Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Hafla ya Makabidhiano ya Vitabu vya Fidia vya Mradi wa Chanzo cha Mto Kiwira

December 15, 2025

WAKUTUBI WAKUTANA MBEYA WAJADILI MFUMO BORA WA MAKTABA NA USOMAJI VITABU KIDIJITALI

December 15, 2025

MKUU WA MKOA WA MBEYA BENNO MALISA AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KULINDA FEDHA ZA UMMA

December 15, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Hafla ya Makabidhiano ya Vitabu vya Fidia vya Mradi wa Chanzo cha Mto Kiwira
  • WAKUTUBI WAKUTANA MBEYA WAJADILI MFUMO BORA WA MAKTABA NA USOMAJI VITABU KIDIJITALI
  • MKUU WA MKOA WA MBEYA BENNO MALISA AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KULINDA FEDHA ZA UMMA
  • Suzi alivyomrejesha mpenzi wake na wakafunga ndoa
  • Jinsi unavyoweza kuibadilisha biashara yako na kukupa faida
  • RAIS DKT. SAMIA AKIWASILI SKUA (TANGA) KWA KIKAO CHA NDANI NA VIONGOZI WA JWTZ
  • WAZIRI MKUU- WATANZANIA TUNZENI AKIBA YA CHAKULA▪️Ahimiza matumizi ya mbolea na mbegu za mazao
  • Ndipo akashinda Sh13 milioni kupitia betting
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TCRA Yapaza Sauti Kupitia Kisaka: Bloga Muwe Mabalozi wa Amani Uchaguzi 2025
Habari za Kitaifa

TCRA Yapaza Sauti Kupitia Kisaka: Bloga Muwe Mabalozi wa Amani Uchaguzi 2025

Mbeya YetuBy Mbeya YetuAugust 4, 2025No Comments9 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Na Mwandishi Wetu

 Agosti 3, 2025 — Wazalishaji wa maudhui mtandaoni wametakiwa kuepuka kuchapisha taarifa zinazoweza kusababisha taharuki au kuchochea machafuko, hususan katika kipindi hiki kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Kitengo cha Huduma za Utangazaji kutoka TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, alipokuwa akiwasilisha mada katika mkutano wa watoa maudhui mtandaoni ulioandaliwa na Tume Huru ya Uchaguzi (INEC).

Mhandisi Kisaka amesema kuwa kipindi cha uchaguzi huwa na hali ya migawanyiko, mivutano na upotoshaji mkubwa, hivyo ni muhimu mabloga na watoa maudhui wengine kujiepusha kusambaza uvumi, kutangaza kwa umakini, kutopendelea upande wowote na kukemea lugha ya chuki.

“Kama unaona maudhui yanaweza kuleta taharuki ni bora kuachana nayo,” amesema Kisaka.

Ametoa mfano wa machafuko ya uchaguzi yaliyotokea Nigeria mwaka 2011, ambapo watu zaidi ya 800 walipoteza maisha, na Kenya mwaka 2007, ambapo zaidi ya watu 1,000 walifariki huku wengine 600,000 wakikosa makazi.

Ameongeza kuwa vyombo vya habari vinaweza kuwa sehemu ya tatizo endapo vitasambaza uvumi au kuonyesha upendeleo wa kisiasa kwa namna isiyozingatia maadili.

“Uvumi ndiyo chanzo kikuu cha vurugu. Vyombo vya habari vinapaswa kuchunguza uvumi na kutoa taarifa sahihi mapema ili kuzuia machafuko ya kulipiza kisasi,” amesema.

Aidha, Kisaka amewataka mabloga kutochapisha au kurudia vichwa vya habari vyenye lugha ya kichochezi, hata kama kauli hizo zimetolewa na wanasiasa. Amesema lugha ya kudhalilisha inaweza kuchochea ghasia na vitendo vya kikatili.

Pia ametoa angalizo kwa mabloga kuacha matangazo ya moja kwa moja ya kampeni, akieleza kuwa kazi hiyo inapaswa kufanywa na waandishi waandamizi waliobobea katika kuripoti wakati wa migogoro.

“Matangazo ya moja kwa moja ya machafuko yanahitaji uzoefu. ‘One Man Show’ wa bloga hauna nafasi katika mazingira hayo ya shinikizo,” amesema.

Kwa mujibu wa TCRA, mafunzo ya namna ya kuripoti wakati wa maafa na katika mazingira ya uchaguzi ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha uchaguzi wa 2025 unafanyika kwa amani kama ilivyokuwa katika chaguzi zilizopita.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

MAHAFALI YA 23 YA TAASISI YA UHASIBU TIA KAMPASI YA MBEYA, RC MALISA AWAALIKA WAWEKEZAJI MKOANI MBEYA.

December 12, 2025

TANZANIA NA MAREKANI ZASONGA MBELE KUKAMILISHA MAKUBALIANO MAKUBWA YA UWEKEZAJI

December 9, 2025

TANZANIA AND U.S. MOVE TO FINALISE MAJOR INVESTMENT AGREEMENTS

December 8, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025258

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025235

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024208

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025130
Don't Miss
Video Mpya

Hafla ya Makabidhiano ya Vitabu vya Fidia vya Mradi wa Chanzo cha Mto Kiwira

By Mbeya YetuDecember 15, 20251

WAKUTUBI WAKUTANA MBEYA WAJADILI MFUMO BORA WA MAKTABA NA USOMAJI VITABU KIDIJITALI

December 15, 2025

MKUU WA MKOA WA MBEYA BENNO MALISA AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KULINDA FEDHA ZA UMMA

December 15, 2025

Suzi alivyomrejesha mpenzi wake na wakafunga ndoa

December 15, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Hafla ya Makabidhiano ya Vitabu vya Fidia vya Mradi wa Chanzo cha Mto Kiwira

December 15, 2025

WAKUTUBI WAKUTANA MBEYA WAJADILI MFUMO BORA WA MAKTABA NA USOMAJI VITABU KIDIJITALI

December 15, 2025

MKUU WA MKOA WA MBEYA BENNO MALISA AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KULINDA FEDHA ZA UMMA

December 15, 2025
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025258

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025235

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024208
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.