Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Vibaka Wamvamia Mwandishi Rashid Mkwinda wa Mbeya Yetu Ajeruhiwa Vibaya Kichwani na Kulazwa

January 22, 2026

Boss Amtesa Mfanyikazi Bila Kujua Ndiye Mke Anayetakiwa Kumuoa, Yaliyojiri Ni Haya

January 22, 2026

Mama Wa Kambo Apata Usaidizi Wa Kudumu Baada Ya Kupata Mateso Kutoka Kwa Mabinti Wakorofi

January 22, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Vibaka Wamvamia Mwandishi Rashid Mkwinda wa Mbeya Yetu Ajeruhiwa Vibaya Kichwani na Kulazwa
  • Boss Amtesa Mfanyikazi Bila Kujua Ndiye Mke Anayetakiwa Kumuoa, Yaliyojiri Ni Haya
  • Mama Wa Kambo Apata Usaidizi Wa Kudumu Baada Ya Kupata Mateso Kutoka Kwa Mabinti Wakorofi
  • Nyota Yangu Ilibiwa na Rafiki Yangu Wa Karibu Lakini Nilipata Mtaalam Aliyerejesha Kila Kitu Nilichopoteza
  • Alinitumia Uchawi Mbaya Nilijaribu Kujilinda Lakini Nilishindwa, Nilihisi Hakuna Njia Suluhisho Hili Lilirudisha Amani Yangu
  • Nilipoteza Kazi, Biashara na Marafiki Lakini Bahati Iliporudi Kila Kitu Kilifuata
  • Walinitakia Mabaya Kwenye Giza Lakini Nuru Ilipowaka Walikimbia
  • Tuligombana Kila Siku Ndani ya Ndoa Nilipoondoa Kitu Kimoja Kisichoonekana, Amani Ilirudi Nyumbani
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » BILIONI NNE KUANZA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA UKEREWE
Uncategorized

BILIONI NNE KUANZA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA UKEREWE

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMarch 13, 2024No Comments8 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya imetenga Tsh: Bilioni Nne katika bajeti ya Mwaka huu 2023/24 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Ukerewe Mkoani Mwanza ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za Afya ikiwemo huduma za Kibingwa.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema hayo leo Machi 13, 2024 wakati wa ziara katika Mkoa wa Mwanza alipoambatana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Stanslaus Nyongo.

“Tunamshukuru sana Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan, tunapoelekea Miaka Mitatu ya Rais Samia kwakweli amefanya mambo makubwa sana katika Sekta ya Afya ikiwemo kutenga fedha kiasi cha Shilingi Bilioni Nne kwa ajili ya kujenga Hospitali mpya ya Rufaa ya Ukerewe ambayo itakua na huduma zote ikiwemo huduma za Kibingwa.” Amesema Waziri Ummy

Na. WAF – Mwanza

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya imetenga Tsh: Bilioni Nne katika bajeti ya Mwaka huu 2023/24 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Ukerewe Mkoani Mwanza ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za Afya ikiwemo huduma za Kibingwa.

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema hayo leo Machi 13, 2024 wakati wa ziara katika Mkoa wa Mwanza alipoambatana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Stanslaus Nyongo.

“Tunamshukuru sana Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan, tunapoelekea Miaka Mitatu ya Rais Samia kwakweli amefanya mambo makubwa sana katika Sekta ya Afya ikiwemo kutenga fedha kiasi cha Shilingi Bilioni Nne kwa ajili ya kujenga Hospitali mpya ya Rufaa ya Ukerewe ambayo itakua na huduma zote ikiwemo huduma za Kibingwa.” Amesema Waziri Ummy

Amesema, fedha hizo zimepelekwa Mkoani watangaze tenda ya kupata mshauri na mkandarasi wa kujenga Hospitali hiyo ili watu wa Ukerewe wapate huduma zote za Afya karibu ikiwemo huduma za Kibingwa katoka Hospitali ya Ukerewe.

Waziri Ummy amesema kazi ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaonekana kwenye dawa, vifaa tiba, kwenye watumishi pamoja na maeneo mengine mengi makubwa aliyoyafanya katika Sekta ya Afya.

Aidha, Waziri Ummy ameutaka uongozi wa Mkoa wa Mwanza kuendelea kuimarisha miundombinu ya maji taka, maji safi pamoja na kutoa elimu ili wananchi wajikinge na magonjwa ya milipuko ikiwemo ugonjwa wa Kipindupindu.

