Close Menu
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from FooBar about art, design and business.

What's Hot

Nilivyorejesha Uhuru Wangu Kitandani Baada ya Miaka ya Kuishi Bila Hamu Wala Hisia

January 7, 2026

Nilivyopambana na Baby Mama Aliyenigeuza Mfadhili Pekee Bila Haki, Mpaka Hatimaye Nikaweza Kuwa Karibu na Watoto Wangu Tena

January 7, 2026

NMB Yaimarisha Ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya

January 7, 2026
Facebook X (Twitter) Instagram
Trending
  • Nilivyorejesha Uhuru Wangu Kitandani Baada ya Miaka ya Kuishi Bila Hamu Wala Hisia
  • Nilivyopambana na Baby Mama Aliyenigeuza Mfadhili Pekee Bila Haki, Mpaka Hatimaye Nikaweza Kuwa Karibu na Watoto Wangu Tena
  • NMB Yaimarisha Ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya
  • Mbunge Patali Aishukuru Serikali kwa Kuimarisha Miradi ya Maendeleo Mbeya Vijijini
  • MHE. MAHUNDI AWASISITIZA WATOTO WA SHULE YA MAADILISHO IRAMBO KUBADILIKA NA KUJENGA MUSTAKABALI MWEMA
  • Nilikuwa Nikipoteza Pesa Bila Kujua Inakwenda Wapi Uamuzi Ulioninusuru
  • Nilijaribu Kushinda Sport Bet Bila Mafanikio Mwongozo Mmoja Ulinifanya Nilivune Milioni
  • HATIMAYE ASANTE MBEYA WAFANYA MAAMUZI MAGUMU WACHAGUA VIONGOZI TAKUKURU KUSIMAMIA MGAWANYO WA MALI
Facebook X (Twitter) Instagram
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
  • Home
  • Habari za Kitaifa
  • Utalii na Utamaduni
  • Elimu na Vijana
  • Matukio ya Kijamii
  • Afya na Ustawi
Mbeya Yetu OnlineMbeya Yetu Online
Home » MHE. MAHUNDI AWASISITIZA WATOTO WA SHULE YA MAADILISHO IRAMBO KUBADILIKA NA KUJENGA MUSTAKABALI MWEMA
Habari za Kitaifa

MHE. MAHUNDI AWASISITIZA WATOTO WA SHULE YA MAADILISHO IRAMBO KUBADILIKA NA KUJENGA MUSTAKABALI MWEMA

Mbeya YetuBy Mbeya YetuJanuary 6, 2026No Comments27 Views
Facebook Twitter Pinterest LinkedIn WhatsApp Reddit Tumblr Email
Share
Facebook Twitter LinkedIn Pinterest Email

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewataka watoto waliopo katika Shule ya Maadilisho Irambo mkoani Mbeya kuchukulia uwepo wao chuoni hapo kama fursa ya mabadiliko chanya na maandalizi ya maisha bora ya baadaye.

Akizungumza wakati wa ziara yake shuleni hapo, Mhe. Mahundi alisema watoto hao hawapaswi kujiona tofauti au waliopotea, bali wajione kama vijana wanaojengwa upya ili kuwa raia wema na viongozi wa kesho.

“Kuwepo kwenu hapa siyo adhabu bali ni mpango wa Mwenyezi Mungu wa kuwajenga upya. Maadilisho ni mabadiliko ya kweli, na kesho yenu bado ni njema,” alisema Mhe. Mahundi.

Amefafanua kuwa Shule ya Maadilisho siyo gereza, bali ni kituo cha malezi na elimu kwa watoto walio chini ya miaka 18 waliokiuka sheria, kwa lengo la kuwarekebisha kimaadili, kielimu na kitabia ili warejee salama kwenye jamii.

Mhe. Mahundi alisema Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ina wajibu wa kisheria na kiserikali kuhakikisha mtoto analindwa, anakuzwa, analelewa na kuandaliwa kuwa raia mwema wa Taifa.

Aidha, aliwahimiza watoto hao kutumia vyema fursa ya elimu inayotolewa shuleni hapo ikiwemo elimu ya msingi na sekondari, akisisitiza kuwa wapo watoto waliopita katika shule hiyo na baadaye kufanikiwa kielimu hadi vyuo vikuu.

