Tarehe 27.11.2024 saa 12:30 jioni eneo la Mbembela Jijini Mbeya katika
barabara kuu ya Mbeya – Tunduma, Gari lori namba T.537 DNC na Tela
namba T.241 ARG aina FAW iliyokuwa imepakia madini ya Sulphur ikitokea
Dar es Salaam kuelekea Tunduma Mkoa wa Songwe ilipoteza uelekeo na
kugonga magari sita, bajaji nne, Pikipiki moja na kusababisha vifo vya watu
watatu, wawili papo hapo na mmoja amefariki dunia leo Novemba 28, 2024
akiwa anaendelea na matibabu.
Magari yaliyohusika katika ajali hiyo ni T.199 DYF Toyota Coaster, SU 44682
Toyota Double Cabin mali ya Shirika la Posta Mbeya iliyokuwa ikiendeshwa na
Fredy Mwasanga [48] mkazi wa Soweto, Gari T.134 DXK Toyota Double Cabin
iliyokuwa ikiendeshwa na Lusekelo Mwaseba [48] mkazi wa Sae, Gari T.370
ABN Toyota Land Cruiser, Gari T.344 BTS Toyota Cresta na Gari T.474
EHL/t.449 EHL aina ya FAW iliyokuwa ikiendeshwa na Alon Ruben [50] mkazi
wa Isanga.
Aidha, katika ajali hiyo Bajaji nne ziligongwa ambazo ni MC.446 DYK, MC.649
DWL, MC.138 DKC na MC.261 EBN na Pikipiki moja ambayo haijafahamika
namba zake za usajili. Waliofariki katika ajali hiyo bado hawajatambulika,
wawili jinsia ya kiume na mmoja jinsia ya kike. Majeruhi tisa wanaendelea na
matibabu katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.
Chanzo cha ajali ni uzembe wa Dereva kushindwa kulimudu Gari kwenye
eneo lenye mteremko. Jitihada za kumtafuta Dereva kwa kushirikiana na
mmiliki wa Gari zinaendelea.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea kutoa wito kwa madereva kuwa
makini na kufuata sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza
kuepukika.
Imetolewa na:
Benjamin Kuzaga – SACP
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.
Trending
- Nilipofahamu Ushirikina Usioonekana Kwenye Familia Yangu, Kila Nilichojuwa Kilikuwa Kinaogopesha
- Kila Nilipopata Pesa, Zilikuwa Zikitoweka Sababu Nilizoigundua Ilinishtua
- Ubishi Wageuka Rekodi: Bodaboda Afika Dar kwa Saa 10
- Huzuni Mbeya: Mwalimu Afia Nyumbani, Mwili Wakutwa Umeharibika Baada ya Wiki Tatu
- Mauaji ya Kikatili Mbeya: Watoto Watatu Wanyongwa kwa Ajili ya Ng’ombe
- Niliona Kila Kitu Kikikwama Nyumbani Mabadiliko Madogo Yalileta Utulivu Uliokosekana
- Bosi Wangu Alitaka Kuniangamiza Kwenye Kazi, Lakini Hatua Niliyopiga Ilimfanya Aniombe Msamaha
- Sikia Mchungaji huyu alivyosema na Wachawi(ABHALOSI KUFWINA INYAMA ZA BHAANDU MUUNDA MMYABHO)

