Author: Mbeya Yetu

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza kuwa Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utafanyika Jumatano, Oktoba 29, 2025.

✅ Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa saa 1:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni.
✅ Vituo vya magereza vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri.
✅ Kila mpiga kura anatakiwa kufika kituoni na kadi yake ya kupigia kura.
✅ Waliopoteza kadi wataruhusiwa kutumia NIDA, leseni au pasi ya kusafiria endapo jina lipo kwenye daftari la wapiga kura.

🗓️ Taarifa hii imetolewa na Ms. Anamary Joseph Mbunga, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mbeya Mjini – tarehe 19 Oktoba 2025.

Read More

Wanachama wa CCM kutoka Mbeya Mjini na Vijijini wamejitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Ndege wa Songwe kumlaki Mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akitokea mkoani Rukwa kuelekea Dar es Salaam.

Wanachama hao walikaa uwanjani tangu saa 1 asubuhi hadi jioni wakisubiri kwa hamasa kumuona kiongozi wao, wakisema wanavutiwa na siasa za hekima, upendo na maendeleo za Dkt. Samia.

Read More

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Beno Malisa, amesema kuna umuhimu mkubwa wa kuwathamini zaidi wataalamu wa afya wanaohudumia watoto wachanga wanaozaliwa kabla ya muda wao (njiti), kutokana na mazingira magumu na changamoto wanazokabiliana nazo katika utoaji wa huduma hizo. Malisa aliyasema hayo Oktoba 17, 2025, wakati wa ufunguzi wa ukarabati wa wodi ya watoto wachanga (Neonatal Care Unit – NCU) katika Hospitali ya Wazazi Meta, ukarabati uliotekelezwa na Taasisi ya Afya Ifakara (Ifakara Health Institute – IHI) kwa ushirikiano na wadau wa NEST360 Tanzania. “Kwa wachache tuliobahatika kuona hali ya wodi hii, imenijengea hofu na kunifanya nione thamani ya maisha…

Read More