Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
  • Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
  • VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII
  • TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
  • Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
  • MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
  • Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WATANZANIA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA UCHAGUZI MKUU WA 2025
Habari za Kitaifa

WATANZANIA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA UCHAGUZI MKUU WA 2025

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJuly 31, 2025No Comments12 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Tume na wawakilishi wa watu wenye ulemavu kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Julai 31,2025. 

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Tume na wawakilishi wa watu wenye ulemavu kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Julai 31,2025. 
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg Kailima Ramadhani akitoa mada wakati wa Kikao cha Tume na wawakilishi wa watu wenye ulemavu kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Julai 31,2025. 

 

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg Kailima Ramadhani akitoa mada wakati wa Kikao cha Tume na wawakilishi wa watu wenye ulemavu kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Julai 31,2025. 

 

 

 

Washiriki wa Mkutano huo wakifuatilia mada.

 

Na Waandishi Wetu, Dar es Salaam
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC)
imeyataka makundi mbalimbali ya kijamii nchini kuyatumia majukwaa yao
kuwahamasisha wananchi kushiriki kwa wingi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Wito huo umetolewa leo, tarehe 31 Julai
2025, jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Mheshimiwa Jaji wa
Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele, wakati akifungua mkutano kati ya Tume na
wawakilishi wa watu wenye ulemavu.

Katika hotuba yake, Jaji Mwambegele ameeleza
kuwa Tume inatambua na kuthamini mchango wa watu wenye ulemavu katika kueneza
taarifa sahihi na kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika uchaguzi.

“Nawasihi kutumia majukwaa yenu kuhimiza
wenzenu kushiriki kwa amani na kuepuka kauli au vitendo vinavyoweza kuhatarisha
utulivu wa nchi yetu wakati wa kampeni,” amesema Mhe. Mwambegele, na kuongeza
kuwa Tume itaendelea kushirikiana nao katika hatua zote muhimu kuelekea
uchaguzi.

Akizungumzia maandalizi ya uchaguzi
mkuu, Jaji Mwambegele amesema kuwa ratiba rasmi imeshatangazwa ambapo utoaji wa
fomu za uteuzi kwa wagombea wa nafasi mbalimbali utafanyika kuanzia tarehe 9
Agosti hadi 27 Agosti 2025, huku kampeni zikipangwa kuanza tarehe 28 Agosti
hadi 28 Oktoba 2025 kwa upande wa Tanzania Bara.

Katika mkutano mwingine na wawakilishi
wa wanawake uliofanyika pia jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Tume,
Mheshimiwa Jaji wa Mahakama ya Rufani (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk, amewahimiza
wanawake kutumia nafasi zao kuwafikishia wananchi taarifa sahihi kuhusu hatua
za maandalizi ya Uchaguzi Mkuu, na kuhamasisha waliojiandikisha kwenye Daftari
la Kudumu la Wapiga Kura kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura.

Aidha, Jaji Mbarouk ametoa pongezi kwa
wanawake kwa ushirikiano mkubwa waliouonyesha katika kipindi chote cha
uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kilichoanza tarehe 20 Julai 2024
na kukamilika tarehe 4 Julai 2025.

“Natoa pongezi kwenu kwa namna
mlivyotuunga mkono wakati wote wa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la
Wapiga Kura. Tunawapongeza na tunawashukuru sana,” alisema Jaji Mbarouk.

Kwa upande wake, Mjumbe wa Tume,
Mheshimiwa Jaji wa Mahakama Kuu Asina Omari, amewahimiza vijana kutumia
mitandao ya kijamii kwa uadilifu, hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.

“Natoa wito kwenu kuwahamasisha vijana
kuhusu matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii na kuepuka mitandao inayosambaza
habari za chuki na uchochezi,” amesema Jaji Asina.

Ameonya pia dhidi ya matumizi mabaya ya
teknolojia ya akiliunde (AI), ambayo kwa sasa inatumika kusambaza taarifa za
upotoshaji na chuki.

“Vilevile, muwakumbushe vijana wenzenu
kuepuka matumizi mabaya ya akiliunde. Vijana ni kundi lenye nguvu, na mkitambua
nafasi yenu, mtaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kufanikisha uchaguzi
mkuu wa mwaka huu,” aliongeza.

Katika mikutano yote hiyo, viongozi wa
Tume wamekumbusha kuwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 utafanyika kwa mujibu wa
sheria mbili mpya zilizopitishwa mwaka 2024, ambazo zimeleta maboresho ya
kiutendaji, kisheria na kiuwazi katika mchakato mzima wa uchaguzi.

Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akifungua Mkutano wa Kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC)  uliowakutanisha Tume na wawakilishi wa wanawake kuhusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025  jijini Dar es Salaam Julai 31, 2025.

 

 

Washiriki katika mkutano huo wa wakilishi wa wanawake wakifuatilia hotuba ya ufunguzi. 

Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Asina Omari akifungua Mkutano wa Kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC)  uliowakutanisha Tume na wawakilishi wa vijana kuhusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam Julai 31, 2025.

 

Washiriki katika mkutano huo wa wakilishi wa Vijana wakifuatilia hotuba ya ufunguzi. 

 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

February 27, 2026

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025360

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Habari za Kitaifa

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

By Mbeya YetuFebruary 28, 202611

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mzee Rashidi Mfaume Kawawa, mwanasiasa mashuhuri na…

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026

TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

February 27, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025360

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.