#MbeyaYetuTv #TRA_Songwe #TRA_Mbeya
Watu Watano wamefariki dunia kutokana na ajali ya gari aina ya Landcruiser yenye nambari za Usajili STL 8825 Mali ya Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA ambalo liligonga Lori aina ya FUSO yenye nambari za usajili T 586 ANE.
Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Hanseketwa Wilayani Mbozi Mkoani Songwe majira ya saa 11 alfajiri leo Agosti 23,2021.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
Meneja Msaidizi Forodha Mkoa Songwe Omar Mzava amewataja marehemu kuwa ni Bernad Mushingi,ambaye ni Mfanyakazi wa Kituo cha Tunduma,Azaria Sivonike (Dereva wa Gari),Joel Mitondwa,Said Budi na Fahad Hassan wote wakiwa ni Wafanyakazi kituo cha Mbeya.
Trending
- Nilinunulia Mtoto Doli Ambayo Ilirudi Kutuhangaisha Sisi Wote, Njia Hii Ndio Iliyotuokoa
- Niliona Watu Wakigeuka Dhidi Yangu Bila Sababu Baadaye Nikagundua Chanzo cha Chuki Isiyoelezeka
- Nilipofahamu Ushirikina Usioonekana Kwenye Familia Yangu, Kila Nilichojuwa Kilikuwa Kinaogopesha
- Kila Nilipopata Pesa, Zilikuwa Zikitoweka Sababu Nilizoigundua Ilinishtua
- Ubishi Wageuka Rekodi: Bodaboda Afika Dar kwa Saa 10
- Huzuni Mbeya: Mwalimu Afia Nyumbani, Mwili Wakutwa Umeharibika Baada ya Wiki Tatu
- Mauaji ya Kikatili Mbeya: Watoto Watatu Wanyongwa kwa Ajili ya Ng’ombe
- Niliona Kila Kitu Kikikwama Nyumbani Mabadiliko Madogo Yalileta Utulivu Uliokosekana
