Author: Mbeya Yetu

Miaka ya hivi karibuni, Mbeya limeendelea kushuhudia mageuzi makubwa ya kiuchumi yanayochochewa na mazingira rafiki ya uwekezaji pamoja na uboreshaji wa miundombinu ya kisasa. Miongoni mwa alama za maendeleo hayo ni ujenzi wa AH City Mall — jengo la kisasa lenye ngazi za umeme (escalator) ambalo limekuwa kivutio kikubwa kwa wakazi wa jiji na maeneo ya jirani. Watu wengi hufika si tu kwa shughuli za kibiashara, bali pia kwa matembezi na kupiga picha, wakivutiwa na hadhi yake ya kuwa jengo la kwanza katika Ukanda wa Nyanda za Juu Kusini kuwa na mfumo huo wa kisasa wa ngazi za umeme.

Read More

Mtu anayedaiwa kuwa mwanafunzi wa Chuo cha Biashara (CBE) Kampasi ya Mbeya, Tido Kadaga (20), amekutwa amefariki dunia baada ya mwili wake kuonekana ukielea kwenye dimbwi la maji katika Mtaa wa Maili Tano, Kata ya Iganzo, Jijini Mbeya.
Kwa mujibu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Tanzania, walipokea taarifa kutoka kwa mashuhuda kuhusu mwili unaoelea majini na kufika eneo la tukio, kisha kuuopoa na kuupeleka Hospitali ya Rufaa Kanda Mbeya kwa uchunguzi zaidi.
Mrakibu Mwandamizi wa Zimamoto Mkoa wa Mbeya, Malumbo Ngata, amesema tukio hilo liliripotiwa majira ya mchana na baada ya uchunguzi wa awali kubainika marehemu ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza CBE.
Kwa upande wake, Mkuu wa chuo hicho, Dk Beny Mwenda, amesema wanangoja taarifa rasmi kutoka Jeshi la Polisi Tanzania kabla ya kutoa ufafanuzi zaidi.

Read More

ZAIDI ya kaya 200 zimepata madhara ya kukosa makazi baada ya nyumba zao kuezuliwa na nyingine kubomoka kufuatia mvua kubwa zilizoambatana na upepo mkali zinazoendelea kunyesha katika Nyanda za Juu Kusini.

Mbali na makazi kuharibika, vyakula na mavazi pia vimeathirika baada ya maji kujaa kwenye nyumba na mali nyingi kufunikwa na tope.

Uharibifu huo umeripotiwa katika kata sita, ambazo ni Iganzo, Isanga, Karobe, Iyunga, Nzovwe na Iwambi, wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Patrick Mwalunenge, aliyefika kujionea hali halisi ya wananchi walioathirika.

Baadhi ya wakazi wamesema chanzo kikubwa cha mafuriko hayo ni mifereji kuziba, hali iliyosababisha maji kuingia moja kwa moja kwenye makazi yao.

Licha ya uharibifu mkubwa wa mali na makazi, hakuna madhara ya kibinadamu yaliyoripotiwa hadi sasa.

Read More

Meneja Uhamasishaji Uwekezaji kutoka TISEZA, Daudi Riganda, amesema mamlaka hiyo inaendelea kuhamasisha uwekezaji ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza fursa za biashara nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea mradi wa Babito Trading Company katika Mbeya, alisema uwekezaji huo unaomilikiwa kwa asilimia 100 na Watanzania umegharimu zaidi ya shilingi bilioni nane.

Alisema mradi huo ni chanzo cha mapato kwa jiji la Mbeya na pia kwa TRA, huku ukiwa mfano wa mafanikio ya uwekezaji wa ndani kutokana na mazingira mazuri ya biashara yaliyopo Tanzania.

Aidha, alibainisha kuwa motisha za uwekezaji, ikiwemo punguzo la kodi na unafuu wa ushuru kwa baadhi ya vifaa vilivyoagizwa kutoka China, zimechangia kupunguza gharama za mradi.

