Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

INEC YAHIMIZA WANANCHI MIKOA 16 KUJITOKEZA UBORESHAJI DAFTARI AWAMU YA PILI

May 14, 2025

ZIARA KAMATI YA SIASA CCM MKOA MBEYA WATEMBELEA BWENIMRADI WA MIL 300 SEKONDARI SAGAMBI CHUNYA

May 14, 2025

KAMATI SIASA MBEYA YAAGIZA STENDI CHUNYA KUJENGWA USIKU NA MCHANA KUKAMILIKA KABLA YA UCHAGUZI MKUU

May 12, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • INEC YAHIMIZA WANANCHI MIKOA 16 KUJITOKEZA UBORESHAJI DAFTARI AWAMU YA PILI
  • ZIARA KAMATI YA SIASA CCM MKOA MBEYA WATEMBELEA BWENIMRADI WA MIL 300 SEKONDARI SAGAMBI CHUNYA
  • KAMATI SIASA MBEYA YAAGIZA STENDI CHUNYA KUJENGWA USIKU NA MCHANA KUKAMILIKA KABLA YA UCHAGUZI MKUU
  • CCM MKOA MBEYA ZIARANI CHUNYA MWALUNENGE AAGIZA KUBORESHWA MFUMO USAJILI WAGONJWA SANGAMBI
  • Wizara ya Mawasiliano Yaendelea Kushirikiana kwa Karibu na Jeshi la Polisi Kukabili Utapeli Mtandaoni – Mhandisi Maryprisca Mahundi
  • TIMU YA MADAKTARI NA WAUGUZI KUTOKA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA, TANZANIA WAMETEMBELEA UBALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NCHINI ZAMBIA, TAREHE 12 MEI, 2025
  • UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA
  • MBEYA CITY YARUDI NBC PREMIER LEAGUE KIBABE FURAHA YAREJEA KWA WAKAZI JIJINI MBEYA
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TUME YATAKA WANANCHI KUTAZAMA DAFTARI LA AWALI,KUHAKIKI TAARIFA ZAO
Habari za Kitaifa

TUME YATAKA WANANCHI KUTAZAMA DAFTARI LA AWALI,KUHAKIKI TAARIFA ZAO

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMay 1, 2025Updated:May 1, 2025No Comments0 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

Wananchi
wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa
wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa
katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa.
Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari
la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025
unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali. 

Wananchi
wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa
wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa
katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa.
Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari
la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025
unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali. 

Mwenyekiti
wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele
akitembelea na kukagua vituo vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
awamu ya pili mkoani Njombe linalokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la
awali la wapiga kura ambapo mikoa 15 imeanza zoezi hilo litafanyika kwa siku
saba kuanzia Mei 1 hadi 7, 2025. 

Mwenyekiti
wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele
akitembelea na kukagua vituo vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
awamu ya pili mkoani Njombe linalokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la
awali la wapiga kura ambapo mikoa 15 imeanza zoezi hilo litafanyika kwa siku
saba kuanzia Mei 1 hadi 7, 2025. 

Wananchi
wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa
wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa
katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa.
Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari
la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025
unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali.

******* 

Na. Mwandishi wetu, Iringa
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka
wananchi kutoka katika mikoa 15 ya Tanzania Bara inayotekeleza mzunguko wa
kwanza katika awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura  na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga
Kura kujitokeza katika vituo walivyojiandikishia na kutazama daftari la awali
lilolowrekwa wazi na kutoa taarifa za wale waliokosa sifa kuwepo kwenye daftari
hilo.

Akizungumza baada ya kutembelea vituo katika
Halmashauri za Manispaa ya Iringa, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Halmashauri
ya Mji wa Mafinga na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa, Mwenyekiti
wa TumeHuru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele amesema
wananchi wameonesha mwitikio katika siku ya kwanza ya zoezi hilo la siku saba
na kuwataka kuhakiki taarifa zao.

Jaji Mwambegele amesema Tume imeweka wazi daftari
la awali la wapiga kura katika vituo vyote vilivyotumika kuandikisha na
kuboresha taarifa za Wapiga kura katika awamu ya kwanza, hivyo wananchi
wajitokeze kuhakiki taarifa zao na kutoa taarifa za wale ambao hawastahili
kuwepo katika Daftari hilo.

“Nawasihi wananchi endapo wataona katika
Daftari ambalo tumeliweka katika kila kituo kuna mwananchi ambaye amekosa sifa kama
vile kufariki basi wawe huru kwa kutumia fomu namba 5B kumuondoa huyo ambaye
amekosa sifa za kuwepo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.”alisema.

Aidha, amesema yeye pamoja na viongozi
wengine wa Tume wakiwepo Wajumbe wa Tume wametembelea mikoa yote inayotekeleza zoezi
hilo na kushuhudia mwitikio wa watu vituoni, huku vituo vikifunguliwa kwa
wakati uliopangwa wa saa 2:00 asubuhi.

“Wananchi wamejitokeza vizuri kuja kuboresha taarifa
zao wale ambao hawakuboresha taarifa zao katika awamu ya kwanza ya uboreshaji
wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,”alisema Jaji Mwambegele.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura awamu ya pili unafanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la
Wapiga Kura kuanzia Mei 01, 2025 na kukamilika tarehe 04 Julai, 2025.

