Kijana dereva wa bodaboda Brown Anthony amevunja rekodi baada ya kusafiri kutoka Mbeya hadi Dar es Salaam kwa saa 10 tu akitumia pikipiki aina ya Boxer 150 HD (MC 473 FKT).
Safari hii ilianza kama ubishani wa kawaida kati yake na bodaboda mwenzake Alex Ndile tarehe 14 Januari 2026, wakibishana kama inawezekana kufika Dar ndani ya masaa 13. Ubishi ukawekwa kwenye makubaliano rasmi, na Brown akaamua kuthibitisha kwa vitendo.