Read More

Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imebainisha haja ya kufanya mapitio ya haraka ya Sera na Sheria ya Huduma za Habari nchini ili kuendana na kasi kubwa ya mabadiliko ya teknolojia ya kidijitali. Hatua hiyo inalenga kuhakikisha kuwa sheria hiyo, iliyotungwa mwaka 2016 kabla ya ukuaji wa sasa wa mitandao ya kijamii, inatoa tafsiri pana itakayowawezesha bloga na watengeneza maudhui ya mtandaoni kutambulika na kusimamiwa kisheria. Kutokana na mazingira ya sasa, JAB inaona kuna umuhimu wa kufanya mapitio hayo ili kuyaingiza katika mfumo makundi hayo mapya yanayochipukia kwa kasi katika tasnia ya habari. Katika wasilisho lililotolewa na Kaimu…

Read More

Mkurugenzi Mtendaji wa Equity For Tanzania Limited- EFTA Bwana Nicomed Bohay akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzindunzi wa Hati Fungani za EFTA tukio lilofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam katika Hotel ya Kilimanjaro Hyatt Regency. Wageni mbalimbali, wakiwemo wadau wa sekta ya fedha, wawekezaji na wawakilishi wa taasisi za kifedha, wakifuatilia kwa makini tukio la uzinduzi wa EFTA Corporate Bond ya Shilingi bilioni 50, lililofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo uliashiria hatua mpya ya kuimarisha upatikanaji wa mtaji wa muda mrefu kwa sekta za uzalishaji nchini. Wajumbe wa jopo la majadiliano…

Read More

KANISA LA MORAVIAN TANZANIA LATOA TUZO MAALUM KWA YONA SONELO BAADA YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA AUSTRALIA

Kanisa la Moravian Tanzania (KMT) limetoa tuzo maalum kwa muumini wake na mfanyabiashara maarufu nchini, Yona Sonelo, kufuatia kutunukiwa Shahada ya Heshima na Chuo Kikuu cha Australia kutokana na mchango wake mkubwa kwa jamii.

Hafla ya kukabidhi tuzo hiyo imefanyika mkoani Tabora, ambapo viongozi wa kanisa, waumini pamoja na wadau mbalimbali walihudhuria kushuhudia tukio hilo muhimu.

Akizungumza katika hafla hiyo, viongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania wamesema kuwa Sonelo amekuwa mfano wa kuigwa kwa kuunganisha imani na vitendo kupitia shughuli zake za kibiashara na kijamii, ikiwemo kusaidia makundi yenye uhitaji na kuchangia maendeleo ya jamii.

Kwa upande wake, Yona Sonelo amelishukuru kanisa kwa kutambua juhudi zake, akisema mafanikio aliyoyapata ni matokeo ya imani, ushirikiano na msaada kutoka kwa familia, kanisa na jamii kwa ujumla.

Tuzo hiyo ni ishara ya kuthamini mchango wake endelevu katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi, huku ikiwahamasisha waumini na Watanzania kwa ujumla kuendelea kufanya kazi kwa bidii na uadilifu.

Read More

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Region, Beno Malisa, amesema Serikali ipo tayari kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wote wanaotaka kuwekeza mkoani humo ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira kwa wananchi.

Amesema hayo wakati wa uzinduzi wa tawi la Strategies Insurance, kampuni inayotoa huduma za bima, uliofanyika jijini Mbeya. Amepongeza uamuzi wa kampuni hiyo kufungua tawi katika mkoa huo, akieleza kuwa hatua hiyo itarahisisha upatikanaji wa huduma za bima kwa wananchi na wafanyabiashara.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Strategies Tanzania, Jabiri Kigoda, amesema kampuni hiyo imejipanga kutoa huduma bora, za haraka na zinazoendana na mahitaji ya wateja.

Aidha, baadhi ya viongozi wa taasisi mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo wamewahimiza wananchi kujiunga na huduma za bima ili kujikinga na athari za majanga yanayoweza kujitokeza, pamoja na kulinda mali na maisha yao.

Read More