Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

KWA MARA NYINGINE, MHANDISI MAHUNDI AWAPA NEEMA WAGONJWA WA MACHO

July 1, 2025

MWAKIPESILE AREJESHA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI

June 30, 2025

Msimu wa pili wa tamasha la michezo na vipaji MZRH

June 30, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • KWA MARA NYINGINE, MHANDISI MAHUNDI AWAPA NEEMA WAGONJWA WA MACHO
  • MWAKIPESILE AREJESHA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI
  • Msimu wa pili wa tamasha la michezo na vipaji MZRH
  • MKULIMA NA MFUGAJI WA MBARALI ATIA TIMU KIPUTE JIMBO LA MBARALI USANGU ACHUKUA FOMU KUWANIA UBUNGE
  • WAKILI MSOMI KAPTENI MSTAAFU SAMBWEE SHITAMBALA ACHUKUA FOMU KUWANIA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI.
  • MWAISUMBE: ALIYEJITOSA UBUNGE 2010 AWANIA TENA MBEYA MJINI AAHIDI KUMUUNGA MKONO ATAKAYETEULIWA
  • MHASIBU SUA AJITOSA UBUNGE JIMBO LA SAME MASHARIKI
  • MWANAHABARI MKONGWE CHARLES MWAKIPESILE AJITOSA UBUNGE MBEYA MJINI
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TUME YATAKA WANANCHI KUTAZAMA DAFTARI LA AWALI,KUHAKIKI TAARIFA ZAO
Habari za Kitaifa

TUME YATAKA WANANCHI KUTAZAMA DAFTARI LA AWALI,KUHAKIKI TAARIFA ZAO

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMay 1, 2025Updated:May 1, 2025No Comments0 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

Wananchi
wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa
wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa
katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa.
Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari
la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025
unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali. 

Wananchi
wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa
wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa
katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa.
Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari
la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025
unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali. 

Mwenyekiti
wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele
akitembelea na kukagua vituo vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
awamu ya pili mkoani Njombe linalokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la
awali la wapiga kura ambapo mikoa 15 imeanza zoezi hilo litafanyika kwa siku
saba kuanzia Mei 1 hadi 7, 2025. 

Mwenyekiti
wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele
akitembelea na kukagua vituo vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
awamu ya pili mkoani Njombe linalokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la
awali la wapiga kura ambapo mikoa 15 imeanza zoezi hilo litafanyika kwa siku
saba kuanzia Mei 1 hadi 7, 2025. 

Wananchi
wa Kata ya Kihesa katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa mkoani Iringa
wakikagua majina yao katika daftari la awali la wapiga Kura lililobandikwa
katika kiuo cha kujiandikishia wapiga Kura kilichopo ofisi ya Mtendaji Kihesa.
Tume Huru ya taifa ya Uchaguzi imeanza awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari
la Wapiga Kura katika mikoa 15 ya Tanzania bara kuanzia Mei Mosi hadi 07, 2025
unaokwenda sambamba na uwekaji wazi wa daftari la awali.

******* 

Na. Mwandishi wetu, Iringa
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka
wananchi kutoka katika mikoa 15 ya Tanzania Bara inayotekeleza mzunguko wa
kwanza katika awamu ya pili ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura  na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga
Kura kujitokeza katika vituo walivyojiandikishia na kutazama daftari la awali
lilolowrekwa wazi na kutoa taarifa za wale waliokosa sifa kuwepo kwenye daftari
hilo.

Akizungumza baada ya kutembelea vituo katika
Halmashauri za Manispaa ya Iringa, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Halmashauri
ya Mji wa Mafinga na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa, Mwenyekiti
wa TumeHuru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele amesema
wananchi wameonesha mwitikio katika siku ya kwanza ya zoezi hilo la siku saba
na kuwataka kuhakiki taarifa zao.

Jaji Mwambegele amesema Tume imeweka wazi daftari
la awali la wapiga kura katika vituo vyote vilivyotumika kuandikisha na
kuboresha taarifa za Wapiga kura katika awamu ya kwanza, hivyo wananchi
wajitokeze kuhakiki taarifa zao na kutoa taarifa za wale ambao hawastahili
kuwepo katika Daftari hilo.

“Nawasihi wananchi endapo wataona katika
Daftari ambalo tumeliweka katika kila kituo kuna mwananchi ambaye amekosa sifa kama
vile kufariki basi wawe huru kwa kutumia fomu namba 5B kumuondoa huyo ambaye
amekosa sifa za kuwepo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.”alisema.

Aidha, amesema yeye pamoja na viongozi
wengine wa Tume wakiwepo Wajumbe wa Tume wametembelea mikoa yote inayotekeleza zoezi
hilo na kushuhudia mwitikio wa watu vituoni, huku vituo vikifunguliwa kwa
wakati uliopangwa wa saa 2:00 asubuhi.

“Wananchi wamejitokeza vizuri kuja kuboresha taarifa
zao wale ambao hawakuboresha taarifa zao katika awamu ya kwanza ya uboreshaji
wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura,”alisema Jaji Mwambegele.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura awamu ya pili unafanyika sambamba na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la
Wapiga Kura kuanzia Mei 01, 2025 na kukamilika tarehe 04 Julai, 2025.

Uboreshaji wa Daftari unafanyika kwa
mizunguko mitatu ambapo mzunguko wa kwanza utajumuisha mikoa 15, mzunguko wa
pili mikao 16 na mzunguko wa tatu utajumuisha vituo vya magereza na vyuo vya
mafunzo.

