Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi amesema yeyote anayefanya kazi za kihabari bila kuwa na Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card) kinachotolewa na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari-JAB anavunja sheria ya Huduma za Habari. Waziri Kabudi ametoa kauli hiyo huku akionesha Press Card yake kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Mabaraza ya Habari Afrika leo tarehe 14 Julai, 2025 alipozungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Phillip Mpango jijini Arusha.
#ithibatitz
#ithibatikidijitali