Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

DAS Mbeya: Kipato Kisiharibu Vyanzo vya Maji

February 10, 2026

KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA

February 10, 2026

Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji

February 9, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • DAS Mbeya: Kipato Kisiharibu Vyanzo vya Maji
  • KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA
  • Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji
  • Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo
  • TGNP na CARE Waimarisha Elimu ya Tabia Nchi Mbeya
  • New Asante Mbeya Yapongeza TAKUKURU Mbeya kwa Elimu ya Uadilifu na Kufungua Uelewa wa Wanachama
  • Utengule Usangu Yapata Jezi, Majiko ya Gesi na Msaada wa Kijamii Kutoka kwa Mbunge Ndingo
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na Aga Khan Zaanzisha Ushirikiano wa Kuboresha Huduma za Afya
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI
Afya na Ustawi

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

Mbeya YetuBy Mbeya YetuAugust 28, 2025No Comments139 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Imeelezwa kuwa uuguzi na ukunga ni fani ya wito wa kipekee na inayohitaji si maarifa na ujuzi bali heshima, moyo wa kujitolea, maadili ya juu na upendo kwa binadamu.

Hayo yamesemwa na Samwel Mwangoka Mkuu wa Chuo cha Uuguzi na Ukunga Tukuyu katika mahafali ya 14 ya kuhitimu mafunzo ya Stashahada ya uuguzi na ukunga chuoni hapo na kuwasihi kuzingatia maadili kila mahali watakapokwenda na kuwa mfano wa nidhamu, bidii na uadilifu katika kazi.

“..mtakuwa na jukumu kubwa la kutoa huduma bora za afya kwa wananchi na mtakabiliana na changamoto mbalimbali na zinaendelea kubadilika, kuanzia kushughulikia matatizo ya afya ya umma hadi kutoa huduma kwa watu binafsi, familia na jamii kwa ujumla. Naamini elimu mliyoipata imewaandaa na mtaitumia vyema kukabiliana na changamoto.” – amesema Mkuu wa Chuo Samwel Mwangoka.

Ameeleza kuwa ni muhimu wahitimu hao kuwa na jitihada za kuendelea kuongeza ujuzi na kutumia miongozo ya kutolea huduma za afya bila kusahau kuhudumia kila mgonjwa kwa heshima, huruma na upendo kwani vina mchango mkubwa ya kuleta mabadiliko katika afya ya wagonjwa na jamii kwa ujumla.

“kumbukeni kuwa kujifunza katika afya ni maisha yote kwani, huduma za afya zinaendelea kubadilika kutokana na mabadliko ya tekinolojia, mabadiliko ya magonjwa na ni wajibu wako kujifunza na kukabiliana na mabadiliko ya teknolojia mpya. Kutumia fursa kujiendeleza kitaaluma, kwa kuwa ni kwa kuendelea kujifunza ndipo utaendelea kutoa huduma bora zaidi.” – alisema Mkuu wa Chuo Samwel Mwangoka

Nae Mgeni Rasmi wa mahafali hayo Ndugu Gabriel Godlove Mwakagenda akimuwakilisha Mhe. Anthony Mwantona Mkurugenzi wa God’s Bridge Development Foundation amepongeza Uongozi wa chuo na kueleza kuwa mafanikio hayo yanathibitisha juhudi na kujituma kwa wahitimu na wafanyakazi wa chuo kwa kuandaa wataalamu wa hali ya juu wanaoweza kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya afya.

“Ninapozungumza leo, nawapongeza sana wahitimu wetu kwa kufanikisha hatua hii muhimu zaidi katika maisha yao. Safari yenu haikuwa rahisi, lakini kwa bidii, uvumilivu, na maono makubwa, mmeweza kufikia malengo yenu. Hii ni ishara kwamba, kwa umoja, juhudi, na maadili mema, tunaweza kuleta maendeleo makubwa katika sekta ya afya hapa nchini.” – alisema Mgeni Rasmi

Amesema “Nawaomba mkiwa wahudumu wa afya, muendelee kueneza upendo, huruma, na heshima katika huduma zenu. Kila mtoa huduma anahusika na maisha ya binadamu, na ni jukumu lenu kuhakikisha mnatoa huduma bora zaidi zinazolingana na maadili ya taaluma hii takatifu. Mtaendelea kuwa nguzo muhimu katika ujenzi wa jamii imara na yenye afya.”

