Author: Mbeya Yetu

Sheikh wa mkoa wa Mbeya Sheikh Msafiri Ayas Njalambaha akiwa na Baadhi Viongozi wa Baraza kuu la Waislamu BAKWATA Mkoa Mbeya walipotembelea mradi wa ujenzi wa shule ya Sekondari ya Kiislamu inayojengwa barabara ya Nane Sokomatola Jijini Mbeya. Miradi huo wa shule ya Sekondari ya Kiislamu unatarajiwa kugharimu kiasi cha Sh Bilioni 4 hadi kukamilika kwake Fedha ambazo zinategemea michango na sadaka za Waislamu na Wadau wa Maendeleo ndani na nje ya Mkoa wa Mbeya

Read More

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele (katikati) akiongoza kikao cha Tume kilichokutana Jijini Dodoma leo Novemba 7, 2025 na kupitisha majina ya wabunge wa viti maalum. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Tume , Mhe. Jaji wa Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk na kushoto ni Katibu wa Tume ambae pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhani Kailima.  Tume ikiwa katika kikao chake hii leo.  ****** Kwa kuzingatia masharti ya Ibara ya 66(1)(b) na 78(1) za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 zikisomwe pamoja na kifungu…

Read More

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa ametoa wito kwa wafanyabiashara kulipa leseni za biashara kwa wakati, ili kuiwezesha Serikali kutekeleza miradi ya maendeleo.

RC Malisa ameyasema hayo wakati akikabidhi madawati 1,000 kwa shule 15 za msingi jijini Mbeya, yaliyotengenezwa kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Mkurugenzi wa Jiji, Justine Kijazi, amesema zaidi ya milioni 130 zimetumika kutengeneza madawati na meza kwa shule mbalimbali.

Read More