Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025

MA-EMSII MBEYA WALIA NA UTITIRI WA TOZO NA KODI KATIKA KAZI ZAO,DC ITUNDA AAHIDI KUTAFUTIA SULUHU

August 28, 2025

Wazazi Wafichua Mbinu Walizotumia Kuwalinda Watoto Wao Dhidi ya Jicho Baya na Uovu

August 28, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI
  • MA-EMSII MBEYA WALIA NA UTITIRI WA TOZO NA KODI KATIKA KAZI ZAO,DC ITUNDA AAHIDI KUTAFUTIA SULUHU
  • Wazazi Wafichua Mbinu Walizotumia Kuwalinda Watoto Wao Dhidi ya Jicho Baya na Uovu
  • MH. MICHAEL MAKAO ALIVYOREJESHA FOMU YA UDIWANI KATA RUJEWA AAHIDI KUENDELEZA ALIPOISHIA
  • Mwanamke Afumaniwa Akipika Chakula Usiku kwa Mtu Asiyeonekana, Jirani Atoa Neno
  • HIKI NDICHO ALICHOKISEMA BAHATI NDINGO ALIPOKUWA AKIREJESHA FOMU KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MBARALI
  • Mwanamke miaka 50 aoana na kijana wa miaka 21 baada ya penzi lao kuvutia kijiji kizima kwa mshangao
  • KAILIMA AFUNGA KIKAO CHA UPANGAJI WA RATIBA YA KAMPENI ZA WAGOMBEA URAIS
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WATENDAJI UCHAGUZI WATAKIWA KUTOA TAARIFA KWA VYAMA VYA SIASA
Habari za Kitaifa

WATENDAJI UCHAGUZI WATAKIWA KUTOA TAARIFA KWA VYAMA VYA SIASA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJuly 21, 2025Updated:July 21, 2025No Comments18 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

 

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 21, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele akizungumza wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wa uchaguzi mkuu kutoka mikoa ya Shinyanga na Simiyu leo Julai 21, 2025. Mafunzo hayo yamefanyika mkoani Shinyanga.

 

Washiriki wa mafunzo hayo ambayo yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo kutoka majimbo yote ya Mikoa ya Shinyanga na Simiyu. 

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Cyprian Mbugano akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ambapo pia alitoa mada.

Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo kama hayo kwa Kisiwani Pemba, Zanzibar ambapo amewaasa watendaji hao kufanya kazi kwa kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Ndg Adam Mkina ambaye ni Mkurugenzi wa INEC ofisi ya Zanzibar akizungumza jambo.

Washiriki wa mafunzo hayo ambayo yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi, wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo kutoka majimbo yote ya Kisiwani Pemba, Zanzibar.

*******

Na. Mwandishi wetu, Shinyanga
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka
watendaji wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kutoa taarifa mapema kwa vyama vya
siasa kuhusu utaratibu wa kuwaapisha mawakala.

Hayo yamesemwa mkoani Shinyanga leo Julai 21,
2025 na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya
Rufani, Jacobs Mwambegele wakati akifungua mafunzo kwa watendaji wa uchaguzi
mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi oktoba mwaka huu kwa tarehe itakayotangazwa
na Tume.

“Wakati wa kuapisha mawakala, toeni taarifa
mapema kwa vyama vya siasa kwa mujibu wa sheria, kanuni na maelekezo ya Tume na
kuvipatia vyama vya siasa orodha ya vituo vya kupigia kura ili kuviwezesha
kupanga mawakala,” amesema Jaji Mwambegele.

Amewasisitiza watendaji hao kuhakikisha vifaa
vya uchaguzi wanavyopokea kutoka Tume, wanavihakiki, kuvikagua na kuhakikisha
vinasambazwa kwenye vituo vyote na kila mkuu wa kituo anapata vifaa vyote vya
uchaguzi vinavyohitajika mapema.

Amewataka kuhakikisha kuwa siku ya uchaguzi
wanaweka utaratibu utakaowezesha kila kituo cha kupigia kura kufunguliwa saa
1:00 kamili asubuhi na kufanya mawasiliano na Tume pale ambapo ushauri
utahitajika kuhusiana na masuala ya uchaguzi.

Akifungua mafunzo kama hayo Kisiwani Pemba,
Zanzibar, Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa
Rufani (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk amewaasa watendaji hao kufanya kazi kwa
kuzingatia Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa
na yatakayotolewa na Tume.

