AJIUA KWA KUJICHOMA MOTO.Mnamo tarehe 08.11.2021 majira ya saa 03:00 asubuhi huko Kijiji cha Ihombekilichopo Kata ya Utengule Usongwe, Tarafa ya Usongwe, Wilaya ya MbeyaVijijini, Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la MASHAKA SAIMON @YOKONIA [35] Mkazi wa Kijiji cha Ihombe alikutwa ndani ya nyumba yakeakiwa amefariki dunia kwa kuungua moto.
Ni kwamba kabla ya tukio hilo marehemu alikuwa akisumbuliwa na maradhi kwamuda mrefu na alitelekezwa na mke wake hali iliyopelekea kukata tamaa yamaisha na siku chache zilizopita alifanya jaribio la kujilipua kwa Petrol kabla yakuokolewa na mdogo wake. Upelelezi wa shauri hili unaendelea.Aidha ninatoa wito kwa wananchi/jamii kwa ujumla kutoa taarifa za mtu/watuwenye hali ya kukata tamaa ya Maisha kwa viongozi wao wa vijiji, mitaa kabla yakutokea madhara makubwa kama ilivyotokea kwa marehemu MASHAKASAIMON @ YOKONIA
Trending
- INEC YAWAPIGA MSASA MAKARANI WAONGOZAJI WAPIGA KURA PERAMIHO, SHIWINGA
- MAHUNDI AONYA VIJANA KUTELEKEZA WAZAZI WAO
- NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATEMBELEA MAKAZI YA WAZEE, ASISITIZA UPENDO NA MATUNZO KWAKUWA WAZEE NI TUNU YA TAIFA.
- DKT. MARY MWANJELWA ATOA USHUHUDA MZITO KWENYE MAZISHI YA ULIMBOKA MWAKILILI
- TAZAMA DKT TULIA NA DKT. MARY MWANJELWA WAKIIMBA WIMBO WA Umbili
- UTANI WA DKT. TULIA ACKSON WAACHA HISIA NZITO MAZISHI YA MWANAHABARI MKONGWE ULIMBOKA MWAKILILI
- MAHUNDI ASEMA SERIKALI INAWATHAMINI WAZEE KAMA HAZINA YA HEKIMA NA MAADILI YA TAIFA
- SUMA FYANDOMO MGENI RASMI BARAZA LA WANAWAKE (UWT) RUNGWE AWASHUKURU KWA MSHIKAMANO
