MFUKO wa hifadhi ya Jamii PSSSF imefanya mkutano maalumu na Waandishi wa Habari kutoka Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Mbeya, MBEYA PRESS CLUB ikiwa ni sehemu ya kuongeza wigo wa kujua utendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF.
Mkutano huo maalumu umefanyika katika ukumbi wa Hotel ya Mgwasi Jijini Mbeya ambapo Waandishi wa Habari wamejengewa uwezo na kuwekewa mazingira mazuri ya kutambua umuhimu wa shughuli zinazofanywa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma PSSSF.
Akizungumza katika mkutano huo Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma PSSSF Rehema Mkamba.
Bi Mkamba amesema hadi sasa PSSSF imeshakutana na Waandishi kutoka Klabu za Waandishi mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Zanzibar na Mbeya na kuwa watakutana pia na Waandishi Klabu ya Waandishi wa Mtwara na Mwanza.
Amesema lengo ni kuzidi kuifikia jamii na kuwaongezea uelewa wanajamii kutokana na uelewa mdogo juu ya Huduma ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa wananchi.
Awali katika mafunzo hayo Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii PSSSF Kanda Nyanda za Juu Kusini Ramadhan Mgaya ameelezea umuhimu wa kujiwekea hifadhi baada ya kustaafu utumishi wa umma na kujiwekea mazingira bora ya maisha baada ya kustaafu utumishi wa umma.
Kwa upande wake Mstaafu wa utumishi wa Umma Vicent Msola amesema awali kulikuwa na sintofahamu juu ya kucheleweshewa mafao yao na kwamba kwa sasa wastaafu wanalipwa mafao yao ndani ya muda mfupi baada ya kustaafu.
Amesema ili kujiwekea mazingira bora ya maisha baada ya kustaafu kwa kuwa na shughuli mbadala zitakazowasaidia kuishi vizuri katika maisha ya kustaafu.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya Joseph Mwaisango amesema uhusiano wa PSSSF na Klabu ya Waandishi wa habari mkoa wa Mbeya Mbeya Press Club utaleta chachu ya mahusiano na wigo wa kuifahamisha jamii juu ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii PSSSF.