Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilinunulia Mtoto Doli Ambayo Ilirudi Kutuhangaisha Sisi Wote, Njia Hii Ndio Iliyotuokoa

January 18, 2026

Niliona Watu Wakigeuka Dhidi Yangu Bila Sababu Baadaye Nikagundua Chanzo cha Chuki Isiyoelezeka

January 18, 2026

Nilipofahamu Ushirikina Usioonekana Kwenye Familia Yangu, Kila Nilichojuwa Kilikuwa Kinaogopesha

January 17, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilinunulia Mtoto Doli Ambayo Ilirudi Kutuhangaisha Sisi Wote, Njia Hii Ndio Iliyotuokoa
  • Niliona Watu Wakigeuka Dhidi Yangu Bila Sababu Baadaye Nikagundua Chanzo cha Chuki Isiyoelezeka
  • Nilipofahamu Ushirikina Usioonekana Kwenye Familia Yangu, Kila Nilichojuwa Kilikuwa Kinaogopesha
  • Kila Nilipopata Pesa, Zilikuwa Zikitoweka Sababu Nilizoigundua Ilinishtua
  • Ubishi Wageuka Rekodi: Bodaboda Afika Dar kwa Saa 10
  • Huzuni Mbeya: Mwalimu Afia Nyumbani, Mwili Wakutwa Umeharibika Baada ya Wiki Tatu
  • Mauaji ya Kikatili Mbeya: Watoto Watatu Wanyongwa kwa Ajili ya Ng’ombe
  • Niliona Kila Kitu Kikikwama Nyumbani Mabadiliko Madogo Yalileta Utulivu Uliokosekana
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » KAMATI YA SIASA CCM WILAYA YA MBEYA YATEMBELEA UWANJA WA KIMATAIFA SONGWE YASIFU UTEKELEZAJI ILANI
Video Mpya

KAMATI YA SIASA CCM WILAYA YA MBEYA YATEMBELEA UWANJA WA KIMATAIFA SONGWE YASIFU UTEKELEZAJI ILANI

Mbeya YetuBy Mbeya YetuDecember 22, 2022No Comments3 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

#MbeyaYetuTv
Serikali inaendelea kujenga jengo kubwa la abiria katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe (SIA) uliopo katika kata ya Bonde la Songwe jimbo la Mbeya vijijini ikiwa ni mkakati wake wa kuboresha sekta ya usafiri wa anga ikiwemo kuweka mazingira rafiki kabla na baada ya abiria kusafiri kutoka na kwenda nchi mbalimbali.

Akitoa taarifa kwa kamati ya siasa ya halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Wilaya ya Mbeya vijijini (Kichama) kwenye ukaguzi wa mradi huo Kaimu Meneja wa wakala wa barabara Tanzania TANROADS Mhandisi Joel Samwel Mwabungu alisema ujenzi huo unatekelezwa na serikali kwa gharama ya zaidi ya Shilingi Bilioni 14 na wanatarajia kukamilisha jengo hilo kufikia march 2023.

Kuhusu uwekaji taa za kuongozea ndege kiongozi huyo alisema tayari zilishakamilika na zinatumika vizuri hivyo ndege zinaweza kutua na kuanza safari usiku na mchana.

Wajumbe wa kamati ya siasa akiwemo Danieli Kapusi, Willium Simwali na Subiraga Mwangoka walieleza kuridhishwa kwao na utekelezwaji miradi mbalimbali kwenye uwanja huo katika kupanua wigo wa kuwahudumia wasafiri.

Michael Ngailo ni Diwani wa Kata ya Bonde la Songwe ulipo uwanja wa ndege wa Songwe alisema uwanja huo umekuwa na faida kwa jamii isipokuwa changamoto ni wanafunzi wa eneo la Iwejele kuzuiliwa kupita kwenye eneo la uwanja kwenda shuleni baada ya mamlaka kujenga uzio kuzunguka uwanja huo na kuiomba serikali kupitia wizara ya uchukuzi kutekeleza ahadi zao kwa wananchi wa Kata ya Bonde la Songwe Mbeya vijijini.

Msafara wa Kamati ya siasa uliongozwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mbeya vijijini Akimu Sebastian Mwalupindi ambapo baada ya kamati kukagua mfumo wa taa za kuongozea ndege uwanjani hapo na baadaye kukagua jengo la abiria alisema utekelezaji wa ilani ya chama hicho ni wa kiwango cha juu na kinachoridhisha.

Pamoja na hayo CCM wilaya ya Mbeya vijijini kupitia Mwenyekiti Mwalupindi imetumia ziara hiyo ya kikazi kumpongeza Rais Dkt. Samia kwa kuchaguliwa kwa kura nyingi kuwa Mwenyekiti wa Chama (CCM) Taifa katika uchaguzi wa hivi karibuni.

Pia imempongeza Rais Samia kwa kuendelea kusimamia ipasavyo utekelezwaji miradi mbalimbali nchini katika kuwatumikia wananchi hususani katika sekta za miundombinu ya usafiri, Maji, Afya, Kilimo na Elimu.

Jengo hilo la abiria linajengwa kwa thamani kwa zaidi ya shilingi bilioni 14 na kampuni ya Kichina ambapo pamoja na miradi mingine ya uwanja wa ndege ya Run Ways na taa za kuongozea ndege jumla yake ni zaidi ya shilingi bilioni 30 zitakazotumika katika miradi hiyo.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Ubishi Wageuka Rekodi: Bodaboda Afika Dar kwa Saa 10

January 17, 2026

Huzuni Mbeya: Mwalimu Afia Nyumbani, Mwili Wakutwa Umeharibika Baada ya Wiki Tatu

January 16, 2026

Mauaji ya Kikatili Mbeya: Watoto Watatu Wanyongwa kwa Ajili ya Ng’ombe

January 16, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025305

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025243

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024217

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025135
Don't Miss
Uncategorized

Nilinunulia Mtoto Doli Ambayo Ilirudi Kutuhangaisha Sisi Wote, Njia Hii Ndio Iliyotuokoa

By Mbeya YetuJanuary 18, 20260

Nilidhani ilikuwa ni zawadi ya kawaida tu. Doli nzuri, ya rangi laini, macho yanayong’aa kama…

Niliona Watu Wakigeuka Dhidi Yangu Bila Sababu Baadaye Nikagundua Chanzo cha Chuki Isiyoelezeka

January 18, 2026

Nilipofahamu Ushirikina Usioonekana Kwenye Familia Yangu, Kila Nilichojuwa Kilikuwa Kinaogopesha

January 17, 2026

Kila Nilipopata Pesa, Zilikuwa Zikitoweka Sababu Nilizoigundua Ilinishtua

January 17, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilinunulia Mtoto Doli Ambayo Ilirudi Kutuhangaisha Sisi Wote, Njia Hii Ndio Iliyotuokoa

January 18, 2026

Niliona Watu Wakigeuka Dhidi Yangu Bila Sababu Baadaye Nikagundua Chanzo cha Chuki Isiyoelezeka

January 18, 2026

Nilipofahamu Ushirikina Usioonekana Kwenye Familia Yangu, Kila Nilichojuwa Kilikuwa Kinaogopesha

January 17, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025305

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025243

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024217
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.