Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amefungua rasmi Mkutano Mkuu wa 148 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) uliofanyika katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha CICG, Geneva nchini Uswisi leo tarehe 24 Machi, 2024. Mkutano huo unatarajiwa kujadili Dhima Kuu ambayo ni “Matumizi ya Diplomasia ya Kibunge katika kuleta Amani na Maelewano Duniani”. Mkutano huo umehudhuriwa na Maspika wa Mabunge 48 na washiriki zaidi ya 1,500 na unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 27 Machi, 2024. Huu unakuwa Mkutano wake wa kwanza kuufungua tangu achaguliwe kuwa Rais wa IPU katika Uchaguzi uliofanyika Oktoba 27, 2023 nchini Angola.
Trending
- CHUNYA YAVUKA MALENGO YAKUSANYA ASILIMIA 142 MAPATO YA NDANI
- T 99 girls watua Hospitali Ya Wazazi Meta Watoa zawadi. Wampongeza Dkt. Mbwanji
- “Hofu Yatanda: Daktari Aishi Kwenye Gari Mbeya”
- MAHUNDI AHAMASISHA WATOTO WA KIKE KUSOMA STEM( Sayansi Teknolojia Uhandisi na Hisabati) na TEHAMA
- Mke wa Mbunge mstaafu Mbeya Afariki dunia Atimiza miaka 90 ni mama wa Meya wa jiji Dodoma
- Mafuriko Kilombero: Timu za Uokoaji Zafuatilia Nyumba kwa Nyumba, Shule Kufungwa Kwa Muda
- MAKANISA YAKUTANA MBEYA KUJADILIDILIANA NAMNA YA KUJIKWAMUA KIUCHUMI
- Tulia Trust Yatoa Msaada kwa Wahanga wa Mafuriko Kyela, Mbeya