Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linapenda kutoa taarifa ya kifo kilichohusisha
watu watano wa familia moja huko Wilaya ya Chunya.
Ni kwamba mnamo 29.12.2024 saa 8:30 usiku katika Kitongoji cha Nkangi
kilichopo Kijiji cha Isangawana, Kata ya Matwiga, Tarafa ya Kipembawe,
Wilaya ya Chunya, watu watano wa familia moja ya Masiganya Scania [39]
mfugaji, mkazi wa Nkangi walifariki dunia baada ya kupigwa radi kwenye
kambi ya kuchungia Ng'ombe wakati wakiwa wamelala.
Waliofariki katika tukio hilo ni Balaa Scania [28], Kulwa Luweja [17], Masele
Masaganya [16], Hema Tati [10] na Manangu Ngwisu [18] wote wakazi wa
Kijiji cha Nkangi. Aidha, katika tukio hilo watu wengine watano walijeruhiwa
ambao ni Gulu Scania [30], Manyenge Masaganya [13], Seni Solo [13],
Paskali Kalezi [16] na Huzuni Kalezi [19] wote wakazi wa Kijiji cha Nkangi.
Chanzo cha tukio hilo ni mvua kubwa iliyonyesha usiku ikiambatana na radi
hivyo kusababisha vifo vya watu watano na wengine watano kujeruhiwa.
Majeruhi walikimbizwa katika Kituo cha Afya Isangawana kwa matibabu na
walitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani baada ya hali zao kuwa nzuri.
Trending
- MWALUNENGE ATOA MILIONI 3 KUWAOKOA VIJANA WA KIWIRA BAADA YA TFS KUTAIFISHA VIFAA VYAO
- “MARUFUKU HUU UKAMATAJI TUMEKUBALIANA NA IGP” SIMBA CHAWENE
- WIZARA YA MAMBO YA NDANI YATOA ONYO MAANDAMANO KESHO/WAZIRI ATOA USHAURI KWA WANANCHI/MSIANDAMANE
- TANZANIA AND U.S. MOVE TO FINALISE MAJOR INVESTMENT AGREEMENTS
- “Hongera! Umeshinda JACKPOT ya Sh6,800,000”
- MFANYAKAZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA APATA TUZO YA MWANAFUNZI BORA WA SHAHADA YA UZAMILI YA UDAKTARI WA MENO MUHAS.
- Ujumbe wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu Maadhimisho ya Sikukuu ya Uhuru.
- Haikuwa tu safari ya kupona, bali safari ya kujikubali