“Niupongeze sana Mkoa wa Mwanza kwa mapambano dhidi ya ugonjwa wa Kipindupindu ambao uliukumba Mkoa huo na kupelekea watu Watatu kupoteza maisha kutokana na ugonjwa huo baada ya kuchelewa kwenda kwenye kituo cha kutolea huduma za Afya.” Amesema Waziri Ummy

Pia, Waziri Ummy amesisitiza kwa Halmashauri pamoja na wadau katika Sekta ya Afya kuajiri watumishi wa Afya wa mikataba ili kuongeza idadi ya watumishi na wananchi wapate huduma bora na kwa haraka.

Mwisho, Waziri Ummy ametoa rai kwa Watanzania kuzingatia ulaji wa vyakula ikiwa ni pamoja na kupunguza matumizi ya sukari, chumvi a mafuta, kuacha tabia bwete, kufanya mazoezi ili kupunguza magonjwa Yasiyoambukiza ikiwemo Kisukari na Shinikizo la Juu la damu kwa kuwa maradhi hayo ni gharama kubwa kuyatibu.

 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Boss Amtesa Mfanyikazi Bila Kujua Ndiye Mke Anayetakiwa Kumuoa, Yaliyojiri Ni Haya

January 22, 2026

Mama Wa Kambo Apata Usaidizi Wa Kudumu Baada Ya Kupata Mateso Kutoka Kwa Mabinti Wakorofi

January 22, 2026

Nyota Yangu Ilibiwa na Rafiki Yangu Wa Karibu Lakini Nilipata Mtaalam Aliyerejesha Kila Kitu Nilichopoteza

January 21, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025309

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025244

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024219

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025136
Don't Miss
Video Mpya

Vibaka Wamvamia Mwandishi Rashid Mkwinda wa Mbeya Yetu Ajeruhiwa Vibaya Kichwani na Kulazwa

By Mbeya YetuJanuary 22, 20262

Mkazi wa eneo la Soweto, jijini Mbeya, Rashidi Mkwinda, ambaye ni mwandishi wa habari wa Mbeya Yetu Online TV, amesimulia tukio la kuvamiwa na kupigwa kichwani na watu wanaodhaniwa kuwa vibaka majira ya saa sita usiku.

Amesema alikuwa akirejea nyumbani baada ya kudownload faili kwenye kompyuta, ndipo alipofuatwa na watu hao na kushambuliwa wakati akifungua geti la nyumba yake. Katika tukio hilo alipigwa mara kadhaa kichwani, akaanguka chini na kupoteza fahamu kwa muda, kisha kuibiwa simu ya mkononi pamoja na fedha.

Baada ya kupata msaada kutoka kwa majirani, alikimbizwa hospitalini ambako alishonwa majeraha sehemu mbalimbali za mwili na kufanyiwa kipimo cha CT Scan, huku majibu yakitarajiwa kutoka leo.

Mkwinda ametoa wito kwa mamlaka husika kuchukua hatua madhubuti dhidi ya vitendo vya kihalifu vinavyoendelea kushamiri mitaani.

Boss Amtesa Mfanyikazi Bila Kujua Ndiye Mke Anayetakiwa Kumuoa, Yaliyojiri Ni Haya

January 22, 2026

Mama Wa Kambo Apata Usaidizi Wa Kudumu Baada Ya Kupata Mateso Kutoka Kwa Mabinti Wakorofi

January 22, 2026

Nyota Yangu Ilibiwa na Rafiki Yangu Wa Karibu Lakini Nilipata Mtaalam Aliyerejesha Kila Kitu Nilichopoteza

January 21, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Vibaka Wamvamia Mwandishi Rashid Mkwinda wa Mbeya Yetu Ajeruhiwa Vibaya Kichwani na Kulazwa

January 22, 2026

Boss Amtesa Mfanyikazi Bila Kujua Ndiye Mke Anayetakiwa Kumuoa, Yaliyojiri Ni Haya

January 22, 2026

Mama Wa Kambo Apata Usaidizi Wa Kudumu Baada Ya Kupata Mateso Kutoka Kwa Mabinti Wakorofi

January 22, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025309

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025244

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024219
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.