#MbeyaYetuTv #TRA_Songwe #TRA_Mbeya
Watu Watano wamefariki dunia kutokana na ajali ya gari aina ya Landcruiser yenye nambari za Usajili STL 8825 Mali ya Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA ambalo liligonga Lori aina ya FUSO yenye nambari za usajili T 586 ANE.
Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Hanseketwa Wilayani Mbozi Mkoani Songwe majira ya saa 11 alfajiri leo Agosti 23,2021.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
Meneja Msaidizi Forodha Mkoa Songwe Omar Mzava amewataja marehemu kuwa ni Bernad Mushingi,ambaye ni Mfanyakazi wa Kituo cha Tunduma,Azaria Sivonike (Dereva wa Gari),Joel Mitondwa,Said Budi na Fahad Hassan wote wakiwa ni Wafanyakazi kituo cha Mbeya.
Trending
- CHUO CHA SAYANSI ZA AFYA K’S ROYAL CHAPONGEZWA KWA JUHUDI ZA KUKUZA UJUZI KWA WANAFUNZI KUKIDHI SOKO LA AJIRA NCHINI
- RUSHWA!! RUSHWA!! NI KILIO CHA KADA WA CCM MBEYA’ ‘AFUNGUKA JUU YA CHAGUZI ZA NDANI ZA CHAMA
- WALIPA KODI: WAOMBA KIGEZO CHA KUPANDISHA VYEO WAFANYAKAZI WA TRA KIBADILIKE
- Mkuu wa Chuo KZ Royal, Edward Azungumzia Mafanikio, Changamoto na Mikakati ya Kuimarisha Elimu Bora
- Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa
- Je unachangamoto ya saratani, umekata tamaa kutokana na kuumwa saratani. Sikiliza hii video
- Ushirikina wapelekea kutumia dawa za kulevya
- KADA WA CCM MBEYA ASIMULIA MIAKA 48 YA NEEMA NA MATUMANI MAKUBWA KWA WATANZANIA