Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Kijana Golden Kidumba (DON. G) Awagusa Watoto wa Mitaani kwa Chakula na Mavazi

November 19, 2025

Biashara ya mbao ilivyobadili maisha yake ikimpa utajiri

November 19, 2025

Rais Dkt Samia aongoza kikao kazi cha Mawaziri Naibu Mawaziri Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu

November 19, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Kijana Golden Kidumba (DON. G) Awagusa Watoto wa Mitaani kwa Chakula na Mavazi
  • Biashara ya mbao ilivyobadili maisha yake ikimpa utajiri
  • Rais Dkt Samia aongoza kikao kazi cha Mawaziri Naibu Mawaziri Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu
  • Safari ya kurejesha hamu ya tendo la ndoa kwa Zuhura iliyofanikiwa
  • Kutoka kusota hadi usukani wenye utajiri
  • Ikulu Dodoma: Rais Samia Azungumza na Mawaziri Baada ya Kuwaapisha
  • Alivyokabiliana na changamoto ya ukosefu wa hamu ya tendo hadi kuishinda
  • DKT. MWIGULU AKABIDHIWA OFISI RASMI
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MALIASILI, MAMBO YA NDANI ZATAKIWA KUSHIRIKIANA KUKUZA UTALII
Utalii na Utamaduni

MALIASILI, MAMBO YA NDANI ZATAKIWA KUSHIRIKIANA KUKUZA UTALII

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJanuary 24, 2025Updated:January 24, 2025No Comments2 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) (kushoto) na Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UN Tourism), Zurab Pololikashvili (kulia) na wakisaini Makubaliano ya Tanzania kuwa mwenyeji wa Kongamano la 2 la Kikanda la Utalii wa Vyakula la Shirika la Umoja wa Mataifa (The 2nd UN Tourism Regional Forum on Gastronomy Tourism for Africa) katika Makao Makuu ya Shirika la Utalii Duniani la Umoja wa Mataifa  jijini Madrid, Hispania leo Januari 24,2025.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) na Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UN Tourism), Zurab Pololikashvili na wakionyesha makubaliano waliosaini kuhusu Tanzania kuwa mwenyeji wa Kongamano la 2 la Kikanda la Utalii wa Vyakula la Shirika la Umoja wa Mataifa katika Makao Makuu ya Shirika la Utalii Duniani la Umoja wa Mataifa  jijini Madrid, Hispania leo Januari 24,2025.

Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UN Tourism), Zurab Pololikashvili akizungumza katika kikao kati yake na Ujumbe wa Tanzania ulioongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) (hayupo pichani) kilichofanyika Makao Makuu ya Shirika la Utalii Duniani la Umoja wa Mataifa  jijini Madrid, Hispania leo Januari 24,2025

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) akizungumza katika kikao kati yake na Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UN Tourism), Zurab Pololikashvili(hayupo pichani) kuhusu Tanzania kuwa mwenyeji wa Kongamano la 2 la Kikanda la Utalii wa Vyakula la Shirika la Umoja wa Mataifa, kilichofanyika Makao Makuu ya Shirika la Utalii Duniani la Umoja wa Mataifa  jijini Madrid, Hispania leo Januari 24,2025.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) katika kikao na Katibu Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani (UN Tourism), Zurab Pololikashvili wakijadili kuhusu namna bora ya kuboresha Kongamano la 2 la Kikanda la Utalii wa Vyakula la Shirika la Umoja wa Mataifa (The 2nd UN Tourism Regional Forum on Gastronomy Tourism for Africa) litakalofanyika nchini Tanzania mwezi Machi,2025, kilichofanyika Makao Makuu ya Shirika la Utalii Duniani la Umoja wa Mataifa  jijini Madrid, Hispania leo Januari 24,2025.

Na Happiness Shayo-Dodoma

Wizara ya Maliasili na Utalii imetakiwa kushirikiana kwa ukaribu na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika kukuza soko la utalii nchini na kurahisisha utoaji wa huduma ya viza kwa watalii.

Hayo yamesemwa leo Januari 14,2025 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhe. Timotheo Mnzava katika kikao kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma.

“Wizara ya Mambo ya Ndani, Uhamiaji na Wizara ya Maliasili na Utalii mshirikiane kuikuza Sekta ya Utalii, tunahitaji mfanye zaidi kuisaidia sekta hii na kama kuna changamoto mkazitatue” Mhe. Mnzava amesisitiza.

