Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
  • Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
  • VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII
  • TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
  • Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
  • MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
  • Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » Wizara ya Mawasiliano Yaendelea Kushirikiana kwa Karibu na Jeshi la Polisi Kukabili Utapeli Mtandaoni – Mhandisi Maryprisca Mahundi
Habari za Kitaifa

Wizara ya Mawasiliano Yaendelea Kushirikiana kwa Karibu na Jeshi la Polisi Kukabili Utapeli Mtandaoni – Mhandisi Maryprisca Mahundi

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMay 12, 2025No Comments18 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amesema kuwa Wizara inaendelea kushirikiana kwa karibu na Jeshi la Polisi katika kukabiliana na vitendo vya utapeli mtandaoni, hasa vinavyofanyika kupitia huduma za simu na miamala ya kifedha (SimBanking).

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Fakharia Shomari Khamisi (Mb.), katika kikao cha Bunge kilichofanyika jijini Dodoma, Mhandisi Mahundi alisema ongezeko la matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) limeleta manufaa makubwa kwa taifa katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kisiasa, huku pia likizua changamoto mbalimbali ikiwemo uhalifu wa mtandaoni.

Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania
(TCRA) kwa robo ya tatu ya mwaka huu wa fedha, idadi ya laini za simu imefikia milioni 90.4, huku watumiaji wa intaneti wakifikia milioni 49.3.

Mhandisi Mahundi alisema mafanikio hayo yameambatana na ongezeko la visa vya utapeli, ambavyo vimekuwa vikiwahadaa wananchi na kusababisha wapoteze fedha zao.

“Serikali kwa kushirikiana na wadau wa mawasiliano imeendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu usalama wa mitandao kupitia kampeni mbalimbali kama vile SITAPELIKI na
NI RAHISI SANA, ili kuongeza uelewa wa wananchi juu ya matumizi salama ya huduma za kidijitali, hususan katika huduma za kifedha,” alisema Mahundi.

Aidha, alisema Serikali kupitia Jeshi la Polisi inaendelea kuimarisha mikakati ya kukabiliana na aina hiyo ya uhalifu na tayari hatua mbalimbali zimechukuliwa dhidi ya wahusika.

Akijibu swali la nyongeza la Mbunge huyo, Mhandisi Mahundi alibainisha kuwa sababu mojawapo inayochochea kuendelea kwa utapeli ni baadhi ya wananchi kushirikiana bila kujua na matapeli kwa kujibu au kufuata maelekezo kutoka kwa ujumbe au simu za kitapeli.

Alitoa wito kwa wananchi kuwa waangalifu na kutotoa ushirikiano kwa mawasiliano yasiyo rasmi au yenye viashiria vya udanganyifu.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

February 27, 2026

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025360

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Habari za Kitaifa

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

By Mbeya YetuFebruary 28, 202611

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mzee Rashidi Mfaume Kawawa, mwanasiasa mashuhuri na…

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026

TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

February 27, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025360

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.