Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA

February 24, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
  • WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI
  • SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA
  • INEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO
  • INEC YAWAPIGA MSASA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA PERAMIHO, SHIWINGA
  • MAHUNDI AONYA VIJANA KUTELEKEZA WAZAZI WAO
  • NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATEMBELEA MAKAZI YA WAZEE, ASISITIZA UPENDO NA MATUNZO KWAKUWA WAZEE NI TUNU YA TAIFA.
  • DKT. MARY MWANJELWA ATOA USHUHUDA MZITO KWENYE MAZISHI YA ULIMBOKA MWAKILILI
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
Habari za Kitaifa

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

Mbeya YetuBy Mbeya YetuFebruary 25, 2026Updated:February 25, 2026No Comments4 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
Mbeya-Katika hatua kubwa ya mapinduzi ya kidigitali, Serikali iko katika hatua za mwisho kukamilisha zoezi la kuunganisha mifumo yake ili iweze kusomana na kubadilishana taarifa kwa ufanisi nchi nzima.

Hatua hiyo inalenga kuimarisha mazingira ya biashara kupitia maboresho ya teknolojia na kupunguza urasimu katika utoaji wa huduma.

Kuunga mkono mageuzi hayo, Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) imezindua mafunzo ya wiki moja mkoani Mbeya kuhusu matumizi ya mfumo mpya wa utoaji wa Vyeti vya Usaili (Certificate of Origin) kupitia Tanzania Chamber Portal (TCP).

Mafunzo hayo yanahusisha mikoa 14 ikiwemo Ruvuma, Morogoro na Dodoma, yakilenga kuwajengea uwezo viongozi wa TNCC pamoja na wafanyabiashara ili waweze kutumia mfumo huo kwa ufanisi.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa katika ufunguzi wa mafunzo hayo, mfumo huo utaongeza uwazi, kupunguza urasimu na kuharakisha utoaji wa huduma kwa wafanyabiashara, huku ukiunganisha moja kwa moja mifumo ya TNCC na Serikali kwa ufanisi zaidi.

Kwa upande wake, Afisa forodha Tunduma wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Gwakisa Mwaikenda, alisema mfumo huo shirikishi utaimarisha ukusanyaji wa mapato na kuziba mianya ya upotevu wa mapato kupitia ufuatiliaji wa kidigitali.

Naye Mwenyekiti wa TNCC Mkoa wa Mbeya, Bw. Erick Sichinga, alisema wafanyabiashara wa mkoa huo watanufaika kwa kiasi kikubwa kupitia mfumo huo mpya.

“Kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Mbeya, mfumo huu utapunguza gharama na muda wa kufuatilia Vyeti vya Usaili, hasa kwa wanaojihusisha na biashara za mipakani na masoko ya nje. Kupitia mfumo huu wa kidigitali, tutakuwa na uhakika wa ushindani bora zaidi kikanda na kimataifa, huku tukiongeza ufanisi na uwazi katika shughuli za biashara.”

Warsha hiyo inaratibiwa na TNCC kwa udhamini wa TradeMark Africa kwa kushirikiana na Serikali kupitia TRA, ikiwa ni sehemu ya mkakati mpana wa kuifanya Tanzania kuwa na mifumo ya kisasa, jumuishi na rafiki kwa biashara za kikanda na kimataifa.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA

February 24, 2026

INEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO

February 23, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025354

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Habari za Kitaifa

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

By Mbeya YetuFebruary 25, 20264

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato Mbeya-Katika hatua kubwa ya mapinduzi…

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA

February 24, 2026

INEC YAWAFUNDA WASIMAMIZI NA WASIMAMIZI WA SAIDIZI WA VITUO VYA KURA JIMBO LA PERAMIHO

February 23, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato

February 25, 2026

WANANCHI PERAMIHO, SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI

February 25, 2026

SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA CHUO CHA USTAWI WA JAMII, KUTOA WATAALAMU BORA

February 24, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025354

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.