“Msikate tamaa. Wapo waliowahi kuwa hapa, wakasoma, wakafaulu, wakaendelea na masomo hadi vyuo vikuu. Na nyinyi mnaweza,” aliongeza.

Katika hotuba yake, Mhe. Mahundi pia aliwasihi watoto hao kumcha Mungu bila kujali dhehebu lao, kuheshimu wakubwa na wadogo, kuwa watiifu, wasikivu na kuacha kabisa mienendo iliyowapeleka kwenye makosa.

Akiwahakikishia jamii, alisema watoto watakaomaliza muda wao wa maadilisho watarejeshwa kwa wazazi na jamii zao, akitoa wito kwa jamii kuwapokea kwa upendo bila kuwanyanyapaa.

Ziara hiyo ilihitimishwa kwa Mhe. Mahundi kukabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto hao, ikiwa ni sehemu ya kuwatia moyo na kuwajengea matumaini mapya ya maisha.

Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr Telegram Email
Mbeya Yetu

Related Posts

NMB Yaimarisha Ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya

January 7, 2026

NAIBU WAZIRI MAHUNDI ASISITIZA UWAJIBIKAJI MIRADI VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII.

January 5, 2026

NAIBU WAZIRI MAHUNDI ATOA TABASAMU KWA KITUO CHA TUMAINI LA WAZEE JIJINI MBEYA.

January 4, 2026

Leave A Reply Cancel Reply

Top Posts

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025296

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025239

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024213

WAHITIMU WA UUGUZI NA UKUNGA WAPEWA WITO WA KUONYESHA MAADILI, UPENDO NA HESHIMA KAZINI

August 28, 2025132
Don't Miss
Uncategorized

Nilivyorejesha Uhuru Wangu Kitandani Baada ya Miaka ya Kuishi Bila Hamu Wala Hisia

By Mbeya YetuJanuary 7, 20261

Miaka mingi nilijikuta nikitumia maisha yangu ya ndoa bila furaha kitandani. Nilikuwa na mume mzuri,…

Nilivyopambana na Baby Mama Aliyenigeuza Mfadhili Pekee Bila Haki, Mpaka Hatimaye Nikaweza Kuwa Karibu na Watoto Wangu Tena

January 7, 2026

NMB Yaimarisha Ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya

January 7, 2026

Mbunge Patali Aishukuru Serikali kwa Kuimarisha Miradi ya Maendeleo Mbeya Vijijini

January 7, 2026
Stay In Touch
  • Facebook
  • Twitter
  • Pinterest
  • Instagram
  • YouTube
  • Vimeo

Subscribe to Updates

Get the latest creative news from SmartMag about art & design.

About Us
About Us

Mbeya Yetu is a dynamic online platform that serves as a comprehensive source for news and information, offering a diverse range of content that caters to the interests and needs of its audience. Focusing on key pillars such as Habari za Kijamii (Social News), Uchumi na Biashara (Economy and Business), Elimu na Vijana (Education and Youth), Afya na Ustawi (Health and Well-being), and Habari za Kitaifa (National News), Mbeya Yetu is committed to keeping its community informed and engaged.

Facebook X (Twitter) Pinterest YouTube WhatsApp
Our Picks

Nilivyorejesha Uhuru Wangu Kitandani Baada ya Miaka ya Kuishi Bila Hamu Wala Hisia

January 7, 2026

Nilivyopambana na Baby Mama Aliyenigeuza Mfadhili Pekee Bila Haki, Mpaka Hatimaye Nikaweza Kuwa Karibu na Watoto Wangu Tena

January 7, 2026

NMB Yaimarisha Ushirikiano na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya

January 7, 2026
Most Popular

Njia rahisi ya kushinda kesi Mahakamani bila kutoa rushwa

February 7, 2025296

LIVE: CCM YATANGAZA MAJINA YA WAGOMBEA UBUNGE BAADA YA KIKAO CHA KAMATI KUU (CCM)

July 29, 2025239

KUMI WAKAMATWA WAKITOROSHA KILO 9.5 ZA DHAHABU

March 19, 2024213
© 2026 Mbeya Yetu. Powered by Digital Media Innovation Program.
  • Home

Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.