 “Jitahidini
na mjiepushe kuwa vyanzo vya malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na wadau wa
uchaguzi. Hakikisheni mnazingatia ipasavyo Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na
maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume,” amesema Jaji
Mwambegele.

Amewataka kuwashirikisha wadau wa uchaguzi kwenye
maeneo wanayopaswa kushirikishwa kwa mujibu wa Katiba, Sheria, Kanuni, miongozo
na maelekezo ya Tume.

Amewakumbusha kuhusu wajibu wao wa kuhakikisha
wanavitambua vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji maalum ya vituo
husika na kuhakikisha kunakuwa na mpangilio mzuri ambao utaruhusu uchaguzi
kufanyika kwa utulivu na amani.

“Ajira za watendaji wa vituo zizingatie
kuajiri watendaji wenye weledi, wanaojitambua, wazalendo, waadilifu na wachapakazi
na kuachana na upendeleo kwa ndugu na jamaa ambao hawana sifa za kufanya
shughuli za uchaguzi,” amesema Jaji Mbarouk.

Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku tatu kwenye
mikoa mbalimbali nchini kwa siku tatu na yanawajumuisha waratibu wa uchaguzi,
wasimamizi wa uchaguzi na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo.


Tume imeyagawa mafunzo hayo kwenye awamu
mbili ambapo awamu hii ya pili inahusisha mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Kusini
Pemba, Kaskazini Pemba, Mwanza, Mara, Dar es Salaam, Pwani, Rukwa, Katavi,
Manyara, Arusha, Songwe na Mbeya.
Awamu ya kwanza ilifanyika tarehe 15 hadi 17
na ilihusisha watendaji kutoka mikoa ya Morogoro, Singida, Dodoma, Kaskazini
Unguja, Kusini Unguja, Mjini Magharibi, Geita, Kagera, Mtwara, Lindi, Tabora,
Kigoma, Tanga, Kilimanjaro, Ruvuma, Iringa na Njombe.
Hakimu mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Goodselda Kalumuna akitoa maelezo kabla ya kuwaapisha washiriki hao wa mafunzo kwa watendaji wa Uchagzi Mkuu ambapo aliwaongoza kula kiapo cha kujitoa uanachama na kutunza siri wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao ya Uchaguzi.


 

Washiriki wamafunzo kutoka Shinyanga na Simiyu wakila kiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kutunza siri. 

 

Washiriki wamafunzo kutoka Kisiwa cha Pemba, Zanzibar wakila kiapo cha kujitoa uanachama wa vyama vya siasa na kutunza siri. 

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

Mbeya Yatikisika! Dkt. Tulia Achukua Fomu Ubunge Jimbo Jipya la Uyole

August 25, 2025

TAKUKURU Mbeya Yaokoa Milioni 47 na Kuongeza Mapato ya Halmashauri Zaidi ya Milioni 200

August 19, 2025

MGOMBEA NCCR MAGEUZI AJITOKEZA KUCHUKUA FOMU ZA UTEUZI

August 15, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025204

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024183

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 202592

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202486
Don't Miss
Afya na Ustawi

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

By Mbeya YetuAugust 28, 202577

Imeelezwa kuwa uuguzi na ukunga ni fani ya wito wa kipekee na inayohitaji si maarifa…

MA-EMSII MBEYA WALIA NA UTITIRI WA TOZO NA KODI KATIKA KAZI ZAO,DC ITUNDA AAHIDI KUTAFUTIA SULUHU

August 28, 2025

Wazazi Wafichua Mbinu Walizotumia Kuwalinda Watoto Wao Dhidi ya Jicho Baya na Uovu

August 28, 2025

MH. MICHAEL MAKAO ALIVYOREJESHA FOMU YA UDIWANI KATA RUJEWA AAHIDI KUENDELEZA ALIPOISHIA

August 28, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025

MA-EMSII MBEYA WALIA NA UTITIRI WA TOZO NA KODI KATIKA KAZI ZAO,DC ITUNDA AAHIDI KUTAFUTIA SULUHU

August 28, 2025

Wazazi Wafichua Mbinu Walizotumia Kuwalinda Watoto Wao Dhidi ya Jicho Baya na Uovu

August 28, 2025
Most Popular

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025204

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024183

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 202592
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.