Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Mradi wa Soko la Matola Wakwama, Meya na MNEC Wakanusha Kukamilika Mei

February 5, 2026

JK KWA MFALME MSWATI III KUJADILI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA KWA NCHI WANACHAMA WA ECSA

February 4, 2026

Halmashauri Yaipongeza Mbeya UWSA Kwa Mradi wa Maji, Asema Utakuza Uwekezaji

February 4, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Mradi wa Soko la Matola Wakwama, Meya na MNEC Wakanusha Kukamilika Mei
  • JK KWA MFALME MSWATI III KUJADILI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA KWA NCHI WANACHAMA WA ECSA
  • Halmashauri Yaipongeza Mbeya UWSA Kwa Mradi wa Maji, Asema Utakuza Uwekezaji
  • Mpango wa Maendeleo 2026/27: Kasaka Apongeza Mafanikio, Aomba Maboresho
  • Msafara Wasimama Soweto, Mbunge Mwalunenge Aamuru TANROADS Kuondoa Dimbwi la Miaka 3 Mara Moja
  • CCM Miaka 49: Mbunge wa Mbarali Akabidhi Mashuka Kituo cha Afya Utengule
  • Dkt. Tulia Ackson Atoa Msaada wa Vifusi Roli 10 kwa Ukarabati wa Barabara ya Chanyasi
  • TGNP na CARE Watoa Mafunzo ya Mabadiliko ya Tabia Nchi kwa Jamii Mbeya
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home ยป KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI,MALIASILI NA UTALII YARIDHISHWA NA MRADI WA UVIKO-19 PUGU KAZIMZUMBWI
Uncategorized

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI,MALIASILI NA UTALII YARIDHISHWA NA MRADI WA UVIKO-19 PUGU KAZIMZUMBWI

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMarch 16, 2024No Comments9 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeridhishwa na matumizi ya fedha za mradi wa UVIKO-19 za kuboresha miundombinu ya utalii katika Msitu wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Pugu Kazimzumbwi uliogharimu takribani shilingi milioni 579.1
Hayo yamesemwa leo Machi 16, 2024 na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Najma Giga walipofanya ziara ya kukagua miradi iliyotekelezwa na Wakala ya Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika msitu huo.

“Kamati imeridhishwa na matumizi ya fedha za UVIKO-19 hasa katika ujenzi wa kituo cha taarifa za utalii, ukiliangalia lina thamani halisi ya fedha” Mhe. Najma amesisitiza.

Aidha, ameitaka TFS kuboresha miundombinu ya barabara pamoja na kuongeza matangazo ya eneo hilo ili kuvutia watalii wengi zaidi.

Naye, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) amesema kuwa msitu wa Pugu Kazimzumbwi ni muhimu kiikolojia, kiutamaduni na kiuchumi kwa jamii ya Kisarawe, Mkuranga, Dar es Salaam na maeneo mengine.

Pia, amesema kuwa msitu huo una faida katika kulinda vyanzo vya maji na kupatikana kwa hewa safi.

Mhe. Kairuki amefafanua kuwa ili kukuza shughuli za utalii katika msitu huo, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya barabara pamoja na kufungua barabara zaidi za kutembelea watalii na kupanda mimea tiba itakayotumika kama tiba ya asili.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeridhishwa na matumizi ya fedha za mradi wa UVIKO-19 za kuboresha miundombinu ya utalii katika Msitu wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Pugu Kazimzumbwi uliogharimu takribani shilingi milioni 579.1

Hayo yamesemwa leo Machi 16, 2024 na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Najma Giga walipofanya ziara ya kukagua miradi iliyotekelezwa na Wakala ya Huduma za Misitu Tanzania (TFS) katika msitu huo.

“Kamati imeridhishwa na matumizi ya fedha za UVIKO-19 hasa katika ujenzi wa kituo cha taarifa za utalii, ukiliangalia lina thamani halisi ya fedha” Mhe. Najma amesisitiza.

