Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Mbeya Zonal: Mafunzo ya Dharura Yaendelea Kuimarisha Uokozi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini

November 26, 2025

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA

November 26, 2025

*DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA*

November 26, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Mbeya Zonal: Mafunzo ya Dharura Yaendelea Kuimarisha Uokozi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini
  • WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA
  • *DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA*
  • WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI
  • Karejesha tabasamu la uso wake na ndoa yake
  • HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAANZA RASMI KUTOA MAFUNZO YA HUDUMA ZA DHARURA KWA LENGO LA KUOKOA MAISHA NA KUPUNGUZA ATHARI ZA AJALI NA DHARURA ZA KIAFYA NYANDA ZA JUU KUSINI
  • TANZANIA NA QATAR ZASAINI HATI YA MAKUBALIANO YA KUTAMBULIANA VYETI VYA MABAHARIA
  • EDEN KATININDA: ”MNUNUZI MASHUHURI WA PARETO NCHINI ATOA SOMO KWA WAKULIMA WA ZAO LA PARETO”
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » DARAJA LA MINYUGHE, WILAYANI IKUNGI, SINGIDA KUFUNGUA FURSA ZA KIUCHUMI
Habari za Kitaifa

DARAJA LA MINYUGHE, WILAYANI IKUNGI, SINGIDA KUFUNGUA FURSA ZA KIUCHUMI

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMarch 24, 2024No Comments9 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Serikali imekamilisha ujenzi wa daraja linalounganisha Kata ya Minyughe na Makilawa, katika wilaya ya Ikungi mkoani Singida, lililokatika miaka mitatu iliyopita, na hivyo kuathiri shughuli za kiuchumi na upatikanaji wa huduma za kijamii ikiwemo afya na elimu. Kukamilika kwa daraja hilo la chuma (Mibey Bridge) lenye urefu wa mita 30 lililogharimu zaidi ya Sh. Bilioni 1.6/-katika barabara ya Mtamaa-Minyughe hadi Mtavira, Wilayani Ikungi, litaenda kufungua fursa ya kiuchumi kwa wananchi wa kata hızo.Meneja wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA), Mkoa wa Singida, Mhandisi Ibrahim Kibasa, alisema kukamilisha uunganishaji wa vyuma kwa ajili ya daraja hilo, kumewezesha mto Minyughe kufunguka, na hivyo kutoa fursa kwa shughuli za uchukuzi kuendelea kati ya maeneo ya vijijini na makao makuu ya mkoa.Mhandisi Kibasa alisema kuwa, sasa wananchi wa kata tatu zinazounganishwa na daraja hilo, wataweza kuzikabili changamoto mbalimbali, zilizokwamisha shughuli zao, hususani wakati wa masika, kutokana na mto kufurika maji, kiasi cha kutishia usalama wao wakati wa kuvuka.

Ikungi

Serikali imekamilisha ujenzi wa daraja linalounganisha Kata ya Minyughe na Makilawa, katika wilaya ya Ikungi mkoani Singida, lililokatika miaka mitatu iliyopita, na hivyo kuathiri shughuli za kiuchumi na upatikanaji wa huduma za kijamii ikiwemo afya na elimu.

Kukamilika kwa daraja hilo la chuma (Mibey Bridge) lenye urefu wa mita 30 lililogharimu zaidi ya Sh. Bilioni 1.6/-katika barabara ya Mtamaa-Minyughe hadi Mtavira, Wilayani Ikungi, litaenda kufungua fursa ya kiuchumi kwa wananchi wa kata hızo.

Meneja wa Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA), Mkoa wa Singida, Mhandisi Ibrahim Kibasa, alisema kukamilisha uunganishaji wa vyuma kwa ajili ya daraja hilo, kumewezesha mto Minyughe kufunguka, na hivyo kutoa fursa kwa shughuli za uchukuzi kuendelea kati ya maeneo ya vijijini na makao makuu ya mkoa.

Mhandisi Kibasa alisema kuwa, sasa wananchi wa kata tatu zinazounganishwa na daraja hilo, wataweza kuzikabili changamoto mbalimbali, zilizokwamisha shughuli zao, hususani wakati wa masika, kutokana na mto kufurika maji, kiasi cha kutishia usalama wao wakati wa kuvuka.

