Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
  • Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
  • VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII
  • TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
  • Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
  • MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
  • Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WATENDAJI UCHAGUZI WATAKIWA KUTOA TAARIFA KWA VYAMA VYA SIASA
Habari za Kitaifa

WATENDAJI UCHAGUZI WATAKIWA KUTOA TAARIFA KWA VYAMA VYA SIASA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJuly 21, 2025Updated:July 21, 2025No Comments24 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 21, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 21, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga.

 

Washiriki wa mafunzo hayo ambayo yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo kutoka majimbo yote ya Mikoa ya Shinyanga na Simiyu. 

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Cyprian Mbugano akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ambapo pia alitoa mada.

Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kama hayo kwa Kisiwani Pemba, Zanzibar ambapo amewaasa watendaji hao kufanya kazi kwa kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Ndg Adam Mkina ambaye ni Mkurugenzi wa INEC ofisi ya Zanzibar akizungumza jambo.

Washiriki wa mafunzo hayo ambayo yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo kutoka majimbo yote ya Kisiwani Pemba, Zanzibar.

*******

Na. Mwandishi wetu, Shinyanga
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka
watendaji wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kutoa taarifa mapema kwa vyama vya
siasa kuhusu utaratibu wa kuwaapisha mawakala.

Hayo yamesemwa mkoani Shinyanga leo Julai 21,
2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya
Rufani, Jacobs Mwambegele wakati akifungua mafunzo kwa watendaji wa uchaguzi
mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi oktoba mwaka huu kwa tarehe itakayotangazwa
na Tume.

“Wakati wa kuapisha mawakala, toeni taarifa
mapema kwa vyama vya siasa kwa mujibu wa sheria, kanuni na maelekezo ya Tume na
kuvipatia vyama vya siasa orodha ya vituo vya kupigia kura ili kuviwezesha
kupanga mawakala,” amesema Jaji Mwambegele.

Amewasisitiza watendaji hao kuhakikisha vifaa
vya uchaguzi wanavyopokea kutoka Tume, wanavihakiki, kuvikagua na kuhakikisha
vinasambazwa kwenye vituo vyote na kila mkuu wa kituo anapata vifaa vyote vya
uchaguzi vinavyohitajika mapema.

Amewataka kuhakikisha kuwa siku ya uchaguzi
wanaweka utaratibu utakaowezesha kila kituo cha kupigia kura kufunguliwa saa
1:00 kamili asubuhi na kufanya mawasiliano na Tume pale ambapo ushauri
utahitajika kuhusiana na masuala ya uchaguzi.

Akifungua mafunzo kama hayo Kisiwani Pemba,
Zanzibar, Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa
Rufani (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk amewaasa watendaji hao kufanya kazi kwa
kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa
na yatakayotolewa na Tume.

 “Jitahidini
na mjiepushe kuwa vyanzo vya malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na wadau wa
uchaguzi. Hakikisheni mnazingatia ipasavyo Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na
maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume,” amesema Jaji
Mwambegele.

Amewataka kuwashirikisha wadau wa uchaguzi kwenye
maeneo wanayopaswa kushirikishwa kwa mujibu wa Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo
na maelekezo ya Tume.

Amewakumbusha kuhusu wajibu wao wa kuhakikisha
wanavitambua vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji maalum ya vituo
husika na kuhakikisha kunakuwa na mpangilio mzuri ambao utaruhusu uchaguzi
kufanyika kwa utulivu na amani.

“Ajira za watendaji wa vituo zizingatie
kuajiri watendaji wenye weledi, wanaojitambua, wazalendo, waadilifu na wachapakazi
na kuachana na upendeleo kwa ndugu na jamaa ambao hawana sifa za kufanya
shughuli za uchaguzi,” amesema Jaji Mbarouk.

Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku tatu kwenye
mikoa mbalimbali nchini kwa siku tatu na yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi,
wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo.


Tume imeyagawa mafunzo hayo kwenye awamu
mbili ambapo awamu hii ya pili inahusisha mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Kusini
Pemba, Kaskazini Pemba, Mwanza, Mara, Dar es Salaam, Pwani, Rukwa, Katavi,
Manyara, Arusha, Songwe na Mbeya.
Awamu ya kwanza ilifanyika tarehe 15 hadi 17
na ilihusisha watendaji kutoka mikoa ya Morogoro, Singida, Dodoma, Kaskazini
Unguja, Kusini Unguja, Mjini Magharibi, Geita, Kagera, Mtwara, Lindi, Tabora,
Kigoma, Tanga, Kilimanjaro, Ruvuma, Iringa na Njombe.
Hakimu mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Goodselda Kalumuna akitoa maelezo kabla ya kuwaapisha washiriki hao wa mafunzo kwa watendaji wa Uchagzi Mkuu ambapo aliwaongoza kula kiapo cha kujitoa uanachama na kutunza siri wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi.


 

Washiriki wamafunzo kutoka Shinyanga na Simiyu wakila kiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kutunza siri. 

 

Washiriki wamafunzo kutoka Kisiwa cha Pemba, Zanzibar wakila kiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kutunza siri. 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

February 27, 2026

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025360

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Habari za Kitaifa

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

By Mbeya YetuFebruary 28, 202611

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mzee Rashidi Mfaume Kawawa, mwanasiasa mashuhuri na…

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026

TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

February 27, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025360

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.