Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amefungua rasmi Mkutano Mkuu wa 148 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) uliofanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha CICG, Geneva nchini Uswisi leo tarehe 24 Machi, 2024.
Mkutano huo unatarajiwa kujadili Dhima Kuu ambayo ni “Matumizi ya Diplomasia ya Kibunge katika kuleta Amani na Maelewano Duniani”. Mkutano huo umehudhuriwa na Maspika wa Mabunge 48 na washiriki zaidi ya 1,500 na unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 27 Machi, 2024.
Huu unakuwa Mkutano wake wa kwanza kuufungua tangu achaguliwe kuwa Rais wa IPU katika Uchaguzi uliofanyika Oktoba 27, 2023 nchini Angola. 
Trending
- WADAU WATAKIWA KUUNGA MKONO MALEZI YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM
- Mwalunenge Achangia Milioni 3 Baada ya Wanawake MZRH Kutoa Mashine ya EEG
- Comfy Mum na TNCC Wawafariji Wakinamama Wodi ya Wanawake Hospitali ya Sinza
- Mbunge CCM,wapinzani waimarisha umoja,wajadili maendeleo ya wana Mbeya
- Dkt. Tulia Aunga Mkono Ujenzi wa Barabara Bombambili kwa Mifuko 100 ya Saruji na tripu 10 za mawe
- SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
- Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
- VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