” Sehemu ya fedha hizo ni bajeti mwaka ya mwaka huu ambapo tumejenga madaraja ikiwemo daraja hili la Minyughe,daraja hili limekuwa likiwasumbua wananchi takribani miaka mitatu na hivyo kukwamisha utekelezaji wa shughuli za kiuchumi kwa wananchi wa Kata tatu pamoja na Mkoa wa jirani wa Tabora, katika wilaya ya Uyui, inayopakana na wilaya hii ya Ikungi, “alisema.
**
Aidha, Mhandisi Kibasa alisema, ujenzi wa daraja hilo umetokana na bajeti ya mwaka iliyotengwa, kiasi cha Sh. Bilioni 4.4/- katika wilaya ya Ikungi kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya barabara na madaraja, katika halmashauri ya Wilaya hiyo.

Baadhi ya wananchi walioshuhudia kukamilika kwa kazi hiyo, akiwemo Bi. Elizabeth Bakari wa Kijiji cha Minyughe, na diwani wa Kata Minyughe , Mhe. Nelson Kiwesi, waliishukuru Serikali kwa mradi huo, ambao baada ya kukamilika, unakwenda kuondoa adha ya usafiri, hasa kwa wajawazito.

Bi. Elizabeth alibainisha kuwa, iliwalazimu kukosa huduma muhimu ikiwemo zile za afya katika kituo cha afya kilichopo ng’ambo ya pili, pia watoto wao kuhatarisha maisha wakati wa kwenda shule na kurudi nyumbani, hususani nyakati za masika, kutokana na mto Minyughe kufurika maji.

Alisema kukamilika kwa daraja hilo, sasa watoto wao hawatakosa masomo, wajawazito na wagonjwa wataenda kupata Huduma za matibabu kwenye kituo cha afya kilichopo ng’ambo ya daraja hilo pamoja na kufungua shughuli za usafirishaji wa mazao na watu.

“Kujengwa kwa daraja hili, ni mafanikio makubwa kwa watoto wetu waliolazimika kushindwa kuhudhuria vipindi vya masomo yao darasani. Serikali itaongeza mapato kutokana na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi , ikiwemo kilimo, na mali asili kupitia misitu, wazalishaji wamerahisishiwa mawasiliano kati ya upande mmoja na ule wa pili,” alisema.

Awali Mhandisi Mshauri Ebenezer Mollel, kutoka TARURA makao makuu, kitengo cha madaraja, alisema daraja hilo ni la tatu kujengwa hapa nchini, likitanguliwa na mengine lililopo Kihansi, huko Kilombero na lile la Mbuchi, kule Kibiti, mkoani Pwani.

Mhandisi Mollel alisema kuwa, madaraja hayo ni ya aina ya kipekee, hivyo kabla ya ujenzi hulazimika kuwapatia mafunzo Wahandisi wa TARURA na TANROADS, lengo likiwa kuwajengea uwezo, kwa ajili ya kupata ujuzi na utaalamu zaidi kuweza kumudu majukumu yao, kulingana na kukua kwa teknolojia, huku wahandisi walioshiriki mafunzo hayo, wakifikia 42.

Kwa mujibu wa mhandisi Mollel, teknolojia ya daraja hilo ni ya kipekee, kutokana kujengwa likiwa ng’ambo ya pili, na baada ya kukamilika husukumwa hadi sehemu yake, kuunganisha kingo mbili, na kuwa tayari kwa ajili ya matumizi ya kivuko.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA

November 26, 2025

TANZANIA NA QATAR ZASAINI HATI YA MAKUBALIANO YA KUTAMBULIANA VYETI VYA MABAHARIA

November 26, 2025

DKT. MWIGULU: TANZANIA NI MALI YETU SOTE, SI MALI YA SERIKALI WALA CHAMA CHA SIASA

November 25, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025236

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025230

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024201

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025128
Don't Miss
Video Mpya

Mbeya Zonal: Mafunzo ya Dharura Yaendelea Kuimarisha Uokozi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini

By Mbeya YetuNovember 26, 20251

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imeanza rasmi kutoa mafunzo ya magonjwa ya Dharura na Mahututi kwa watoa huduma za afya, wanafunzi wa kada za Afya pamoja Jamii Nyanda za Juu Kusini kwa lengo la kuokoa maisha na kupunguza athari za ajali na dharura za kiafya.

