Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

USHIRIKI BENKI NMB MAONESHO KILIMO NANE NANE MBEYA,ELIMU UJASIRIAMALI HUDUMA ZA KIBENKI ZATOLEWA

August 5, 2025

“Rais wa IPU Dkt. Tulia Kuongoza Uzinduzi wa Kitabu cha Ndoto ya Yatima”Mbeya, Septemba 13

August 5, 2025

Aliyenitapeli mtandaoni anirudishia fedha zangu

August 5, 2025
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • USHIRIKI BENKI NMB MAONESHO KILIMO NANE NANE MBEYA,ELIMU UJASIRIAMALI HUDUMA ZA KIBENKI ZATOLEWA
  • “Rais wa IPU Dkt. Tulia Kuongoza Uzinduzi wa Kitabu cha Ndoto ya Yatima”Mbeya, Septemba 13
  • Aliyenitapeli mtandaoni anirudishia fedha zangu
  • Mwamba atangaza ndoa na Bibi wa miaka 84, ataja sababu
  • TCRA Yapaza Sauti Kupitia Kisaka: Bloga Muwe Mabalozi wa Amani Uchaguzi 2025
  • WATOTO WA VIJIJI VYA USANGU MBARALI MBEYA WASHINDANA KUSOMA VITABU WAJENGEWA HAMASA YA KUSOMA
  • Mafunzo ya Wasimamizi wa Uchaguzi Ngazi ya kata jimbo la Mbeya Yasisitiza Utii wa Sheria
  • TANZANIA WENYEJI WA WARSHA YA WAKUU WA TAASISI ZA KUPAMBANA NA RUSHWA KUTOKA NCHI ZA SADC
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » TCRA Yapaza Sauti Kupitia Kisaka: Bloga Muwe Mabalozi wa Amani Uchaguzi 2025
Habari za Kitaifa

TCRA Yapaza Sauti Kupitia Kisaka: Bloga Muwe Mabalozi wa Amani Uchaguzi 2025

Mbeya YetuBy Mbeya YetuAugust 4, 2025No Comments7 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Na Mwandishi Wetu

 Agosti 3, 2025 — Wazalishaji wa maudhui mtandaoni wametakiwa kuepuka kuchapisha taarifa zinazoweza kusababisha taharuki au kuchochea machafuko, hususan katika kipindi hiki kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika mwishoni mwa mwaka huu.

Wito huo umetolewa na Meneja wa Kitengo cha Huduma za Utangazaji kutoka TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, alipokuwa akiwasilisha mada katika mkutano wa watoa maudhui mtandaoni ulioandaliwa na Tume Huru ya Uchaguzi (INEC).

Mhandisi Kisaka amesema kuwa kipindi cha uchaguzi huwa na hali ya migawanyiko, mivutano na upotoshaji mkubwa, hivyo ni muhimu mabloga na watoa maudhui wengine kujiepusha kusambaza uvumi, kutangaza kwa umakini, kutopendelea upande wowote na kukemea lugha ya chuki.

“Kama unaona maudhui yanaweza kuleta taharuki ni bora kuachana nayo,” amesema Kisaka.

Ametoa mfano wa machafuko ya uchaguzi yaliyotokea Nigeria mwaka 2011, ambapo watu zaidi ya 800 walipoteza maisha, na Kenya mwaka 2007, ambapo zaidi ya watu 1,000 walifariki huku wengine 600,000 wakikosa makazi.

Ameongeza kuwa vyombo vya habari vinaweza kuwa sehemu ya tatizo endapo vitasambaza uvumi au kuonyesha upendeleo wa kisiasa kwa namna isiyozingatia maadili.

“Uvumi ndiyo chanzo kikuu cha vurugu. Vyombo vya habari vinapaswa kuchunguza uvumi na kutoa taarifa sahihi mapema ili kuzuia machafuko ya kulipiza kisasi,” amesema.

Aidha, Kisaka amewataka mabloga kutochapisha au kurudia vichwa vya habari vyenye lugha ya kichochezi, hata kama kauli hizo zimetolewa na wanasiasa. Amesema lugha ya kudhalilisha inaweza kuchochea ghasia na vitendo vya kikatili.

Pia ametoa angalizo kwa mabloga kuacha matangazo ya moja kwa moja ya kampeni, akieleza kuwa kazi hiyo inapaswa kufanywa na waandishi waandamizi waliobobea katika kuripoti wakati wa migogoro.

“Matangazo ya moja kwa moja ya machafuko yanahitaji uzoefu. ‘One Man Show’ wa bloga hauna nafasi katika mazingira hayo ya shinikizo,” amesema.

Kwa mujibu wa TCRA, mafunzo ya namna ya kuripoti wakati wa maafa na katika mazingira ya uchaguzi ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha uchaguzi wa 2025 unafanyika kwa amani kama ilivyokuwa katika chaguzi zilizopita.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

TANZANIA WENYEJI WA WARSHA YA WAKUU WA TAASISI ZA KUPAMBANA NA RUSHWA KUTOKA NCHI ZA SADC

August 4, 2025

WAZALISHAJI WA MAUDHUI MTANDAONI WAHIMIZWA KUHAMASISHA WANANCHI KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025

August 4, 2025

WAANDISHI WA HABARI WAHIMIZWA KUHAMASISHA USHIRIKI WA WANANCHI KUPIGA KURA

August 2, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024179

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025157

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202485

UCHAGUZI MKUU 2025: MAJIMBO MAPYA NANE YAANZISHWA, 12 YABADILISHWA MAJINA

May 12, 202581
Don't Miss
Video Mpya

USHIRIKI BENKI NMB MAONESHO KILIMO NANE NANE MBEYA,ELIMU UJASIRIAMALI HUDUMA ZA KIBENKI ZATOLEWA

By Mbeya YetuAugust 5, 20250

#mbeyayetutv

“Rais wa IPU Dkt. Tulia Kuongoza Uzinduzi wa Kitabu cha Ndoto ya Yatima”Mbeya, Septemba 13

August 5, 2025

Aliyenitapeli mtandaoni anirudishia fedha zangu

August 5, 2025

Mwamba atangaza ndoa na Bibi wa miaka 84, ataja sababu

August 5, 2025
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

USHIRIKI BENKI NMB MAONESHO KILIMO NANE NANE MBEYA,ELIMU UJASIRIAMALI HUDUMA ZA KIBENKI ZATOLEWA

August 5, 2025

“Rais wa IPU Dkt. Tulia Kuongoza Uzinduzi wa Kitabu cha Ndoto ya Yatima”Mbeya, Septemba 13

August 5, 2025

Aliyenitapeli mtandaoni anirudishia fedha zangu

August 5, 2025
Most Popular

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024179

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025157

TULIA TRUST YATOA MIFUKO 400 YA SARUJI KWA SHULE 3 JIJINI MBEYA

March 26, 202485
© 2025 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.