Author: Mbeya Yetu

Mkuu wa Progamu za Urithi wa Dunia wa Tume ya Taifa ya UNESCO Eric Kajiru akiwasilisha mada katika Semina ya wadau Maeneo ya Hifadhi za Asili ikiwa ni Maadhimisho ya Siku ya Urithi wa Dunia Afrika yaliyofanyika Kitaifa wilayani Kondoa mkoani Dodoma *Fursa hiyo ipo kwa sasa kabla ya vigezo havijabadilika Na Mwandishi Wetu Tume ya taifa ya UNESCO imewataka wadau ambao wanataka kuziingiza maeneo yao katika orodha urithi wa dunia kuanza mchakato kabla ya 2027 kwani huenda taratibu zikabadilika na kuwa ngumu zaidi. Akiwasilisha mada kwa wadau wa maeneo ya hifadhi za asili na utamaduni katika maadhimisho ya…

Read More

Naibu Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mhandisi Maryprisca Mahundi amekabidhi msaada wa nondo zaidi ya hamsini kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)Mbalizi Road Jijini Mbeya. Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mbalizi Road Mheshimiwa Adam Simbaya amesema Mheshimiwa Mahundi aliombwa kuchangia nondo thelathini lakini yeye ametoa nondo hamsini ikiwa ni zaidi ya kiwango kilichoombwa.”Hii itakuwa ofisi ya mfano nchini kutokana na ubora wa ujenzi unaoendelea ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mbeya Patrick…

Read More

Mara baada ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari kutamatika mkoani Dodoma, Uongozi wa Juu wa UTPC ukiongozwa na Rais wa UTPC Deo Nsokolo umekutana na viongozi wa Klabu za Waaandishi wa Habari wakiwemo waratibu kwenye mkutano maalumu wa kukumbushana majukumu ya uongozi kwenye klabu za waandishi wa habari. Katika hotuba yake ya ufunguzi, mambo makuu aliyosema Rais wa UTPC ni pamoja na viongozi wa Press Clubs kusimamia dhamana waliyonayo kwa wanachama wanaowaongoza lakini pia viongozi kuwa wawazi kwa wanachama na kusimamia utelekezaji wa maazimio yaliyowekwa ili kupunguza migogoro ambayo imekuwa inaibuka mara kwa mara kwenye klabu.…

Read More

Mkuu wa Mkoa wa Lindi umezindua mpango mkakati wa elimu ya msingi na Sekondari kwa mwaka 2024 kwa lengo la kuongeza ufaulu wa elimu kwa wanafunzi wanaosoma katika mkoa huo. Akizungumza wakati wa sherehe za utoaji tuzo za elimu kwa wadau mbalimbali wa sekta ya elimu Mkuu wa mkoa wa Lindi Zainab Telack alisema kuwa wamezindua mpango mkakati wa elimu kwa lengo la kutatua changamoto 15 zilizopo katika elimu ya msingi na sekondari katika mkoa huo. Telack alisema kuwa baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na hali ya ikama ya walimu wa Shule za Msingi na Sekondari na hali ya…

Read More

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imeendelea kung’ara na kuvunja rekodi kwa kutoa wafanyakazi hodari kwa vipindi viwili (mwaka 2022 na 2024). Hatua hii imefikiwa baada ya mfanyakazi hodari Joshua J. Kusaga, Fundi Sanifu vifaa tiba, kuchaguliwa kuwa mfanyakazi hodari Mei Mosi kitaifa. Katika hafla iliyofanyika jijini Arusha, Joshua alikabidhiwa zawadi na Makamu wa Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika sherehe hizo. Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya inajivunia kuwa na wafanyakazi wenye uwezo mkubwa na inaendelea kuweka msisitizo katika kutoa huduma bora za afya kwa wananchi. Mfanyakazi huyu ameonyesha uwezo, bidii na…

Read More

20 WAFIKISHWA MAHAKAMANI 6 WAHOJIWA KWA KUTENGENEZA MFUMO BANDIA(POSS)WA KUKUSANYIA MAPATO MBEYA

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU)Mkoa wa Mbeya imewakamata na kuwafikisha mahakamani watu ishirini kwa kutengeneza mfumo bandia wa kukusanyia mapato kwa njia ya mtandao(Poss) na kutakatisha fedha na wengine sita wakiendelea kuhojiwa na TAKUKURU Mkoa wa Mbeya na ikithibitika watafikishwa mahakamani ambapo kwa pamoja wanadaiwa kuisababishia hasara Serikali zaidi ya shilingi bilioni moja.

Akitoa taarifa kwa wanahabari Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mbeya Maghela Ndimbo amesema taarifa iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali imeeleza kuwepo na udukuzi wa fedha na kutengeneza mfumo bandia wa ukusanyaji ushuru wa mazao kutoka Halmashauri za Makete, Mbarali, Tunduma,Ileje,Rungwe,Busokelo,Jiji la Mbeya, Mbeya,Pangani na Manispaa ya Sumbawanga mfumo ambao hausomani na mtandao wa Serikali.

