Author: Mbeya Yetu

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 23, 2026 ametembelea mafunzo ya Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma na kuzungumza nao ambapo amewasisitiza kutekeleza majukumu yao kwa weledi kwa kufuata Sheria, Kanuni na maelekezo ya Tume. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele leo Februari 23, 2026 ametembelea mafunzo ya Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya vituo katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma…

Read More

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele akizungumza leo Februari 22, 2026 na washiriki wa mafunzo ya makarani waongozaji wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Peramiho unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Februari, 2026.  Na Waandishi wetu, Ruvuma na Songwe Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewataka Makarani Waongozaji wapiga kura katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma kutekeleza majukumu yao bila woga kwa kufuata Sheria, Kanuni, maelekezo ya Tume.   Wito huo umetolewa na  Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC),…

Read More

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi amewasihi watu wenye uwezo kuwatunza wazazi na ndugu ili kuenzi mchango wao katika jamii. Mhandisi Mahundi amesema hayo wakati wa ziara ya kutembelea makazi ya wazee yanayomilikiwa na taasisi binafsi ya Tushikamane Pamoja Foundation,Kwembe, Manispaa ya Ubungo Jijini Dar Es Salaam ambapo amesema jamii inapaswa kubadili mtazamo na kuhakikisha wazee wanapewa upendo, ulinzi na matunzo wanayostahili bila kujali changamoto zilizopita. Ameeleza kwamba hata kama walipitia changamoto au walikosewa, ni muhimu kulipa kwa wema na si kwa mabaya, kwa sababu wazee ni tunu ya taifa na…

Read More

Serikali imeendelea kuimarisha huduma na mazingira katika Makazi ya Wazee na Wasiojiweza kwa lengo la kuhakikisha wazee wanaishi kwa heshima, usalama na kupata huduma stahiki za kijamii na afya. Hayo yamesema na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi tarehe 20, Februari 2026 wakati alipotembelea Makazi ya wazee Nunge yaliyopo Kigamboni, mkoani Dar Es Salaam kwa lengo la kujionea hali ya utoaji wa huduma na kusikiliza changamoto zinazowakabili wazee wanaoishi katika kituo hicho. Mhandisi Mahundi amesema Serikali inawatambua Wazee kama tunu, hazina ya hekima na msingi wa maadili ya Taifa hivyo Serikali…

Read More

Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk leo Februari 19, 2026 akiwa na Mjumbe wa Tume, Mhe. Dkt. Zakia Mohamed Abubakar wamemtembelea  ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Jabiri Omari Makame.    Viongozi hao wa Tume wapo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ambapo wametembelea na kukagua maandalizi ya Uchaguzi mdogo wa Udiwani Kata ya Shiwinga, Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mkoani Songwe unaotarajiwa kufanyika Februari 26, 2026.

Read More