Mhe. Mnzava amezitaka Wizara hizo kuoanisha mifumo ya malipo kwa watalii na kuweka mikakati madhubuti ya kutambua masoko muhimu ya watalii na kuwavuta waje nchini sambamba na kurahisisha michakato ya kupata viza kwa watalii hao.

Naye, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) ameiahidi kamati hiyo kwamba Wizara ya Maliasili na Utalii itahakikisha inafanya kazi kwa ukaribu na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuhakikisha soko la utalii linakua ili kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kukuza Sekta ya Utalii nchini.

“Tutahakikisha tunatambua masoko muhimu ya utalii na kuweka mikakati madhubuti ya kuvutia watalii kwa kushirikiana ”Mhe. Chana amesema.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Viongozi na Watendaji mbalimbali kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii na Taasisi zake pamoja na Viongozi kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ndani ya Nchi na Uhamiaji.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

WAKULIMA 18,000 KUNUFAIKA NA KILIMO MISITU – WAZIRI CHANA

August 6, 2025

WADAU WA UTALII DUNIANI WAVUTIWA KUWEKEZA NCHINI TANZANIA

March 7, 2024

TALII NA MAMA SAMIA HIFADHI YA TAIFA KITULO

December 19, 2023

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025230

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025226

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024200

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025127
Don't Miss
Video Mpya

Kijana Golden Kidumba (DON. G) Awagusa Watoto wa Mitaani kwa Chakula na Mavazi

By Mbeya YetuNovember 19, 20251

Kijana Golden Kidumba, maarufu kama DON. G, amewagusa watoto wa mitaani kwa kuwapatia chakula, kuwanunulia nguo na kutumia muda wa siku nzima akiwa nao, ikiwa ni sehemu ya jitihada zake za kuikumbuka jamii aliyotokea.

Golden, mzaliwa na mkazi wa zamani wa Njombe, anasema maisha magumu aliyoyapitia utotoni ndiyo yamemfanya kuwa na moyo wa huruma na kujitoa kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

“Nimekulia kwenye maisha magumu sana. Lakini namshukuru Mungu kwa kunibariki na kunifanya niweze kuwakumbuka hawa wadogo zangu wa mitaani. Nimekula nao, nimesherehekea nao na pia nimewanunulia nguo ili wajisikie wanathaminiwa kama watoto wengine,” amesema DON. G.

Amesema kusaidia watoto wa mitaani si tukio la leo pekee, bali ni jambo alilolianza miaka kadhaa iliyopita, ikiwemo kutembelea hospitali na kuwasaidia watu wenye uhitaji.

Golden ameweka wazi kuwa ndoto yake ya baadaye ni kuanzisha taasisi ya msaada na hata kujenga shule maalum kwa ajili ya watoto hao, ili kuwapa elimu, malezi na fursa za kuanza maisha mapya.

Baadhi ya watoto wa mitaani waliopokea msaada huo wameeleza machungu ya maisha yao, ikiwemo vipigo, njaa, manyanyaso na mara nyingi kudharauliwa kama wahalifu bila kujua historia zao.

Kijana Brian Edwin, anayelelewa katika kituo cha Mtama, amesema:
“Maisha ya mitaani ni magumu. Tunapigwa, tunanyanyaswa na tunaishi bila uhakika. Lakini leo tumepata faraja kubwa kutoka kwa DON. G. Mungu ambariki.”

Wengine kama Anody Nyondo na Gifty wameeleza jinsi walivyokimbia nyumbani kutokana na migogoro ya kifamilia na manyanyaso, hali iliyowalazimu kuingia mitaani.

Watoto hao wameiomba jamii na serikali kutowatenga, bali kuwaona kama watoto wanaohitaji msaada na si wahalifu.

Golden ameendelea kutoa wito huo huo:
“Tusishikilie mali bila sababu. Tukiondoka duniani, hatuchukui chochote. Tuwakumbuke watoto wa mitaani; wanahitaji upendo na msaada wetu.”

Biashara ya mbao ilivyobadili maisha yake ikimpa utajiri

November 19, 2025

Rais Dkt Samia aongoza kikao kazi cha Mawaziri Naibu Mawaziri Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu

November 19, 2025

Safari ya kurejesha hamu ya tendo la ndoa kwa Zuhura iliyofanikiwa

November 19, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Kijana Golden Kidumba (DON. G) Awagusa Watoto wa Mitaani kwa Chakula na Mavazi

November 19, 2025

Biashara ya mbao ilivyobadili maisha yake ikimpa utajiri

November 19, 2025

Rais Dkt Samia aongoza kikao kazi cha Mawaziri Naibu Mawaziri Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu

November 19, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025230

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025226

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024200
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.