Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linapenda kutoa taarifa ya kifo kilichohusisha
watu watano wa familia moja huko Wilaya ya Chunya.
Ni kwamba mnamo 29.12.2024 saa 8:30 usiku katika Kitongoji cha Nkangi
kilichopo Kijiji cha Isangawana, Kata ya Matwiga, Tarafa ya Kipembawe,
Wilaya ya Chunya, watu watano wa familia moja ya Masiganya Scania [39]
mfugaji, mkazi wa Nkangi walifariki dunia baada ya kupigwa radi kwenye
kambi ya kuchungia Ng'ombe wakati wakiwa wamelala.
Waliofariki katika tukio hilo ni Balaa Scania [28], Kulwa Luweja [17], Masele
Masaganya [16], Hema Tati [10] na Manangu Ngwisu [18] wote wakazi wa
Kijiji cha Nkangi. Aidha, katika tukio hilo watu wengine watano walijeruhiwa
ambao ni Gulu Scania [30], Manyenge Masaganya [13], Seni Solo [13],
Paskali Kalezi [16] na Huzuni Kalezi [19] wote wakazi wa Kijiji cha Nkangi.
Chanzo cha tukio hilo ni mvua kubwa iliyonyesha usiku ikiambatana na radi
hivyo kusababisha vifo vya watu watano na wengine watano kujeruhiwa.
Majeruhi walikimbizwa katika Kituo cha Afya Isangawana kwa matibabu na
walitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani baada ya hali zao kuwa nzuri.
Trending
- Nyuki Wazingira Nyumba yake Kisa Mume wa Mtu, Majirani Wadai Sio Tukio la Kawaida
- Harusi Yasimamishwa Baada ya Mama Mkwe Kupiga Mayowe Kanisani Sababu Yake Yakaa Siri kwa Saa 24
- Kila Mara Nilipopata Pesa, Zilikuwa Zikitoweka Nilibaini Sababu Baada ya Miezi Kadhaa
- Usiku Mmoja Urithi Wangu Mkubwa Ulipotea Na Niligundua Majirani Walikuwa Wakiandaa Uchawi Dhidi Yangu
- Nilivyogundua Siri Ya Kuweka Bahati Yangu Kwenye Biashara Niliyoianza Kutokuwa Na Kila Kitu
- Nilivyopata Mtoto Wa Kike Niliyemuhitaji Baada ya Miaka Ya Kutafuta Bila Mafanikio
- Salama za Rambirambi kwenye Msiba wa Dada yake MNEC Ndele Mwaselela jijini Mbeya
- Nilivyorejesha Furaha ya Kuwa Baba Baada ya Watoto Kunikataa Kwa Muda Mrefu