Uchunguzi wa awali uliwakamata watu thelathini na moja wakiwemo Wataalamu wa TEHAMA kutoka Halmashauri ambapo ishirini wamefikishwa mahakamani kwa kuisababishia hasara Serikali na kumi na moja kuachiwa huru.

Maghela Ndimbo amesema watu hao wamesababisha hasara ya zaidi ya shilingi milioni mia tatu.

Maghela amewataja watuhumiwa kuwa ni pamoja na Robert Mpeleta,Anold Nzali,Isaya Andembwisye,Mbwigane Mawamelo,Peter Joseph, Benedict Milinga,Hyeli Mkwama,Harid Habib,Fadhili Fredy,Lwesya Shukuru, Daniel Tweve,Ezekia Adam,Paul Samson na Ulimboka Adamson.

Watuhumiwa sita walifunguliwa mashitaka ya uhujumu uchumi katika Wilaya ya Mbarali kesi namba 24/2023 Asante Mwilapa, Stanford Bukuku na Afrika Mwambogo kwa pamoja wanadaiwa kuisababishia hasara ya shilingi laki mbili na elfu tisini na sita ambapo kesi ya uhujumu uchumi namba 25/2023 ambapo Ndundu Hitla anadaiwa kuisababishia hasara Serikali shilingi laki sita na elfu thelathini na sita pia kesi namba 26/2023 watuhumiwa wawili Elieck Luwale na Luwi Godigodi ambao wanatuhumiwa kuisababishia hasara Serikali shilingi laki moja hamsini na nne elfu na nne.

Aidha Ndimbo amesema watuhumiwa katika kesi namba 24/2023 na 26/2023 wapo nje kwa dhamana isipokuwa mshitakiwa kesi namba 20/2023 yupo mahabusu baada ya kukiuka masharti ya dhamana na washitakiwa wengine katika kesi ya uhujumu uchumi namba 03/2023 wamekosa dhamana kwa kuwa makosa ya utakatishaji fedha hayana dhamana.

Katika hatua nyingine TAKUKURU Mkoa wa Mbeya kwa kishirikiana na Afisa Mtendaji wa Kata ya ya Chimala Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali imefanikiwa kurejesha nyumba ya mjane aitwaye Bi Emelda Omary Pangani mkazi wa Chimala ambaye nyumba yake ilitwaliwa kwa nguvu na Baraka Ally Mboya baada ya mtoto wa mjane aitwaye Tamimu Halifa Mwenda kukopa kwa Baraka shilingi milioni sita na kuiba hati ya nyumba na kuikabidhi kwa Baraka ambapo Mahakama ya Mwanzo Chimala ilimhukumu kifungo cha miezi sita na kuamriwa kurejesha fedha kwa Baraka.

Pia katika hatua nyingine TAKUKURU Mkoa wa Mbeya imefuatilia miradi ya maendeleo ishirini na sita yenye thamani ya shilingi 149,728,128,096.32 ya sekta za Elimu,umwagiliaji, Maji na Mifugo.

Read More

Watumishi wa Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI)leo Mei Mosi 2024 wameungana na Wafanyakazi Duniani kote kuadhimisha Siku yao adhimu ambapo kitaifa maadhimisho yanaendelea katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijinu Arusha na Mgeni Rasmi wa Sherehe hizo ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor MpangoTAWIRI tunajivuni mchango mkubwa wa watumishi katika kusimamia, kuratibu na kufanya tafiti za wanyamapori nchini kwa ustawi wa uhifadhi na kukuza utalii nchini. Aidha, Kauli mbiu ya siku hii ya Wafanyakazi Duniani kwa mwaka huu ni *”Nyongeza ya Mishahara ni Msingi wa Mafao Bora na kinga Dhidi…

Read More

Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Taifa ya UNESCO Tanzania Profesa Hamis Malebo akiwasilisha ujumbe waTanzania katika Mkutano wa 23 wa Jukwaa la kudumu la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Watu wa Asili (UNPFII) uliomalizika jijini New York nchini Marekani PROFESA MALEBO:HAKUNA KABILA LENYE HAKI ZAIDI YA LINGINE *Ni ujumbe wa Umoja kwa Umoja wa Mataifa uliotolewa na Tanzania kabila lenye haki zaidi ya lingine KATIBA YETU NA SHERIA ZETU NA SHERIA ZA KIMATAIFA HATUNA KUNDI MAHUSUSI LA WATU tiba WA ASILI yetu na sheria NCHINI. Na Mwandishi Wetu Serikali ya Tanzania imesema kuwa watu wake hakika haina…

Read More