Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linapenda kutoa taarifa ya kifo kilichohusisha
watu watano wa familia moja huko Wilaya ya Chunya.
Ni kwamba mnamo 29.12.2024 saa 8:30 usiku katika Kitongoji cha Nkangi
kilichopo Kijiji cha Isangawana, Kata ya Matwiga, Tarafa ya Kipembawe,
Wilaya ya Chunya, watu watano wa familia moja ya Masiganya Scania [39]
mfugaji, mkazi wa Nkangi walifariki dunia baada ya kupigwa radi kwenye
kambi ya kuchungia Ng'ombe wakati wakiwa wamelala.
Waliofariki katika tukio hilo ni Balaa Scania [28], Kulwa Luweja [17], Masele
Masaganya [16], Hema Tati [10] na Manangu Ngwisu [18] wote wakazi wa
Kijiji cha Nkangi. Aidha, katika tukio hilo watu wengine watano walijeruhiwa
ambao ni Gulu Scania [30], Manyenge Masaganya [13], Seni Solo [13],
Paskali Kalezi [16] na Huzuni Kalezi [19] wote wakazi wa Kijiji cha Nkangi.
Chanzo cha tukio hilo ni mvua kubwa iliyonyesha usiku ikiambatana na radi
hivyo kusababisha vifo vya watu watano na wengine watano kujeruhiwa.
Majeruhi walikimbizwa katika Kituo cha Afya Isangawana kwa matibabu na
walitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani baada ya hali zao kuwa nzuri.
Trending
- Suzi alivyomrejesha mpenzi wake na wakafunga ndoa
- Jinsi unavyoweza kuibadilisha biashara yako na kukupa faida
- RAIS DKT. SAMIA AKIWASILI SKUA (TANGA) KWA KIKAO CHA NDANI NA VIONGOZI WA JWTZ
- WAZIRI MKUU- WATANZANIA TUNZENI AKIBA YA CHAKULA▪️Ahimiza matumizi ya mbolea na mbegu za mazao
- Ndipo akashinda Sh13 milioni kupitia betting
- WAZIRI ULEGA AAGIZA UPANUZI BARABARA YA TUNDUMA KWA HARAKA KUPUNGUZA MSONGAMANO WA MALORI MPAKANI
- HIVI NDIVYO MWILI WA MAREHEMU JENISTA MHAGAMA ULIVYOWASILI NA KUPOKEWA SONGEA MKOANI RUVUMA
- MTARO ULIOFUKIWA MTAA WA LUMBILA IWAMBI MBEYA WAFURIKA MAJI YA MVUA NA KUIBUA KIZAAZAA KWA WANANCHI

