Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

MSHTUKO MBEYA: MTOTO DARASA LA SABA AUAWA KWA KIPANDE CHA MTI KWA TUHUMA ZA WIZI WA MAYAI

December 23, 2025

Nilipoteza Amani Bila Sababu Inayoonekana Ufafanuzi wa Kienyeji Ulinipa Mwanga

December 23, 2025

MH. MAHUNDI AWAHIMIZA VIJANA KUISHI KWA MISINSI YA UWAJIBIKAJI NA UTU

December 23, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • MSHTUKO MBEYA: MTOTO DARASA LA SABA AUAWA KWA KIPANDE CHA MTI KWA TUHUMA ZA WIZI WA MAYAI
  • Nilipoteza Amani Bila Sababu Inayoonekana Ufafanuzi wa Kienyeji Ulinipa Mwanga
  • MH. MAHUNDI AWAHIMIZA VIJANA KUISHI KWA MISINSI YA UWAJIBIKAJI NA UTU
  • Familia Yetu Ilikosa Baraka ya Utulivu Tulipoelewa Chanzo, Njia Ikafunguka
  • Tulikaa Ndoa Bila Amani Mazungumzo Moja Yalibadili Mwelekeo Wetu
  • Maumivu ya Ghafla Yalinifanya Nidhani Ni Mwisho, Baadaye Nikagundua Mawe ya Figo Yanatibika Kwa Mitishamba
  • Tazama alichoimba Dkt. Tulia Ackson Atoa sadaka kwa kaya 13 zisizo na uwezo kata ya Ilemi
  • WANA KIKUNDI STAR FAMILY MBEYA WALIVYOMALIZA MWAKA KWA KUTOA SADAKA KWA WATOTO YATIMA
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WAANDISHI WA HABARI KUANZA KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA TAI-HABARI – MSIGWA
Habari za Kitaifa

WAANDISHI WA HABARI KUANZA KUJISAJILI KWENYE MFUMO WA TAI-HABARI – MSIGWA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuMay 3, 2025No Comments13 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Na Mwandishi Wetu, JAB

Serikali imesema vitambulisho vya Uandishi wa Habari (Press Card), vitaanza kutolewa wakati wowote baada ya siku saba kuanzia leo Mei 3, 2025 baada ya Waandishi wa Habari kuanza kujisajili rasmi kwenye mfumo wa TAI-Habari.

Mwandishi wa Habari ataanza kujisajili kupitia kiunganishi cha https://taihabari.jab.go.tz kisha kufuata maelekezo yaliyotolewa ili kukamilisha kujaza fomu yake kwenye mfumo huo wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari.

Kauli hiyo imetolewa tarehe 03 Mei, 2025 na Katibu Mkuu wa Wizara Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa, katika Kijiji cha Sayu mkoani Shinyanga wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu masuala mbalimbali ya Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa na Serikali mkoani humo.

“Tuliwaahidi kwamba tunawaletea Press Card (Vitambulisho vya kidijitali), ninayofuraha kuwajulisha kwamba ‘press card’ hizi za kidijital mchakato umekamilika, ziko tayari kwa matumizi, siku saba kuanzia sasa mtaingia kwenye kiunganishi cha Bodi ya lthibati ya Waandishi wa Habari na utaomba kitambulisho…,” alisema Bw. Gerson Msigwa.

Alisema Mwandishi wa Habari akishajaza taarifa zake sahihi, Bodi itapokea maombi na kuyahakiki na kama yamekidhi vigezo kitambulisho kitachapishwa na kutumwa mahali alipo kupitia Klabu za Waandishi wa Habari katika maeneo yao.

“Ombi langu kwenu Waandishi wa Habari mtambue kitambulisho hiki ni mali ya Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari Tanzania…, hivyo ukipewa wewe ndiye utakayewajibika kwa lolote litakalofanyika kwa utambulisho wa kitambulisho hiki, siyo kitambulisho umekiacha huko, mtu amekichukua kaenda kufanya utapeli tutambaini kwa sababu sasa tutakuwa tunaweza kufuatilia kwa kupitia mfumo, tukibaini tutakupata wewe,” alisema Bw. Msigwa na kuongeza;

“Ninachowaomba kitunzeni kama mboni ya jicho, huu ndiyo utambulisho wenu wa kazi, muwe nacho mfukoni, usikiache hovyo hovyo.”

Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo, Wakili Patrick Kipangula, ili kurahisisha zoezi la kutuma na kupokea Press Card hizo, Waandishi wa Habari wanahimizwa kujisajili kwenye Klabu za Waandishi wa Habari zilizopo maeneo yao.

Wakili Kipangula alisema wakati wa kujisajili Waandishi wa Habari wanapaswa kuweka kwenye mfumo vyeti vilivyo halali na kwamba ikiwa Mwandishi ataweka cheti cha kughushi, Bodi ya Ithibati itachukua hatua kali za kisheria kwa sababu hilo ni kosa la jinai.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

MH. MAHUNDI AWAHIMIZA VIJANA KUISHI KWA MISINSI YA UWAJIBIKAJI NA UTU

December 23, 2025

DKT. TULIA ACKSON AANZA ZOEZI LA KUWAFIKIA KAYA ZENYE UHITAJI ZAIDI UYOLE, KAYA 130 ZANUFAIKA KUELEKEA SIKUKUU

December 21, 2025

MAHUNDI AWATUNUKU WAHITIMU 530 CHUO CHA MAENDELEO YA JAMII(CDTI)UYOLE

December 20, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025271

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025237

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024211

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025131
Don't Miss
Video Mpya

MSHTUKO MBEYA: MTOTO DARASA LA SABA AUAWA KWA KIPANDE CHA MTI KWA TUHUMA ZA WIZI WA MAYAI

By Mbeya YetuDecember 23, 20252

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Furaha Mwile Nyelele, mkazi
wa Kijiji cha Shilanga kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wa jirani yake
aliyekuwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Shilanga darasa la saba
aitwaye Boniventure Elia Lazaro [12] mkazi wa Shilanga.
Awali kabla ya tukio hilo tarehe 21.12.2025 saa 10:15 jioni huko Kijiji cha
Shilanga, Kata ya Ilembo, Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Mbeya Vijijini
mtuhumiwa Furaha Mwile Nyelele alimpiga kwa kipande cha mti kichwani
mtoto Boniventure Elia Lazaro [12] ambaye kwa sasa ni marehemu na
kumsababishia jeraha ambapo alikimbizwa katika Hospitali Teule ya Ifisi
kwa matibabu.
Tarehe 22.12.2025 saa 6:30 mchana akiwa anaendelea kupatiwa matibabu
katika Hospitali Teule ya Ifisi alifariki dunia. Uchunguzi wa awali umebaini
kuwa chanzo cha tukio hili ni kujichukulia sheria mkononi baada ya
mtuhumiwa kumtuhumu mtoto kuiba mayai ya kuku.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa kwa jamii kuacha tabia ya
kujichukulia sheria mkononi ili kuepuka madhara. Aidha, wazazi na walezi
wanakumbushwa kuzingatia suala la ulinzi na usalama wa mtoto kwa
kuhakikisha haki za mtoto zinaheshimiwa na kulindwa.

Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.

Nilipoteza Amani Bila Sababu Inayoonekana Ufafanuzi wa Kienyeji Ulinipa Mwanga

December 23, 2025

MH. MAHUNDI AWAHIMIZA VIJANA KUISHI KWA MISINSI YA UWAJIBIKAJI NA UTU

December 23, 2025

Familia Yetu Ilikosa Baraka ya Utulivu Tulipoelewa Chanzo, Njia Ikafunguka

December 23, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

MSHTUKO MBEYA: MTOTO DARASA LA SABA AUAWA KWA KIPANDE CHA MTI KWA TUHUMA ZA WIZI WA MAYAI

December 23, 2025

Nilipoteza Amani Bila Sababu Inayoonekana Ufafanuzi wa Kienyeji Ulinipa Mwanga

December 23, 2025

MH. MAHUNDI AWAHIMIZA VIJANA KUISHI KWA MISINSI YA UWAJIBIKAJI NA UTU

December 23, 2025
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025271

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025237

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024211
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.