Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilipoteza Mali Yote Baada ya Talaka, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinirudishia Kila Kitu

September 18, 2025

BENKI YA NMB YATAHADHARISHA WALIMU UTAPELI MATUMIZI YA ATM CARD

September 18, 2025

Nilishindwa Mitihani Mara Nne, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Nifaulu Kwa Alama za Juu

September 18, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilipoteza Mali Yote Baada ya Talaka, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinirudishia Kila Kitu
  • BENKI YA NMB YATAHADHARISHA WALIMU UTAPELI MATUMIZI YA ATM CARD
  • Nilishindwa Mitihani Mara Nne, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Nifaulu Kwa Alama za Juu
  • PASTOR EZEKIEL ODERO AWAOMBA WATANZANIA KUDUMISHA AMANI KUELEKEA UCHAGUZ! MKUU
  • Nilikataliwa na Wanaume Wote Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Niolewe na Tajiri
  • Aibu!! Askofu Mkuu abainika kuiba fedha kanisa lake
  • Kongamano la Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050 Kufanyika Mbeya
  • Prof. Makulilo: Watanzania Wajiandae kwa Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TUME YATAKA WANANCHI KUTAZAMA DAFTARI LA AWALI,KUHAKIKI TAARIFA ZAO
Habari za Kitaifa

TUME YATAKA WANANCHI KUTAZAMA DAFTARI LA AWALI,KUHAKIKI TAARIFA ZAO

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMay 1, 2025Updated:May 1, 2025No Comments0 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

Wananchi
wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa
wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa
katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa.
Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari
la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025
unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali. 

Wananchi
wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa
wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa
katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa.
Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari
la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025
unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali. 

Mwenyekiti
wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele
akitembelea na kukagua vituo vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
awamu ya pili mkoani Njombe linalokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la
awali la wapiga kura ambapo mikoa 15 imeanza zoezi hilo litafanyika kwa siku
saba kuanzia Mei 1 hadi 7, 2025. 

Mwenyekiti
wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele
akitembelea na kukagua vituo vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
awamu ya pili mkoani Njombe linalokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la
awali la wapiga kura ambapo mikoa 15 imeanza zoezi hilo litafanyika kwa siku
saba kuanzia Mei 1 hadi 7, 2025. 

Wananchi
wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa
wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa
katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa.
Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari
la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025
unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali.

******* 

Na. Mwandishi wetu, Iringa
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka
wananchi kutoka katika mikoa 15 ya Tanzania Bara inayotekeleza mzunguko wa
kwanza katika awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura  na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga
Kura kujitokeza katika vituo walivyojiandikishia na kutazama daftari la awali
lilolowrekwa wazi na kutoa taarifa za wale waliokosa sifa kuwepo kwenye daftari
hilo.

Akizungumza baada ya kutembelea vituo katika
Halmashauri za Manispaa ya Iringa, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Halmashauri
ya Mji wa Mafinga na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa, Mwenyekiti
wa TumeHuru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele amesema
wananchi wameonesha mwitikio katika siku ya kwanza ya zoezi hilo la siku saba
na kuwataka kuhakiki taarifa zao.

Jaji Mwambegele amesema Tume imeweka wazi daftari
la awali la wapiga kura katika vituo vyote vilivyotumika kuandikisha na
kuboresha taarifa za Wapiga kura katika awamu ya kwanza, hivyo wananchi
wajitokeze kuhakiki taarifa zao na kutoa taarifa za wale ambao hawastahili
kuwepo katika Daftari hilo.

“Nawasihi wananchi endapo wataona katika
Daftari ambalo tumeliweka katika kila kituo kuna mwananchi ambaye amekosa sifa kama
vile kufariki basi wawe huru kwa kutumia fomu namba 5B kumuondoa huyo ambaye
amekosa sifa za kuwepo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.”alisema.

Aidha, amesema yeye pamoja na viongozi
wengine wa Tume wakiwepo Wajumbe wa Tume wametembelea mikoa yote inayotekeleza zoezi
hilo na kushuhudia mwitikio wa watu vituoni, huku vituo vikifunguliwa kwa
wakati uliopangwa wa saa 2:00 asubuhi.

“Wananchi wamejitokeza vizuri kuja kuboresha taarifa
zao wale ambao hawakuboresha taarifa zao katika awamu ya kwanza ya uboreshaji
wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,”alisema Jaji Mwambegele.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura awamu ya pili unafanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la
Wapiga Kura kuanzia Mei 01, 2025 na kukamilika tarehe 04 Julai, 2025.