Mikoa itakayohusika kwenye mzunguko wa kwanza
wa uboreshaji ni pamoja na Iringa, Geita, Kagera, Mara, Shinyanga, Mwanza,
Simiyu, Rukwa, Tabora, Katavi, Kigoma, Ruvuma, Mbeya, Njombe na Songwe ambapo
zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 1 hadi 7 mwaka huu.

Aidha, mzunguko wa pili utahusisha mikoa ya
Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es
Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja,
Kaskazini Pemba na Kusini Pemba ambapo zoezi hilo litafanyika kuanzia Mei 16
hadi 22, 2025.

Mzunguko wa tatu wa zoezi la uboreshaji wa
Daftari utahusisha vituo 130 vilivyopo kwenye magereza ya Tanzania Bara na
vituo 10 vilivyopo katika Vyuo vya Mafunzo Tanzania Zanzibar kwa wakati mmoja
na utafanyika kwa muda wa siku saba kuanzia Juni 28 hadi Julai 04, 2025.

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura kwa awamu ya pili, utafanyika ngazi ya kata kwa Tanzania Bara na ngazi ya
jimbo kwa Tanzania Zanzibar, ambapo jumla ya vituo 7,869 vitahusika, vituo
7,659 vipo Tanzania Bara na vituo 210 vipo Tanzania Zanzibar.

Katika awamu ya pili ya uboreshaji, wapiga
kura wapya 1,396,609 wataandikishwa, wapiga kura 1,092,383 wataboresha taarifa
zao na wapiga kura 148,624 watafutwa kwenye Daftari kwa kukosa sifa za
kuendelea kuwepo kwenye Daftari,” amesema Jaji Mwambegele.

Mambo mengine ni kuhamisha taarifa za wapiga
kura waliohama kutoka kata au jimbo walipoandikishwa awali na kuondoa  taarifa za wapiga kura waliopoteza sifa za
kuwemo kwenye Daftari kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo.

Lengo la uwekaji wazi wa Daftari hilo ni
kutoa fursa kwa wananchi kukagua, kufanya marekebisho ya taarifa za wapiga kura
na uwekaji wa pingamizi dhidi ya wapiga kura waliomo kwenye daftari ambao
hawana sifa na litabandikwa katika vituo vyote vilivyotumika wakati wa
uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya kwanza.

Tume iliboresha Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura awamu ya kwanza kuanzia tarehe 20 Julai, 2024 na kukamilisha tarehe 25
Machi, 2025.

 

 

 

 


 

 

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza na baadhi ya vijana waliojitokeza kujiandikisha kwa mara ya kwanza katika moja ya vituo Mkoani Iringa.

 

 

 

Matukio mbalimbali ya ziara ya Mwenbyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi wakati akitembelea vituo mkoani Iringa 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

MHASIBU SUA AJITOSA UBUNGE JIMBO LA SAME MASHARIKI

June 28, 2025

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI MAGEREZA NA VYUO VYA MAFUNZO WANOLEWA

June 22, 2025

VIJANA CCM MBEYA DC WAJIPANGA KUPIGA KURA OKTOBA 2025.

June 13, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024173

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202482

UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA

May 12, 202568

DKT. TULIA ATOA MSAADA WA VIPAZA SAUTI MSIKITI WA MASJID BI FATMA NZOVWE JIJINI MBEYA

March 29, 202459
Don't Miss
Video Mpya

KWA MARA NYINGINE, MHANDISI MAHUNDI AWAPA NEEMA WAGONJWA WA MACHO

By Mbeya YetuJuly 1, 20250

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi Julai 1,2025 amefungua kambi ya matibabu bila gharama kwa wagonjwa wa macho Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya inayolenga kuwafikia wagonjwa zaidi ya mia mbili.

Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema gharama zote za uchunguzi,dawa na matibabu ni bure kupitia wadau wake kutoka Ujerumani na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

Dkt Fariji Kilewa Mkuu wa Kitengo cha macho Hospitali ya Mkoa wa Mbeya amesema lengo ni kuwafikia wagonjwa zaidi ya mia mbili waliopo Mkoa wa Mbeya na mikoa jirani.

Aidha amesema mbali ya upasuaji wa mtoto wa jicho pia wanawafanyia uchunguzi wa macho kwa matatizo mengine ya macho.

Hata hivyo Dkt Fariji Kilewa amesema gharama za upasuaji wa mtoto wa jicho zinagharimu zaidi ya shilingi laki tatu ambazo ni watu wachache wanaoweza kumudu gharama hizo.

Afisa uhusiano Hospitali ya Mkoa wa Mbeya Agrey Mwaijande amesema gharama zote zinatolewa bure hivyo wito umetolewa kwa wananchi kuitumia vizuri fursa hiyo.

Baadhi ya wagonjwa waliojitokeza kupatiwa watibabu wamepongeza huduma hiyo kutokana na wengi wao kushindwa kumudu gharama za matibabu ya macho.

Hii ni kambi ya pili kwa Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi kuandaa kambi ya macho iliyoanza juni 30,2025 itakayotamatika julai 5,2025kwa ushirikiano na Hospitali ya Mkoa wa Mbeya.

MWAKIPESILE AREJESHA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI

June 30, 2025

Msimu wa pili wa tamasha la michezo na vipaji MZRH

June 30, 2025

MKULIMA NA MFUGAJI WA MBARALI ATIA TIMU KIPUTE JIMBO LA MBARALI USANGU ACHUKUA FOMU KUWANIA UBUNGE

June 30, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

KWA MARA NYINGINE, MHANDISI MAHUNDI AWAPA NEEMA WAGONJWA WA MACHO

July 1, 2025

MWAKIPESILE AREJESHA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA MBEYA MJINI

June 30, 2025

Msimu wa pili wa tamasha la michezo na vipaji MZRH

June 30, 2025
Most Popular

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024173

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202482

UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA

May 12, 202568
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.