Aidha, ameitaka TFS kuboresha miundombinu ya barabara pamoja na kuongeza matangazo ya eneo hilo ili kuvutia watalii wengi zaidi.

Naye, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) amesema kuwa msitu wa Pugu Kazimzumbwi ni muhimu kiikolojia, kiutamaduni na kiuchumi kwa jamii ya Kisarawe, Mkuranga, Dar es Salaam na maeneo mengine.

Pia, amesema kuwa msitu huo una faida katika kulinda vyanzo vya maji na kupatikana kwa hewa safi.

Mhe. Kairuki amefafanua kuwa ili kukuza shughuli za utalii katika msitu huo, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya barabara pamoja na kufungua barabara zaidi za kutembelea watalii na kupanda mimea tiba itakayotumika kama tiba ya asili.

Kwa upande wake Kamishna Uhifadhi wa Wakala ya Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo amesema fedha za UVIKO-19 zilitengwa kwa ajili ya kufungua barabara mpya yenye urefu wa kilomita 12 kutoka Kimani- Maguruwe, ujenzi wa lango la kuingilia lenye ofisi, kituo cha taarifa za utalii, ofisi ya malipo, kibanda cha mlinzi na vyoo.

Ziara hiyo imehudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi pamoja na Watendaji na Menejimenti ya Wakala ya Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Nilipata Miscarriage Mara Tano Hadi Nikapoteza Ndoto Zangu Za Kuwa Mama Mpaka Nilipopata Usaidizi Usio na Madhara

January 25, 2026

Nilifanya Kazi Kwa Miaka Miwili Bila Kupata Promotion Ila Nilijitafutia Hiyo Promotion Mwenyewe

January 25, 2026

Ndoa Yangu Ilikuwa Karibu Kuvunjika Lakini Siri Hii ya Mwisho Iliokoa Mapenzi Yetu

January 24, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025330

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025251

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024226

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025139
Don't Miss
Video Mpya

Mradi wa Soko la Matola Wakwama, Meya na MNEC Wakanusha Kukamilika Mei

By Mbeya YetuFebruary 5, 20260

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa, Ndg. Salim Abri Asas, ameonyesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa Mradi wa Soko la Matola jijini Mbeya, akieleza kuwa haiwezekani kukamilika mwezi Mei kama ilivyopangwa.
Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi katika maadhimisho ya miaka 49 ya CCM, Asas alisema mradi unasuasua licha ya fedha kuwepo. Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya, Mhe. Dk. Mohamed Issa, alimweleza kuwa mkandarasi ameshindwa kusimamia fedha za mradi ipasavyo.
Kwa upande wake, MNEC Ndg. Ndele Mwaselela alisema idadi ndogo ya wafanyakazi na kasi ndogo ya ujenzi ni sababu kuu zinazoathiri ukamilishaji wa mradi.
Ndg. Asas alisema atawasilisha taarifa ya kweli kwa mamlaka husika, akisisitiza kuwa hatakubali kutoa taarifa ya kukamilika kwa mradi wakati hali halisi ni tofauti.

JK KWA MFALME MSWATI III KUJADILI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA KWA NCHI WANACHAMA WA ECSA

February 4, 2026

Halmashauri Yaipongeza Mbeya UWSA Kwa Mradi wa Maji, Asema Utakuza Uwekezaji

February 4, 2026

Mpango wa Maendeleo 2026/27: Kasaka Apongeza Mafanikio, Aomba Maboresho

February 4, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Mradi wa Soko la Matola Wakwama, Meya na MNEC Wakanusha Kukamilika Mei

February 5, 2026

JK KWA MFALME MSWATI III KUJADILI UPATIKANAJI WA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA KWA NCHI WANACHAMA WA ECSA

February 4, 2026

Halmashauri Yaipongeza Mbeya UWSA Kwa Mradi wa Maji, Asema Utakuza Uwekezaji

February 4, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025330

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025251

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024226
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.