Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linapenda kutoa taarifa ya kifo kilichohusisha
watu watano wa familia moja huko Wilaya ya Chunya.
Ni kwamba mnamo 29.12.2024 saa 8:30 usiku katika Kitongoji cha Nkangi
kilichopo Kijiji cha Isangawana, Kata ya Matwiga, Tarafa ya Kipembawe,
Wilaya ya Chunya, watu watano wa familia moja ya Masiganya Scania [39]
mfugaji, mkazi wa Nkangi walifariki dunia baada ya kupigwa radi kwenye
kambi ya kuchungia Ng'ombe wakati wakiwa wamelala.
Waliofariki katika tukio hilo ni Balaa Scania [28], Kulwa Luweja [17], Masele
Masaganya [16], Hema Tati [10] na Manangu Ngwisu [18] wote wakazi wa
Kijiji cha Nkangi. Aidha, katika tukio hilo watu wengine watano walijeruhiwa
ambao ni Gulu Scania [30], Manyenge Masaganya [13], Seni Solo [13],
Paskali Kalezi [16] na Huzuni Kalezi [19] wote wakazi wa Kijiji cha Nkangi.
Chanzo cha tukio hilo ni mvua kubwa iliyonyesha usiku ikiambatana na radi
hivyo kusababisha vifo vya watu watano na wengine watano kujeruhiwa.
Majeruhi walikimbizwa katika Kituo cha Afya Isangawana kwa matibabu na
walitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani baada ya hali zao kuwa nzuri.
Trending
- CHAKAMWATA KUWAFIKISHA MAHAKAMANI CWT NA WAKURUGENZI
- JK AWASILISHA UJUMBE WA RAIS SAMIA KWA RAIS MUSEVENI WA UGANDA LEO JIJINI KAMPALA
- Spika wa Bunge la Tanzania aongoza Waombolezaji kutoa Rambirambi kwa Kifo cha Katibu wa Bunge la Zambia
- RAIS SAMIA AUNGWA MKONO NA WATUMISHI WA AFYA KATIKA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA NCHINI
- CHAUMMA YATANGAZA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025
- Tulia Trust yaendelea kutoa tabasamu kwa kujenga nyumba tatu katika kata za Itezi, Uyole na Igawilo
- Dkt. Tulia Ackson Afungua Kikao cha 39 cha Jukwaa la Wanawake wa IPU Jijini Tashkent
- VIONGOZI MBALIMBALI WASHIRIKI MAZISHI YA KATIBU WA UWT MKOA WA MBEYA