Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100
  • Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari
  • VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII
  • TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
  • Mfumo wa kidigitali wa Vyeti vya Uasili kupitia Chemba ya Taifa ya Biashara Tanzania (TNCC) waanza rasmi Machi 2, 2026
  • MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA
  • Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya na NHIF Mkoa wa Mbeya waelimisha walemavu kuhusu Bima ya Afya
  • Serikali na TNCC Kuunganisha Mifumo Kidigitali, TRA Yaimarisha Ukusanyaji Mapato
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MATIBABU YA KIBINGWA YA HUDUMA MKOBA YA MADAKTARI WA DT. SAMIA UKOMBOZI MKUBWA KWA WANANCHI WA MKOA WA SONGWE.
Habari za Kitaifa

MATIBABU YA KIBINGWA YA HUDUMA MKOBA YA MADAKTARI WA DT. SAMIA UKOMBOZI MKUBWA KWA WANANCHI WA MKOA WA SONGWE.

Mbeya YetuBy Mbeya YetuSeptember 15, 2025Updated:September 15, 2025No Comments9 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mhe. Jabiri Omari Makame leo tarehe 15/09/2025 amezindua rasmi huduma mkoba za Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia mkoani Songwe ikiwa ni juhudi za Serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhakikisha huduma bora za afya zinawafikia wananchi wote kwa ukamilifu.

Katika hotuba yake, Mhe. Jabiri Makame ameeleza kuwa ujio wa kambi hiyo ya Madaktari Bingwa wa Dkt. Samia ni ishara ya dhamira ya dhati ya Serikali ya kuimarisha huduma za afya mkoani Songwe. Amebainisha kuwa, kuanzia mwaka 2020 hadi 2025, mkoa umepata maendeleo makubwa ikiwa ni pamoja na ongezeko la vituo vya afya kutoka 205 hadi 273, na hospitali kutoka 2 hadi 5, vyote kwa lengo la kuboresha huduma za msingi na za kitaalamu kwa wananchi.

“Serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 40.6 kwa ajili ya kuboresha miundombinu, ununuzi wa dawa, vifaa, na vitendanishi, pamoja na kuanzisha afua mbalimbali za tiba ikiwemo lishe, kudhibiti malaria, kifua kikuu, na magonjwa ya zinaa na UKIMWI. Kupitia juhudi hizi, upatikanaji wa dawa umeongezeka kwa asilimia 90, hali inayorahisisha upatikanaji wa huduma na kupunguza vifo vya watoto wachanga kutoka 320 mwaka 2022 hadi 146 mwaka 2023, mkoa umepokea watumishi wa sekta ya afya 725 kuanzia mwaka 2021 hadi 2025, ikiwa ni jitihada za kukabiliana na upungufu wa watumishi wa afya, na kufanya huduma kuwa za karibu zaidi kwa wananchi”. – amesema Mhe. Jabiri Makame

Aidha Mhe. Jabiri Makame, ametoa rai kwa viongozi na watendaji wa mkoa kuhakikisha wanatoa ushirikiano wa karibu kwa madaktari ili kuhakikisha huduma zinazotolewa zinafikia viwango vya juu, na wananchi wanafaidika kwa kiwango cha juu. Pia, amewataka wananchi kushirikiana na wataalamu wa afya ili kufanikisha malengo ya afya bora kwa wote.

Naye Bi. Pasclina Andrew Mratibu wa Huduma Mkoba ya Madaktari wa Mama Samia Mkoa wa Songwe kutoka Wizara ya Afya amesema kuwa uwekezaji huu mkubwa wa Serikali katika sekta ya afya ni hatua muhimu katika kuimarisha afya ya wananchi wa Songwe na kuboresha huduma za matibabu, kwani sasa wananchi hawatalazimika kusafiri kwenda mikoa jirani kwa huduma za kibingwa. Hii ni ahadi na matokeo ya moyo wa Serikali wa kuwaletea wananchi maendeleo na ustawi wa afya.

“ujio wa kambi hii ya matibabu unaleta faida kubwa ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za tiba za kitaalamu zilizokuwa zinahitaji kusafiriwa hadi mikoa mikubwa kama Dar es Salaam na Mbeya, hivyo kuokoa muda na gharama za wananchi. Pia, kambi hii itaimarisha uwezo wa wataalamu wa afya kwa kuwapa mafunzo na ushauri wa kitaalamu (mentorship), na kusogeza huduma za kibingwa kwa wananchi wa mkoa wa Songwe” – Pasclina

Timu ya madaktari 30 kutoka kada mbalimbali za afya zikiwa ni pamoja Madaktari wa Uzazi na Magonjwa ya wanawake, Madaktari wa Watoto, Madaktari bingwa wa usingizi na ganzi salama, madaaktari wa magonjwa ya ndani, madaktari wa meno, madaktari wa upasuaji na wauguzi Bingwa wanatarajia kutoa huduma mkoba kwa muda wa wiki moja katika halmashauri 5 za mkoa wa Songwe..

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

February 27, 2026

MAHUNDI: SERIKALI KUIMARISHA ELIMU YA MALEZI KUPITIA KAMPASI YA KISANGARA

February 26, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025360

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236

Vijana Wamchana Waziri wa Vijana, ”Si Wananchi, Ila Watumishi Ndio Watakaoniangusha”

December 1, 2025140
Don't Miss
Habari za Kitaifa

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

By Mbeya YetuFebruary 28, 202611

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mzee Rashidi Mfaume Kawawa, mwanasiasa mashuhuri na…

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026

TAKUKURU MBEYA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 100, YAIMARISHA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

February 27, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

SIMBA WA VITA MZEE RASHIDI MFAUME KAWAWA AMBAYE ANGEKUWA HAI JANA ANGETIMIZA UMRI WA MIAKA 100

February 28, 2026

Mwalupindi Akabidhi Tuzo Vitabu na kufuturisha wanafunzi Kuimarisha Elimu Sangu Sekondari

February 28, 2026

VIONGOZI WA KIDINI,MAKUNDI YA KIJAMII WAPEWA SEMINA SAPOTI YA KISAIKOLOJIA KWA JAMII

February 28, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025360

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025253

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024236
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.