Subscribe to Updates
Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.
- MAKAMU MWENYEKITI INEC NA WAJUMBE WA TUME WAMTEMBELEA RC SONGWE
- Dkt. Godlove Mbwanji, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, ashiriki kampeni ya kitaifa ya uwekezaji wa ndani.
- MBEYA YAANDIKA HISTORIA: NGazi ZA UMEME ZA KWANZA NYANDA ZA JUU KUSINI
- ZIMAMOTO WAOPOA MWILI WA KIJANA ALIYEDAIWA KUWA MWANAFUNZI WA CBE MBEYA
- Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya
- TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA
- AB YAPENDEKEZA MAPITIO MAKUBWA KULINDA BLOGA NA WATENGENEZA MAUDHUI
- SHEIKH WA MKOA MBEYA ATOA UJUMBE KWA WAISLAMU KUELEKEA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN
Author: Mbeya Yetu
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Region, Beno Malisa, amesema Serikali ipo tayari kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wote wanaotaka kuwekeza mkoani humo ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kwa wananchi.
Amesema hayo wakati wa uzinduzi wa tawi la Strategies Insurance, kampuni inayotoa huduma za bima, uliofanyika jijini Mbeya. Amepongeza uamuzi wa kampuni hiyo kufungua tawi katika mkoa huo, akieleza kuwa hatua hiyo itarahisisha upatikanaji wa huduma za bima kwa wananchi na wafanyabiashara.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Strategies Tanzania, Jabiri Kigoda, amesema kampuni hiyo imejipanga kutoa huduma bora, za haraka na zinazoendana na mahitaji ya wateja.
Aidha, baadhi ya viongozi wa taasisi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo wamewahimiza wananchi kujiunga na huduma za bima ili kujikinga na athari za majanga yanayoweza kujitokeza, pamoja na kulinda mali na maisha yao.
Kuelekea Maadhimisho ya siku maalum ya familia ya Polisi Mbeya, 2026, Benki ya CRDB Mbeya imetoa msaada wa vifaa vya michezo kwa Jeshi la Polisi Mbeya. Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo, Meneja wa CRDB Mbeya ndugu Harrison Andrew amesema kuwa wao kama CRDB wanatekeleza kauli mbiu yao ya “ULIPO TUPO” kwa kuungana na jamii katika shughuli au matukio mbalimbali. Aliongeza kuwa, wanashirikiana katika mambo mbalimbali na Jeshi la Polisi ikiwemo jitihada za kuzuia na kutokomeza uhalifu hivyo kuelekea sikukuu maalum ya familia ya Polisi Mbeya watakuwepo kuungana na jamii. Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya…
Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Bw. Azizi Faki, ametoa onyo kali juu ya kuendelea kwa uharibifu wa vyanzo vya maji wilayani humo, akisema hali halisi ya uchafuzi na upungufu wa maji inaonekana wazi kutokana na shughuli za kibinadamu zisizozingatia sheria.
Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa chanzo cha maji cha Mtombalizi, kilichopo katika Kata za Utengule Usongwe na Nsalala, Bw. Faki alisema uchimbaji wa mchanga na mawe katikati ya mto pamoja na uharibifu wa kingo za maji umepelekea mto huo kupoteza mwelekeo wake wa asili, maji kuchafuka na kupungua kwa kiasi kikubwa.
Bw. Faki alisema licha ya kuwepo kwa maelekezo ya awali ya kulinda kingo za mito, kupanda miti na kuacha mita sitini kutoka kwenye chanzo cha maji bila shughuli za kibinadamu, hali bado ni mbaya kutokana na kuendelea kwa shughuli haramu, hali inayohatarisha vyanzo vya maji vinavyotegemewa na wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.
Alitoa wito kwa taasisi zote husika ikiwemo TFS, mamlaka za maji, mamlaka ya madini, Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Rukwa, pamoja na viongozi wa serikali za mitaa, kata na tarafa kushirikiana kikamilifu katika kulinda chanzo hicho. Alisisitiza kuwa jitihada za kutafuta kipato haziwezi kuwa sababu ya kuvunja sheria na kuharibu mazingira.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Mohamed Fakii, ametoa onyo dhidi ya uharibifu wa vyanzo vya maji unaotokana na ukataji miti ovyo na kilimo karibu na vyanzo vya maji.
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa Chanzo cha Maji cha Mbawe, kijiji cha Mbawe, Fakii alisema kuwa shughuli za kibinadamu zinaendelea kuhatarisha uendelevu wa vyanzo vya maji licha ya kuwepo kwa maji kwa sasa kutokana na mvua. Alisisitiza kuwa ni marufuku kufanya shughuli zozote ndani ya mita 60 kutoka chanzo cha maji.
Aliwaagiza wananchi wote wanaolima au kufanya shughuli karibu na vyanzo hivyo kuondoka mara moja, huku akizitaka serikali za vijiji na kata kushirikiana kikamilifu katika ulinzi wa vyanzo vya maji na kutoa elimu kwa wananchi.
Ziara hiyo ilifanywa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mheshimiwa Solomon Itunda, akiwa ameambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya.
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na Shirika la CARE wametoa mafunzo kwa wawezeshaji wa ngazi ya jamii kuhusu mabadiliko ya tabia nchi mkoani Mbeya kupitia Mradi wa Ustahimilivu Wake, Dunia Yetu unaotekelezwa katika vijiji 300 vya Mbeya, Njombe na Iringa.
Mafunzo hayo ya siku tatu yamefanyika kijiji cha Chimala, wilayani Mbarali, yakilenga kuwajengea wakulima na wafugaji uelewa wa masuala ya jinsia, utunzaji wa mazingira na mbinu za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Mbunge wa Jimbo la Mbarali, Bahati Ndingo, amegawa jezi, sufuria, majiko ya gesi pamoja na sabuni kwa wananchi na vikundi mbalimbali vya vijana katika Kata ya Utengule Usangu, wilayani Mbarali, mkoani Mbeya.
Msaada huo umetolewa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kuzaliwa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) yaliyofanyika kiwilaya, yakilenga kuimarisha michezo, matumizi ya nishati safi na ustawi wa jamii.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mbunge Ndingo amesisitiza umuhimu wa vijana kukuza vipaji vyao, akibainisha kuwa michezo, hususan soka, ni ajira. Aidha, ametangaza mpango wa kuanzisha mashindano ya soka yajulikanayo kama “Bahati Ndingo Cup” baada ya msimu wa mavuno.
