#MbeyaYetuTv #TRA_Songwe #TRA_Mbeya
Watu Watano wamefariki dunia kutokana na ajali ya gari aina ya Landcruiser yenye nambari za Usajili STL 8825 Mali ya Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA ambalo liligonga Lori aina ya FUSO yenye nambari za usajili T 586 ANE.
Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Hanseketwa Wilayani Mbozi Mkoani Songwe majira ya saa 11 alfajiri leo Agosti 23,2021.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
Meneja Msaidizi Forodha Mkoa Songwe Omar Mzava amewataja marehemu kuwa ni Bernad Mushingi,ambaye ni Mfanyakazi wa Kituo cha Tunduma,Azaria Sivonike (Dereva wa Gari),Joel Mitondwa,Said Budi na Fahad Hassan wote wakiwa ni Wafanyakazi kituo cha Mbeya.
Trending
- Nilijeruhiwa na Maneno ya Niliyekuwa Ninamwamini Safari ya Kujiponya Ilinisaidia Kuamua Hatua Ijayo
- JUMUIYA YA WAZAZI CCM MKOA WA MBEYA YAVUNJA UKIMYA YATOA TAMKO RASMI BAADA YA UCHAGUZI MKUU OKT 29
- Dkt. Tulia na watoto wake
- Nilidhani Msongo wa Mawazo Umenishinda, Nilijifunza Kuponya Akili Yangu
- Pombe Ilinifanya Nipoteze Kazi, Marafiki na Heshima—Safari ya Kuacha Ilikuwa Ngumu, Inawezekana
- MAHUNDI AWATUNUKU WAHITIMU 530 CHUO CHA MAENDELEO YA JAMII(CDTI)UYOLE
- Naibu Waziri Kundo: Mradi wa Maji Mto Kiwira Umefikia Asilimia 98
- Madaktari Walimwambia Ataishi na Maumivu Milele Lakini Ndani ya Miezi Sita Kila Kitu Kilibadilika
