Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linapenda kutoa taarifa ya kifo kilichohusisha
watu watano wa familia moja huko Wilaya ya Chunya.
Ni kwamba mnamo 29.12.2024 saa 8:30 usiku katika Kitongoji cha Nkangi
kilichopo Kijiji cha Isangawana, Kata ya Matwiga, Tarafa ya Kipembawe,
Wilaya ya Chunya, watu watano wa familia moja ya Masiganya Scania [39]
mfugaji, mkazi wa Nkangi walifariki dunia baada ya kupigwa radi kwenye
kambi ya kuchungia Ng'ombe wakati wakiwa wamelala.
Waliofariki katika tukio hilo ni Balaa Scania [28], Kulwa Luweja [17], Masele
Masaganya [16], Hema Tati [10] na Manangu Ngwisu [18] wote wakazi wa
Kijiji cha Nkangi. Aidha, katika tukio hilo watu wengine watano walijeruhiwa
ambao ni Gulu Scania [30], Manyenge Masaganya [13], Seni Solo [13],
Paskali Kalezi [16] na Huzuni Kalezi [19] wote wakazi wa Kijiji cha Nkangi.
Chanzo cha tukio hilo ni mvua kubwa iliyonyesha usiku ikiambatana na radi
hivyo kusababisha vifo vya watu watano na wengine watano kujeruhiwa.
Majeruhi walikimbizwa katika Kituo cha Afya Isangawana kwa matibabu na
walitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani baada ya hali zao kuwa nzuri.
Trending
- MAHUNDI ASEMA SERIKALI INAWATHAMINI WAZEE KAMA HAZINA YA HEKIMA NA MAADILI YA TAIFA
- SUMA FYANDOMO MGENI RASMI BARAZA LA WANAWAKE (UWT) RUNGWE AWASHUKURU KWA MSHIKAMANO
- MAKAMU MWENYEKITI INEC NA WAJUMBE WA TUME WAMTEMBELEA RC SONGWE
- Dkt. Godlove Mbwanji, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, ashiriki kampeni ya kitaifa ya uwekezaji wa ndani.
- MBEYA YAANDIKA HISTORIA: NGazi ZA UMEME ZA KWANZA NYANDA ZA JUU KUSINI
- ZIMAMOTO WAOPOA MWILI WA KIJANA ALIYEDAIWA KUWA MWANAFUNZI WA CBE MBEYA
- Mvua na upepo mkali waathiri zaidi ya kaya 200 Mbeya
- TISEZA YASIFIA UWEKEZAJI WA BILIONI 8 WA BABITO TRADING COMPANY MBEYA

