatikanaji wa fedha za kufadhili miradi ya afya kutoka kwa wafadhili waliozoeleka.…
Mbunge wa Jimbo la Lupa, Mhe. Masache Kasaka, akichangia Mpango wa Maendeleo wa Serikali 2026/27 bungeni, amepongeza Serikali kwa mwelekeo mzuri wa mpango huo na kusisitiza umuhimu wa kuimarisha miundombinu ya usambazaji wa umeme, hususan Chunya. Ameshauri ujenzi wa kituo cha umeme (substation) na upanuzi wa umeme kwenye maeneo ya wachimbaji ili kupunguza gharama za uendeshaji, kuongeza uzalishaji, na kuchochea ukuaji wa sekta ya madini na sekta binafsi kwa ujumla.
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mheshimiwa Patrick Adkin Mwalunenge, amesimamisha ghafla msafara wake baada ya kukutana na dimbwi kubwa la maji katika Barabara ya Soweto, jijini Mbeya, kero ambayo wananchi walimweleza kuwa imekuwepo kwa zaidi ya miaka mitatu bila kuchukuliwa hatua stahiki.
Mbunge wa Jimbo la Mbarali, Mhe. Bahati Kenneth Ndingo, amekabidhi mashuka kwa Kituo cha Afya Utengule ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Maadhimisho hayo yamefanyika katika Kata ya Utengule Usongwe, wilayani Mbarali.
Hatua hiyo inalenga kuboresha mazingira na huduma kwa wagonjwa wanaofika kupata matibabu katika kituo hicho cha afya. Baadhi ya wananchi wameeleza kuwa msaada huo utasaidia kupunguza changamoto zilizokuwepo awali na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya.
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la CARE wametoa mafunzo kwa wawezeshaji wa ngazi ya jamii kuhusu mabadiliko ya tabia nchi katika mkoa wa Mbeya, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Ustahimilivu Wake, Dunia Yetu. Mradi huo unatekelezwa katika vijiji 300 vya mikoa ya Mbeya, Njombe na Iringa kwa lengo la kuimarisha uwezo wa jamii kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi pamoja na kuboresha utunzaji wa mazingira. Katika mkoa wa Mbeya, mafunzo hayo yamefanyika kwa siku tatu wilayani Mbarali, kijiji cha Chimala, yakilenga zaidi wakulima na wafugaji ili kuwajengea uelewa kuhusu…
