Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Dkt. Tulia Aongoza kwa Vitendo, Apiga Kura na Kuhamasisha Ushindi wa CCM Uyole

October 29, 2025

DKT MARY MWANJELWA AUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA AHAMASISHA KUJITOKEZA KWA WINGI AMANI IMETAWALA

October 29, 2025

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

October 27, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Dkt. Tulia Aongoza kwa Vitendo, Apiga Kura na Kuhamasisha Ushindi wa CCM Uyole
  • DKT MARY MWANJELWA AUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA AHAMASISHA KUJITOKEZA KWA WINGI AMANI IMETAWALA
  • Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu
  • MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”
  • “Tunatiki CCM, Tunatunza Amani” — Kauli ya Bodaboda Kiwira Yakonga Moyo wa Suma Fyandomo
  • Nilivyomfanya Mtu Aliyenidharau Kuniheshimu na Kunitegemea Kwa Mambo Mengi
  • NABII MPANJI AUTANGAZIA UMMA, WAKRISTO WASISHIRIKI MAANDAMANO WAJITOKEZE KWA WINGI KUPIGA KURA
  • Nilivyookoa Biashara Yangu Baada ya Wateja Wote Kupotea Ghafla
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MATIBABU YA KIBINGWA YA HUDUMA MKOBA YA MADAKTARI WA DT. SAMIA UKOMBOZI MKUBWA KWA WANANCHI WA MKOA WA SONGWE.
Habari za Kitaifa

MATIBABU YA KIBINGWA YA HUDUMA MKOBA YA MADAKTARI WA DT. SAMIA UKOMBOZI MKUBWA KWA WANANCHI WA MKOA WA SONGWE.

Mbeya YetuBy Mbeya YetuSeptember 15, 2025Updated:September 15, 2025No Comments8 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Jabiri Omari Makame leo tarehe 15/09/2025 amezindua rasmi huduma mkoba za Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia mkoani Songwe ikiwa ni juhudi za Serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhakikisha huduma bora za afya zinawafikia wananchi wote kwa ukamilifu.

Katika hotuba yake, Mhe. Jabiri Makame ameeleza kuwa ujio wa kambi hiyo ya Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia ni ishara ya dhamira ya dhati ya Serikali ya kuimarisha huduma za afya mkoani Songwe. Amebainisha kuwa, kuanzia mwaka 2020 hadi 2025, mkoa umepata maendeleo makubwa ikiwa ni pamoja na ongezeko la vituo vya afya kutoka 205 hadi 273, na hospitali kutoka 2 hadi 5, vyote kwa lengo la kuboresha huduma za msingi na za kitaalamu kwa wananchi.

“Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 40.6 kwa ajili ya kuboresha miundombinu, ununuzi wa dawa, vifaa, na vitendanishi, pamoja na kuanzisha afua mbalimbali za tiba ikiwemo lishe, kudhibiti malaria, kifua kikuu, na magonjwa ya zinaa na UKIMWI. Kupitia juhudi hizi, upatikanaji wa dawa umeongezeka kwa asilimia 90, hali inayorahisisha upatikanaji wa huduma na kupunguza vifo vya watoto wachanga kutoka 320 mwaka 2022 hadi 146 mwaka 2023, mkoa umepokea watumishi wa sekta ya afya 725 kuanzia mwaka 2021 hadi 2025, ikiwa ni jitihada za kukabiliana na upungufu wa watumishi wa afya, na kufanya huduma kuwa za karibu zaidi kwa wananchi”. – amesema Mhe. Jabiri Makame

Aidha Mhe. Jabiri Makame, ametoa rai kwa viongozi na watendaji wa mkoa kuhakikisha wanatoa ushirikiano wa karibu kwa madaktari ili kuhakikisha huduma zinazotolewa zinafikia viwango vya juu, na wananchi wanafaidika kwa kiwango cha juu. Pia, amewataka wananchi kushirikiana na wataalamu wa afya ili kufanikisha malengo ya afya bora kwa wote.

Naye Bi. Pasclina Andrew Mratibu wa Huduma Mkoba ya Madaktari wa Mama Samia Mkoa wa Songwe kutoka Wizara ya Afya amesema kuwa uwekezaji huu mkubwa wa Serikali katika sekta ya afya ni hatua muhimu katika kuimarisha afya ya wananchi wa Songwe na kuboresha huduma za matibabu, kwani sasa wananchi hawatalazimika kusafiri kwenda mikoa jirani kwa huduma za kibingwa. Hii ni ahadi na matokeo ya moyo wa Serikali wa kuwaletea wananchi maendeleo na ustawi wa afya.

“ujio wa kambi hii ya matibabu unaleta faida kubwa ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za tiba za kitaalamu zilizokuwa zinahitaji kusafiriwa hadi mikoa mikubwa kama Dar es Salaam na Mbeya, hivyo kuokoa muda na gharama za wananchi. Pia, kambi hii itaimarisha uwezo wa wataalamu wa afya kwa kuwapa mafunzo na ushauri wa kitaalamu (mentorship), na kusogeza huduma za kibingwa kwa wananchi wa mkoa wa Songwe” – Pasclina

Timu ya madaktari 30 kutoka kada mbalimbali za afya zikiwa ni pamoja Madaktari wa Uzazi na Magonjwa ya wanawake, Madaktari wa Watoto, Madaktari bingwa wa usingizi na ganzi salama, madaaktari wa magonjwa ya ndani, madaktari wa meno, madaktari wa upasuaji na wauguzi Bingwa wanatarajia kutoa huduma mkoba kwa muda wa wiki moja katika halmashauri 5 za mkoa wa Songwe..

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

TUME YATOA MAELEKEZO YA KISERA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025

October 23, 2025

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI WA UDIWANI KATIKA KATA YA NYAKASUNGWA JIMBO LA BUCHOSA

October 18, 2025

RC Malisa Azindua Wodi ya Watoto Wachanga Hospitali ya Meta Mbeya kwa Ushirikiano wa IHI na NEST360 Tanzania

October 18, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025202

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024196

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025126
Don't Miss
Video Mpya

Dkt. Tulia Aongoza kwa Vitendo, Apiga Kura na Kuhamasisha Ushindi wa CCM Uyole

By Mbeya YetuOctober 29, 20258

DKT MARY MWANJELWA AUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA AHAMASISHA KUJITOKEZA KWA WINGI AMANI IMETAWALA

October 29, 2025

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

October 27, 2025

MWAKIPESILE: ”TUKAANDAMANE OKTOBA 29 KWA AJILI KUWAPIGIA KURA VIONGOZI KWA AMANI”

October 27, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Dkt. Tulia Aongoza kwa Vitendo, Apiga Kura na Kuhamasisha Ushindi wa CCM Uyole

October 29, 2025

DKT MARY MWANJELWA AUNGANA NA WANANCHI KUPIGA KURA AHAMASISHA KUJITOKEZA KWA WINGI AMANI IMETAWALA

October 29, 2025

Nilivyookoa Ndoa Yangu Baada ya Migogoro Kila Usiku Kuhusu Pesa na Wivu

October 27, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025222

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025202

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024196
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.