Uboreshaji wa Daftari unafanyika kwa
mizunguko mitatu ambapo mzunguko wa kwanza utajumuisha mikoa 15, mzunguko wa
pili mikao 16 na mzunguko wa tatu utajumuisha vituo vya magereza na vyuo vya
mafunzo.

Mikoa itakayohusika kwenye mzunguko wa kwanza
wa uboreshaji ni pamoja na Iringa, Geita, Kagera, Mara, Shinyanga, Mwanza,
Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Ruvuma, Mbeya, Njombe na Songwe ambapo
zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 1 hadi 7 mwaka huu.

Aidha, mzunguko wa pili utahusisha mikoa ya
Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es
Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja,
Kaskazini Pemba na Kusini Pemba ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 16
hadi 22, 2025.

Mzunguko wa tatu wa zoezi la uboreshaji wa
Daftari utahusisha vituo 130 vilivyopo kwenye magereza ya Tanzania Bara na
vituo 10 vilivyopo katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar kwa wakati mmoja
na utafanyika kwa muda wa siku saba kuanzia Juni 28 hadi Julai 04, 2025.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura kwa awamu ya pili, utafanyika ngazi ya kata kwa Tanzania Bara na ngazi ya
jimbo kwa Tanzania Zanzibar, ambapo jumla ya vituo 7,869 vitahusika, vituo
7,659 vipo Tanzania Bara na vituo 210 vipo Tanzania Zanzibar.

Katika awamu ya pili ya uboreshaji, wapiga
kura wapya 1,396,609 wataandikishwa, wapiga kura 1,092,383 wataboresha taarifa
zao na wapiga kura 148,624 watafutwa kwenye Daftari kwa kukosa sifa za
kuendelea kuwepo kwenye Daftari,” amesema Jaji Mwambegele.

Mambo mengine ni kuhamisha taarifa za wapiga
kura waliohama kutoka kata au jimbo walipoandikishwa awali na kuondoa  taarifa za wapiga kura waliopoteza sifa za
kuwemo kwenye Daftari kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo.

Lengo la uwekaji wazi wa Daftari hilo ni
kutoa fursa kwa wananchi kukagua, kufanya marekebisho ya taarifa za wapiga kura
na uwekaji wa pingamizi dhidi ya wapiga kura waliomo kwenye daftari ambao
hawana sifa na litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika wakati wa
uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza.

Tume iliboresha Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura awamu ya kwanza kuanzia tarehe 20 Julai, 2024 na kukamilisha tarehe 25
Machi, 2025.

 

 

 

 


 

 

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na baadhi ya vijana waliojitokeza kujiandikisha kwa mara ya kwanza katika moja ya vituo Mkoani Iringa.

 

 

 

Matukio mbalimbali ya ziara ya Mwenbyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wakati akitembelea vituo mkoani Iringa 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

INEC YAHIMIZA WANANCHI MIKOA 16 KUJITOKEZA UBORESHAJI DAFTARI AWAMU YA PILI

May 14, 2025

Wizara ya Mawasiliano Yaendelea Kushirikiana kwa Karibu na Jeshi la Polisi Kukabili Utapeli Mtandaoni – Mhandisi Maryprisca Mahundi

May 12, 2025

TIMU YA MADAKTARI NA WAUGUZI KUTOKA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA, TANZANIA WAMETEMBELEA UBALOZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NCHINI ZAMBIA, TAREHE 12 MEI, 2025

May 12, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024170

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202481

UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA

May 12, 202558

DKT. TULIA ATOA MSAADA WA VIPAZA SAUTI MSIKITI WA MASJID BI FATMA NZOVWE JIJINI MBEYA

March 29, 202457
Don't Miss

INEC YAHIMIZA WANANCHI MIKOA 16 KUJITOKEZA UBORESHAJI DAFTARI AWAMU YA PILI

By Mbeya YetuMay 14, 20251

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele…

ZIARA KAMATI YA SIASA CCM MKOA MBEYA WATEMBELEA BWENIMRADI WA MIL 300 SEKONDARI SAGAMBI CHUNYA

May 14, 2025

KAMATI SIASA MBEYA YAAGIZA STENDI CHUNYA KUJENGWA USIKU NA MCHANA KUKAMILIKA KABLA YA UCHAGUZI MKUU

May 12, 2025

CCM MKOA MBEYA ZIARANI CHUNYA MWALUNENGE AAGIZA KUBORESHWA MFUMO USAJILI WAGONJWA SANGAMBI

May 12, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

INEC YAHIMIZA WANANCHI MIKOA 16 KUJITOKEZA UBORESHAJI DAFTARI AWAMU YA PILI

May 14, 2025

ZIARA KAMATI YA SIASA CCM MKOA MBEYA WATEMBELEA BWENIMRADI WA MIL 300 SEKONDARI SAGAMBI CHUNYA

May 14, 2025

KAMATI SIASA MBEYA YAAGIZA STENDI CHUNYA KUJENGWA USIKU NA MCHANA KUKAMILIKA KABLA YA UCHAGUZI MKUU

May 12, 2025
Most Popular

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024170

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202481

UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA

May 12, 202558
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.