Akiongea wakati wa kufungua mafunzo hayo leo tarehe 26 novemba,2025 katika kituo cha kutolea mafunzo hayo kwa vitendo kilichojengwa chini ya udhamini wa taasisi ya Abbott Fund, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Dkt. Godlove Mbwanji amesema, kuanzishwa kwa mafunzo hayo kutasaidia upatikanaji wa wataalamu wenye weredi kwani kumekuwa na ongezeko la wanafunzi wengi kuliko miundo mbinu ya kufundishia mafunzo haya kwa vitendo.

“…wote tunajua kwamba miaka ya karibuni kumekuwa na ongezeko la wanafunzi kwenye vyuo vyetu ambalo haliendi sambamba na miundombinu ya kufundishia kwa vitendo.” – Dkt. Mbwanji

Aidha Dkt. Mbwanji ameishukuru taasisi ya Abbott Fund Tanzania, Wizara ya Afya pamoja (EMAT) kwa ushirikiano katika ujenzi wa kituo hicho cha kutolea mafunzo hayo.

“…lilianza kama wazo na sasa linaonekana hivyo niwashukuru sana Abbott Fund Tanzania, Wizara ya afya pamoja na (EMAT) kwa kuratibu upatikanaji wa kituo hiki”. – Dkt. Mbwanji

Kwa upande wake Dkt. Raya Mussa, Meneja Mradi huduma za dharura akiongea kwa niaba ya Taasisi ya Abbott Fund Tanzania ameishukuru Wizara ya Afya kupitia Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya kwa ushirikiano waliouonyesha kwa kukubali ujenzi wa kituo ambacho kitawanufaisha watoa huduma za afya, wanafunzi pamoja wataalamu wote wanapatikana Kanda ya Nyanda za Juu Kusini katika idara za Magonjwa ya Dharura na Ajali kutokana na miundombinu pamoja na vifaa ya kisasa vinavyopatikana katika kituo hicho.

“…lengo la kituo hiki si kunufaisha watu wa ndani tu lakini pia itanufaisha wanafunzi pamoja na watu wengine watakaohitaji kujifunza mafunzo haya hata kama si watoa huduma za afya”. – Dkt. Raya Mussa

Dkt. Prosper Bashaka ni Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya amesema, maboresho ya upatikanaji wa huduma za dharura imekuwa ni kipaumbele kikubwa cha serikali, hivyo amewapongeza wadau wote walioshiriki katika jitihada za uanzishwaji wa kituo hicho cha kutolea mafunzo ya Magonjwa ya Dharura na Mahututi kwani kitaleta tija kwa hospitali na jamii hasa kwa wakazi wa Nyanda za Juu Kusini.

“…nitoe pongezi kwa wadau wote walioshiriki katika ujenzi wa kituo hiki kwani kitaleta tija kwa hospitali na zaidi wakazi wa Nyanda za Juu Kusini”. – Dkt. Prosper Bashaka.

Hadi sasa vituo hivyo vya kutolea mafunzo ya Magonjwa ya Dharura na Mahututi vimejengwa zaidi ya 6 nchi nzima kwa ushirikiano wa taasisi ya Abott Fund, Wizara ya Afya pamoja na EMART.

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA

November 26, 2025

*DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA*

November 26, 2025

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI

November 26, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Mbeya Zonal: Mafunzo ya Dharura Yaendelea Kuimarisha Uokozi Kanda ya Nyanda za Juu Kusini

November 26, 2025

WILAYA YA RUNGWE YAMKABIDHI RASMI MKANDARASI WA KAGWA GENERAL SUPPLIES KUANZA KUJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA KIWILA

November 26, 2025

*DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA*

November 26, 2025
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025236

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025230

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024201
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.