Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri

September 17, 2025

Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake

September 17, 2025

Kongamano la Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050 Kufanyika Mbeya

September 17, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri
  • Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake
  • Kongamano la Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050 Kufanyika Mbeya
  • Prof. Makulilo: Watanzania Wajiandae kwa Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050
  • Tajiri wa madini aliyefilisika arejea tena katika biashara kwa kishindo
  • Nilirogwa Nipoteze Kila Kitu ila Hatua Niliyopiga Ilinivunja Minyororo Ya Uchawi
  • Niliibiwa Gari Yangu Usiku, Lakini Hatua Niliyopiga Ilifanya Wezi Wenyewe Walirudishe Hadi Getini
  • Nilipoteza Mume Wangu Kwa Mpango wa Kando ila Kitu Nilichojaribu Kilimfanya Aombe Radhi Hadharani
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » Prof. Makulilo: Watanzania Wajiandae kwa Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050
Habari za Kitaifa

Prof. Makulilo: Watanzania Wajiandae kwa Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050

Mbeya YetuBy Mbeya YetuSeptember 17, 2025No Comments3 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Mbeya – Mwenyekiti wa Kongamano na Mgoda wa Kigoda cha Uprofesa cha Mwalimu J.K. Nyerere katika Taaluma za Umajumui wa Afrika, Profesa Alexander Makulilo, amezungumza na waandishi wa habari mkoani Mbeya akitoa mwito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika maandalizi ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Prof. Makulilo alizungumza leo wakati akitoa taarifa rasmi kuhusu Kongamano la Uchumi Jumuishi kuelekea Dira 2050, ambalo limeandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kupitia Kigoda cha Uprofesa cha Mwalimu J.K. Nyerere kwa kushirikiana na Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP Centre). Kongamano hilo limepangwa kufanyika tarehe 18 Septemba 2025, katika Ukumbi wa Nkrumah Lecture Theatre wa Chuo Kikuu Mzumbe – Ndaki ya Mbeya, kuanzia saa 5:00 asubuhi.

Umuhimu wa Kongamano

Akieleza sababu za kuandaliwa kwa kongamano hilo, Prof. Makulilo amesema uhitaji wake unatokana na mambo makubwa matatu. Kwanza, ni uzinduzi wa Dira 2050 uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Julai 2025 jijini Dodoma. Wakati huo, Rais alisisitiza juu ya kuimarishwa kwa mijadala ya kitaifa kuhusu maendeleo na nafasi ya vijana katika kuibeba Tanzania mpya.

“Mheshimiwa Rais alisisitiza kuwa ni lazima mijadala ya maendeleo irejee katika jamii yetu. Vijana ndio nguvu kazi ya taifa letu, na wao ndio wanapaswa kujipanga vyema ili kutimiza malengo ya Dira 2050,” alisema Prof. Makulilo.

Sababu ya pili ni maandalizi ya bajeti ya mwaka wa fedha 2026/27, ambapo utekelezaji wa Dira 2050 utaanza rasmi. Kwa hiyo, kongamano litawajengea wananchi na wadau uwezo wa kutoa mapendekezo yatakayoingizwa kwenye utekelezaji wa mpango huo wa muda mrefu.

Sababu ya tatu ni maandalizi ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2025/26 – 2029/30), ambao utajengwa kwa kuzingatia mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika mpango unaomalizika (2020/21 – 2025/26).

Mada Kuu

Kongamano hili litajadili mada nne kuu:

  1. Maudhui na Vipaumbele vya Dira 2050.

  2. Msingi wa Uchumi Jumuishi kuelekea Dira 2050, kwa kuangazia mafanikio na changamoto za utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano unaomalizika.

  3. Nafasi ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP).

  4. Uzoefu wa Sekta Binafsi kama kichocheo cha maendeleo endelevu na jumuishi.

Prof. Makulilo alisema kuwa mijadala hii inalenga kuleta uelewa wa pamoja, ushirikiano na mshikamano wa kitaifa katika utekelezaji wa dira hiyo kubwa ya maendeleo.

Washiriki Wakuu

Kongamano litashirikisha wadau mbalimbali kutoka serikalini, sekta binafsi, asasi za kiraia, vyuo vikuu na washirika wa maendeleo. Baadhi ya watoa mada wakuu watakuwa:

  • Dkt. Fred Msemwa, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango.

  • Ndugu David Kafulila, Mkurugenzi Mtendaji wa PPP Centre.

  • Dkt. Gladness Salema, Mbunge katika Bunge la Afrika Mashariki.

  • Dkt. Mwajuma Hamza, Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Wanawake Tanzania.

  • Prof. Humphrey Moshi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

  • Dkt. Jasinta Kahyoza, Chuo Kikuu Mzumbe.

Mwito kwa Wananchi

Akihitimisha mkutano wake na waandishi wa habari, Prof. Makulilo ametoa mwito kwa wananchi na wadau wote kushiriki kikamilifu katika kongamano hilo, ama kwa kufika Mbeya au kupitia vyombo vya habari.

“Kongamano hili ni la kitaifa. Tunawaalika wananchi wote na wadau kutoka sekta mbalimbali kushiriki nasi, kujifunza na kutoa maoni. Taarifa zitakuwa zikifikishwa mubashara kupitia ITV, na kupitia YouTube za Jambo TV na Global TV,” alisema.

Kwa mujibu wake, kongamano hili ni sehemu ya kuandaa taifa kuelekea safari ya kujenga Tanzania jumuishi, shirikishi na endelevu ifikapo mwaka 2050.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

MATIBABU YA KIBINGWA YA HUDUMA MKOBA YA MADAKTARI WA DT. SAMIA UKOMBOZI MKUBWA KWA WANANCHI WA MKOA WA SONGWE.

September 15, 2025

DKT. TULIA: NITAHAKIKISHA JIMBO JIPYA LA UYOLE LINAPATA HALMASHAURI

September 14, 2025

TUME YATOA MWALIKO KWA WAANDISHI WA HABARI WENYE NIA YA KURIPOTI MATUKIO WAKATI WA UCHAGUZI

September 3, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025209

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024184

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025126

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025125
Don't Miss
Uncategorized

Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri

By Mbeya YetuSeptember 17, 20251

Baadhi yao waliniambia waziwazi kuwa hawawezi kuwa na mwanamke mwenye ulemavu. Nilipita katika aibu nyingi…

Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake

September 17, 2025

Kongamano la Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050 Kufanyika Mbeya

September 17, 2025

Prof. Makulilo: Watanzania Wajiandae kwa Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050

September 17, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri

September 17, 2025

Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake

September 17, 2025

Kongamano la Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050 Kufanyika Mbeya

September 17, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025209

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024184

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025126
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.