Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

DED Yegella: Ahamasisha Upigaji Kura, Kamanda Kuzaga Asema Jeshi la Polisi Lipo Tayari Kulinda Amani

October 25, 2025

RC Malisa Atoa Wito wa Kulipa Leseni Wakati Akikabidhi Madawati 1,000 kwa Shule 15 Jijini Mbeya

October 25, 2025

ISAACK MWAKIBOMBAKI MGOMBEA UDIWANI KATA RUANDA MBEYA AELEZA DHAMIRA YAKE KWA WAKAZI WA RUANDA

October 25, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • DED Yegella: Ahamasisha Upigaji Kura, Kamanda Kuzaga Asema Jeshi la Polisi Lipo Tayari Kulinda Amani
  • RC Malisa Atoa Wito wa Kulipa Leseni Wakati Akikabidhi Madawati 1,000 kwa Shule 15 Jijini Mbeya
  • ISAACK MWAKIBOMBAKI MGOMBEA UDIWANI KATA RUANDA MBEYA AELEZA DHAMIRA YAKE KWA WAKAZI WA RUANDA
  • Kijana Asiyeamini Katika Bahati Anashangaza Wote Baada ya Kushinda Kiasi Kikubwa Kwenye Bet
  • Nilivyopata Flat Tummy Baada ya Kuteseka na Kitambi kwa Miaka Mitatu
  • Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa Atoa Rai ya Kudumisha Amani Kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 29
  • MKONGOMAN ATOA USHUHUDA MZITO KUTOWEKA KWA AMANI NCHINI JAMHURI YA KONGO
  • DKT HARRISON MWAKYEMBE ATOA SOMO ZITO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WAANDISHI WA HABARI WAHIMIZWA KUHAMASISHA USHIRIKI WA WANANCHI KUPIGA KURA
Habari za Kitaifa

WAANDISHI WA HABARI WAHIMIZWA KUHAMASISHA USHIRIKI WA WANANCHI KUPIGA KURA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuAugust 2, 2025No Comments12 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email


Mwenyekiti
wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs
Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutanio wa Tume na Waandishi wa
Habari kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja
kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 02 , 2025.

 

Mwenyekiti
wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs
Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutanio wa Tume na Waandishi wa
Habari kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja
kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 02 , 2025.

 

 

Mkurugenzi
wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Ramadhani Kailima
akizungumza wakati wa kuwasilisha mada katika mkutano wa Tume na Waandishi wa
Habari kuhusu uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja
kilifanyika jijini Dar es Salaam leo Agosti 02 , 2025. 
***************

 

Na Waandishi Wetu, Dar es Salaam
Waandishi wa habari nchini wametakiwa kutumia taaluma yao kuhamasisha na kuelimisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura ifikapo tarehe 29 Oktoba, 2025.
Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele, wakati akifungua Mkutano wa Kitaifa kati ya Tume na Waandishi wa Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu, uliofanyika tarehe 2 Agosti, 2025 katika ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.
Mhe. Jaji Mwambegele amesema vyombo vya habari vina mchango mkubwa katika kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu kwenye uchaguzi mkuu kwa kuwapatia taarifa sahihi na kwa wakati kuhusu masuala mbalimbali ya uchaguzi.
Ameeleza kuwa waandishi wa habari wana wajibu mkubwa wa kutumia taaluma yao kuwaelimisha wananchi waliojiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, ili waweze kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kupiga kura.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani amewakumbusha wanahabari wajibu wao wa kuhakikisha vyama vya siasa na wagombea wanapata nafasi ya kufikisha ujumbe wao kwa wapiga kura katika kipindi cha kampeni.
Aidha, Bw. Kailima amewataka wanahabari kutoa taarifa sahihi kwa umma na kuepuka kusambaza taarifa potofu katika hatua zote za mchakato wa uchaguzi, huku akisisitiza umuhimu wa kuzingatia sheria na maadili ya taaluma ya habari.
Amewahimiza waandishi hao kutumia kalamu na nyenzo zao kueneza ujumbe wa amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi, ili kulinda mshikamano wa kitaifa na kuimarisha misingi ya demokrasia.
Pia amewaasa kuepuka kuchapisha au kurusha habari zinazoweza kuwavunja moyo wananchi na kuwafanya waone kama hakuna umuhimu wa kushiriki katika uchaguzi, iwe ni kama wapiga kura au wagombea.
Mkutano kati ya Tume na Waandishi wa Habari ni sehemu ya mfululizo wa mikutano ya wadau mbalimbali ambayo Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imekuwa ikiitisha katika maandalizi ya kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.
Mikutano hiyo ilianza tarehe 27 Julai 2025 kwa kukutana na Viongozi wa Vyama vya Siasa, ikafuatiwa na mkutano na Wawakilishi wa Asasi Zisizo za Kiserikali kisha Wawakilishi wa Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu, pamoja na Wahariri wa Vyombo vya Habari.
Mfululizo huu wa mikutano unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 4 Agosti 2025, baada ya mkutano na Waandaji wa Maudhui Mtandaoni, utakaofuatiwa na mafunzo kwa Wahariri na Waandishi wa Habari.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

TUME YATOA MAELEKEZO YA KISERA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025

October 23, 2025

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI WA UDIWANI KATIKA KATA YA NYAKASUNGWA JIMBO LA BUCHOSA

October 18, 2025

RC Malisa Azindua Wodi ya Watoto Wachanga Hospitali ya Meta Mbeya kwa Ushirikiano wa IHI na NEST360 Tanzania

October 18, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025194

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024194

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025126
Don't Miss
Video Mpya

DED Yegella: Ahamasisha Upigaji Kura, Kamanda Kuzaga Asema Jeshi la Polisi Lipo Tayari Kulinda Amani

By Mbeya YetuOctober 25, 20250

RC Malisa Atoa Wito wa Kulipa Leseni Wakati Akikabidhi Madawati 1,000 kwa Shule 15 Jijini Mbeya

October 25, 2025

ISAACK MWAKIBOMBAKI MGOMBEA UDIWANI KATA RUANDA MBEYA AELEZA DHAMIRA YAKE KWA WAKAZI WA RUANDA

October 25, 2025

Kijana Asiyeamini Katika Bahati Anashangaza Wote Baada ya Kushinda Kiasi Kikubwa Kwenye Bet

October 25, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

DED Yegella: Ahamasisha Upigaji Kura, Kamanda Kuzaga Asema Jeshi la Polisi Lipo Tayari Kulinda Amani

October 25, 2025

RC Malisa Atoa Wito wa Kulipa Leseni Wakati Akikabidhi Madawati 1,000 kwa Shule 15 Jijini Mbeya

October 25, 2025

ISAACK MWAKIBOMBAKI MGOMBEA UDIWANI KATA RUANDA MBEYA AELEZA DHAMIRA YAKE KWA WAKAZI WA RUANDA

October 25, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025194

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024194
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.