Uboreshaji wa Daftari unafanyika kwa
mizunguko mitatu ambapo mzunguko wa kwanza utajumuisha mikoa 15, mzunguko wa
pili mikao 16 na mzunguko wa tatu utajumuisha vituo vya magereza na vyuo vya
mafunzo.

Mikoa itakayohusika kwenye mzunguko wa kwanza
wa uboreshaji ni pamoja na Iringa, Geita, Kagera, Mara, Shinyanga, Mwanza,
Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Ruvuma, Mbeya, Njombe na Songwe ambapo
zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 1 hadi 7 mwaka huu.

Aidha, mzunguko wa pili utahusisha mikoa ya
Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es
Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja,
Kaskazini Pemba na Kusini Pemba ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 16
hadi 22, 2025.

Mzunguko wa tatu wa zoezi la uboreshaji wa
Daftari utahusisha vituo 130 vilivyopo kwenye magereza ya Tanzania Bara na
vituo 10 vilivyopo katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar kwa wakati mmoja
na utafanyika kwa muda wa siku saba kuanzia Juni 28 hadi Julai 04, 2025.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura kwa awamu ya pili, utafanyika ngazi ya kata kwa Tanzania Bara na ngazi ya
jimbo kwa Tanzania Zanzibar, ambapo jumla ya vituo 7,869 vitahusika, vituo
7,659 vipo Tanzania Bara na vituo 210 vipo Tanzania Zanzibar.

Katika awamu ya pili ya uboreshaji, wapiga
kura wapya 1,396,609 wataandikishwa, wapiga kura 1,092,383 wataboresha taarifa
zao na wapiga kura 148,624 watafutwa kwenye Daftari kwa kukosa sifa za
kuendelea kuwepo kwenye Daftari,” amesema Jaji Mwambegele.

Mambo mengine ni kuhamisha taarifa za wapiga
kura waliohama kutoka kata au jimbo walipoandikishwa awali na kuondoa  taarifa za wapiga kura waliopoteza sifa za
kuwemo kwenye Daftari kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo.

Lengo la uwekaji wazi wa Daftari hilo ni
kutoa fursa kwa wananchi kukagua, kufanya marekebisho ya taarifa za wapiga kura
na uwekaji wa pingamizi dhidi ya wapiga kura waliomo kwenye daftari ambao
hawana sifa na litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika wakati wa
uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza.

Tume iliboresha Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura awamu ya kwanza kuanzia tarehe 20 Julai, 2024 na kukamilisha tarehe 25
Machi, 2025.

 

 

 

 


 

 

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na baadhi ya vijana waliojitokeza kujiandikisha kwa mara ya kwanza katika moja ya vituo Mkoani Iringa.

 

 

 

Matukio mbalimbali ya ziara ya Mwenbyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wakati akitembelea vituo mkoani Iringa 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Prof. Makulilo: Watanzania Wajiandae kwa Uchumi Jumuishi Kuelekea Dira 2050

September 17, 2025

MATIBABU YA KIBINGWA YA HUDUMA MKOBA YA MADAKTARI WA DT. SAMIA UKOMBOZI MKUBWA KWA WANANCHI WA MKOA WA SONGWE.

September 15, 2025

DKT. TULIA: NITAHAKIKISHA JIMBO JIPYA LA UYOLE LINAPATA HALMASHAURI

September 14, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025210

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024184

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025127

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025125
Don't Miss
Uncategorized

Nilipoteza Mali Yote Baada ya Talaka, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinirudishia Kila Kitu

By Mbeya YetuSeptember 18, 20251

Jiji lote lilijua kesi yangu ya talaka. Ilikuwa gumzo mitaani na hata kazini. Siku ya…

BENKI YA NMB YATAHADHARISHA WALIMU UTAPELI MATUMIZI YA ATM CARD

September 18, 2025

Nilishindwa Mitihani Mara Nne, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Nifaulu Kwa Alama za Juu

September 18, 2025

PASTOR EZEKIEL ODERO AWAOMBA WATANZANIA KUDUMISHA AMANI KUELEKEA UCHAGUZ! MKUU

September 18, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilipoteza Mali Yote Baada ya Talaka, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinirudishia Kila Kitu

September 18, 2025

BENKI YA NMB YATAHADHARISHA WALIMU UTAPELI MATUMIZI YA ATM CARD

September 18, 2025

Nilishindwa Mitihani Mara Nne, Lakini Hatua Niliyopiga Ilinifanya Nifaulu Kwa Alama za Juu

September 18, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025210

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024184

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025127
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.