Ameipongeza na kuishukuru Serikali kwa jitihada kubwa zilizofanyika katika kuwekeza katika miundo mbinu na kukamilisha jengo la Bweni ambalo ujenzi wake ulisimama tangu mwaka 2011 lakini katika awamu hii serikali imeleta kiasi cha shilingi 432,332,471.00 zilizokamilisha ujenzi huu na kutatua changamoto ya malazi bora, salama na yenye heshima kwa wanafunzi, haya ni maendeleo makubwa katika chuo hiki.

“Uwekezaji huu ni uthibitisho wa nia ya dhati ya serikali katika kuleta ustawi wa wananchi na kuhakikisha kwamba huduma za msingi zinapatikana kwa urahisi na ubora wa hali ya juu. Maboresho haya yamewezesha chuo chetu kutoa mazingira rafiki kwa wanafunzi na wafanyakazi”.

Wakisoma risala yao Judith Mbano na Daudi Malimi wahitimu wa mwaka wa tatu ngazi ya stashahada wa Chuo cha Uuguzi na Ukunga Tukuyu wameeleza kuwa Katika kipindi cha miaka mitatu, wamepata fursa ya kujifunza masomo ya nadharia na vitendo, wameshiriki katika mafunzo ya vitendo vijijini, hospitalini na maeneo mbalimbali ya kijamii, jambo lililowapa uzoefu wa moja kwa moja na kujiandaa kwa maisha ya kitaaluma.

Idadi ya wanafunzi wa mwaka tatu tunaohitimu mafunzo ya Stashahada ya Uuguzi na Ukunga katika chuo cha Uuguzi na Ukunga Tukuyu ni 63, ikiwa idadi ya wasichana ni 32 na idadi ya wavulana ikiwa ni 31.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

TAASISI ZA PICTERUS AS NA GOAL 3 KUANZISHA TEKNOLOJIA YA KISASA YA KUPIMA MANJANO KWA WATOTO WACHANGA TANZANIA

January 28, 2026

MFANYAKAZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA APATA TUZO YA MWANAFUNZI BORA WA SHAHADA YA UZAMILI YA UDAKTARI WA MENO MUHAS.

December 8, 2025

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAANZA RASMI KUTOA MAFUNZO YA HUDUMA ZA DHARURA KWA LENGO LA KUOKOA MAISHA NA KUPUNGUZA ATHARI ZA AJALI NA DHARURA ZA KIAFYA NYANDA ZA JUU KUSINI

November 26, 2025

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025337

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024227

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025139
Don't Miss
Video Mpya

DAS Mbeya: Kipato Kisiharibu Vyanzo vya Maji

By Mbeya YetuFebruary 10, 20261

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbeya, Bw. Azizi Faki, ametoa onyo kali juu ya kuendelea kwa uharibifu wa vyanzo vya maji wilayani humo, akisema hali halisi ya uchafuzi na upungufu wa maji inaonekana wazi kutokana na shughuli za kibinadamu zisizozingatia sheria.

Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa chanzo cha maji cha Mtombalizi, kilichopo katika Kata za Utengule Usongwe na Nsalala, Bw. Faki alisema uchimbaji wa mchanga na mawe katikati ya mto pamoja na uharibifu wa kingo za maji umepelekea mto huo kupoteza mwelekeo wake wa asili, maji kuchafuka na kupungua kwa kiasi kikubwa.

Bw. Faki alisema licha ya kuwepo kwa maelekezo ya awali ya kulinda kingo za mito, kupanda miti na kuacha mita sitini kutoka kwenye chanzo cha maji bila shughuli za kibinadamu, hali bado ni mbaya kutokana na kuendelea kwa shughuli haramu, hali inayohatarisha vyanzo vya maji vinavyotegemewa na wananchi wa sasa na vizazi vijavyo.

Alitoa wito kwa taasisi zote husika ikiwemo TFS, mamlaka za maji, mamlaka ya madini, Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Rukwa, pamoja na viongozi wa serikali za mitaa, kata na tarafa kushirikiana kikamilifu katika kulinda chanzo hicho. Alisisitiza kuwa jitihada za kutafuta kipato haziwezi kuwa sababu ya kuvunja sheria na kuharibu mazingira.

KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA

February 10, 2026

Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji

February 9, 2026

Tazama muonekano mpya wa Soko la Kariakoo

February 8, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

DAS Mbeya: Kipato Kisiharibu Vyanzo vya Maji

February 10, 2026

KUMBUKUMBU YA EDWARD NGOYAI LOWASSA

February 10, 2026

Wilaya ya Mbeya Yapiga Marufuku Kilimo na Ukataji Miti Kwenye Vyanzo vya Maji

February 9, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025337

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025252

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024227
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.